Uuzaji wa vidole vya miguu Zimbabwe

Uuzaji wa vidole vya miguu Zimbabwe

Maskini, watu wana dhambi sana, hivi si kosa la jinai kweli? Anaenda kufanyia nini? Serikali yao inachukuliaje hilo?

Hao ni ushirikina tu mzungu aache kubeba mafuta, madini, na gesi
Abebe Gumba REALLY?

Hata sisi Albino wanasakwa sana na Ndio maana umasikini hauishi na ndio mwisho wa kufikiri kwetu , eti utajiri wa shirk
Kama mzungu ananunua vidole vyetu Basi itakuwa ajabu ya mwaka
 
Ulimwengu Wa Kiroho una Siri kubwa,
Na shetani huzitumia kutokana tumeacha kufata yaliyofichwa.

Madaraka na Utajiri yapo kwenye kidole gumba

Waamuzi 1:7 BHN
Adoni-bezeki akasema, “Wafalme sabini waliokatwa vidole gumba vya mikono na miguu waliokota makombo chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa kama nilivyotenda.” Wakampeleka Yerusalemu, akafia huko.


Walawi 14:28 BHND
Kuhani atampaka huyo mtu anayetakaswa mafuta katika ncha ya sikio lake la kulia, katika kidole gumba cha mkono wake wa kulia, na kidole gumba cha mguu wake wa kulia. Atampaka mahali pale ambapo alimpaka ile damu ya sadaka ya kuondoa hatia
 
Kwa hali ya mabadiliko ya tabia nchi, na bei ya MBOLEA na ukosefu wa mvua za kutosha na uhaba na ufinyu wa mavuno, wakija Bongo, theluthi nzima ya nchi itapanga foleni!

Chakula kutakuwa adimu Sana mwaka huu! Labda hiyo vuli ije mapema, na mvua zinyeshe za uhakika!
 
Dah!.. inasikitisha na kutisha...kisa milioni 16 tu ubaki na ulemavu wa kudumu ?
 
Mzungu wa wapi huyo anaenunua dole?
Umejiridhisha kabisa kuwa wananunua?
Mbona kutwa tunaenda ma hospitali yao na hawatufyeki mavidole haya

Natamani nijue ni wazungu gani hao
Hao ni waafrika wanaonunua kwa shirk zao na bado masikini tu
Rudi usome Uzi
 
Rudi usome Uzi

Mimi nimesoma upuuzi huu ila Hakuna mahali BBC Swahili wamesema ni wazungu wewe umezisoma wapi hizi habari
Napenda habari kamili na vyanzo vya uhakika Sasa wewe unanirudisha kusoma ukifikiri umejibu hoja

Leta habari kamili nijiridhishe ila habari za WhatsApp ni porojo tu
Hizi habari ni utani sio za Kweli
Muwe mnajiridhisha kwanza kwa kuchimba deep
Huwa sikurupuki kuamini mpaka nimetafuta vyanzo vyake

Na wewe kajiridhishe sasa kabla ya kujibu hoja
 
Uzi una picha.

Nimesikitika sana kitendo cha Waafrika wenzetu tuliowapambania kipindi cha kumtoa mkoloni Leo hii wanauza vidole vyao vya mguu kwa wazungu tena kwa bei nafuu ya USD 7000 mpaka 10000.

Dole gumba ni $7000
Kidole cha Kati cha mguu ni $9000
Nakidole kidogo cha mguu ni $10000.

Swali langu ni kuwa kwani hawa wazungu haya mavidole wanapeleka wapi? Kwanini wasiwakate huko kwao mpaka waje kwetu Afrika lakini. Au ndokulipiza hasira kwa alichowafanyia Mugabe Gabriel kuwapora Ardhi. Yani Kuna mambo Waafrika tunakuwa treated kama Mavi vile maana ukienda Dubai Dada zetu wanalishwa kinyesi ukija Africa tunakatwa vidole sasa sijui nini Kosa letu mpaka watufanyie hivi.

Yani kwa siku wazimbabwe zaidi ya buku tatu wanakatwa vidole vya mguu sasa hawa wazungu haya mavidole wanapeleka wapi. Serikali iingilie Kati maana Kuna watu watataka wauze vyote. View attachment 2248380View attachment 2248381
Yetu hatujamaliza kuyajadili, mauaji yanaendelea kila kona ya nchi, kila kukicha tumevuka mipaka mpaka Zimbabwe
 
Back
Top Bottom