Watanzania tujiulize Maswali muhimu ya Kibiashara kuhusu bandari zetu kwa dunia ya leo

Watanzania tujiulize Maswali muhimu ya Kibiashara kuhusu bandari zetu kwa dunia ya leo

Ww utakua umeolewa huko uarabuni, maana unawahusudu sana hao masultan
Tuwe na lugha za kuheshimiana kwenye huu mjafaa mkitaka lugha za kuoana kuna jukwaa la mahusiano, hata mimi nimetangaza huko, jionee:

 
Leo tuwache jazba, kejeli, matusi na ujinga. Hii kwa pande zote mbili, zinzoona DP World haifai na zinazoona DP World inafaaa tujadiliane kiustaarabu tuone "options " zetu ni zipi, zile zenye faida tuishauri serikali izifate, zile zisizo na faida tuishauri serikali isizifate.

Kama una jibu au majibu sawa, kama hauna majibu bali una swali lako pia, uliza tulijadili. Maswali na majibu yawe mafupi ili mjadala unoge.

Wale wa zamani tujikumbushe mijadala ya Jambo Frums ilivyokuwa inanoga na wale wa sasa wapunguze jazba.

Uongozi wa JF, @moderators tunahitaji muulinde huu uzi kwa uwepo wenu wa karibu, ili mjadala uende vizuri. Au nipeni u moderator wa mjadala huu tu ili niuendeshe inavyopaswa, mkiona siuendeshi kwa haki, mauodoa u miderator wangu.

Tuwe great thinkers ambao hata mtu atakaesoma huu mjadala aseme aaah, hyu ana point, aah huyu hili tumeliona.

Tuwe na maswali mengi ya kujiuliza lakini tujikite kwenye mada. Nalianzisha:

1) Sasa hivi nielewavyo mimi DP World wala Dubai hawaendeshi bandari yetu yoyote, kweli siyo kweli?

Kasome kwanza MoU ndiyo uje kuandika hapa. Hakuna watu ambao hawaipendi DP World. Yaliyomo kwenye hiyo MoU ndiyo baadhi ya watu wanaona yana ukakasi.
 
Sasa hata hayo unayotaka tuyazungumzie hayana nafasi kwasasa maana hatuyajui mkataba unasemaje.
Upo sahihi kabisa, tusubiri mikataba. Maana ni mikataba mingi sana ijayo, bandari inahusisha mabao mengi sana.

Hapa ndiyo kama hivyo tunaelemishana, labda kwanza ulifikiri mkataba upo, sasa itakuwa umeelewa kuwa kinachosubiriwa ni mikataba.

Kwa kuwa hii ni biashara kubwa na inawagusa wengi ambao wanafaidika na hali, kwa hiyo lazima fitina zinakuwa kubwa.

Wengi wanapinga lakini ukiwauliza unachokipinga nini, kimya. Au wanajibu "ukakasi", sasa kama kuna ukakasi si waweke chumvi. Swali moja tu lipo post namba moja na nimelirudia humu mara chungu nzima, hakuna anaelijibu. Mpaka najiuliza, kwanini?
 
Upo sahihi kabisa, tusubiri mikataba. Maana ni mikataba mingi sana ijayo, bandari inahusisha mabao mengi sana.

Hapa ndiyo kama hivyo tunaelemishana, labda kwanza ulifikiri mkataba upo, sasa itakuwa umeelewa kuwa kinachosubiriwa ni mikataba.

Kwa kuwa hii ni biashara kubwa na inawagusa wengi ambao wanafaidika na hali, kwa hiyo lazima fitina zinakuwa kubwa.

Wengi wanapinga lakini ukiwauiza unachokipinga nini, kimya. Swali moja tu lipo post namba moja na nimelirudia humu mara chungu nzima, hakunn anaelijibu.
Mi ninavyojua huyo mwarabu katangulizwa na mmarekani ila cc akili ndogo tunafikiri tumewin
 
Pantosha

Mbona unaniwekea maneno yako kwenye post zangu? Tafadhali zifanyie editing.
 
Mi ninavyojua huyo mwarabu katangulizwa na mmarekani ila cc akili ndogo tunafikiri tumewin
Upo huru na fikra zako. Hakuna kisichowezekana.

Kikwete aliwahi kusema "kula uliwe".
 
Mkuu 'Proved':, nashukuru kwa kunialika hapa kwenye mada hii, ambayo mwanzilishi wake..., aaahaaa; acha nisiende huko.

