UPDATE: Padri afikishwa Mahakamani kwa tuhuma za kulawiti watoto 10 Moshi

UPDATE: Padri afikishwa Mahakamani kwa tuhuma za kulawiti watoto 10 Moshi

Huu ni upuuzi wa mashetani wa kanisa katoliki. Mbona nyuzi nyingi za huu upuuzi wao, hujaziona hizi; Chato: Katekista wa kanisa Katoliki akamatwa kwa tuhuma za kubaka mtoto wa miaka 8
Jiongeze wewe ficha ujinga wako, kwani kanisa ndio limemtuma afanye hayo makosa yake. Hakuna masheikh waliowahi kubaka au kulawiti huko madrasa na sehemu zingine, je uislam ndio umewatuma?

Hakuna anayemtetea huyu padri, kafanya makosa sheria ifuate mkondo wake ila kitendo cha kulaumu taasisi kana kwamba ndio iliyomtuma ni kukosa akili.
 
Suluhisho la hili ni rahisi sana. Acheni kuwapeleka watoto kwenye hayo yanayoitwa mafundisho ya dini. Mnawakosea sana na kuwaharibia future zao kwa mambo yasiyohitajika katika umri wao
Zamani ilikuwa ni sifa kwa Wakatoliki na Waanglikana (High church) kuwapeleka Watoto wao kutumikia misa kanisani na kulelewa katika mashirika ya Mapadri

LAKINI kwasasa, ni bora kabisa Mtoto hata asipate mafundisho ya kutumikia wala komunio kama ndio upumbavu huu unafanywa na mapadri namna hii.
 
Martin Luther was a Padre and Failed to stay alone

Let them Marry.
 
UPDATES:

Sostenes Bahati Soka, Padri wa Kanisa Katoliki, Parokia Teule ya Mtakatifu Deonis Aropagita, Jimbo la Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro amesomewa mashtaka matatu katika Mahakama mbili tofauti. Padri huyo mwenye miaka 41, amesomeshwa mashataka hayo leo Jumatatu, Septemba 26, 2022 kwa nyakati tofauti akianza na Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi kisha Mahakama ya Wilaya ya Moshi.

Kesi ya kwanza ilisomwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Salome Mshasha ambapo Padri huyo anakabiliwa na shtaka moja la kumbaka mtoto wa miaka 12. Wakili wa Serikali, Kasimu Nasiri amesema upelelezi wa kesi hiyo umekamilika

Mshtakiwa huyo amekana shtaka hilo huku Wakili wa Serikali, Kasimu Nasiri akisema upelelezi umekamilika na Hakimu Salome ameiahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 10, 2022 ambapo atafikishwa kusomewa maelezo ya awali. Mshtakiwa huyo alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wakazi wa Kilimanjaro ambao wawe na uwezo wakuweka bondi ya Sh10 milioni, kika mmoja.

Padri Soka amekosa dhamana kutokana na wadhamini kutokidhi vigezo. Katika kesi nyingine, mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya, Erasto Phily mshtakiwa huyo amesomewa shtaka moja la ubakaji wa mtoto. Kesi hiyo namba 349 ya mwaka 2022, mwendesha mastaka wa Serikali, Verediana Mlenza na Nitike Immanuel wamesema upelelezi umekamilika. Hata hivyo, mshtakiwa huyo amepata dhamana na kesi hiyo itakuja tena Oktoba 12, 2022 kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali.

Aidha, katika kesi ya tatu, padri huyo ameshtakiwa kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka 12, eneo la kanisa alilokuwa anahudumu. Kesi hiyo ya Jinai namba 44 ya 2022, imetajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Jenipha Edward ambapo padri huyo nadaiwa kutenda kosa hilo Agosti 2022. Waendesha mashtaka wa Serikali, Kambarage Samson na Veridiana Mlenza wameieleza Mahakama hiyo upelelezi umekamilika.

Mshtakiwa ameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili wa kuweka bondi ya Sh2 milioni. Kesi hiyo imehairishwa hadi Oktoba 18, 2022 ambapo kesi itakuja kwaajili ya kusomewa maelezo ya awali
==============================

Vitendo vya udhalilishaji wa kingono kwa watoto vinazidi kuitikisa nchi na sasa padri mmoja wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwabaka na kuwalawiti watoto zaidi ya 10.

