Wakuu naomba mnieleweshe concept ya Mungu katika ukristo

Wakuu naomba mnieleweshe concept ya Mungu katika ukristo

MUNGU HANA NAFSI TATU
Leo watu wanapotea kutokana na mapokeo waliyokuta katika madhehebu yao mfano karika suala hili la ''Utatu'' yaani MUNGU kuwa na nafsi tatu sasa tuangalie kulingana na Biblia inasemaje?;
1)MUNGU anasema ana nafsi moja Isaya 45:21-23
[21]Hubirini, toeni habari; naam, na wafanye mashauri pamoja; ni nani aliyeonyesha haya tangu zamani za kale? Ni nani aliyeyahubiri hapo zamani? Si mimi, BWANA? Wala hapana Mungu zaidi ya mimi; Mungu mwenye haki, mwokozi; hapana mwingine zaidi ya mimi.
[22]Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.
[23]Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.
Unaona katika mstari wa 23 MUNGU mwenyewe anasema ana nafsi moja.
Pia tuone andiko jengine Waebrania 6:13-14
[13]Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake,
[14]akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.
Vile vile unaweza kusoma maandiko mengine kuthibitisha
Zaburi 11:5
[5]BWANA humjaribu mwenye haki;
Bali nafsi yake humchukia asiye haki,
Na mwenye kupenda udhalimu.
Maandiko yapo mengi zaidi ya hayo yanayothibitisha kuwa Mungu ana nafsi moja tu .

Sasa acha kwa ufupi tuone nafsi nini kulingana na Biblia ;
Nafsi kwa namna ya kuelewa kirahisi ni Mtu mwenyewe Mwanzo 2:7
[7]BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Sasa tunaweza kusema mfano kuna watu wawili maana yake ni nafsi mbili yaani watu wawili Mwanzo 46:15
[15]Hao ndio wana wa Lea, aliomzalia Yakobo katika Padan-aramu, na Dina, binti yake. Nafsi zote za wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
Kutoka 1:5
[5]Na nafsi zile zote zilizotoka viunoni mwa Yakobo zilikuwa ni nafsi sabini; na huyo Yusufu alikuwa huko ndani ya Misri tangu hapo. Unaona katika maandiko badala ya kusema watu inasema ''Nafsi'' maana vyote ni sawa na ndio maana sisi tumeumbwa kwa mfano wa MUNGU yeye ana nafsi moja na sisi tuna nafsi moja.
KWA HITIMISHO ;Huyo MUNGU Mwenye nafsi moja si mwingine bali ni BWANA YESU KRISTO Tito 2:13-14
[13]tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;
[14]ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.
NB Ndugu zangu leo hii madhehebu ndio njia shetani anatumia kuwapoteza watu mapokeo hayaokoi bali ni Neno la MUNGU la kweli lisilo pita.
 
Mujibu kwa maandiko na sio maelezo.hakuna Mungu roho,mungu mwana katika biblia.
Yesu ana uungu lakini yeye si Yule Mungu yule ambae biblia inasema hakuna aliyewai muona AKAISHI
Ndiyo maana biblia inasema" yesu ni mfano wa MUNGU yule asiyeoneka"
Naona umetoa andiko kabisa kuthibitisha maelezo yako. 👏
 
Yesu ni Mungu by nature kwasababu Baba yake ni Mungu.
Ana uungu ndani yake so kumuita Yesu Mungu si kosa.
Mtoto wa simba ni simba,mtoto wa binadamu ni binadamu na mtoto wa Mungu ni Mungu.

Mtume Muhammad(PBH) anasema"kama Mungu angelikuwa na mtoto mimi ningelikuwa wa kwanza kumuabudu mtoto huyo maana ni Mungu.
Ila yeye kuitwa Mungu haina maana yeye ndiye yule ambaye hakuna mtu aliyewai muona.
Yohana 1:18 “Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua”.
Mungu ni yupi sasa mkuu? Ni yesu aliyemwana wa Mungu au Mungu au wote ni Mungu?
 
