dronedrake
JF-Expert Member
- Dec 25, 2013
- 23,901
- 58,103
safi sana mpaka useme
KATAA NDOA
NDOA NI UJAMBAZI
KATAA NDOA
NDOA NI UJAMBAZI
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Weee! Huyo na mke. Yaani nipangiwe masharti Kwa mke wangu ninapo muhitaji.Haiko sawa angeenda polisi kufungua RB kuwa mke katelekeza watoto huwezi mtoa Padri Altereni au kumkamata muumini akisali kanisani bila ruksa ya uongozi wa kanisa
Huwezi kamata mtu kanisani bila kuwa na RB na kuwa na uongozi wa serikali ya mtaa au Kijiji ukiwa umeongozana na polisi Huwezi kamata mtu kienyeji hivyo mkamataji hakuzingatia Sheria ya ukamataji mhalifu
Kuna makosa makubwa kafanya polisi waweza muweka ndani aende na wadhamini kabisa
Taratibu za kisheria za kumkamata mtuhumiwa mke hakuzingatia .Waliomfungulia RB polisi wako sahihi
Mchungaji ana akili kuzidi wewe. Ukitaka kumsaidia mkeo, jiunge ila uwe mjaja maana mbinguni tunaenda kwa kuamini Mungu na siyo vinginevyo then tafuta ufahamu zaidi ili mkeo akuone unajua ili umuomdoe huo mtego wa ubaya
Imani ziko tofauti mfano Kwa katoliki Ibada Huwa haizidi hata dakika 45 maximum saa moja mengine ibada masaa mawili ,mengine mfano kanisa la sabato siku nzima Huwa kanisani sababu huamini hiyo siku ni ya Mungu hivyo siku nzima lazima watumie kanisani kumaliza ibada mapema au la hutegemea Imani na Imani wengine hubaki kanisani siku nzima wengine Huwahi mapema ibada iishe haraka wakakumbatiane na wake au waume zao nadhani kuwahi au kuchelewa kumaliza ibada sio kigezo sana Cha kusema kanisa Fulani ni genuine or not Kwa muda wanatumia kwenye ibada ni hoja dhaifu sana hii umetoaKwenye ulokole Kuna makanisa genuine kabisa ambayo hayana vitu vya kijinga jinga na ratiba zinaisha mapema,watu wanapata muda wa kuhudumia familia zao ukiona kanisa Lina Imani mara chumvi,mafuta,udongo,na mavitu hayaeleweki jua hao ni wahuni kama wahuni wengine
Kanisa genuine ni lazima lijali Hali za washirika wake,maandiko yanasema yule asiyejali wa nyumbani kwake ni mbaya kuliko asiyeamini`kama mchungaji Hana matumizi mazuri ya muda ni tatizo,Kwa kuwa kwenye ibada Kuna watoto na mchana watakuwa wale chakula Cha kawaida,huwezi kuwashindisha watu Kutwa nzima na njaa Kwa kigezo Cha ibada,mtu mwingine ana hiyo jumapili peke yake Kwa ajili ya mapumziko,kuona familia na watoto,kufua kufanya usafi n.kImani ziko tofauti mfano Kwa katoliki Ibada Huwa haizidi hata dakika 45 maximum saa moja mengine ibada masaa mawili ,mengine mfano kanisa la sabato siku nzima Huwa kanisani sababu huamini hiyo siku ni ya Mungu hivyo siku nzima lazima watumie kanisani kumaliza ibada mapema au la hutegemea Imani na Imani wengine hubaki kanisani siku nzima wengine Huwahi mapema ibada iishe haraka wakakumbatiane na wake au waume zao nadhani kuwahi au kuchelewa kumaliza ibada sio kigezo sana Cha kusema kanisa Fulani ni genuine or not Kwa muda wanatumia kwenye ibada ni hoja dhaifu sana hii umetoa
🙆🙆🙆🙆 Yaani hayo yanafanyikia nchi gani huko uliko mkuu?Wasaalam?
Ipo hivi juzi asubuhi Jumapili niliingia nyumbani nilikuwa SA kwa mambo ya kikazi, kufika nyumbani nilimkuta binti yangu wa kwanza pamoja na dada wa kazi kumuuliza mama yako yuko wapi? Akasema ameenda kanisani, nikamuuliza mbona hajaenda na watoto(watoto ni mapacha wana miezi 4) wakashindwa kunipa jibu nikapiga kimya nikaenda kupumzika kutokana na uchovu.
Imefika saa 7 mchana nikashtushwa na kelele za watoto walikuwa wanalia mno nahisi walikuwa wanataka kunyonya kuangalia makopo ya maziwa yameisha nikatoa pesa wakaenda kununua lakini nilipiga marufuku matumizi ya maziwa ya kopo.
Nimebuy time mpaka saa 10 jioni kimya mtu hajarudi nikipiga simu inaita tu haipokelewi, nikashikwa na gadhabu sana nikachukua watoto nikawatupia kwenye gari safari mpaka kanisani kwa wife.
Nimefika kanisani nimemkuta wife yupo madhabauni anaombea watu nikachukua watoto nikawaweka pale pale madhabauni nikamwambia awanyonyeshe watoto wana njaa, akagoma akasema nimemfanyia vitendo vya aibu!!