Watoto hao ni wanafunzi wa kuanzia darasa la sita hadi kidato cha kwanza waliokuwa wakihudhuria mafundisho ya komunio ya kwanza na kipaimara.

Inadaiwa kila alipomaliza haja zake, padri huyo humpa kila mmoja kati ya Sh3, 000 na Sh5,000.

Wakati Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa, akikataa kuthibitisha au kukanusha kukamatwa kwa padri huyo, Mkuu wa Mkoa huo, Nurdin Babu amethibitisha uwepo wa tukio hilo alilosema “ni baya linalofedhehesha”.

Tukio hilo ambalo ni la kwanza kusikika likifanywa na kiongozi wa dini mkoani Kilimanjaro, huku likihusisha idadi kubwa ya wanafunzi, limeibua taharuki kwa wazazi na walikuwa wamejipanga kuandamana kwenda kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Wananchi hao walikuwa wamepanga kuandamana kwenda kwa Waziri Mkuu aliyekuwa mgeni rasmi katika Siku ya Amani Duniani ambayo kitaifa ilifanyika mjini Moshi, ili kupaza sauti zao kutokana na kigugumizi cha kukamatwa kwa padri huyo.

Baada ya polisi kupata fununu za wazazi kujipanga kuandamana na mabango kwenda kwa Waziri Mkuu, ndipo jioni ya Septemba 20, siku moja kabla ya kiongozi huyo kuwasili mkoani Kilimanjaro, walikwenda kumkamata.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alipotafutwa juzi ofisini kwake kuzungumzia uwepo wa tukio hilo, alikataa kuthibitisha au kukanusha kukamatwa kwa padri huyo zaidi ya kusema wanaendelea kuchunguza tukio hilo.

“Siwezi kusema kama tumemkamata au hatujamkamata, ila suala hili tunaendelea kulichunguza ili kujua ukweli wake, kwa sababu tuhuma hizi zinaelekezwa kwa kiongozi wa dini, hatuwezi kukurupuka kutoa taarifa,” alisema Maigwa.

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali, zinadai kuwa baada ya wazazi, kubaini watoto wao kufanyiwa vitendo hivyo, walitoa taarifa hizo kwenye vyombo husika ikiwemo uongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi na Polisi.

Jina la padri huyo na kituo chake cha kazi tunavihifadhi kwa sasa kwa sababu za kimaadili, hasa kwa kuwa hatujapata upande wake wala vyombo vinavyomshikilia.

Jana, gazeti hili lilimtafuta kwa simu Askofu wa Jimbo Katoliki la Moshi, Ludovick Minde na baada ya kuulizwa taarifa za padri huyo, alisema wapo katika kipindi cha sala, hivyo asingeweza kuzungumza chochote kwa wakati huo (ilikuwa saa 7:12 mchana).

Ilipofika saa 10 jioni Mwananchi, lilimpigia tena simu Askofu Minde ambapo ilikuwa ikiita bila kupokelewa.

Hata hivyo, akizungumza na Mwananchi kuhusu tukio hilo, Mkuu wa mkoa Babu alisema tukio hilo lipo na kwamba ameviagiza vyombo vya usalama kwamba mtu yeyote atakayekamatwa kwa matukio hayo na ushahidi upo, hakuna kurudi nyuma wanapaswa kuchukuliwa hatua kali.

“Katika tabia mbaya zisizo za watu waliostaarabika ni hizo, inaonekana mkoa wetu umezidi kuwa na matukio kama haya. Naviagiza vyombo vya usalama kwamba mtu yeyote atakayekamatwa na ushahidi upo hakuna kurudi nyuma,” alisema RC Babu.

“Kwa sababu haiwezekani kiongozi wa dini kama huyo afanye mambo kama hayo yanayofedhehesha hata waumini wake. Mambo kama haya kwa nchi yetu ni ya kuchafua taswira ya mkoa na nchi na nitaomba mahakama impe adhabu kali,” alisema.

