Uturuki imewapiga Wakurdi zaidi mara 1000 ndani siku nne kuretaliate shambulio la kigaidi lilifofanyika. Cha ajabu hatusikii wanaharakati mkilaani

Special case kivipi kuua askari wa inchi inayo kuunga mkono eti kisa kumsaidia rais muislamu (idd amini) dhidi ya rais mkristo ( Nyerere) bila kujali alikua anawaunga mkono. Waarabu hawafugiki
Kipindi kile huu mgogoro ulikua umechukuliwa kidini zaidi.
Ila hilo haliondoi kuwa Palestina inatakiwa ipate uhuru wake.
 
Hivi hawa ndio wakaldayo?? Enzi za yesu??
Wakurd wanapitia hali mbaya kama tu Wapalestina, na pengine mbaya zaidi maana wameipitia kwa miaka mingi. Waturuki walihamia hapo waliwakuta Wakurd. Leo wanawapiga mabomu. Ni jamii kubwa kabisa ya watu duniani ambayo haina taifa lao wenyewe.
 
Jamaa wanamngangania hadi Steve Jobs ilhali hajawahi kuishi Syria na kalelewa Kikatoliki'
Kulelewa kikatoliki kunaondoa vipi asili yake? Kama ni mwarabu wa Syria ni mwarabu wa Syria haijalishi Kulelewa kikatoliki ama ki budha.

Kabla ya 2011 Syria population ya Wakristo ilikuwa zaidi ya 10% kuna wakatoliki wa kutosha kama hufahamu.

Imagine Steve Jobs angekua ni asili ya jew, mngemuabudu na kumsifia kila sehemu walivyo Genious hata kama angekua Atheist.
 
Propaganda hasi hizi...
 
Wakurd wanapitia hali mbaya kama tu Wapalestina, na pengine mbaya zaidi maana wameipitia kwa miaka mingi. Waturuki walihamia hapo waliwakuta Wakurd. Leo wanawapiga mabomu. Ni jamii kubwa kabisa ya watu duniani ambayo haina taifa lao wenyewe.
Hata wasukuma ni jamii kubwa hapa nchini. Je, na wao wadai nchi yao ?
 
Uko sahihi mkuu, wakurd wanaonewa sana

Hahah uturuki ingekuwa ni nchi ya kikristu ndio ungeona malalamiko mitandaoni
Ndio maana Israel ameziba masikio, yuko busy kushughulika na magaidi ya kipalestina.
 
So huna source yoyote kutetea maneno yako? Mahaba Niue hadi unabishana na Ashkenaz wenyewe wenye asili yao? Wasalimie sina time ya maneno ya Kanga.
Sources zako zote zimekukataa ulizoleta zimekukataa
 
Wanachopigania Wakurdi hiki hapa Kurdistan Republic
Kama wanakosea kupigania ardhi yao ambayo haikuwepo basi Wapalestina vilevile wanakosea kupigania ardhi yao ambayo haikuwepo. Kama unadai Palestina ilikuwepo maana yake ilikuwa na utawala, Mfalme/Emir/Rais/Chifu wa Palestina aliitwa nani?

Wakurdi wanapigania nchi zote hizo sababu wao wako mipakani wanagawanywa pande zote kisha wanakataliwa kila upande hivyo basi wawe na kwao. Kama wanachofanya Wakurdi ni ugaidi, na wanachofanya Hamas na Hezbollah ni ugaidi vilevile.
 
Wanaua wanawake na watoto ama wanapigana na wanajeshi wanaume wenzao? Hili ndio jambo la kwanza linalo Discriminate vita vingi Duniani na kinachoendelea Israel.
Hizi ngonjera za kuuwa wanawake na watoto zimepitwa na wakati kipigo kinaendelea hapo Gaza na Lebanon
 
Hizi ngonjera za kuuwa wanawake na watoto zimepitwa na wakati kipigo kinaendelea hapo Gaza na Lebanon
Sawa wakitumaliza sisi wanafuatia ni wajukuu zako, Juzi tu babu zako walikua wanawekwa kwenye Museum kama wanyama watu wanaenda kuwa angalia, leo ni watoto wa Gaza kesho watakuwa wa Egpty kesho kutwa ni wako.
 
Wote dini moja, mbwa kala mbwa, aidha waiache hiyo dini waokolewe la sivyo shetani atawatumia sana maana wote ni wake.
 
Nani kaweka hio mipaka na kuwatenganisha Wakurdi?
 