Kaandika vizuri, sasa sijui kama kweli anatafuta ufumbuzi wa haya maswala mazito yanayotukabili sasa hivi kama taifa, au ni gheresha tu, kama aliyofanya kwenye ile mada nyingine inayofanana na hii.

Maoni yangu (mchango) wangu kwenye maswala ya namna hii ni rahisi kabisa na wala sina kusita juu yake.

DP World, au mwingine yeyote anayetafuta biashara ya kuja kufanya hapa kwetu, akipata faida halali ya kazi yake , nasi tukipata manufaa ya uwekezaji wake bila kuhatarisha mali zetu... anakaribishwa sana.

Sijui kama kuna mTanzania anayekataa jambo kama hilo.
Mzozo uliopo na unaokwepwa kama ukoma na hawa wenzetu wanaokomalia huyu DP World, ni kama kwamba ni huyo huyo pekee ndiye anayeweza kufanya kazi hiyo kwa ufanisi, na hakuna mwingine yeyote anayeweza kama yeye. Kuweka ushahidi juu ya hili, ni kuwa huyu DP World hakushindanishwanna mwingine yeyote katika kuwania kazi hiyo.

Mbaya zaidi, ni hapo waTanzania wanaposoma yanayoitwa "Makubaliano" yaliyofikiwa baina ya Tanzania na hiyo nchi nyingine, anakotoka huyo DP World.
"Makubaliano" ambayo wengi wanayatafsiri kama "Mkataba" yanayo 'demand' kwa Tanzania kufanya mambo ambayo haijawahi kuyafanya tokea nchi yetu iwe huru. Haya ndiyo yanayowastua watu wengi na kuhoji, na sasa kupiga kelele kabisa kwa hofu kuwa raslimali zetu zinauzwa kwa wageni bila ya uwepo wa ukomo, na kupitia katika hali hiyo, nasi raia tunaingizwa kwenye mpango wa kuwatumikia hawa wageni kama watumwa wao.

Acha nisiandike mengi, kwa sababu hapa ninatiririka tu bila kupumua.

Nimalize kwa hili ninalolichukulia kuwa la muhimu zaidi kuliko yote niliyoandika huko juu; nalo ni hili:

Nchi yetu tumepata uhuru tokea 1961, tuna umri zaidi ya miaka 60 sasa. Sisi kama binaadam ni watu wenye umri mkubwa sasa.
Ninasikitika sana kwa viongozi wetu kutoona maana ya umri wetu huu. Tutakuwa wategemezi wa kufanyiwa mambo yetu, hata madogomadogo kama haya ya kuendesha bandari hadi lini?
Ni lini sisi tutaanza kufikiria angalao kujijengea uwezo, hata kama ni taratibu ili lengo likiwa kufanya mambo yalliyomo katika uwezo wetu?

TICTS tumekaa naye hapo bandarini takribani zaidi ya miaka 20 hivi. Hatukujifunza chochote kutoka kwake katika muda wote huo? Hii kazi ya bandari inaugumu kiasi gani hicho?

Hapana. Ninafahamu wapo waTanzania wenye uwezo kabisa wa kufanya kazi pale bandarini, ni wao wanaofanya kazi zote hadi sasa.
Juzijuzi tumesikia sifa bandari yetu ikionyesha ufanisi katika kazi zao. Serikali ilizisikia hizi habari? Serikali ilifanya juhudi gani kuwatia moyo hawa wazalendo ili ufanisi zaidi uendelee kuwepo hapo bandarini?

Tunachosikia sasa ni "mifumohaisomani", ndiyo maana lazima tumlete DP World asomeshe mifumo..., kwa masharti gani? Kuuza raslimali za waTanzania na kuwapeleka utumwani?

Watu wanasema hatuna pesa za kuwekeza pale, sawa; lakini mbona tumekopa WB ili kupapendezesha kabla hatujagawa chee kwa DP World?

Viongozi na watu vipofu wa akili wanasema waTanzania hawawezi kufanya chochote cha maana, ndiyo maana ni lazima tulete DP World afanye kazi.

Na mimi ninasema hivi, kwa mantiki hiyo hiyo, tunahitaji kuwaondoa akina Samia na serikali yake yote, tulete wenye uwezo wa kuendesha serikali kwa ufanisi zaidi.

Ukiona makosa humo ndani, fahamu kwamba nilikuwa ni kama nakimbia marathon wakati nikiyaandika haya.