Habari

1. Wengine wanasema kuna Mungu Baba, mwana na roho mtakatifu

2. Wengine wanasema Mungu mmoja

3. Wengine nasikia wanasema ana nafsi tatu

Na je kama ana nafsi tatu kwa nini munamuabudu sana YESU kuliko huyu Mungu Baba

Lengo ni kuelewa kipi ni kipi maana naona kama wanatofautiana sana juu ya concept ya Mungu

Shukrani
Wewe fahamu tu kuwa, katika ukristo Mungu ni mmoja (na kweli ni mmoja) lakini katika nyakati mbalimbali amejidhihirisha katika ukuu, utukufu na utendaji wa namna tatu tofauti, yaani ubaba, umwana na uroho mtakatifu.
 
Mungu ni mmoja baba yake Yesu
Lakini kuna mwenzako ananipa concept tofauti na hii mkuu...soma hapa👇👇👇
Yesu ni Mungu by nature kwasababu Baba yake ni Mungu.
Ana uungu ndani yake so kumuita Yesu Mungu si kosa.
Mtoto wa simba ni simba,mtoto wa binadamu ni binadamu na mtoto wa Mungu ni Mungu.

Mtume Muhammad(PBH) anasema"kama Mungu angelikuwa na mtoto mimi ningelikuwa wa kwanza kumuabudu mtoto huyo maana ni Mungu.
Ila yeye kuitwa Mungu haina maana yeye ndiye yule ambaye hakuna mtu aliyewai muona.
Yohana 1:18 “Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua”.
 
Hakuna namna yoyote ile utamjua, kumpenda na kumwabudu Mungu pasipo kupitia kwa Yesu kristo, pia hakuna namna yoyote ile Mungu atakufikia ili kukuokoa na kukubariki pasipo Yesu kristo na hakuna namna yoyote Mungu atakuongoza pasipo Roho mtakatifu. Na mwisho hakuna namna utaweza kumtenganisha Yesu kristo na Roho mtakatifu katika uungu.
 
Fikiri hili, wewe mleta mada ni mtoto (mbele ya mzazi wako), ni mume (mbele ya mkeo), ni baba (mbele ya watoto wako), mfanyabiashara (mbele ya wateja wako). Je, wewe ni mtu yule yule au mtu tofauti?
 
Hakuna namna yoyote ile utamjua, kumpenda na kumwabudu Mungu pasipo kupitia kwa Yesu kristo, pia hakuna namna yoyote ile Mungu atakufikia ili kukuokoa na kukubariki pasipo Yesu kristo na hakuna namna yoyote Mungu atakuongoza pasipo Roho mtakatifu. Na mwisho hakuna namna utaweza kumtenganisha Yesu kristo na Roho mtakatifu katika uungu.
Nakubaliana na wewe asilimia 100% na hapa lengo sio kumtenganisha kristo ... swali Mungu ni huyu Kristo au kuna Mungu au wote ni Mungu?
 
Fikiri hili, wewe mleta mada ni mtoto (mbele ya mzazi wako), ni mume (mbele ya mkeo), ni baba (mbele ya watoto wako), mfanyabiashara (mbele ya wateja wako). Je, wewe ni mtu yule yule au mtu tofauti?
mimi ni mtu yuleyule ambaye ni mtoa mada ... mtoa mada nikiwa na mtoto mtoto wangu nae ni mtoa mada?
 
Wote wako sawa!............

...........
......
Haya mambo ukitumia akili za kibinadamu huwezi kuelewa!


Uzi uishie hapa.

Maana nilianza kuwaza, kama wapo sawa inakuwaje mmoja anamtuma mwengine!

Mmoja anamuomba mwengine!

Mmoja anajitoa sadaka, ili mwengine awasamehe wanadamu!

