Vijana tuacheni kubeti, kindege (aviator) kimenimaliza milioni 7 yote ya mtaji

Vijana tuacheni kubeti, kindege (aviator) kimenimaliza milioni 7 yote ya mtaji

Bora hata usikijue maana ukikijua unaweza kukijaribu.

Ukiingia kinakutamanisha kwa kukupa pesa kubwa ndani ya dakika moja alafu ukinogewa ujue ndiyo unafilisika.

Akilia inakuja kuzinduka una buku kutoka milion
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nishifikia asilimia 95 ya mawazo ya kujiua siku nilipomalizwa kabisa nikabaki na zero.

Ila kwa sasa niko 60 % karibu na kujiuq.

Hasa nikiwaza namna ya kuipata tena hiyo pesa, sina kazi, umri umesonga sijaoa ndiyo kunanipa stress kabisa.
Hayo mawazo ya kujiua yafute kabisa maana unayaruhusu we mwenyewe, anza upya tafuta kibarua cha kujimudu, jipange jipe muda then tafuta mwanamke wa kuanza nae maisha, kamari hiyo ya hivyo acha kabisa bora ubet mpira kuliko hayo ma aviator.

Naelewa situation yako maana hata mim nilipitia haya lakini nikavuka salama. Kukata tamaa ni mwiko kumbuka sababu ni tamaa zako, R I P kwa hela zote zilizopotea ukiwa unatafuta hela.

Aisee katika kitu namshukuru Mungu mimi ni mgumu sana kukata tamaa hata niwe kwenye gumu gani najua nitavuka tu hata kama litanigharimu na kuniumiza. We mkamaria kama umeweza maumivu ya kupoteza unashindwaje kuanza upya? Komaa kiume dunia na mafanikio haiitaji watu wanyonge, be strong meeeeeen, act tough meeeeeen.
 
Hayo mawazo ya kujiua yafute kabisa maana unayaruhusu we mwenyewe, anza upya tafuta kibarua cha kujimudu, jipange jipe muda then tafuta mwanamke wa kuanza nae maisha, kamari hiyo ya hivyo acha kabisa bora ubet mpira kuliko hayo ma aviator.

Naelewa situation yako maana hata mim nilipitia haya lakini nikavuka salama. Kukata tamaa ni mwiko kumbuka sababu ni tamaa zako, R I P kwa hela zote zilizopotea ukiwa unatafuta hela.

Aisee katika kitu namshukuru Mungu mimi ni mgumu sana kukata tamaa hata niwe kwenye gumu gani najua nitavuka tu hata kama litanigharimu na kuniumiza. We mkamaria kama umeweza maumivu ya kupoteza unashindwaje kuanza upya? Komaa kiume dunia na mafanikio haiitaji watu wanyonge, be strong meeeeeen, act tough meeeeeen.
Nice words.

Mpaka hapa nahisi nimepunguza asilimia kadhaa za karibu na kifo.
 
Nice words.

Mpaka hapa nahisi nimepunguza asilimia kadhaa za karibu na kifo.
Achana na mawazo ya kujiua sio solution ya matatizo yako, ukipitia changamoto yeyote acha kabisa kuwaza kifo kama suluhu, huo ni udhaifu uliotukuka.

Kama mimi nilipitia hayo na nikavuka licha ya maumivu makali kwanini wewe ushindwe?

Uza simu anza upya tafuta cha kufanya kadri muda unavyoenda mambo yatakuwa sawa.

Epuka kuazima hela kwa watu na kuahidi kurejesha ukiwa na hiyo simu yenye uwezo wa kukufanya ucheze aviator, kwa sasa hata ukipewa hela utakimbilia kucheza tena(najua hili wengi watakataa/utakataa) ila nimepitia na ninajua kwa kuyaona kwa wengi. Jijenge mwenyewe taratibu taratibu na usifosi uazime hela usiomudu kurudisha, utajivunjia uaminifu na upo kwenye kipindi kigumu cha kusimama upya kuna muda utahitaji msaada na wakukusaidia ndio hao wanaokuamini, usiwapoteze.

Nakuandikia magazeti kwa sababu nimeyapitia haya na sipendi kuona mtu anayapitia naelewa maumivu yake.
 
Aviator wakat naijua niliambiwa na walionielekeza kuwa niweke pesa ndogo sana kujifunza, niliambiwa mia 2 lakin mimi nikaweka 1000 ndani ya dakika chache nikapiga 10000

Nikaona mbona mchezo ni rahis Sana, nikaamua kudeposit 60,000,
Kindege kilivyoona hyo hela kikapandisha mashetani, yaan sasa kikawa hakihesabu tena,kikiruka kidogo kinaanguka mpaka hela yote ikaisha
 
Mbona zako waga unatunga na bado tunasoma, Kwahiyo unataka uendelee kutunga wewe tu au sio

Kama katunga fresh, sie hayatuhusu kikubwa alichotunga kuna watu kinawatokea kwenye real life kila siku
MI siandiki msome.
 
