Wazazi Mnaosomesha Watoto Shule za Private jifunzeni kufanya tathmini ya Pesa mnayowekeza katika Elimu hiyo na matokeo yake (Hawatazeekea Nyumbani)?

Wazazi Mnaosomesha Watoto Shule za Private jifunzeni kufanya tathmini ya Pesa mnayowekeza katika Elimu hiyo na matokeo yake (Hawatazeekea Nyumbani)?

Hao wahindi na waarabu hawasomeshi watoto wao? Kwa taarifa yako hao matajiri unaowajua wanasomesha watoto wao kwenye shule bora za gharama. Mo Dewji kasoma IST na chuo Georgetown University. Unadhani kuitoa biashara ya milioni hadi ifike bilioni itawezekana kwa hiyo elimu duni unayotaka kuwapa wanao?
Tofautisha international schools na English medium, Na mleta hoja kasema ni bora mwanao aende international schools mfano hyo IST… na sio hzo Ems ambazo ni kayumba zilizochangamka.
 
Tunashukuru kwa maoni na ushauri wako.
Kila mtu atachagua mwenyewe matumizi ya pesa zake.
Kusomesha kwa gharama au kuzitunza au kuwekeza kwenye assets.
Kila mtu anafanikiwa au anakwama kimaisha kwa njia yake.
 
Katika kila jamii, elimu hupewa nafasi ya kipekee kama nyenzo ya kufanikisha maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla. Wazazi huwekeza kwa gharama kubwa kuhakikisha watoto wao wanapata elimu bora, wakiamini kuwa elimu ni ufunguo wa maisha bora. Lakini swali la msingi linabaki: Je, uwekezaji huu unatoa faida inayolingana na gharama zinazotumika?

Katika makala hii, nitachambua gharama za kumsomesha mtoto hadi chuo kikuu, nikiilinganisha na hali halisi ya soko la ajira nchini Tanzania. Pia, nitatoa tafakari mbadala kuhusu thamani ya ardhi kama uwekezaji, pamoja na mbinu ambazo mzazi anaweza kutumia kupunguza gharama za elimu bila kuathiri ubora wa maarifa anayoyapata mtoto wake.

GHARAMA ZA KUMSOMESHA MTOTO: TAKWIMU ZINASEMAJE?

Wazazi wengi hujitoa kwa hali na mali kugharamia elimu ya watoto wao. Kwa mujibu wa makadirio yafuatayo, mzazi anayemsomesha mtoto mmoja kutoka darasa la kwanza hadi chuo kikuu anahitaji angalau:

1. Elimu ya Msingi (Darasa la 1 - 7):

Tsh 800,000 kwa mwaka x 7 miaka = Tsh 5,600,000

2. Elimu ya Sekondari (Kidato cha 1 - 4):

Tsh 1,200,000 kwa mwaka x 4 miaka = Tsh 4,800,000

3. Elimu ya Juu ya Sekondari (Kidato cha 5 - 6):

Tsh 1,200,000 kwa mwaka x 2 miaka = Tsh 2,400,000

4. Chuo Kikuu (Mwaka wa 1 - 3):

Tsh 2,500,000 kwa mwaka x 3 miaka = Tsh 7,500,000

Jumla ya gharama kwa mtoto mmoja inakuwa Tsh 20,300,000, na kwa watoto watatu inafikia Tsh 60,900,000.

Lakini je, mzazi anayefanya uwekezaji huu ana uhakika wa kupata faida kupitia ajira ya mtoto wake baada ya kuhitimu?

HALI YA SOKO LA AJIRA: UHALISIA ULIOPO

Kwa mujibu wa takwimu za Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), mwaka wa masomo wa 2023/2024 uliona ongezeko la udahili wa wanafunzi wa shahada ya kwanza kufikia 186,289 (Mwananchi).

Hata hivyo, soko la ajira haliwezi kuwahudumia wote. Takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonyesha kuwa kila mwaka nafasi za kazi mpya serikalini na sekta binafsi hazizidi 50,000. Kwa hesabu rahisi:

Wahitimu wa vyuo kwa mwaka:
186,289

Nafasi za ajira zilizopo: 50,000

Wahitimu wasiopata ajira mara moja: ~136,289

Uwezekano wa kupata ajira mara moja: ~27%

Kwa maneno mengine, asilimia 73 ya wahitimu wa vyuo vikuu hawapati ajira mara moja.