Hali ilivyo kanisani

Mwananchi lilifika katika kanisa analohudumu padri huyo na kukuta ofisi zimefungwa, lakini wahudumu waliokuwepo walidai padri huyo aliongoza ibada Jumapili Septemba 18 na baada ya hapo alienda kwenye mafungo.

“Baada ya misa ya Jumapili aliondoka kwenda mafungo na bado hajarudi, lakini Jumapili ijayo (leo) anaweza kuwepo, kama mnamuhitaji mnaweza kuja kumuona,” alisema mmoja wa wahudumu kanisani hapo ambaye hata hivyo hakutaka kutaja jina lake.

Vilevile, Mwananchi lilizungumza na wananchi wa kada mbalimbali wakiwamo madereva bodaboda wa eneo hilo, ambapo walionyesha kulifahamu suala hilo na kueleza kusikitishwa na kitendo kinachodaiwa kufanywa na kiongozi huyo.

Kauli ya wazazi "Tukio limetuumiza"

Mmoja wa wazazi wa watoto wanaodaiwa kufanyiwa kitendo hicho, alisema kitendo hicho kimemuumiza na kimemfanya apoteze imani kwa kuwa kiongozi wao huyo walimuamini na watoto walimchukulia kama baba yao.

Akisimulia namna alivyofahamu tukio hilo, alidai alipigiwa simu na mtu mmoja akimtaka amchunguze mwanaye kwa kuwa wapo watoto wanaodaiwa kubakwa na padri huyo na mwanaye ni miongoni mwa waliotajwa na wenzake.

“Mwanangu anasoma mafundisho kanisani hapo, nilipopata taarifa hizo, nilimbana akanieleza kuwa amekuwa akiingiliwa na padri huyo tangu Januari mwaka huu,” alisema mzazi huyo ambaye aliomba jina lihifadhiwe.

“Aliniambia wanapokwenda mafundisho, huambiwa waingie ofisini kuungama ambapo huingia mmoja mmoja na ndipo huwafanyia ukatili huo na kuwaambia kuwa wasiwe na shida na wamchukulie kama baba yao,” alieleza mama huyo.

“Taarifa hiyo iliniumiza sana, na ndipo nilipoenda kutoa taarifa kanisani na baadaye polisi, ambapo watoto ikiwemo wa kwangu walipelekwa hospitali ya Mawenzi na kubainika ameingiliwa, jambo ambalo mpaka sasa linaniumiza.”

“Kibaya zaidi baada ya kumbana na kunieleza ukweli, aliniambia baada ya kufanyiwa ukatili huo, hupewa Sh3,000 hadi Sh5,000 ambazo huenda nazo shule na sikuwahi kujua haya, mpaka nilipombana baada ya kuambiwa nimchunguze”.

Mzazi mwingine alisema hawezi kuzungumza kwa undani kuhusiana na tukio hilo kwa kuwa limemuumiza moyoni na limemuathiri mwanaye, kutokana na jamii inayomzunguka kufahamu unyama huo.

“Tukio hili limeniumiza sana, maana mwanangu bado ni mdogo amefanyiwa unyama na ukatili huo na aliyefanya ni kiongozi wa dini tuliyemuamini na hata watoto walipokwenda kanisani hatukupata shaka.”

Baadhi ya wananchi katika eneo hilo, walieleza tukio hilo limeibua taharuki kubwa na kuchafua hali ya hewa, kutokana na kudaiwa kufanywa na kiongozi wa kiroho ambaye wanasema ukimtazama ni mtu mnyenyekevu na asiyedhaniwa kufanya unyama huo.

“Watoto waliofanyiwa ukatili huu wameathirika sana, kwani wapo wanaosoma shule za hapa jirani na wanafahamika na baada ya tukio hili hawawezi kwenda shule kwa sababu ya kunyooshewa vidole na wenzao,” alisema.

Mkazi mwingine wa eneo lilipo kanisa hilo, alisema, “jambo hili limetushtua sana wananchi na baadhi ya wazazi tunaambiwa tayari wamewasitisha watoto wao kwenda mafundisho. Tunaiomba Serikali ilifanyie uchunguzi wa kina suala hilo ili kubaini ukweli wake,” alisema.

