Ushahidi wa Nyaraka na vielelezo kuhusu UZanzibar wa Rais Samia huu hapa

Ushahidi wa Nyaraka na vielelezo kuhusu UZanzibar wa Rais Samia huu hapa

Halafu mbona mnangaika na huyo bibi kizee aliepata uraisi Kwa mgongo wa magufuli
 
CHADEMA tafuteni hoja zenye mashiko, huu usanii wa TUNDU LISSU hauwezi kuwaongezea chochote kwenye kukubalika na wananchi. Kwani kuna tatizo gani kwa Samia kuwa na kitambulisho cha Mzanzibar mkazi?

Samia hakutengeneza Muungano bali ni waasisi wa Taifa letu wakiongozwa na JK Nyerere na Abeid Aman Karume.

Wakati wa muungano Tundu Lissu alikuwa hajazaliwa. Leo anapata wapi uwezo wa kukosoa makubaliano ya waasisi wa Taifa hili.

Tundu Lissu anamkejeli Rais Samia ambaye ndiye kiongozi wa juu aliyemtembelea hospitali Nairobi kumjulia hali wakati akiwa amelazwa baada ya WATU WASIOJULIKANA kumshambulia akiwa Bungeni Dodoma.

Samia alimtembelea pia Brussels alikokuwa anaishi maisha ya ombaomba kama mkimbizi baada ya kumkimbia Magufuli immwdiately baada ya uchaguzi wa mwaka 2020.

Huyu Samia ndiye aliyemfutia kesi za kubambikiza nankumlipa stahiki alizodhulumiwa kama mbunge wakati wa Magufuli.

Mtu hana shukrani kwa huyu Rais aliyemjali kama mdogo wake.

Nawahakikishia mashabiki wa Tundu Lissu kuwa cheo cha mwisho cha juu cha Tundu Lissu kupata maishani itabaki ni Makamu Mwenyekiti tu wa CHADEMA.
Wewe sio Mungu
 
Na hapo Ndo kuna Hoja ya walio wengi..
Kwamba Kwanini Tanganyika inakuwa Ngumu Midomoni mwa watu ila wazanzibar wako Proud na Nchi yao??

Na kwanini Tanzania Iwe Ni Muungano ila Ukichunguza kwa Makini ni Tanganyika Inayobeba Zanzibar??

Sijui umenielewa Maneno ya mwalimu Nyerere Bado mpaka Leo Yana Mashaka sana..

Hii Ni Page ya Kitabu chake kilichochapwa mwaka 1993 Kuhusu kwanini hakuna Serkali moja na kwanini hakuna Serkali Tatu..

Ukisoma Hoja zake Ni dhahiri kwamba Zina Gape kubwa sana..
View attachment 2977652
Ni kweli Tanganyika imejificha pale TAMISEMI. Maana ukiangalia kwa makini TAMISEMI ndio Tanganyika yenyewe.

Bado tumebaki kwenye muundo uliochukuliwa sababu ya aina ya itikadi za ulimwengu wa wakati ule. Kwa sasa ni wazi haziwezi kukidhi mahitaji.

Mjadala ni mrefu sana.
 
Ni kweli Tanganyika imejificha pale TAMISEMI. Maana ukiangalia kwa makini TAMISEMI ndio Tanganyika yenyewe.

Bado tumebaki kwenye muundo uliochukuliwa sababu ya aina ya itikadi za ulimwengu wa wakati ule. Kwa sasa ni wazi haziwezi kukidhi mahitaji.

Mjadala ni mrefu sana.
Lakini Tukijitoka kwenye TAMISEM..
Twende kwenye Serikali ya Muungano..

Kwanini Waziri Mkuu Wa JMT hana Usemi Zanzibar ???
 
Gud mbona nape anasema Samia ni mngoni
Kama kweli Nape amesema kuwa Samia ni mngoni, walio karibu naye wamwahishe haraka Milembe hospital.

"Sisi kule Zanzibar hatuna makabila. Mtu akiniuliza wewe ni kabila gani, namwambia mimi ni Mzanzibari" - Rais Samia.
 
Mimi nadhani ni heshima kubwa na Uzalendo kwa mtu kuitwa kwa Utaifa wake, Sioni haja ya kuficha Utaifa wa mtu kwa sababu zozote zile.

