Wanaume wengi wa dini ya kiislamu ni waaminifu kwa wake zao

Kitu ninachokipenda kwa waislam, ni suala la maadili, ikiwemo mavazi. Huwezi kukuta binti wa kiislam aliyefunzwa vyema akiwa kavaa hovyo hovyo tuu mtaani, japo wapo wa imani nyingine pia wanavaa kwa stara. Kikweli, I admire it.
Hayo mengine nadhani ni tabia tu ya mtu.
 
Ukiniambia wanawake wa Kiislam wengi wao watiifu kwa waume zao hapo na kuelewa, ila wanaume anauwezo wa kuacha asaubuhi jioni anaoa mwengine.

Mabinti wakiislam wengi wao watiifu sana kwa waume zao.Mimi 50+ ya marafiki zangu wa kislam niliokuwa nao kitaa washaoa oa na kuacha sasa hivi wapo na wanawake wengine,sitowashangaa wakiwaacha sababu tabia zao na zijua.
 
Wewe ndio huwa unawachunguza wakiwa faragha?
 
Wala sijaolewa mathna, uzuri dini naijua, kuolewa mathna ni chaguo langu....nazungumzia hao wanawake wasio na elimu ya dini wanavyonyanyaswa.
Na hao ndo wanaumia kwa vile hawana elimu ya kutosha.
 

Naunga mkono hoja
Kuna mbunge mmoja Nchini Kenya (Mama ambaye hata sio Muislam) alisimama Bungeni na kusema;
Waislam wanadhamini Ndoa kuliko madhehebu mengine na hata wakiwa na Michepuko ila kwao Ndoa ni kipa umbele. Alisema mifano ipo wazi na akatoa mfano mmoja kuwa; Nairobi inaongoza kwa kuwa na watoto wadogo waliotelekezwa mitaani kwa mamia kama sio maefu na Single mother, ila ukienda mji kama Mombasa ambapo ni mji mkubwa tu/ulioendelea vizuri ambapo asilimia kubwa ya wakaazi ni waislam, tatizo la watoto wa mtaani na single mother ni dogo sana.
Alilisema; watu waache unafiki wakujidanganya kuwa wameoa mke mmoja huku wamezaa na kutelekeza watoto huko mitanaani; hiyo dhambi ni kubwa zaidi.....
 
Hapa watu wanabisha tu...SI Bora mwanaume aliyeoa wake watatu na anahudumia watoto/mke kuliko Hawa wanaozaa hovyo na kutelekeza watoto ambao hata yule baba akifa watoto hawajulikanj wala nini..
Mi naona Bora sana ndoa za waisilamu na wake zao pia wanatunzwa sana
 
Atuulize sie wanawake wa kiislamu[emoji1787][emoji1787][emoji1787] mwanaume WA kiislamu mtamu akiwa hana hela, kosa apate hela....anajikuta mwarabu anataka aoe shombeshombe[emoji1787] na huna cha kumwambia anajificha kwenye kivuli cha dini.
Nilijua ni huyu wangu tu akipata hela anabadilika ,kumbe wapo wengi.
 
Mh unaongea kama unagadithiwa vile
 
Wanaume wengi waislam wanaogopa na kuipinga waziwazi zinaa kuliko wakristo
Emu anza upya research yako na hio survey jaribu kuiweka sawa itakua hujawajua vizuri, dini sio mtu dini ni dini na mtu ni mtu usichanganye hivyo vitu viwili sehemu moja utalia mdomo juu km mbwa alienasiwa kwa nyuma
 
Huwajui hawa makobazi vizuri.
 
Unaota we mdada
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…