Mkuu 'Proved', yangu ndiyo hayo. nakushukuru tena kwa kunialika hapa.
Kumbe hoja yako si bandari bali kina Samia. Umeeleweka.


Kazi ya Mungu haina makosa.
 
Bandari za tanganyika hatuwezi kukubali ziuzwe au zikodishwe na wazanzibar!
Kama ni hivyo basi ni vizuri sana kwani hata makubaliano yalikuwa ni baina ya Serikali ya Tanzania na Falme ya Dubai. Siyo Tanganyika.

Hivi Tanganyika iko wapi? Mimi sijaiona tokea mwaka 1964. Si Nyerere alimkatalia Mzee Jumbe alivyotaka kuwe na Tanganyika mpka akamtowa kwenye Urais wa Zanzibar?

Sisi tunafahamu chadema kizingiti chao ni kura za Zanzibar, ndiyo maana hawaitaki kabisa Zanzibar. Kama wewe ni chadema nakushauri muwahini Ali Karume, mtakuwa mmeshamaliza kazi. Lakini hapa kwenye bandari hata Mmarekani mwenye hisa zake Dubai hatokubali. Na hivi alivyofurahi kampuni ya Kichina kuondolewa pale banarini, ndiyo kabisa.

Na G55 kama unawakumbuka, si walizimishwa madai yao ya Tanganyika na Nyerere au ulikuwa bado siku hizo?

Kuirudisha Tanganyika ni mpaka wakubali walioruhusu ifutwe kwenye uso wa dunia. Mmarekani na Muingereza.
 
Lione swali lililoulizwa, unalo jibu au una swali lako tulijadili? Au mawazo yako tuyajadili. Hao wanaoona "haya" achana nao.
Hebu tupe kidogo ukomo wa makubaliano yaliyofikiwa. Ni kile kipengele kinachosema mpaka shughuli za bandari zikome? Halafu una justify vipi kukodisha bandari zote nchini? Hii wewe unaona sawa? Mikataba yeyote midogo itakayokuja lazima iwe ina comply na.makubaliano mama.
Jambo jengine, unadhani mkataba kama huu kwa maslahi na mustakbali wa nchi, ukizingatia uwekezaji uliofanywa, kwamba ujadiliwe tu bungeni na kuridhiwa ndani ya siku moja? Kulikuwa na uharaka gani? Unatafakari vitu kama hivi?
Eti kwamba tuuridhie kwanza halafu ndo tutumie nguvu kubwa kutoa ufafanuzi kwa hoja mbalimbali za.wananchi? Kwa maslahi ya nani?
 
Waulize wao serikali wameshindwa nn kuiboresha hii bandari kama Mombasa wameweza?.
Hata Mombasa kwa sasa wanaendesha kusogeza siku, wanajenga kwa mkataba bandari mpya kubwa zaidi huko Lamu.

Dunia ya biashara ya bandari imebadilika sana. Ina ushindani mkubwa sana. Kama hauna mitaji mikubwa hufiki popote, utabaki kuambulia vimizigo uchwara tu. Tanzania leo unaweza kuagiza mali kutoka Ulaya basi ukaipata baada ya miezzi minne. Wakati inatakiwa ndani ya 14 ikichelewa sana mwezi mmoja tu uwe umeshapata mzigo wako. Unafahamu sababu zake?
 
Kwanza hakuna mtu hata mmoja mpaka sasa niliyemsikia akipinga uwekezaji wa DPW kwenye bandari zetu, kinachopingwa ni baadhi ya vipengele vinavyompa muwekezaji mamlaka makubwa kuliko wenye mali huku faida hazijawekwa wazi.
 
Huwezi ukajadili jambo na mtu aliyetanguliza chuki,hii issue wengi wanaendeshwa na chuki tu na ubaguzi,

Subiri uone wakakavyokuja na matusi badala ya kujikita kwenye hoja.

Naona wameshaanza maneno maneno, ndio maana wanaDP WORLD wamewafungia kukomenti kwenye page yao, si unawajua watanzania mkuu, wengi wao nimefuatilia komenti zao wanatukana wanadhani ile page ni ya udaku.


Asanteni sana dp world kuwablock
 
Huo ndiyo ukwe;i, hakukutana nae kwa bahati mbya, Tanzania walishiriki hayo maonesho na Mama alitembelea, na kwa protokali kaenda makamo wa Rais ikabidi apokewe na Makamo wa Rais.