Kwa nia njema kabisa naweka nyaraka za wazi za Uzanzibar wa Rais wetu Samia Suluhu Hassan

View attachment 2977513View attachment 2977516

Hata kwa Sheria za Tanzania, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano anapotokea Tanganyika(Tanzania Bara), Mgombea Mwenza (Makamu wa Rais) ni lazima awe Raia wa Zanzibar, Kwahiyo kumbe Wazanzibar wapo na ni lazima wawe Wazanzibar ili kugombea Uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO

Pia soma
Akamatwe kuishi Bara bila kibali
 
CHADEMA mnafeli sana, daima mnatafuta kura kwa migawanyo, mara mkae kidini, mara kikanda mara kama hivi kizanzibar na Bara, yan mnatapa tapa kwa kila mbinu kuhakikisha mnafika ikulu, ila kibaya mnajiharibia, kwa style hii ya ubaguzi watu wa mipakani wanawaogopa tayari, zenji hawatakaa wawakubali,
Jibu hoja za Lisu acha kulialia.Huu Muungano unatakiwa upitiwe upya na upigiwe kura ya maoni kuuhalalisha.
Una mambo mengi ya hovyo
 
Kwa wananchi wa kawaida (wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara), tutumie muungano kama fursa badala changamoto. Fikra zielekezwe kwenye kupanuka kwa masoko, ushirika wa kibiashara na ubunifu, urafiki na hata mahusiano ya kijamii.
Migogoro na kero za kisiasa zitaondoka pole pole baada ya wananchi kuwa wamoja.
Pande zote ziangalie maboresho ya muungano kwa uelekeo chanya zaidi.
Hata hivyo, changamoto za wanasiasa ni kawaida na muhimu katika kuweka mambo sawa kwenye jamii au taifa lolote (hoja zijibiwe kwa hoja).
 
Unajua maana Ya Sovereign state..
Zanzibar ina mamlaka yote ina Raia , Inaserekali ina Ardhi na ina power..

Wana Jeshi la Ulinzi pia Na Jeshi La mambo ya. Ndani pia Japo yanafanya kazi ndani ya Zanzibar..

For Your Info Zanzibar Ni Nchi ambayo Ina umri Mkubwa kuliko Hata Tanganyika..
Zanzibar Inakwenda Far Beyond Mwaka 1570s Na Tanganyika Ilianzishwa Mwak 1920s na waJeruman
Hizi ni pumba, peleka wakale nguruwe. Jeshi la ulinzi liko wapi na Mkuu wa Majeshi ni nani?

Mwaka 1920 Wajerumani walikuwa hawatawali Tanganyika kwa kuwa walishindwa vita vya kwanza mwaka 1919 na Tanzania ikawa colony la League of Nations. Muingereza akawa anastasia kama trustee.

Acha kuandika pumba, kajipange upya
 
CHADEMA mnafeli sana, daima mnatafuta kura kwa migawanyo, mara mkae kidini, mara kikanda mara kama hivi kizanzibar na Bara, yan mnatapa tapa kwa kila mbinu kuhakikisha mnafika ikulu, ila kibaya mnajiharibia, kwa style hii ya ubaguzi watu wa mipakani wanawaogopa tayari, zenji hawatakaa wawakubali,
mimi naona hoja za Lissu ziko sawa na za Jussa mbona jussa anaeleweka huko zanzibar watanganyika sisi ndiyo tatizo kwenye muungano kwa ukinyonga wetu kuhusu nafasi ya Tanganyika kwenye muungano hata km ilikufa,Kuna watu wananifaika na koti hili
 
Hizi ni pumba, peleka wakale nguruwe. Jeshi la ulinzi liko wapi na Mkuu wa Majeshi ni nani?

Mwaka 1920 Wajerumani walikuwa hawatawali Tanganyika kwa kuwa walishindwa vita vya kwanza mwaka 1919 na Tanzania ikawa colony la League of Nations. Muingereza akawa anastasia kama trustee.

Acha kuandika pumba, kajipange upya
BAada ha Vita vya Kwanza vya Dunia 1918 Ujerumani aliachia Baadhi ya Makoloni na hapo ndiyo Muingereza alipoanza kutawala..

Muingereza ilibidi kubadilisha Jina kutoka Ujerumani ya Africa Mashariki (East African German) na kuwa Tanganyika na hiyo ilifanykka Kutoka mwaka 1918 mpaka 1920..

