Vijana tuacheni kubeti, kindege (aviator) kimenimaliza milioni 7 yote ya mtaji

Vijana tuacheni kubeti, kindege (aviator) kimenimaliza milioni 7 yote ya mtaji

Miaka 20 iliyopita nikiwa na umri wako huo nilipata janga kubwa sana nikaona dunia si yangu tena. Nilifanya upambavu mkubwa sana na nikapoteza kazi nzuri huku jela ikinisubiri. Hapo nina familia na wananitegemea mimi, nilichukua uamuzi wa kujitoa roho, nikanunua frajili 20, nikachukua bia (Tusker) moja nikachanganya na Konyagi nikabugia yote. Nilikwenda kuponea hospitali kwa msaada mkubwa wa wife. Leo maisha yanaendelea na yote yaliyopita yalishapita. Tulia jipange upya, maisha ni zawadi muhimu sana na thamani yake haipimiki, tunapaswa kuyakumbatia kwa nguvu zetu zote hadi pale yatakapoondolewa kwetu.
Unajua kuna makosa ya kibinadamu kiasi kwamba hata ukikosea unaweza usijutie sana.

Ila broo kwenye kubeti siyo kosa la kibinadamu ni tamaa na kujiendekeza tu.

Inaniuma sana kupoteza pesa kwenye kubeti.

Ni bora hata ningekamatwa huko na dawa za kulevya nikafungwa nisingeumia sana maana nilikuwa natafta utajiri japo kwa njia haramu.

Ila kubeti milion 7.5 kwa siku 5, kuna najidharau sana natamani hata nijichome visu vingi tumboni maana najiona sina akili hata ile moja
 
Unajua kuna makosa ya kibinadamu kiasi kwamba hata ukikosea unaweza usijutie sana.

Ila broo kwenye kubeti siyo kosa la kibinadamu ni tamaa na kujiendekeza tu.

Inaniuma sana kupoteza pesa kwenye kubeti.

Ni bora hata ningekamatwa huko na dawa za kulevya nikafungwa nisingeumia sana maana nilikuwa natafta utajiri japo kwa njia haramu.

Ila kubeti milion 7.5 kwa siku 5, kuna najidharau sana natamani hata nijichome visu vingi tumboni maana najiona sina akili hata ile moja
Hakuna kosa lisilokuwa la kibinadamu chini ya jua, unaweza ukamuamini mtu na akakufix ukaishia kupoteza kila kitu kama ilivyokuwa kwangu. Cha msingi ni kukubaliana na kilichotokea na kusonga mbele. Hilo ni funzo kubwa sana kwa maisha yako, lifanye kuwa ngazi ya kupanda juu zaidi.
Kuna mzee wangu mmoja, alikuwa ni tajiri mkubwa sana miaka ya 80, operesheni uhujumu uchumi ikamfilisi kila kitu hadi akawa anatembelea baiskeli. Alikuwa akichekwa na kudhihakiwa, kutoka kumiliki gari za mizigo (Scania) miaka hiyo, na biashara zingine kibao. Kuna wenzie walijitoa roho yule mzee alikomaa, ikatokea bahati ya biashara ya Sangara miaka ya 90 mwishoni kuelekea 2000, akatoboa ile mbaya.
 
Nashindwa kuwaambia jinsi nilivyojikatia tamaa kiasi cha kuwa kichaa.

Ila ninachoweza kuwaambia tu vijana wenzangu tuacheni kubeti kwa malengo kwamba tunapata pesa huko haraka haraka.

Fikiria nimefanya kazi ya kuajiriwa kwa miaka 8, nikafukuzwa kazi nikaenda NSSF nikachukua milion 7.5 niliyokuwa nakatwa alafu yote nimeimaliza kwenye kindege cha aviator ndani ya siku 5 tu.

Nahisi kuna roho flani iliniongoza kwa sababu kwa akili ya kawaida najiona siyo mimi.