Akizungumzia tukio hilo mwenyekiti mmoja wa kitongoji jirani na wananchi hao, alikiri kupata taarifa za watoto hao kufanyiwa ukatili huo na kwamba vyombo vya dola likiamo Jeshi la Polisi vinaendelea kulichunguza, hivyo viachwe vifanye kazi.

“Nikiwa mtaani hapa, nilipata taarifa za watoto 10 kufanyiwa ukatili na kiongozi huyo wa dini, naambiwa wazazi tayari walitoa taarifa kwa uongozi wa kanisa na polisi na tayari vyombo husika vimeanza kulichunguza,” alisema.

Matukio ya udhalilishaji wa kingono kwa watoto yanazidi kushika kasi na uchunguzi unaonyesha ndugu, walimu na viongozi wa dini hushiriki.

MWANANCHI
Serikali ichunguze au iunde tume ya kuchunguza mapadri wote wa Hilo kanisa katoliki nchini

Kuna wengi wanafanyiwa huo uchafu hila hawasemi tu, hata Hawa mashoga wengi asilimia kubwa walianza kuliwa na hao watu, haiwezekani dume zima linaambiwa heti lisioe mke, nyege zake apeleke wapi sasa?

Ndio chanzo Cha kuwa na mashoga wengi nchini na duniani kote, hata humu mitandaoni wengi ambao wanamtetea huyo padri au mapadri, unakuta nao Ni mashoga na walisababishiwa na hao watu,

Mimi mkristo lakini Hawa watu hawafai wachunguzwe haraka wanatuletea mambo machafu aisee, japo sio wote, hila asilimia kubwa Ni waffiraji hao watu
 

Attachments

  • Screenshot_20220929-072853.png
    Screenshot_20220929-072853.png
    140.2 KB · Views: 10
Serikali ichunguze au iunde tume ya kuchunguza mapadri wote wa Hilo kanisa katoliki nchini

Kuna wengi wanafanyiwa huo uchafu hila hawasemi tu, hata Hawa mashoga wengi asilimia kubwa walianza kuliwa na hao watu, haiwezekani dume zima linaambiwa heti lisioe mke, nyege zake apeleke wapi sasa?

Ndio chanzo Cha kuwa na mashoga wengi nchini na duniani kote, hata humu mitandaoni wengi ambao wanamtetea huyo padri au mapadri, unakuta nao Ni mashoga na walisababishiwa na hao watu,

Mimi mkristo lakini Hawa watu hawafai wachunguzwe haraka wanatuletea mambo machafu aisee, japo sio wote, hila asilimia kubwa Ni waffiraji hao watu
Mapadri wasifae kwa sababu ya uovu wa watu wachache?, hakuna masheikh ma ustadh ambao wameoa lakini wanalawiti, hakuna watu wa familia walio oa lakini wanalawiti na wanabaka. Hivi vitu vipo na ni hulka ya mtu binafsi sio taasisi

Wewe una chuki zako binafsi ila makosa kama haya watu wa angle zote wanayafanya.
Ushoga umetokana na utandawazi hao ma padri utakua unawasingizia tu, je nchi za kiarabu au nchi ambazo ukatoliki haupo kwa kiasi kikubwa hakuna mashoga?,

Simtetei padri wala siungi mkono alichokifanya, na naomba achukuliwe adhabu kali kwa alichokifanya
 
Hawa mapadri wanakula na kunywa vizuri wana usafiri bado wanalala pazuri

Hio protini wanayozalisha halafu eti wasioe wala kuonja papuchi


Mnajisumbua bure waruhusuni tu wale hata ma sister
 
Martin Luther was a Padre and Failed to stay alone

Let them Marry.
Upadri ni wito mkuu, bahati mbaya mapadri waovu kama hawa ndio wanaochafua taswira nzima ya nia njema ya wito huu.
Mapadri hawaoi kwa sababu upadri mbali ya kua wito ni sadaka (lengo nzima lipo hivyo achana na hawa wanaoharibu kazi)

Sadaka ya upadri ni ile ya kutokuoa, Rejea mfano wa Mathayo 19:12 Yesu alipoongea kuhusu Matowashi (Japo hapa padri lazima awe mzima upande wa nguvu za kiume kwa sababu lengo kuu la sadaka ni lazima ikuumize, uitoe kwa moyo wote) mfano: sio mtu tu hana uwezo wa kusimamisha alafu anaamua kua padri ili kuficha matatizo yake hapana.

