Habari za jumapili wakubwa.
Juzi kati nikamtembelea jamaa yangu flani hivi ni msukuma anaishi nje kidogo ya mji.
Ebana sijawahi kuona watu wanakula kama hawa watu.
Imeletwa nguna ya watu watatu tu mezani lkn hiyo nguna kwa wanaume wazembe kama wa dar wangeweza kula mwezi mzima.
Tumepiga nguna weeeee me nikasarenda nikawaacha wenyeji wakaisukuma mpaka ikaisha nikabaki mdomo wazi tu.
Ndugu zangu punguzeni huu ulaji wa hovyo namna hii.
Aisee hadi mimi nilishangaa kuona binti mdogo tu ameshusha mzigo mithiri ya gogo asee😂😂Wanaona sifa kula chakula kingi, wanasema kwao hakuna njaa wanalima sana. Mtoto mdogo anaanza kulishwa chakula kingi ili tumbo lipanuke awe anapakia chakula kingi hatimaye akiwa mkubwa awe na umbo kubwa. Mshangao ni pale wakienda chooni mtu anashusha kimba la kilo mbili! Kwa ulaji huo choo kitaachaje kujaa haraka?
Na ndugu zao wanyaturu wanakula kama mchwa
kabisa mkuu, usukuman wanawake wenye vitambi kama uchagan hakuna na watu wanakula chakula cha asili wana nguvu nyingi na ni imara hata akizeeka, nimewahi kukaa na wasukuma nakuunga mkono uliyosema ni ya kweli.Chooni huwa unafuatilia.
Binafsi mimi ni Msukuma, kwa miaka 15 liyopita nimehamia Uchagani huku. Na niko huku nakula kama niliyokua nakula nyumbani. Tunatwanga ugali maziwa, na mboga za kutosha.
SIna overweight km wanaokula kidogo.Huku wanawache wanavutambi ila usukukumani hakuna mwanamke mwenye kitambi.
Maisha ni zaidi ya kula, wabongo tujaribu kuwa na imaginations pana zaidi ya kuzaa na kushiba tu.Binafsi isingekuwa haya maisha ya Kisasa na kufata mambo ya Dini ya Mke mmoja, ningeshakuwa na Watoto 20 saivi
Ukienda Vijijini unauziwa ekari 50 Kwa shilingi milioni 2.5 tu, wastani wa ekari Moja shilingi 50,000
Hapo ukijenga yale maboma kila Mke na boma lake, Kila boma umefunga Umeme wa Solar kwaajili ya mwanga
Wakati huo umenunua majembe ya kuvutwa na ng'ombe, ni mwendo wa kulima tu
Chakula hakikauki ndani, magunia na magunia
Siku hizi Elimu ni bure, watasoma kuanzia Shule ya msingi hadi wanafika Chuo Kikuu ambapo wanakutana na boom la Serikali
ugali wa kinyaturu unafanana ugumu na ugali wa kisukuma, ugali wa uwele ndio ugali asilia wa kinyaturu, akibadilisha ni ugali wa mtama, ugali wa mahindi haushibishi vema, uwele unakaa muda mrefu tumboniNa ndugu zao wanyaturu wanakula kama mchwa
Soma Biblia, Ibrahim Baba wa Imani alikuwa na Watoto wangapi?Maisha ni zaidi ya kula, wabongo tujaribu kuwa na imaginations pana zaidi ya kuzaa na kushiba tu.
Hatuishi tena zama za Biblia au karne ya 7 enzi za Muhammad.Soma Biblia, Ibrahim Baba wa Imani alikuwa na Watoto wangapi?
Mfalme Suleiman alikuwa na Watoto wangapi
Mtume Mohamed SWS, alikuwa na Watoto wangapi
Maisha yafaa nini kama hatuli na kuzalisha ili Koo zetu ziendelee
Nyumba huanza na msingi, hiyo ilikuwa ni misingi tuliyoachiwa na Mitume wetu, ni lazima tuifateHatuishi tena zama za Biblia au karne ya 7 enzi za Muhammad.
Sio lazima muifuate, mnaamua wenyewe kuifuata au kutoifuata kwa kuangalia uhalisia, pia itafika wakati nyakati na hali halisi zitawafanya mshindwe kabisa kuifuata.hiyo ilikuwa ni misingi tuliyoachiwa na Mitume wetu, ni lazima tuifate
Watu awajui kuwa injini ya tractor ni tofauti na injini ya ISTJe, kuna namna yyte ulaji wao unawasababishia njaa? Mkuu ebu kuwa na hoja basi yaani unataka msukuma ambaye akienda shambani saa kumi na mbili asbuhi natoka saa kumi na moja jioni huku amelima nusu heka ale sawa sawa na mtu ambaye amekaa ofisini au kijiweni? Unajua nguvu alizopoteza? Maana nyie watu wa daslamu mnakoelekea utasema waanze na kula sembe dona sio chakula.
Kila mtu aishi kwenye mfumo wake wa chakula na ndio matabaka ya maisha wewe hapo unakula kidg unajiona mjanja wakat kuna watu wanakushangaa pia