Wanachama UN wapiga kura mzozo wa Urusi - Ukraine

Wanachama UN wapiga kura mzozo wa Urusi - Ukraine

Mbona unasimama na Israel dhidi ya Palestina na waarabu wengine wakati Marekani yuko nyuma ya Israel?!

Jifunze kujadili mambo katika uelewa unaoeleweka halafu ujifunze kufananisha na kulinganisha vitu vinavyofanana. Habari zako za kumlinganisha kobe na chui kwenye mbio zinaboa

Kwa kukusaidia zaidi zijue sababu za America kumsupport Ukraine uzijue na zile zinampelekea kumsupport Israel ili ujenge hoja kwa kutazama hali halisi na sio taifa kama taifa
 
Maamuzi katika vita kuli ya pili ya Dunia tulipo jinasibisha kuwa ni/tu nchi isiyo fungamana na upande wowote, hili limetuathiri kama nchi mpaka leo.
Salsa tumejiingiza katika mtego mwingine.

Sisi (Watanzania) ni "NDUMIRAKUWILI".
 
Kwa hiyo kwa sababu tu Marekani yupo nyuma ya Ukraine, ni heri kwako waendelee kuuliwa?

Hakuna niliposema Ukraine wauwawe. Nilichosema mwanzo kabisa hicho hapo chini
Kama nchi hatufungamani na upande wowote, ila wananchi mmojammoja wana maoni yao

Mungu Ibariki Tanzania

Mungu wabadilishe viongozi wa Russia na Ukraine mioyo yao watafute Suluhu nje ya vita

Tuelewane
 
Kumepigwa kura UN kuhusiana na nani ni nani kwenye uvamizi wa Ukraine.

Upande wa Russia kuna North Korea, Syria, Belarus na Eritrea.

View attachment 2137041

Kwa mujibu wa Tutu na bwana Martin Luther yumkini na sisi tumewakilisha:

View attachment 2137034

View attachment 2137035

Source: NPR Cookie Consent and Choices
Tanzania ya sasa ni boya tu! Waziri wetu wa nje naye kama mtoto anayejifunza kuongea. UNawezaje kujitokeza vita hii wakati vita ya Libya tulikuwa kama mabwege tu
 
Tanzania ya sasa ni boya tu! Waziri wetu wa nje naye kama mtoto anayejifunza kuongea. UNawezaje kujitokeza vita hii wakati vita ya Libya tulikuwa kama mabwege tu

Zimekwenda zama za rais Julius Nyerere Waziri mambo ya nje Ben Mkapa.

Zimekwenda zama za South South Commission.

Zimekwenda zama za nchi zisizofungamana na upande wowote za akina rais Tito.

Zimekwenda zama za Tanzania yenye kuheshimika kimataifa.

Zimekuja zama za watu tokea majalalani.

Tutegemee nini hapo?
 
Wewe ulitaka tusemaje? Na kwa sababu zipi?
Sheria za kimataifa na za kiasili zipo wazi. Mrusi kamvamia Ukraine ilihali Ukraine hajafanya chochote dhidi ya mamlaka ya Urusi.

Sababu za kusema Ukraine kutaka kujiunga na NATO kunahatarisha usalama wa Urusi, ni falsafa duni na ya kufikirika. Ukraine, kama nchi ina mamlaka ya kujiunga na jumuia yoyote alimradi havunji sheria za kimataifa.

Urusi imajaza makombora ya nuklia, je nchi nyingine zinazopakana na Urusi hazipo kwenye hatari kutokana na Urusi kumiliki makombora hayo? Je, mataifa hayo yana haki ya kuua raia wa Urusi?

Urusi inaendesha primitive politics ambazo hazikubaliki na mtu yeyote mstaarabu, mwenye hekima na akili timamu.
 
Sheria za kimataifa na za kiasili zipo wazi. Mrusi kamvamia Ukraine ilihali Ukraine hajafanya chochote dhidi ya mamlaka ya Urusi.

Sababu za kusema Ukraine kutaka kujiunga na NATO kunahatarisha usalama wa Urusi, ni falsafa duni na ya kufikirika. Ukraine, kama nchi ina mamlaka ya kujiunga na jumuia yoyote alimradi havunji sheria za kimataifa.

Urusi imajaza makombora ya nuklia, je nchi nyingine zinazopakana na Urusi hazipo kwenye hatari kutokana na Urusi kumiliki makombora hayo? Je, mataifa hayo yana haki ya kuua raia wa Urusi?

Urusi inaendesha primitive politics ambazo hazikubaliki na mtu yeyote mstaarabu, mwenye hekima na akili timamu.