Ukatoliki unaamini kumtumikia Mungu kumegawanyika katika wito wa aina mbili,
1. Wito wa Utawa (Mapadri, Masista n.k)
2. Wito wa Ndoa

Hakuna mtu analazimishwa kua mtawa wala mtu analazimishwa kufuata wito wa ndoa, haya ni maamuzi na uhuru wa mtu mwenyewe kuchagua. Hivyo siamini kama itatokea mapadri wakaruhusiwa kuoa sababu uhuru wa kuchagua upo before mtu haja execute uchaguzi wake

Pia kwa maoni yangu binafsi naona mapadri wakiruhusiwa kuoa sasa kila mtu si atataka kua padri, atakua na familia focus itapungua na kuhamia katika familia yake, pia gharama za kuwalea wao na familia zao zitakua kubwa na ghali zaidi.
 
Hawa mapadri wanakula na kunywa vizuri wana usafiri bado wanalala pazuri

Hio protini wanayozalisha halafu eti wasioe wala kuonja papuchi


Mnajisumbua bure waruhusuni tu wale hata ma sister
Sharti moja muhimu sana katika mchakato wa kuwapata watu wa kusomea/kuandaliwa kuwa mapadre ni kuwa muhusika lazima awe rijali. Ili mtu awe padre mkamilifu, anatakiwa azishinde tamaa hizi (za kingono). Hii itaonyesha kuwa kweli ulidhamiria kumtumikia Mungu. Lakini ukishindwa kushindana na tamaa hizi, basi, huko ulienda kwa bahati mbaya.

Kwa wakatoliki, upadre na ndoa, ni madaraja matakatifu mawili tofauti. Ukibahatika kupata daraja moja kati ya haya mawili, basi daraja lingine huwezi kulipata (they are mutually exclusive). Hata masista na mabruda, nao hawatakiwi kuoa au kuolewa, maana nao pia wamejitoa ili kumtumikia Mungu kikamilifu.

Mtume Paulo ameandika katika waraka wake kwa Wakorinto, kwamba, mtu akishindwa kuishinda tamaa ya mwili (uzinzi), basi na aoe, kuliko kuendelea kuwaka tamaa ya mwili. Lakini, alipendelea zaidi watu wabaki kama alivyokuwa yeye (wasioe), ili wawe na muda mzuri na wa kutosha wa kumtumikia Mungu.

Hapa mtume Paulo anasema kuoa au kutooa si dhambi, lakini ukiamua kumtumikia Mungu (kuwa padre), basi inakupasa uachane na masuala ya ndoa (na uzinzi). Haiyumkini mtume Paulo alisema haya ili kuepusha muingiliano wa masuala ya kibinadamu na yale ya kumtumikia Mungu (mgongano wa kimaslahi). Ukiamua kumtumikia Mungu, basi mtumikie kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu Padre anatakiwa asshughulikiwe kama panya road!
Ni aibu sana sana kwa Kanisa langu katoliki!

Ni aibu kubwa sana kwa Jimbo la Moshi!
Askofu Minde please huyu shetani msimfiche!
Enzi za askofu Amani aliwasafisha wote wenye tabia kama hizo naona wamerudi kwa kasi ya tozo
 
Huu ni upuuzi wa mashetani wa kanisa katoliki. Mbona nyuzi nyingi za huu upuuzi wao, hujaziona hizi; Chato: Katekista wa kanisa Katoliki akamatwa kwa tuhuma za kubaka mtoto wa miaka 8
hili siyo kwa kanisa Katoliki peke yake,hata misikitini ,mashuleni ,na kwenye familia zetu hizi tabia zinakuwa kwa kasi ya ajabu.
ni lazima Kama Watanzania bila kujali dini zetu na tofauti zetu kila mmoja aombe kwa Imani yake na kukemea hili jambo ambalo linakwenda kuliangamiza taifa letu
 