Nakuelewa kwa sababu unayopitia yanatokea kwa vijana wengi sana ila wengi wao hawasemi tu

Kupitia betting kuna watu hadi leo wamekuwa vichaa kutokana na kushindwa Ku handle madhara ya kisaikolojia waliyoyapata huko

wapo baadhi ambao tunawajua kabisa kuwa yule kawa chizi kutokana na betting/kamari baada ya kupoteza pesa nyingi au mali Fulani

Kwahiyo kwako hakuna kipya ni rejeo tu la kinachotokea kila siku na wengine wanasalimika baada ya kupata kadhia kama yako kwa sababu ndio huacha mazima Kamali

Betting/kamari ina uraibu mbaya sana bora ata vilevi vingine, hivo hii loss uliyopata tumia kama njia ya kujitathimini na fundisho kwa sababu pesa zinatafutwa tu na sio issue sana, issue ni kupoteza Muda

Epuka mawazo ya kusema IPO siku utakuja kurudisha hiyo 7.5M kupitia betting, hiyo hela sio nyingi sana wala wala sio ndogo sana na unaweza kuipata kupitia betting, ila unaweza kuja kupata 7M wewe ukiwa umeliwa 50M

Kwenye betting in long run, waga asilimia kubwa ni hasara tu kwa yule anaebett na Faida kwa kampuni anayotumia kubeti, itabakia kuwa addiction tu kuwa mtu hawezi kuacha kubeti ila ukweli kashapigwa sana za USO, ila akila anafarijika sana kumbe analishwa Chambo
Muda muda muda muda.

Napata tumaini kupitia wewe kwa sababu umeamua kuishi kwenye hisia za maumivu yangu.

Ila Baba muda plus rasilimali ndiyo changamoto.

Imagine mwanaume 30 years single, economically kwa sasa niko zero, job opportunity zero, rasilimali ya kuanza nayo ili niinuke upya nijitetee ni zero.

Nilipata opporrunity ya kutokea (hiyo 7 milion) lakini nika lose the chance.

Ama kweli hakuna rangi nitaacha kuona kama wadau wanavyosema.

Kila nikiwaza nilicho kipoteza nahisi moto unaniunguza tumboni.

I feel more than hell.

Bora basi ningepoteza 7 milion lakini nna kazi ya kuingiza chochote kwa mwezi, nako hamna.

Ningepoteza basi seven milion lakini nna rasilimali ya kuuza nianze upya, nako hamna zaidi ya hii samsung galaxy A 14.

Yaana mimi najiona kabisa ni marehemu anaesogeza siku tu hapa
 
Nashindwa kuwaambia jinsi nilivyojikatia tamaa kiasi cha kuwa kichaa.

Ila ninachoweza kuwaambia tu vijana wenzangu tuacheni kubeti kwa malengo kwamba tunapata pesa huko haraka haraka.

Fikiria nimefanya kazi ya kuajiriwa kwa miaka 8, nikafukuzwa kazi nikaenda NSSF nikachukua milion 7.5 niliyokuwa nakatwa alafu yote nimeimaliza kwenye kindege cha aviator ndani ya siku 5 tu.

Nahisi kuna roho flani iliniongoza kwa sababu kwa akili ya kawaida najiona siyo mimi.

Lengo ilikuwa kubetia elfu 50 kama mtaji wa kubetia lakini kilichofata ni kupoteza milion 7.5 zote bila kubaki hata mia ndani ya siku 5 tu.

Hapa nilipo I wish hata nijitoe roho tu maana sijui ni wapi naanzia maisha tena pesa yote nishaipoteza kwenye uraibu wa kamari.

Kila nikiwaza nna miaka 30, sijaoa, sina biashara yoyote niliyoisimamisha kunilinda, sina maisha, kwa kifupi hiyo milion 7.5 nilitegemea ndiyo niingie nayo mtaani inilinde.

Lakini shetani kanikamata na kunikanda kisawa sawa.

Najiona mjinga wa kiwango cha Phd ndiyo maana nimejiita Zero Brainer, sina wa kumlaumu ila tujiepushe sana na uraibu hasa wa kubeti.

Mimi naweza nikafa leo ila sitaki vijana wenzangu yaje yawakute yaliyonikuta mimi sasahivi.

Mimi hali nnayopitia sasa kwa sababu ya kubeti nakosa maneno ya kuwaelezea ila siku nikifa mjua KINDEGE cha AVIATOR kimesababisha kifo changu .
Miaka 20 iliyopita nikiwa na umri wako huo nilipata janga kubwa sana nikaona dunia si yangu tena. Nilifanya upambavu mkubwa sana na nikapoteza kazi nzuri huku jela ikinisubiri. Hapo nina familia na wananitegemea mimi, nilichukua uamuzi wa kujitoa roho, nikanunua frajili 20, nikachukua bia (Tusker) moja nikachanganya na Konyagi nikabugia yote. Nilikwenda kuponea hospitali kwa msaada mkubwa wa wife. Leo maisha yanaendelea na yote yaliyopita yalishapita. Tulia jipange upya, maisha ni zawadi muhimu sana na thamani yake haipimiki, tunapaswa kuyakumbatia kwa nguvu zetu zote hadi pale yatakapoondolewa kwetu.
 
Back
Top Bottom