Ghafla mchungaji mkuu akaja akauliza kuna nini? Mimi nikamwambia mchungaji hayakuhusu nataka watoto wanyonye niondoke nao nyie endeleeni na ibada zenu,mchungaji akadakia akasema ibada ya leo inahitaji utulivu ndio maana tulitangaza watoto wote wabaki majumbani.
Nikamvuta kinguvu wife nikaondoka nae nikamwambia Leo ndio mwanzo na mwisho kusali katika makanisa ya kiroho kama hauwezi kusali roman Catholic pumzika nyumbani tu.
Nimepigiwa simu sasa hivi natakiwa kituo cha polisi kwa kosa la kufanya fujo kanisani na kufanya shambulio la kimwili dhidi ya wife, niende au nisiende? Kwa sababu kesho asubuhi inabidi niende Bujumbura kikazi.
Asante
MREJESHO.
Nimeripoti police nimewekwa selo kwa dakika 30 mama mkwe amekuja ameniwekea dhamana nimetoka.
Cha ajabu muda huu nimerudi nyumbani nimemkuta dada wa kazi tu.. kuuliza naambiwa ameenda kanisani yeye na watoto wote .
Kusikia kwa kenge mpaka damu zimtoke ngoja niende kwanza Bujumbura.
Asante
Mstari wa 3 unasadifu jina lako.Nenda tuu..
Ila nimependa msimamo wako..
Pia inabidi mambo mengine utumie busara sana..
Mimi ningechoma kanisa kabisa wanangu hawawezi kushinda njaa kwa sababu wapumbavu wachache.Haiko sawa angeenda polisi kufungua RB kuwa mke katelekeza watoto huwezi mtoa Padri Altereni au kumkamata muumini akisali kanisani bila ruksa ya uongozi wa kanisa
Huwezi kamata mtu kanisani bila kuwa na RB na kuwa na uongozi wa serikali ya mtaa au Kijiji ukiwa umeongozana na polisi Huwezi kamata mtu kienyeji hivyo mkamataji hakuzingatia Sheria ya ukamataji mhalifu
Kuna makosa makubwa kafanya polisi waweza muweka ndani aende na wadhamini kabisa
Taratibu za kisheria za kumkamata mtuhumiwa mke hakuzingatia .Waliomfungulia RB polisi wako sahihi
Kitendo cha wewe kupewa RB ya kuitwa Polisi kwa kufanya shambulio la kimwili kwa wife wako kina maanisha kua Wife wako pia ameridhia wewe kuitwa Polisi/Kushtakiwa,
Hii inanipa tafsiri kua,mkeo anawasikiliza/anawaheshimu zaidi hao watu wa huko Kanisani kuliko wewe coz kabla ya Kanisa kufikia maamuzi ya kukushtaki ni lazima walishauriana na mkeo,
Anza kudeal na mkeo kwanza na solution ni kukazia hapo hapo kua asiende tena huko kwenye hilo Kanisa.
Naunga mikono hoja.Mkuu sio poa uliwatupiaje watoto kwenye gari hawakuumia?
Akikubali hio kesi iendelee,Huna mke hapo. Na hakikisha unapima DNA may be mchungaji kakusaidia kujaza idadi duniani
Duuu! Inasikitisha Sana.Mfanyakazi mwenzangu naishi nae kwenye nyumba ya shirika, mkewe amevuka mipaka hadi ya kupeleka kodi ya meza kanisani.
Huyu mwanamke kwao ni waislamu typically, ila kaanza kwenda kwa wahubiri na kaiva hasa na sanaa zao.
Jamaa yangu anasali RC. Kila siku mwanamke anakuja na wito kuwa anaitwa na Mchungaji kuwa ameona kuna watu wanachezea ndoa yao (wanarogwa). Yaani mwamba anapigwa hela hadi basi.
Mwanzoni nilijaribu kumpa ushauri, na kila nilichomwambia alikipeleka kwa mkewe. Nikaamua kukausha na sasa kila akitaka ushauri namkwepa.
Mbaya zaidi watoto wakiumwa ni mwendo wa kuwapaka na kuwaogesha maji yenye mafuta ya kanisani, hospital ni mpaka mtoto afikie hatua mbaya.
Kuna wakati jamaa alifiwa na mama yake na tulienda Moshi kwa ajili ya mazishi. Ilikaribia 40 ya kumaliza msiba, jamaa hakuwa vizuri mfukoni na aliona auze asset yake moja kwa 3,000,000/= ili akamalize msiba.
Akamshirikisha mwanamke na mwanamke akaenda kumshirikisha Mchungaji. Na baadaye majibu ya mwanamke yalikuwa kwamba wagawane 50% ya mauzo na mwanaume akatumie ile ya kwake kwenda kumalizia msiba ila ya mwanamke itabidi akatoe fungu la kumi kanisani. Imepita miezi minne sasa hawajaenda kumalizia msiba wa Mama wa mwanaume.
Kuna siku nilishangaa zaidi mwanamke alipomletea bahasha yenye fomu inayohitaji kujazwa taarifa za kazi ya mwanaume, ikiwamo mshahara. Nilimwambia mwamba huo ni mtego, ila baada ya siku mbili akaniambia kabanwa sana na mkewe na ikabidi ajaze ile fomu na kuirudisha kanisani.
USHAURI:
Wanaume tuwe makini sana na haya makanisa ya kiroho, mengi yamejaa wasanii.
Wanachofanya ni kuangalia weakness ya mwanamke ili waweze kucheza na akili yake na hatimaye kukuteka mwanaume na uchumi wa familia nzima.