Nikawaza labda ni mmoja tu! Ila inakuwaje mmoja huyo huyo anakasirishwa na wanadamu, halafu anajituma mwenyewe, anauwawa ili yeye mwenyewe tena awasamehe wanadamu kwa damu yake.
 
Mimi si mkristo lakini issue hapa ni Mungu katika ukristo yupoje... na lengo la mada hii sio kujua dini ipi ni sahihi
Kwa jibu hili. Unataka uambiwe Kuhusu Mungu katika imani ya kikirsto ili upate nini?
Kwa nini usingeleta elimu kuisemea imani yako?
 
MUNGU HANA NAFSI TATU
Leo watu wanapotea kutokana na mapokeo waliyokuta katika madhehebu yao mfano karika suala hili la ''Utatu'' yaani MUNGU kuwa na nafsi tatu sasa tuangalie kulingana na Biblia inasemaje?;
1)MUNGU anasema ana nafsi moja Isaya 45:21-23
[21]Hubirini, toeni habari; naam, na wafanye mashauri pamoja; ni nani aliyeonyesha haya tangu zamani za kale? Ni nani aliyeyahubiri hapo zamani? Si mimi, BWANA? Wala hapana Mungu zaidi ya mimi; Mungu mwenye haki, mwokozi; hapana mwingine zaidi ya mimi.
[22]Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.
[23]Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.
Unaona katika mstari wa 23 MUNGU mwenyewe anasema ana nafsi moja.
Pia tuone andiko jengine Waebrania 6:13-14
[13]Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake,
[14]akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.
Vile vile unaweza kusoma maandiko mengine kuthibitisha
Zaburi 11:5
[5]BWANA humjaribu mwenye haki;
Bali nafsi yake humchukia asiye haki,
Na mwenye kupenda udhalimu.
Maandiko yapo mengi zaidi ya hayo yanayothibitisha kuwa Mungu ana nafsi moja tu .

Sasa acha kwa ufupi tuone nafsi nini kulingana na Biblia ;
Nafsi kwa namna ya kuelewa kirahisi ni Mtu mwenyewe Mwanzo 2:7
[7]BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Sasa tunaweza kusema mfano kuna watu wawili maana yake ni nafsi mbili yaani watu wawili Mwanzo 46:15
[15]Hao ndio wana wa Lea, aliomzalia Yakobo katika Padan-aramu, na Dina, binti yake. Nafsi zote za wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu.
Kutoka 1:5
[5]Na nafsi zile zote zilizotoka viunoni mwa Yakobo zilikuwa ni nafsi sabini; na huyo Yusufu alikuwa huko ndani ya Misri tangu hapo. Unaona katika maandiko badala ya kusema watu inasema ''Nafsi'' maana vyote ni sawa na ndio maana sisi tumeumbwa kwa mfano wa MUNGU yeye ana nafsi moja na sisi tuna nafsi moja.
KWA HITIMISHO ;Huyo MUNGU Mwenye nafsi moja si mwingine bali ni BWANA YESU KRISTO Tito 2:13-14
[13]tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;
[14]ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.
NB Ndugu zangu leo hii madhehebu ndio njia shetani anatumia kuwapoteza watu mapokeo hayaokoi bali ni Neno la MUNGU la kweli lisilo pita.
Nimekupata mkuu... changamoto kila mtu anakuja na concept yake tofauti hakuna common ground nashindwa kujua nichukue ipi
 
Kwa jibu hili. Unataka uambiwe Kuhusu Mungu katika imani ya kikirsto ili upate nini?
Kwa nini usingeleta elimu kuisemea imani yako?
Naweza nikaingia kwenye ukristo mkuu lengo ni kujua msingi wa dini ya kikristo au nikosa?
 
Ninachojua mimi ni kwamba Mungu ni mmoja, hana baba wala mama, hakuzaa wala hakuzaliwa, hana umbo wala mfano. Yeye ni Mungu wa wote, habagui dini wala kabila.
 
Back
Top Bottom