Hili linaibua swali muhimu: Je, mzazi aliyelipa ada kwa miaka 16-20 anaweza kupata mrejesho wa uwekezaji wake ndani ya muda mfupi?

UWEKEZAJI MBADALA: THAMANI YA ARDHI JIJINI DAR ES SALAAM

Hebu tuchukulie mfano wa mzazi aliyekuwa akitumia wastani wa Tsh 3,000,000 kwa mwaka kwa mtoto mmoja katika elimu tangu miaka ya 1990s. Kama angewekeza pesa hii kwenye kununua viwanja jijini Dar es Salaam, leo hii thamani yake ingekuwa ya mamilioni.

Kwa mfano, mnamo 1995, viwanja katika maeneo kama Tegeta vilikuwa vinauzwa kwa kati ya Tsh 500,000 – 2,000,000. Leo hii, kiwanja cha ukubwa wa 1,200m² katika Mbweni kinauzwa kwa Tsh 85,000,000 (Jiji.co.tz).

Kwa maneno mengine, mzazi aliyenunua kiwanja miaka ya 1990s kwa Tsh 2,000,000 leo anaweza kuwa na mali yenye thamani ya zaidi ya Tsh 200,000,000.

Hii inaonyesha kuwa kuna uwezekano mkubwa wa mzazi kupata faida kubwa zaidi kwa kuwekeza katika ardhi badala ya kutegemea ajira za watoto wao kama njia ya kupata mrejesho wa gharama za elimu.

NJIA YA KUOKOA GHARAMA ZA ELIMU PASIPO KUPOTEZA UBORA

Je, kuna namna mzazi anaweza kumpa mtoto elimu bora kwa gharama nafuu?

Jibu ni ndiyo!

Njia mojawapo ni kumpeleka mtoto shule za serikali na kisha kuongeza maarifa kwa njia ya tuition.

Mfumo huu umefanikiwa katika nchi kama Kanada, ambako homeschooling na masomo ya ziada (tutoring) vimeongezeka kwa 36% kila mwaka, huku gharama ya elimu kwa mtoto mmoja ikiwa chini kwa 90% ukilinganisha na shule binafsi (Moe.go.tz).

Kwa hesabu rahisi, mzazi anaweza kutumia Tsh 120,000 kwa mwaka kwa tuition bora badala ya Tsh 1,200,000 kwa shule binafsi, hivyo kuokoa hadi Tsh 1,080,000 kwa mwaka kwa mtoto mmoja.

HITIMISHO: NI WAKATI WA KUHOJI UWEKEZAJI WETU KATIKA ELIMU

Hakuna anayepinga thamani ya elimu, lakini ni muhimu wazazi kuhoji kama njia wanazotumia kugharamia elimu zina manufaa makubwa kwa watoto na familia kwa ujumla.

Kwa kutumia shule za serikali pamoja na masomo ya ziada, mzazi anaweza kuokoa hadi 90% ya gharama za shule binafsi na kutumia fedha hizo kwa uwekezaji wa muda mrefu kama ardhi, biashara au hisa.

Uamuzi wa leo utaathiri maisha ya kesho. Je, ni busara kuwekeza zaidi ya Tsh 60,900,000 kwa watoto watatu bila uhakika wa faida, au ni heri kutumia kiasi hicho kwa uwekezaji wenye uhakika wa marejesho?
Maisha ya sasa ni kuchagua na kuamua.
 
Nunua kiwanja hata Kisarawe au chanika huko, huyo mtoto hadi amalize chuo kiwanja hicho hicho ulichonunua hata milioni 2 utauza hata 20M
Kisarawe hii hii, na value ya hela ya Leo na kipindi hicho inalingana?