Unaona kaka sasa unavyokua unayabananga mambo!??
Palestina ilikuwepo toka enzi.
Na ndio maana hata katika historia ya Muingereza miongoni mwa maeneo aliyoyatawala ni Palestina.
JE UNAWEZA KUNIAMBIA KURDISTAN ILIWAHI KUWEPO KABLA!???
Kurdi ni kabila kama unavyoona Fursi.
Kurdi ilikua kabila ndani ya Anatolia au Persia.
NARUDIA TENA,KURDI ILIKUA KABILA NDANI YA ANATOLIA/PERSIA/IRAN.
KURDI walitakiwa wawe chini ya IRAN HADI SASA KWASABABU KURDI ILIKUA NI MIONGONI MWA MAKABILA YA KIAJEMI.
Ni sawa useme wamaasai waanze kupambania taifa lao.
Huo si uwendawazimu!??
Mbona tangia karne zilizopita walikubali kuwa chini ya himaya moja ya Persia???
Kwanini karne hii ndio watake kujitenga!??
Huko Syria na Iraq hapamuhusu huyo KURDI.
Kurdi panapomuhusu ni IRAN na Uturuki ambapo Uturuki yenyewe imeiba sehemu ya IRAN/ANATOLIA ilipohama toka Central Asia.
Wewe zunguka lakini kurdi ni kabila na lilikua chini ya tawala ya Hajemi na Ottoman.
Huwezi kufananisha na Palestina ambayo ni taifa lenye makabila ndani yake.
Yani ufananishe Wamaasai kutaka kujitenga kama taifa na upiganiaji wa uhuru wa Uganda!??
Je hivyo vinafanana!??
 
Huyo jamaa huwa sio mleta hoja za mashiko.
Na ukimpa hoja ngumu si ajabu akakukimbia ama kukuzungusha na maneno mengi.
 
Unaona kaka sasa unavyokua unayabananga mambo!??
Palestina ilikuwepo toka enzi.
Mfalme au watawala wa Palestina walikuwa kina nani. Mji mkuu wa Palestina ulikuwa upi.
Na ndio maana hata katika historia ya Muingereza miongoni mwa maeneo aliyoyatawala ni Palestina.
Palestina ilikuwa kama mkoa wa Ottoman empire. Haina historia, haina milki, haina watawala waliopita, sasa taifa gani halijulikani limetoka wapi.

Meanwhile Wayahudi wana historia ya watawala, ushahidi wa kihistoria wa tangu enzi na enzi. Tangu watawala wa dola la Kirumi wapo hata hiyo Ottoman haijakuwepo. Kabla hata tawala za Kiislamu wala dini yenyewe ya Kiislamu kuwepo Middle East tiyari Wayahudi wana rekodi ardhi hiyo.
JE UNAWEZA KUNIAMBIA KURDISTAN ILIWAHI KUWEPO KABLA!???
Haijawahi kuwepo kama ambavyo Palestina haijawahi kuwepo. Sasa kesi zao ni moja, kwanini Wapalestina wawe wapigania haki alafu Wakurdi wawe magaidi?
Kurdi ni kabila kama unavyoona Fursi.
Kurdi ilikua kabila ndani ya Anatolia au Persia.
NARUDIA TENA,KURDI ILIKUA KABILA NDANI YA ANATOLIA/PERSIA/IRAN.
Kama ambavyo Palestina ulikuwa mkoa tu ndani ya Ottoman empire. Ndio maana hakuna Mfalme wa Palestina wala royal family wala Repuplic wala mji mkuu wala historia ya taifa.
KURDI walitakiwa wawe chini ya IRAN HADI SASA KWASABABU KURDI ILIKUA NI MIONGONI MWA MAKABILA YA KIAJEMI.
Ni sawa useme wamaasai waanze kupambania taifa lao.
Wakurdi wana claims zaidi ya ndani ya Iran. Wamasai hawana historia kama taifa, hawajawahi kuwa na mji mkuu ingawa wana machifu wao, hawajawahi kuwa na mpaka sasa wakianza kudai nchi yao tutawashangaa kama Wakurdi na Wapalestina.

Hata hivyo Wakurdi wananyanyaswa kila nchi walipo, hivyo basi wapewe ardhi ya asili yao kama nchi ili ambapo kote hawatakiwi warudi kwao. Huwezi goma kuwashirikisha kitaifa alafu unagoma wasijitenge. Biafra ingekuwa taifa sababu ya kutengwa, South Sudan imetokana na hiyo sababu.
Huo si uwendawazimu!??
Mbona tangia karne zilizopita walikubali kuwa chini ya himaya moja ya Persia???
Sasa remnants wa Persia hawawataki, na hawatakiwi kwingineko wanabaguliwa. Ni sawa kulazimisha Austria na Hungary kurudia kuwa nchi moja kisa "mbona zamani zilikubali kuwa Austro-Hungary".
Kwanini karne hii ndio watake kujitenga!??
Huko Syria na Iraq hapamuhusu huyo KURDI.
Kurdi panapomuhusu ni IRAN na Uturuki ambapo Uturuki yenyewe imeiba sehemu ya IRAN/ANATOLIA ilipohama toka Central Asia.
Hawajataka kujitenga karne hii, wameanza tangu karne iliyopita. Walianza wanataka watambuliwe, ikashindikana wakataka basi wakae peke yao. Kila jamii zinazowazunguka zinawaona makafiri.

Wakurdi unaosema panapowahusu ni Iran tu ndio haohao wana jimbo la Kurdistan ndani ya Iraq, wana special representative bungeni. Na wanatengwa wamevamiwa na Repuplican Forces ya Iraq enzi za Saddam Hussein. Unasemaje wanahusika na Iran pekee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…