Lengo ilikuwa kubetia elfu 50 kama mtaji wa kubetia lakini kilichofata ni kupoteza milion 7.5 zote bila kubaki hata mia ndani ya siku 5 tu.

Hapa nilipo I wish hata nijitoe roho tu maana sijui ni wapi naanzia maisha tena pesa yote nishaipoteza kwenye uraibu wa kamari.

Kila nikiwaza nna miaka 30, sijaoa, sina biashara yoyote niliyoisimamisha kunilinda, sina maisha, kwa kifupi hiyo milion 7.5 nilitegemea ndiyo niingie nayo mtaani inilinde.

Lakini shetani kanikamata na kunikanda kisawa sawa.

Najiona mjinga wa kiwango cha Phd ndiyo maana nimejiita Zero Brainer, sina wa kumlaumu ila tujiepushe sana na uraibu hasa wa kubeti.

Mimi naweza nikafa leo ila sitaki vijana wenzangu yaje yawakute yaliyonikuta mimi sasahivi.

Mimi hali nnayopitia sasa kwa sababu ya kubeti nakosa maneno ya kuwaelezea ila siku nikifa mjua KINDEGE cha AVIATOR kimesababisha kifo changu .
Aisee
 
Ndo maana ukaitwa zero brain sheikh

Mi majuzi niligombana na wife, nikachepuka kwa kitoto kina neema za allah kama zote, baada ya kuzoeana nikakapangia mahali ukiweka Kodi na vitu vyake vya ndani na ukijumlisha kaduka nilichomfungulia pale pale maana Kuna frame kwa nje haizidi 5M, yaani ni kama nimeoa mke wa pili kwa 5M na Kila siku napata Huduma ndo niende home.... Au naweza kuweka kambi hapo hata wiki kwa safari za kufata mizigo ya biashara za uongo


Nikiskia vijana mnapoteza 5M nahuzunika sana, kama unabeti beti hata buku tu aisee, m5 ukienda dar uswahilini huko unavuta wake watatu utakatikiwa mpaka ukimbie Jiji
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 qmmmmk jamaa unawaza ngono tu
 
Virtual bet ya betpawa ni fake na haina uhalisia kwani kitu kimoja kinamatokeo tofauti i.e game moja inamatokeo tofauti. Virtual ni uwongo nimetafiti vya kutosha sana.
Hatuachi kubeti Jana nimeanza na 30,000 tu kubeti kwenye soka Sasa hivi usiku huu Nina 200k ,unaniambiaje nibeti we utakuwa junior kwenye kubeti pia hauwezi zuia hisia na haujui betting inaendaje,na unaendaje kushindana na computer,betting zote izo aviator na virtual games ni computer ata siku Moja hauwezi shindana nazo
 
Ninachoshukuru sijui kuendesha kindege, sijui kuzungusha lile tairi na wala sijui kucheza dubwi la mchina.

Ila kuna siku nimewahi kupoteza laki 2 kizembe sana ilikuwa 2020 kama sikosei.

Ni kupitia 1xbet nilikuwa nimebet football nikala.
Sasa ukatokea ujumbe kuwa naweza kudouble my winning, nikakubali.
Ukaja mchezo wa kupiga penalt halafu kuna goalkeeper anadaka.

Ninachokumbuka nilikula kama mara 2 tu, nyingine goalkeeper alikuwa anadaka na kutema hadi nikakauka kau.
 
Virtual bet ya betpawa ni fake na haina uhalisia kwani kitu kimoja kinamatokeo tofauti i.e game moja inamatokeo tofauti. Virtual ni uwongo nimetafiti vya kutosha sana.
Upo sahihi ni virtual games ni computer inasetiwa imnyooshe mtu,ukitaka kujua kaeni wawili wekeni matokeo mawili tofauti mechi iyo iyo muone kama mtashinda
 
Back
Top Bottom