Kwani ni huyo tu? Makasisi na mapadri wa Kanisa katoliki wanayafanya hayo dunia nzima, tena hawakuanza leo wala jana, ni uozo wa miaka na miaka, Mpaka Umoja wa Mataifa umepiga kelele.
Kama walivyo walimu wa madrasa..wote wale wale
 
UPDATES:

Sostenes Bahati Soka, Padri wa Kanisa Katoliki, Parokia Teule ya Mtakatifu Deonis Aropagita, Jimbo la Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro amesomewa mashtaka matatu katika Mahakama mbili tofauti. Padri huyo mwenye miaka 41, amesomeshwa mashataka hayo leo Jumatatu, Septemba 26, 2022 kwa nyakati tofauti akianza na Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi kisha Mahakama ya Wilaya ya Moshi.

Kesi ya kwanza ilisomwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Salome Mshasha ambapo Padri huyo anakabiliwa na shtaka moja la kumbaka mtoto wa miaka 12. Wakili wa Serikali, Kasimu Nasiri amesema upelelezi wa kesi hiyo umekamilika

Mshtakiwa huyo amekana shtaka hilo huku Wakili wa Serikali, Kasimu Nasiri akisema upelelezi umekamilika na Hakimu Salome ameiahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 10, 2022 ambapo atafikishwa kusomewa maelezo ya awali. Mshtakiwa huyo alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wakazi wa Kilimanjaro ambao wawe na uwezo wakuweka bondi ya Sh10 milioni, kika mmoja.

Padri Soka amekosa dhamana kutokana na wadhamini kutokidhi vigezo. Katika kesi nyingine, mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya, Erasto Phily mshtakiwa huyo amesomewa shtaka moja la ubakaji wa mtoto. Kesi hiyo namba 349 ya mwaka 2022, mwendesha mastaka wa Serikali, Verediana Mlenza na Nitike Immanuel wamesema upelelezi umekamilika. Hata hivyo, mshtakiwa huyo amepata dhamana na kesi hiyo itakuja tena Oktoba 12, 2022 kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali.

Aidha, katika kesi ya tatu, padri huyo ameshtakiwa kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka 12, eneo la kanisa alilokuwa anahudumu. Kesi hiyo ya Jinai namba 44 ya 2022, imetajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Jenipha Edward ambapo padri huyo nadaiwa kutenda kosa hilo Agosti 2022. Waendesha mashtaka wa Serikali, Kambarage Samson na Veridiana Mlenza wameieleza Mahakama hiyo upelelezi umekamilika.

Mshtakiwa ameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili wa kuweka bondi ya Sh2 milioni. Kesi hiyo imehairishwa hadi Oktoba 18, 2022 ambapo kesi itakuja kwaajili ya kusomewa maelezo ya awali

===================

Vitendo vya udhalilishaji wa kingono kwa watoto vinazidi kuitikisa nchi na sasa padri mmoja wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwabaka na kuwalawiti watoto zaidi ya 10.

Watoto hao ni wanafunzi wa kuanzia darasa la sita hadi kidato cha kwanza waliokuwa wakihudhuria mafundisho ya komunio ya kwanza na kipaimara.

Inadaiwa kila alipomaliza haja zake, padri huyo humpa kila mmoja kati ya Sh3, 000 na Sh5,000.

Wakati Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa, akikataa kuthibitisha au kukanusha kukamatwa kwa padri huyo, Mkuu wa Mkoa huo, Nurdin Babu amethibitisha uwepo wa tukio hilo alilosema “ni baya linalofedhehesha”.

Tukio hilo ambalo ni la kwanza kusikika likifanywa na kiongozi wa dini mkoani Kilimanjaro, huku likihusisha idadi kubwa ya wanafunzi, limeibua taharuki kwa wazazi na walikuwa wamejipanga kuandamana kwenda kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Wananchi hao walikuwa wamepanga kuandamana kwenda kwa Waziri Mkuu aliyekuwa mgeni rasmi katika Siku ya Amani Duniani ambayo kitaifa ilifanyika mjini Moshi, ili kupaza sauti zao kutokana na kigugumizi cha kukamatwa kwa padri huyo.

