Wazazi Mnaosomesha Watoto Shule za Private jifunzeni kufanya tathmini ya Pesa mnayowekeza katika Elimu hiyo na matokeo yake (Hawatazeekea Nyumbani)?

Tofautisha international schools na English medium, Na mleta hoja kasema ni bora mwanao aende international schools mfano hyo IST… na sio hzo Ems ambazo ni kayumba zilizochangamka.
 
Tunashukuru kwa maoni na ushauri wako.
Kila mtu atachagua mwenyewe matumizi ya pesa zake.
Kusomesha kwa gharama au kuzitunza au kuwekeza kwenye assets.
Kila mtu anafanikiwa au anakwama kimaisha kwa njia yake.
 
Maisha ya sasa ni kuchagua na kuamua.
 
Nunua kiwanja hata Kisarawe au chanika huko, huyo mtoto hadi amalize chuo kiwanja hicho hicho ulichonunua hata milioni 2 utauza hata 20M
Kisarawe hii hii, na value ya hela ya Leo na kipindi hicho inalingana?

Pia ukiweza kusomesha mtoto Ada million 2 utashindwa kweli kununua kiwanja cha million 2
Nunua kiwanja hata Kisarawe au chanika huko, huyo mtoto hadi amalize chuo kiwanja hicho hicho ulichonunua hata milioni 2 utauza hata 20M
 
Hadhi ya mtoto huku anazidiwa IQ na mtoto aliyesoma Kayumba?
we ungekua na hiyo IQ ungeelewa nilichoandika.
nilisema hadhi ya mzazi.

pia kuna suala la usalam, imagine, mtoto wa mtu kama Mafwele alivyovuma kama angekua anasoma changanyikeni, watu wangepita nae. think think
 
Heshima Gani mtoto wako mwaka wa Tano tangu kamaliza chuo anasugua rimoti sebuleni wakati wewe magonjwa ya kizee kama gout yanazidi kukunyemelea
maana yake hukua nahadhi ya kumpeleka uko. wenye hadhi hiyo watoto wao hawakosi cha kufanya.
 
Tofautisha international schools na English medium, Na mleta hoja kasema ni bora mwanao aende international schools mfano hyo IST… na sio hzo Ems ambazo ni kayumba zilizochangamka.
Wewe na mleta uzi mna urafiki wa karibu mno na umaskini. Always misery loves company.
 
kuna sababu nyingi zinafanya wazazi wanapeleka watoto wao Em ,mojawapo ni malezi.Miaka ya 90 walimu walikuwa walezi pia kwa wanafunzi ,mwl anahandle mwanafunzi kama mwanae,leo hii elimu inachangamoto nyingi shule zenyewe watoto wanakaa chini ,wewe mtoto wako anaenda na kiroba cha kukalia ,wakati mtoto wa mwenzako akifika shule anapata mkate na chai kabla ya kipindi
watoto wanapata mafunzo ya kiroho,malezi bora na heshima waangalie hata mtaani utahisi tofauti ,kayumba watoto wanapigana miti wakiwa na umri mdogo for sure
Mimi nawasomesha EM angalau wapate foundation huku chini ,serikali imeharibu elimu komaa mzee baba watoto wapate hata basic nzuri
 
Kwa hiyo return uliyoona wewe ni kuajiriwa tu? Kiukweli nakuonea huruma mno. Benj Fernandes kazaliwa na baba milionea akasoma elimu bora akaja kujiajiri kupitia elimu aliyopata na kwa sasa anafanya biashara kubwa ya kimataifa kumzidi baba yake. Kwa hiyo elewa sio lazima ukimsomesha mtoto aje kurithi biashara zako. Mtoto wa Kighoma Malima ni bingwa kwenye fani yake anapiga noti ndefu huko USA. Angekuwa na akili kama zako angerudi kurithi biashara za baba yake. Hivyo vitu vyako vitunze vije kukusaidia wewe na mkeo uzeeni.
 
utasema mnasave kumbe mnanywea na pombe na kuhonga malaya, milion 60 ni kitu gani ukitumia kwa watoto wako?

ambacho ningekuelewa pamoja na kusomesha basi tujitahidi kutengeneza mazingira ya hao watoto wanapomaliza masomo yao, ni kweli serikali haiajiri basi tuwaelekeze watoto katika kujiajiri, nawapenda wakinga watoto wao wanasoma kozi zinazoendana na kazi anayofanya mzazi utaona kozi kama BBA, BCOM, BAF, ACCOUNTING, MARKETING AND SALES, watoto wao wanasoma hizo ili kuendeleza biashara za wazazi wao, wamewafundisha watoto wao biashara siku hizi wanaoenda china kufunga mzigo ni watoto wao
 