Kuhusu Majeshi..
Jeshi la Wananchi Lilianzishwa mwaka 1964 baada ya Tishio la Mapinduzi lilifanyka mwaka huo na Rais kuvunja Jeshi la Tanganyika Riffles ambao ndo walikuwa wanajeshi wa Nchi..

Japo.Zanzibar walikuwa nao wana majeshi yao na kumbuka kabla ya Kuungana na Tanganyika walikuwa na Kiti Umoja wa Mataifa (Usisahau Hilo)..

Hata Hivyo zanzibar Pia wana Majeshi yao ambayo sio mali ya Muungano kama KMKM, JKU, Etc..

Nafikiri Kama Una hoja Weka mezani tujadili..
Kejeli, matusi wala hasira hazitakusaidia kitu..

Mimi naongea Facts na Uhalisia uliopo
 
Kitambulisho cha Mkazi wa Zanzibar siyo sawa na Hati ya Uraia aka Passport. Wazanzibari hawana Passport yao wenyewe wanatumia passport ya JMT. Labda tuangalie nini lengo la Wazanzibari kuwa na Kitambulisho cha Mkazi wa Zanzibar. Jee, Mtanzania Bara anaruhusiwa kupewa Kitambulisho cha Mkazi wa Zanzibar, na kama ni ndiyo, ni kwa vigezo gani?
Zamani Walikuwa Na passport yao ila Sijui ilifikia wapi waliamua Kuifuta..
Mtanzania Bara ni nani?
Kwanini mnaweza kutamka Mzanzibari lakini manashindwa kutamka Mtanganyika..?

Vipi mtu anayeishi Ukerewe Yeye haishi Visiwani??
Vipi anayeishi Mafia sio Mtanzania Bara??

Ok hiyo Sio Mada yangu ila Kikubwa zamani alikuwa nayo passport ila baadaye ikapurushwa..
Na kuhusu Kupewa Kitambulisho cha Mkazi ni Mara nyingi lazma uwe mzawa wa Zanzibar kwa mujibu wa katiba ya zanzibar...

download (9).jpeg
 
Kwa wananchi wa kawaida (wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara), tutumie muungano kama fursa badala changamoto. Fikra zielekezwe kwenye kupanuka kwa masoko, ushirika wa kibiashara na ubunifu, urafiki na hata mahusiano ya kijamii.
Migogoro na kero za kisiasa zitaondoka pole pole baada ya wananchi kuwa wamoja.
Pande zote ziangalie maboresho ya muungano kwa uelekeo chanya zaidi.
Hata hivyo, changamoto za wanasiasa ni kawaida na muhimu katika kuweka mambo sawa kwenye jamii au taifa lolote (hoja zijibiwe kwa hoja).
Miaka 60 hamkufanya kitu ndio iwe wiki moja ?
 
Mimi nadhani ni heshima kubwa na Uzalendo kwa mtu kuitwa kwa Utaifa wake, Sioni haja ya kuficha Utaifa wa mtu kwa sababu zozote zile.

Kwa nia njema kabisa naweka nyaraka za wazi za Uzanzibar wa Rais wetu Samia Suluhu Hassan

View attachment 2977513View attachment 2977516

Hata kwa Sheria za Tanzania, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano anapotokea Tanganyika(Tanzania Bara), Mgombea Mwenza (Makamu wa Rais) ni lazima awe Raia wa Zanzibar, Kwahiyo kumbe Wazanzibar wapo na ni lazima wawe Wazanzibar ili kugombea Uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO

Pia soma
Dah, mbona hili linafahamika muda mrefu; kwamba Tanzania tuna waTanzania raia wa Zanzibar, ambao uraia wao huo ni muhimu zaidi ya uTanzania wao?
U-Tanzania kwao, ni nafasi tu ya kujinufaisha wao wenyewe na waZanzibar wenzao.
Kwa hiyo hili lisitushangaze sana, labda kwa vile tui watu ni 'slow learners', sasa ndiyo Tundu Lissu kawastua akili zao na kuanza kulitambua hili.
Watu wana bendera yao, katiba yao, serikali yao, na wanajitambulisha wao ni waZanzibari; bado mtu utakuwaje na mashaka nao kuhusu uraia wao?

Wanaweka mbele uZanzibar wao, lakini inapokuja wakati wa maslahi yao kulindwa, hapo hawasiti hata mara moja kujitambulisha kama waTanzania.
 
Back
Top Bottom