Baada ya polisi kupata fununu za wazazi kujipanga kuandamana na mabango kwenda kwa Waziri Mkuu, ndipo jioni ya Septemba 20, siku moja kabla ya kiongozi huyo kuwasili mkoani Kilimanjaro, walikwenda kumkamata.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alipotafutwa juzi ofisini kwake kuzungumzia uwepo wa tukio hilo, alikataa kuthibitisha au kukanusha kukamatwa kwa padri huyo zaidi ya kusema wanaendelea kuchunguza tukio hilo.

“Siwezi kusema kama tumemkamata au hatujamkamata, ila suala hili tunaendelea kulichunguza ili kujua ukweli wake, kwa sababu tuhuma hizi zinaelekezwa kwa kiongozi wa dini, hatuwezi kukurupuka kutoa taarifa,” alisema Maigwa.

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali, zinadai kuwa baada ya wazazi, kubaini watoto wao kufanyiwa vitendo hivyo, walitoa taarifa hizo kwenye vyombo husika ikiwemo uongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi na Polisi.

Jina la padri huyo na kituo chake cha kazi tunavihifadhi kwa sasa kwa sababu za kimaadili, hasa kwa kuwa hatujapata upande wake wala vyombo vinavyomshikilia.

Jana, gazeti hili lilimtafuta kwa simu Askofu wa Jimbo Katoliki la Moshi, Ludovick Minde na baada ya kuulizwa taarifa za padri huyo, alisema wapo katika kipindi cha sala, hivyo asingeweza kuzungumza chochote kwa wakati huo (ilikuwa saa 7:12 mchana).

Ilipofika saa 10 jioni Mwananchi, lilimpigia tena simu Askofu Minde ambapo ilikuwa ikiita bila kupokelewa.

Hata hivyo, akizungumza na Mwananchi kuhusu tukio hilo, Mkuu wa mkoa Babu alisema tukio hilo lipo na kwamba ameviagiza vyombo vya usalama kwamba mtu yeyote atakayekamatwa kwa matukio hayo na ushahidi upo, hakuna kurudi nyuma wanapaswa kuchukuliwa hatua kali.

“Katika tabia mbaya zisizo za watu waliostaarabika ni hizo, inaonekana mkoa wetu umezidi kuwa na matukio kama haya. Naviagiza vyombo vya usalama kwamba mtu yeyote atakayekamatwa na ushahidi upo hakuna kurudi nyuma,” alisema RC Babu.

“Kwa sababu haiwezekani kiongozi wa dini kama huyo afanye mambo kama hayo yanayofedhehesha hata waumini wake. Mambo kama haya kwa nchi yetu ni ya kuchafua taswira ya mkoa na nchi na nitaomba mahakama impe adhabu kali,” alisema.

Hali ilivyo kanisani

Mwananchi lilifika katika kanisa analohudumu padri huyo na kukuta ofisi zimefungwa, lakini wahudumu waliokuwepo walidai padri huyo aliongoza ibada Jumapili Septemba 18 na baada ya hapo alienda kwenye mafungo.

“Baada ya misa ya Jumapili aliondoka kwenda mafungo na bado hajarudi, lakini Jumapili ijayo (leo) anaweza kuwepo, kama mnamuhitaji mnaweza kuja kumuona,” alisema mmoja wa wahudumu kanisani hapo ambaye hata hivyo hakutaka kutaja jina lake.

Vilevile, Mwananchi lilizungumza na wananchi wa kada mbalimbali wakiwamo madereva bodaboda wa eneo hilo, ambapo walionyesha kulifahamu suala hilo na kueleza kusikitishwa na kitendo kinachodaiwa kufanywa na kiongozi huyo.

Kauli ya wazazi "Tukio limetuumiza"

Mmoja wa wazazi wa watoto wanaodaiwa kufanyiwa kitendo hicho, alisema kitendo hicho kimemuumiza na kimemfanya apoteze imani kwa kuwa kiongozi wao huyo walimuamini na watoto walimchukulia kama baba yao.

Akisimulia namna alivyofahamu tukio hilo, alidai alipigiwa simu na mtu mmoja akimtaka amchunguze mwanaye kwa kuwa wapo watoto wanaodaiwa kubakwa na padri huyo na mwanaye ni miongoni mwa waliotajwa na wenzake.