Benj Fernandes kazaliwa na baba milionea akasoma elimu bora akaja kujiajiri kupitia elimu aliyopata na kwa sasa anafanya biashara kubwa ya kimataifa kumzidi baba yake
Sasa Baba mmiliki wa king'amuzi cha TING unategemea nini kutoka kwa mtoto? Kina Fernandes hilo jina tu linampa connection mtoto mpaka nchi za nje huko; huwezi compare huyo na sisi huku ambao urithi wetu ni vyeti vya elimu tu na sio connection wala pesa za kusoma shule za maana
 
utasema mnasave kumbe mnanywea na pombe na kuhonga malaya, milion 60 ni kitu gani ukitumia kwa watoto wako?
hiyo 60 M naongelea watu ambao wachamungu na wanapambana kweli, sio hao ambao wanataka kukwepa majukumu; naongelea watu ambao wanapambana kweli kufanikisha hichi
 
hiyo 60 M naongelea watu ambao wachamungu na wanapambana kweli, sio hao ambao wanataka kukwepa majukumu; naongelea watu ambao wanapambana kweli kufanikisha hichi
Wacha Mungu nao zinashia kwa manabii
 
Watu wangapi tunazunguka nao maofisini humu hawajajenga na wanahangaika sana kulipa ada za watoto na hata viwanja hawana?
Hio sio sawa, ada haitakiwi ikutese tena ada ya shule sio chuo.

Somesha kadri ya uwezo, kama una uwezo wa ada million 10 na mambo mengine yakaenda somesha Tu, kama kipato hakigawanyiki peleka kayumba au shule ya private ya size yako.
 
Shule sio urithi wa mtoto,mtoto inapaswa apewe urithi wa hela,mashamba,nyumba na kampuni ili aviendeleze….! Acheni utapeli wenu huko
Nani kasema shule ndo urithi? Binafsi binti yangu atasoma huko na miradi ataikuta ashindwe yeye!!! Kumpa mtoto elimu bora sio urithi ni wajibu wetu kama wazazi kumpatia hayo..... kama hela huna peleka kayumba” wewe unaamini hao wanaosomesha kayumba ndo watawapa urithi watoto wao? Ashindwe kumpa elimu bora atoe urithi!!! Anatoa wapi? Wengi wanaopiga hizi kelele kama zako kibunda hawana
 
Uamuzi wa leo utaathiri maisha ya kesho. Je, ni busara kuwekeza zaidi ya Tsh 60,900,000 kwa watoto watatu bila uhakika wa faida, au ni heri kutumia kiasi hicho kwa uwekezaji wenye uhakika wa marejesho?
Miaka ya kusoma ukiweka na chekechea ni 20
Kifupi wewe unaangukia kundi la watu maskini

Hata kusomesha tu shule za kayumba kwa kipato hicho ni changamoto

Kipato cha Milioni 60 kwa miaka 20 sio pesa nyingi

Nianze kukudhibitishia kuwa wewe maskini wa kutupwa.Tukichukua hiyo milioni 60 kwa miaka 20 ina maana kipato chako wewe kwa mwezi ni shilingi 250,000

Ukichukua hicho kipato chako cha mwezi 250,000 ukigawa kwa siku 30 za mwezi ina maana kipato chako kwa siku ni shilingi 8,300

Asubuhi tuchukilie chai mnatumia shilingi 1,300 .unabakiwa na shilingi elfu 7 kwa ajili ya chakula cha mchana na jioni .Yaani shilingi 3,500 mchana na shilingi 3 500 chakula cha jioni
Hela hata ya daftari tu au kulipa mwalimu wa tuition shule ya kayumba hapo huna hapo hujalipa umeme, maji,nauli ,kodi ya nyumba nk

Hiyo milioni 60 kwa miaka 20 mfano ulioutoa na kwa ajili ya malofa wa kutupwa sio hela hiyo ndogo mno hata kwa kujikimu tu

Ok labsa wewe tueleze kwa kujibana kwako na ubahili wako unamiliki ndege za abiria au ? Na umewapa watoto wako biashara gani za maana zinazowafanya watembee kifua mbele mjini.Umewapa nini kama fidia ya ubahili wako kuwasomesha shule nzuri?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…