Sema ukweli buana. Huyo mrusi kamvamia Ukraine bila Ukraine mwenyewe kumchokonoa??

Ukraine wameingizwa mkenge na America

Na sasa America wenyewe wametulizwa na Putin haswa baada ya Kim na China kuwa wakweli

Mungu saidia marais wa Ukraine na Russia wapate mioyo ya huruma kwa watu wao na ufahamu wa kuwajua maadui zao
 
Kama nchi hatufungamani na upande wowote, ila wananchi mmojammoja wana maoni yao

Mungu Ibariki Tanzania

Mungu wabadilishe viongozi wa Russia na Ukraine mioyo yao watafute Suluhu nje ya vita
Maccm hamtabiriki mmemsaliti dikteta mwenzenu rassia
 
Hakuna niliposema Ukraine wauwawe. Nilichosema mwanzo kabisa hicho hapo chini


Tuelewane
Mama D, inaonekana hukuelewa hata falsafa ya kutofungamana na upande wowote.

Fuatilia msimamo wa Tanzania kwa mambo yanayofanana na haya ya Ukraine.

Kutofungamana na upande wowote, haikumaanisha kutokuwa na msimamo uovu unapotokea, bali ni kutofungwa na blocks zile kubwa mbili. Ni kuwa na maamuzi yetu kufuatana na tukio. Kama tunaamini mauaji ya raia ni tukio baya, litakuwa ni baya bila ya kujali tukio hilo limefanywa na block ipi dhidi ya ipi.
 
Ni upuuzi mkubwa kwa Tanzania kushindwa kupiga kura kwa jambo lililo wazi ka hili. Ni aibu kubwa!!

Tanzania ya Mwalimu, haikuwahi kuwa na kigugumizi katika sualq lolote linalohusu haki. Tulikemea kwa haki na kuoiga kura dhidi ya Israel pale Israel ilipowaua raia wqkqti wanawashambulia wapiganaji wa kipalestina, licha ya kwamba israel ilikuwa imetufanyia mambo mengi: kutujengea UDSM, mafunzo ya JKT, mafunzo ya makamanda wetu, na hata miradi ya kilimo.

Tusifikiri tupo salama sana kwa kujifanya popo. Tutasuswa na wote.
KAA KMYA
 
Silence sometimes is betrayal

IMG_20220201_083950_789.jpg
 
Sema ukweli buana. Huyo mrusi kamvamia Ukraine bila Ukraine mwenyewe kumchokonoa??

Ukraine wameingizwa mkenge na America

Na sasa America wenyewe wametulizwa na Putin haswa baada ya Kim na China kuwa wakweli

Mungu saidia marais wa Ukraine na Russia wapate mioyo ya huruma kwa watu wao na ufahamu wa kuwajua maadui zao
Ninaamini una uelewa wa kutosha. Usisikilize habari za vijiweni. Ukraine amefanya nini dhidi ya Russia? Nimekaa kidogo Urusi, Ukraine, Poland, na zaidi nchi za Magharibi.

Hivi unafahamu kuwa si mara ya kwanza Russia kuivamia Ukraine, na kufanya mauaji? Kwenye ule uvamizi wa mwanzo, Ukraine hakuwa member wa NATO wala EU.

Ukifuatilia, utajua wazi kuwa mataifa yale yaliyokuwa chini ya USSR, yalijitenga na Russia bila Russia kutaka. Baada ya kujitenga, Urusi ilitaka iendelee kuwa na mamlaka juu yake, na kuyaamlia nani awe Rais, nani awe rafiki yao, na nani awe adui wao. Katika members wote waliokuwa chini ya USSR, ukiiacha Russia, ni Ukraine ndiyo iliyo na potentials nyingi kuliko mwingine yeyote. Hali hii haimpi Mrusi amani. Na Ukraine baada ya kuumizwa na Urusi safari iliyopita, imekuwa ikihangaika sana kuingia NATO ili ipate hakikisho la kutoingiliwa na Urusi. Jambo ambalo Urusi haitaki. Urusi imekuwa ikitaka kuimega sehemu ya Ukraine ili kupunguza nguvu ya Ukraine. Na imefanya hivyo kwa kupandikiza makundi yanayotaka kujitenga na Ukraine, mashariki ya Ukraine.

Maisha ya raia wa Ukraine yanazidi kupotea, lakini lengo la Urusi halitafanikiwa. Marekani, China, pamoja na nguvu zote, waliishindwa Vietnam, ndivyo itakavyokuwa kwa Urusi.
 
Back
Top Bottom