“Mwanangu anasoma mafundisho kanisani hapo, nilipopata taarifa hizo, nilimbana akanieleza kuwa amekuwa akiingiliwa na padri huyo tangu Januari mwaka huu,” alisema mzazi huyo ambaye aliomba jina lihifadhiwe.

“Aliniambia wanapokwenda mafundisho, huambiwa waingie ofisini kuungama ambapo huingia mmoja mmoja na ndipo huwafanyia ukatili huo na kuwaambia kuwa wasiwe na shida na wamchukulie kama baba yao,” alieleza mama huyo.

“Taarifa hiyo iliniumiza sana, na ndipo nilipoenda kutoa taarifa kanisani na baadaye polisi, ambapo watoto ikiwemo wa kwangu walipelekwa hospitali ya Mawenzi na kubainika ameingiliwa, jambo ambalo mpaka sasa linaniumiza.”

“Kibaya zaidi baada ya kumbana na kunieleza ukweli, aliniambia baada ya kufanyiwa ukatili huo, hupewa Sh3,000 hadi Sh5,000 ambazo huenda nazo shule na sikuwahi kujua haya, mpaka nilipombana baada ya kuambiwa nimchunguze”.

Mzazi mwingine alisema hawezi kuzungumza kwa undani kuhusiana na tukio hilo kwa kuwa limemuumiza moyoni na limemuathiri mwanaye, kutokana na jamii inayomzunguka kufahamu unyama huo.

“Tukio hili limeniumiza sana, maana mwanangu bado ni mdogo amefanyiwa unyama na ukatili huo na aliyefanya ni kiongozi wa dini tuliyemuamini na hata watoto walipokwenda kanisani hatukupata shaka.”

Baadhi ya wananchi katika eneo hilo, walieleza tukio hilo limeibua taharuki kubwa na kuchafua hali ya hewa, kutokana na kudaiwa kufanywa na kiongozi wa kiroho ambaye wanasema ukimtazama ni mtu mnyenyekevu na asiyedhaniwa kufanya unyama huo.

“Watoto waliofanyiwa ukatili huu wameathirika sana, kwani wapo wanaosoma shule za hapa jirani na wanafahamika na baada ya tukio hili hawawezi kwenda shule kwa sababu ya kunyooshewa vidole na wenzao,” alisema.

Mkazi mwingine wa eneo lilipo kanisa hilo, alisema, “jambo hili limetushtua sana wananchi na baadhi ya wazazi tunaambiwa tayari wamewasitisha watoto wao kwenda mafundisho. Tunaiomba Serikali ilifanyie uchunguzi wa kina suala hilo ili kubaini ukweli wake,” alisema.

Akizungumzia tukio hilo mwenyekiti mmoja wa kitongoji jirani na wananchi hao, alikiri kupata taarifa za watoto hao kufanyiwa ukatili huo na kwamba vyombo vya dola likiamo Jeshi la Polisi vinaendelea kulichunguza, hivyo viachwe vifanye kazi.

“Nikiwa mtaani hapa, nilipata taarifa za watoto 10 kufanyiwa ukatili na kiongozi huyo wa dini, naambiwa wazazi tayari walitoa taarifa kwa uongozi wa kanisa na polisi na tayari vyombo husika vimeanza kulichunguza,” alisema.

Matukio ya udhalilishaji wa kingono kwa watoto yanazidi kushika kasi na uchunguzi unaonyesha ndugu, walimu na viongozi wa dini hushiriki.

MWANANCHI
Inasikitisha kwakweli, mbona Hawa viongozi wa dini ya kikristo hizi tuhuma zinawaandama Sana, nashauri wafanyiwe uchunguzi na wengineo, huenda haya yanafanyika Sana ila Kuna wahanga Wengine wanashindwa malalamiko yao wapeleke wapi
 
hili siyo kwa kanisa Katoliki peke yake,hata misikitini ,mashuleni ,na kwenye familia zetu hizi tabia zinakuwa kwa kasi ya ajabu.
ni lazima Kama Watanzania bila kujali dini zetu na tofauti zetu kila mmoja aombe kwa Imani yake na kukemea hili jambo ambalo linakwenda kuliangamiza taifa letu
Kanisa limezidi huo uchafu
 
Back
Top Bottom