Vijana tuacheni kubeti, kindege (aviator) kimenimaliza milioni 7 yote ya mtaji

Vijana tuacheni kubeti, kindege (aviator) kimenimaliza milioni 7 yote ya mtaji

Nashindwa kuwaambia jinsi nilivyojikatia tamaa kiasi cha kuwa kichaa.

Ila ninachoweza kuwaambia tu vijana wenzangu tuacheni kubeti kwa malengo kwamba tunapata pesa huko haraka haraka.

Fikiria nimefanya kazi ya kuajiriwa kwa miaka 8, nikafukuzwa kazi nikaenda NSSF nikachukua milion 7.5 niliyokuwa nakatwa alafu yote nimeimaliza kwenye kindege cha aviator ndani ya siku 5 tu.

Nahisi kuna roho flani iliniongoza kwa sababu kwa akili ya kawaida najiona siyo mimi.

Lengo ilikuwa kubetia elfu 50 kama mtaji wa kubetia lakini kilichofata ni kupoteza milion 7.5 zote bila kubaki hata mia ndani ya siku 5 tu.

Hapa nilipo I wish hata nijitoe roho tu maana sijui ni wapi naanzia maisha tena pesa yote nishaipoteza kwenye uraibu wa kamari.

Kila nikiwaza nna miaka 30, sijaoa, sina biashara yoyote niliyoisimamisha kunilinda, sina maisha, kwa kifupi hiyo milion 7.5 nilitegemea ndiyo niingie nayo mtaani inilinde.

Lakini shetani kanikamata na kunikanda kisawa sawa.

Najiona mjinga wa kiwango cha Phd ndiyo maana nimejiita Zero Brainer, sina wa kumlaumu ila tujiepushe sana na uraibu hasa wa kubeti.

Mimi naweza nikafa leo ila sitaki vijana wenzangu yaje yawakute yaliyonikuta mimi sasahivi.

Mimi hali nnayopitia sasa kwa sababu ya kubeti nakosa maneno ya kuwaelezea ila siku nikifa mjua KINDEGE cha AVIATOR kimesababisha kifo changu .
Sasa kwanini ujimalize na ushajua ulipoangukia
 
Pesa jumla nilitupa kwenye betting toka nilipoanza 2013 mpaka sasa ni equivalent to milioni 20. Na bado kuna pesa nilitupa kwenye project mil 9. Kawaida tu usipagawe. Utazoea utasahau ndani ya muda mfupi. La muhimu acha kamari.
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Nilijaribu niliweka buku ikapanda adi elf 5 nilipoweka iongezeke zaidi ikaliwa yote
Sina ham na aviator
Sasa kama buku iliniuma hivi je wewe wa milioni 7
Muhindi akamatwe🤣🤣🤣🤣
 
Kindege ni program ya kubet ipo kwenye playstore.
Unadownload na kuanza kucheza kwa kutia hela ili upate fedha.
Mh mbona Playstore hua haiweki app za betting? Hawa wamepenyaje
 
Pole sana mkuu, kubali kuwa umepoteza na anza upya ikiwezekana badili mazingira uza ulichonacho kaanze maisha upya sehem nyingine na usijejaribu kusema utairudisha hiyo hela na kutaka kuirudisha kupitia kamari, utapoteza kila kitu mpaka uhai.
Nishifikia asilimia 95 ya mawazo ya kujiua siku nilipomalizwa kabisa nikabaki na zero.

Ila kwa sasa niko 60 % karibu na kujiuq.

Hasa nikiwaza namna ya kuipata tena hiyo pesa, sina kazi, umri umesonga sijaoa ndiyo kunanipa stress kabisa.
 
Jipige kifuani mara3 kisha utamke maneno aya
->Mimi ni mjinga sana
->Mimi ni mpuuzi na kilaza kiwango cha Sgr
->Mimi ni Zumbukoko nimepeleka mafao yangu kwenye kamari

->Mimi nina nyota ya umaskini

ukisha maliza kutamka ayo njoo nikupe odds 5 za uhakika ufute huo ujinga ulio jaa akilini mwako
 
Nashindwa kuwaambia jinsi nilivyojikatia tamaa kiasi cha kuwa kichaa.

Ila ninachoweza kuwaambia tu vijana wenzangu tuacheni kubeti kwa malengo kwamba tunapata pesa huko haraka haraka.

Fikiria nimefanya kazi ya kuajiriwa kwa miaka 8, nikafukuzwa kazi nikaenda NSSF nikachukua milion 7.5 niliyokuwa nakatwa alafu yote nimeimaliza kwenye kindege cha aviator ndani ya siku 5 tu.

Nahisi kuna roho flani iliniongoza kwa sababu kwa akili ya kawaida najiona siyo mimi.

Lengo ilikuwa kubetia elfu 50 kama mtaji wa kubetia lakini kilichofata ni kupoteza milion 7.5 zote bila kubaki hata mia ndani ya siku 5 tu.

Hapa nilipo I wish hata nijitoe roho tu maana sijui ni wapi naanzia maisha tena pesa yote nishaipoteza kwenye uraibu wa kamari.

Kila nikiwaza nna miaka 30, sijaoa, sina biashara yoyote niliyoisimamisha kunilinda, sina maisha, kwa kifupi hiyo milion 7.5 nilitegemea ndiyo niingie nayo mtaani inilinde.

Lakini shetani kanikamata na kunikanda kisawa sawa.

Najiona mjinga wa kiwango cha Phd ndiyo maana nimejiita Zero Brainer, sina wa kumlaumu ila tujiepushe sana na uraibu hasa wa kubeti.

Mimi naweza nikafa leo ila sitaki vijana wenzangu yaje yawakute yaliyonikuta mimi sasahivi.

Mimi hali nnayopitia sasa kwa sababu ya kubeti nakosa maneno ya kuwaelezea ila siku nikifa mjua KINDEGE cha AVIATOR kimesababisha kifo changu .
Pole sana kijana. Unaweza kunicheki pm kwa msaada zaidi. Tafadhali naomba usipuuze
 
Back
Top Bottom