Usifanye hii Kazi, Hata Kama Maisha yakiwa magumu sana

Umekuja na mashaka liko wapi suluhisho lake .Unataka wafanye kazi gani .Mimi nasema fanya kazi yoyote ilokuwa halali upate rizki yako ili maisha yaendelee plus uwe na malengo nafanya kazi hii lengo langu ni hili tatizo la vijana wetu hawana vision.
Siyo kila kazi ni ya kufanya ndugu, zingine unaziacha.
Kweli ni kazi halali ila anza kuokota makopo uone kitakachokutokea
 
mjomba wako ameokota makopo na amejenga nyumba mbili ambazo profession boxing haikumpa
 
Kudanga sio kazi, zingine zote ni kazi halali. Mtu anayedanga ni mchuuzi wa uchi, anajiuza na ni malaya.

Kuwa bodaboda ni kazi, japo kweli hakuna anayependa mtoto wake aendeshe bodaboda ila hata simba hula nyasi mambo yakiwa magumu, ni heri akaendeshe hiyo boda kuliko kuwa mwizi.

Udalali ni kazi, ukiwa na mtaji udalali unalipa, kuna real estate agents, automobile agents n.k. Tatizo ni kuwa hata serikali haioni kuwa ni kazi halali, hawaihalalishi.

Kuokota machupa ni kazi, japo ni ya kuushusha sana utu lakini simba akikosa nyama anakula nyasi.

Hakuna mzazi anayependa mtoto wake afanye kazi za viwango duni ila maisha yakikuchapa huna budi.
 
Kwaiyo tufanye kazi gani maisha yakiwa magumu?
 
Huwa najiuliza kurukwa na Akili Kuna uhuaiano Gani na kazi ya kuokota makopo maana hata mtu mzima akiamza hiyo kazi baada ya muda unamuona kabisa anaanza kuelekea kwenye hiyo hali!? Au ni ile hali ya kutojijali!?
Hakuna uhusiano wowote ila wengi huwa wapo stage za kwanza za kurukwa na akili kwaiyo akingia kwenye hiyo kazi ndo mazima
 
Kama hana mbadala utamlisha yeye na familia yake? Au unataka akaibe? Huo ndio urefu wa kamba yake.
 
hizo zote ni kazi za kuingiza kipato

 
Sawa
 
Wanasiasa wanatuambia bodaboda ni ajira!
 
Mbona hujaiweka kazi ya ualimu! Kuna watu humu wakiongozwa na dogo mmoja kwa jina la Mpwayungu, wamekuwa wakiwaaminisha wadau wengine humu jukwaani ya kwamba hiyo kazi siyo ya kufanya eti!

Je, ni kweli au ni wivu, majungu na uzushi tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…