Mbona hilo kawaida sana kwenye maonesho makubwa ya kibiashara. Hata sabasaba Tanzania tumeshapoke Marais na viongozi wengi wa duniani.

Unafikiri sababu za nchi kutumia mabilioni kufanya maonesho ya kibiashara ni zipi? Uende wewe ukanunuwe pipi?

Unaona ajabu kitu amabcho kipo dunia nzima. Dah Watanzania mna maajabu sana.

Wewe hujawahi jutenbelea maonesho ya sabasaba au nanenane au mara kwa mara Dar Diamond Jubilee tunatangaziwa leo Syria wana maonesho, leo Turkey wana maonesho siku nyingine KOREA WANA MAONESHO.

Kwa kukujuza tu, stendi yote ya mabasi ya zamani ya Ubungo sasa hivi ni maonesho ya boiashara za Wachina, wanakwambia China imehamia Tanzania. Uanfikiri ni wajinga wale? Rais wako hatotembelea pale, wewe hutotembelea pale, viongozi wa nje hawatotembelea pale?
Acha UONGO!! Dubai Expo 2020 imefanyika 2021 kwa sababu ya Corona.
Screenshot_20230709-065406.png
 
Leo tuwache jazba, kejeli, matusi na ujinga. Hii kwa pande zote mbili, zinzoona DP World haifai na zinazoona DP World inafaaa tujadiliane kiustaarabu tuone "options " zetu ni zipi, zile zenye faida tuishauri serikali izifate, zile zisizo na faida tuishauri serikali isizifate.

Kama una jibu au majibu sawa, kama hauna majibu bali una swali lako pia, uliza tulijadili. Maswali na majibu yawe mafupi ili mjadala unoge.

Wale wa zamani tujikumbushe mijadala ya Jambo Frums ilivyokuwa inanoga na wale wa sasa wapunguze jazba.

Uongozi wa JF, @moderators tunahitaji muulinde huu uzi kwa uwepo wenu wa karibu, ili mjadala uende vizuri. Au nipeni u moderator wa mjadala huu tu ili niuendeshe inavyopaswa, mkiona siuendeshi kwa haki, mauodoa u miderator wangu.

Tuwe great thinkers ambao hata mtu atakaesoma huu mjadala aseme aaah, hyu ana point, aah huyu hili tumeliona.

Tuwe na maswali mengi ya kujiuliza lakini tujikite kwenye mada. Nalianzisha:

1) Sasa hivi nielewavyo mimi DP World wala Dubai hawaendeshi bandari yetu yoyote, kweli siyo kweli?
Kwanza Faiza huwezi endesha mjadala huu maana msimamo wako unajulikana unaunga mkono kutwaliwa milele kwa bandari kwa kivuli cha uwekezaji. Pili wale wanaoupinga tayari wametishiwa maisha yao, na tayari moja ameponea chupuchupu kwenye jaribio la utekeji. Hivyo kuweka hoja hapa za kupinga utwaliwaji milele wa Bandari kwa malipo yasiyojulikana ni kujihatarishia uhai. Tatu waziri wa mambo ya ndani ameonya wale wanaotumia lugha za matusi kwenye mjadala huu. Ukweli watu wazima wanajua ni kawaida CCM wakizidiwa hoja utaona waziri wa mambo ya ndani anaibuka na kuonya dhidi ya matusi, UKWELI HAKUNA MATUSI YOYOTE ni kutengeneza njia ya kuwakamata na kuwababimbikia kesi wakosoaji. Mwisho hoja za kina kitenge, Steve Nyerere, Manara, Zembwele za kuunga hoja za utwaliaji milele kwa malipo yasiyojulikana tumezisikia, DHIDI ya Hoja za Proffesa Shivji, Lissu, Mbowe, Tibaijuka, Mawakili, Maaskofu nk.
Sentesi ya mwisho ni ya muhimu zaidi unless ni mwathirika wa CCM mentality ya kuunga mkono kila kitu bila ya kutumia neema ya akili uliyojaliwa na Mola wako.
 
Waziri mkuu alisema, TICTS haikuwa na ufanisi unaoridhisha, Kwa maana hiyo DPW wamekuja kuwa mbadala wa TICTS, na TICTS mkataba wao ulikuwa na ukomo, Je DPW world ukomo wake ni miaka mingapi? wakiunderperform kama TICTS itakuaje?
 
Back
Top Bottom