Pia ukiweza kusomesha mtoto Ada million 2 utashindwa kweli kununua kiwanja cha million 2
Nunua kiwanja hata Kisarawe au chanika huko, huyo mtoto hadi amalize chuo kiwanja hicho hicho ulichonunua hata milioni 2 utauza hata 20M
 
Hadhi ya mtoto huku anazidiwa IQ na mtoto aliyesoma Kayumba?
we ungekua na hiyo IQ ungeelewa nilichoandika.
nilisema hadhi ya mzazi.

pia kuna suala la usalam, imagine, mtoto wa mtu kama Mafwele alivyovuma kama angekua anasoma changanyikeni, watu wangepita nae. think think
 
Heshima Gani mtoto wako mwaka wa Tano tangu kamaliza chuo anasugua rimoti sebuleni wakati wewe magonjwa ya kizee kama gout yanazidi kukunyemelea
maana yake hukua nahadhi ya kumpeleka uko. wenye hadhi hiyo watoto wao hawakosi cha kufanya.
 
Tofautisha international schools na English medium, Na mleta hoja kasema ni bora mwanao aende international schools mfano hyo IST… na sio hzo Ems ambazo ni kayumba zilizochangamka.
Wewe na mleta uzi mna urafiki wa karibu mno na umaskini. Always misery loves company.
 
kuna sababu nyingi zinafanya wazazi wanapeleka watoto wao Em ,mojawapo ni malezi.Miaka ya 90 walimu walikuwa walezi pia kwa wanafunzi ,mwl anahandle mwanafunzi kama mwanae,leo hii elimu inachangamoto nyingi shule zenyewe watoto wanakaa chini ,wewe mtoto wako anaenda na kiroba cha kukalia ,wakati mtoto wa mwenzako akifika shule anapata mkate na chai kabla ya kipindi
watoto wanapata mafunzo ya kiroho,malezi bora na heshima waangalie hata mtaani utahisi tofauti ,kayumba watoto wanapigana miti wakiwa na umri mdogo for sure
Mimi nawasomesha EM angalau wapate foundation huku chini ,serikali imeharibu elimu komaa mzee baba watoto wapate hata basic nzuri
 
Generational poverty mnaidumisha kwa kushindwa kukombolewa kifikra na hili jinamizi litawatafuna vizazi na vizazi
Kumpa mwanao investment kubwa ambayo guarantee ya return (kuajirika) ni chini ya 50% ni sawasawa Simba icheze na lipuli afu uchore mkeka kwamba Lipuli atashinda 5 - 0
Yaani hiyo mwanao bila hata kulipa ada kubwa hivyo unaweza ukashangaa ukamtafutia kadi ya maktaba ya mkoa akiwa kayumba huko huko tena akafanya vizuri zaidi ya hata wale wa kayumba
Kwa hiyo return uliyoona wewe ni kuajiriwa tu? Kiukweli nakuonea huruma mno. Benj Fernandes kazaliwa na baba milionea akasoma elimu bora akaja kujiajiri kupitia elimu aliyopata na kwa sasa anafanya biashara kubwa ya kimataifa kumzidi baba yake. Kwa hiyo elewa sio lazima ukimsomesha mtoto aje kurithi biashara zako. Mtoto wa Kighoma Malima ni bingwa kwenye fani yake anapiga noti ndefu huko USA. Angekuwa na akili kama zako angerudi kurithi biashara za baba yake. Hivyo vitu vyako vitunze vije kukusaidia wewe na mkeo uzeeni.
 
utasema mnasave kumbe mnanywea na pombe na kuhonga malaya, milion 60 ni kitu gani ukitumia kwa watoto wako?

ambacho ningekuelewa pamoja na kusomesha basi tujitahidi kutengeneza mazingira ya hao watoto wanapomaliza masomo yao, ni kweli serikali haiajiri basi tuwaelekeze watoto katika kujiajiri, nawapenda wakinga watoto wao wanasoma kozi zinazoendana na kazi anayofanya mzazi utaona kozi kama BBA, BCOM, BAF, ACCOUNTING, MARKETING AND SALES, watoto wao wanasoma hizo ili kuendeleza biashara za wazazi wao, wamewafundisha watoto wao biashara siku hizi wanaoenda china kufunga mzigo ni watoto wao
 
Benj Fernandes kazaliwa na baba milionea akasoma elimu bora akaja kujiajiri kupitia elimu aliyopata na kwa sasa anafanya biashara kubwa ya kimataifa kumzidi baba yake
Sasa Baba mmiliki wa king'amuzi cha TING unategemea nini kutoka kwa mtoto? Kina Fernandes hilo jina tu linampa connection mtoto mpaka nchi za nje huko; huwezi compare huyo na sisi huku ambao urithi wetu ni vyeti vya elimu tu na sio connection wala pesa za kusoma shule za maana
 
utasema mnasave kumbe mnanywea na pombe na kuhonga malaya, milion 60 ni kitu gani ukitumia kwa watoto wako?
hiyo 60 M naongelea watu ambao wachamungu na wanapambana kweli, sio hao ambao wanataka kukwepa majukumu; naongelea watu ambao wanapambana kweli kufanikisha hichi
 
hiyo 60 M naongelea watu ambao wachamungu na wanapambana kweli, sio hao ambao wanataka kukwepa majukumu; naongelea watu ambao wanapambana kweli kufanikisha hichi
Wacha Mungu nao zinashia kwa manabii
 
Watu wangapi tunazunguka nao maofisini humu hawajajenga na wanahangaika sana kulipa ada za watoto na hata viwanja hawana?
Hio sio sawa, ada haitakiwi ikutese tena ada ya shule sio chuo.

Somesha kadri ya uwezo, kama una uwezo wa ada million 10 na mambo mengine yakaenda somesha Tu, kama kipato hakigawanyiki peleka kayumba au shule ya private ya size yako.
 
Shule sio urithi wa mtoto,mtoto inapaswa apewe urithi wa hela,mashamba,nyumba na kampuni ili aviendeleze….! Acheni utapeli wenu huko
Nani kasema shule ndo urithi? Binafsi binti yangu atasoma huko na miradi ataikuta ashindwe yeye!!! Kumpa mtoto elimu bora sio urithi ni wajibu wetu kama wazazi kumpatia hayo..... kama hela huna peleka kayumba” wewe unaamini hao wanaosomesha kayumba ndo watawapa urithi watoto wao? Ashindwe kumpa elimu bora atoe urithi!!! Anatoa wapi? Wengi wanaopiga hizi kelele kama zako kibunda hawana
 
Uamuzi wa leo utaathiri maisha ya kesho. Je, ni busara kuwekeza zaidi ya Tsh 60,900,000 kwa watoto watatu bila uhakika wa faida, au ni heri kutumia kiasi hicho kwa uwekezaji wenye uhakika wa marejesho?
Miaka ya kusoma ukiweka na chekechea ni 20
Kifupi wewe unaangukia kundi la watu maskini

Hata kusomesha tu shule za kayumba kwa kipato hicho ni changamoto

Kipato cha Milioni 60 kwa miaka 20 sio pesa nyingi

Nianze kukudhibitishia kuwa wewe maskini wa kutupwa.Tukichukua hiyo milioni 60 kwa miaka 20 ina maana kipato chako wewe kwa mwezi ni shilingi 250,000

Ukichukua hicho kipato chako cha mwezi 250,000 ukigawa kwa siku 30 za mwezi ina maana kipato chako kwa siku ni shilingi 8,300

Asubuhi tuchukilie chai mnatumia shilingi 1,300 .unabakiwa na shilingi elfu 7 kwa ajili ya chakula cha mchana na jioni .Yaani shilingi 3,500 mchana na shilingi 3 500 chakula cha jioni
Hela hata ya daftari tu au kulipa mwalimu wa tuition shule ya kayumba hapo huna hapo hujalipa umeme, maji,nauli ,kodi ya nyumba nk

Hiyo milioni 60 kwa miaka 20 mfano ulioutoa na kwa ajili ya malofa wa kutupwa sio hela hiyo ndogo mno hata kwa kujikimu tu

Ok labsa wewe tueleze kwa kujibana kwako na ubahili wako unamiliki ndege za abiria au ? Na umewapa watoto wako biashara gani za maana zinazowafanya watembee kifua mbele mjini.Umewapa nini kama fidia ya ubahili wako kuwasomesha shule nzuri?
 
Back
Top Bottom