Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Jafo
Tume
CCM
Serikali

Kila hoja wanayotoa kuhalalisha mazonge yao inakosa mashiko na ndio watu wanazidi kuiona hila yao

Yani hizi wiki tatu zimekua Ni za aibu kuu kwa gvt

Pole Sana jafo ivumayo haidumu.
MANCHESTER CITY matokeo yenu tunayo
 
Namuonea huruma kwa jinsi alivyotumika duh magufuli siku ukimsikia itakuwa ni siku ya uteuzi.
 
Nimeipenda hii kauli ya Msimamizi mkuu wa uchaguzi wa serikali za mitaa Waziri Jaffo.

" Hakuna Kukimbiana Lazima Kieleweke"

Chadema msiweke mpira kwapani rudini uwanjani refa anawaita.

Maendeleo hayana vyama!

cc: Daudi Mchambuzi


..REFA mwenyewe mkereketwa wa CCM.

..Jafo hakutakiwa kuongea kishabiki namna hiyo.
 
kuna game zingine refarii unashindwa kuwa neutro Kama game ya Leo MAN CITY VS LIVERPOOL
Mkuu utawafanya watu wanune.....

Umekosa mfano mwingine wowote, Bali utoe mfano wa mechi kati ya Liverpool VS Man City
 
Wanabodi, Hakika ule usemi usemao akili sio ukubwa wa kichwa umetimia kwa huyu waziri Seleman Jafo,

Leo unaitisha vyombo vya habari kuomba wale ulioshiriki kuwafuta warudishwe kugombea, Tulishauri bandikeni majina ya wanaccm tu kwenye mbao hapa JF na umetekeleza ushauri wetu hapa JF, Tunakupongeza kwa hilo, Sasa tu nakushauri tena endelea na sera za kifashisti na kibaguzi ili wewe na kundi lako mje mvune mnachokipanda

Jafo alichagua kuwa wa moto kufuata sheria za kifashisti na kibaguzi, Jafo uliamua kuigawa jamii makundi mawili ili lengo lako la watu kupigana na kuchomeana mali lipate kutimia na umeshalitimiza baadhi ya maeneo, Uliamua kukaa kimya ulipoambiwa watendaji wanafunga ofisi hawataki kupokea fomu za vyama vingine

Jafo Leo umegeuka vuguvugu hujawa moto wala baridi, Hujui la kufanya, Mamlaka iliyokuteua imekuzidi akili, Kwa elimu yako ungeandika barua kwa mamlaka ya uteuzi upumzike, Umegeuka kituko mbele ya Jamii

Wewe ni mmoja ya wacheza ngoma wa Pwani uliepata elimu kidogo hivyo tulitegemea utaijenga jamii yako kwa fikra na mawazo, Sasa umegeuka katuni mbele ya jamii

Unaongea huku Facial impression au muonekano wake usoni ni dhahiri una mawazo mengi Sana lakini hujui hatima ya uwaziri wako

Umetumia neno mpira kwapani zaidi ya mara nne huku ukibabaika na kutetemeka wakati wa kuongea, Ni dhahiri mambo kwako ni magumu sana, Huelewi mwisho wa siasa zako za kikatili na kifashisti itakuaje? Leo umeongea kama mtu uliyebanwa sana na kivuli tusichokiona


Seleman Jafo wewe ni sadaka inayosubiriwa na maamuzi ya wananchi, Bosi wako anasubiri reaction ya wananchi Halafu wewe utatolewa sadaka kuwa hujasikiliza wananchi

Maelezo uliyoyatoa Leo yanapingana na ndugu yako Humprey pole pole aliyesema CCM na watendaji wa kata na vijiji walichofanya kuwafuta wagombea wengine ni sahihi,

Jafo unasikiliza chama au unasikiliza aliyekuteua, Kwa ufupi ulipaswa kusimamia ukatili uliouonyesha toka mwanzo na kufa na tai shingoni

Ulisahau kuwa asilimia 90 ya watanzania hawana vyama ni Raia tu wa kawaida, Wewe na kundi lako mlifikiri wale viongozi wa mitaa na watendaji wanaongoza ccm, Act na Chadema

Kumbuka kuna maelfu ya watanzania wamekua maskini, hawana ajira, Hawa hawana vyama bali uchaguzi ni sehemu ya kupunguza hasira na mawazo

Pambana na maisha ya wananchi, CCM na Chadema hamfiki hata asilimia 11 ya watanzania

Sasa waziri Jafo jamii inakutazama kama kituko ambae hujui hatma ya maisha ya siasa zako za moto
Kile kikao cha ikulu kile cha watendaji, niseme
Asante Mungu majibu yamewahi mno kutoka.
Ni 1 ya kikao ambacho mi sijui kilichojadiliwa ni nini! Chaguzi zote awamu hii tu ndo wagombea wakosee kujaza form?
Mtendaji anaenda chooni siku nzima?
Kwenye hii sarakasi ya huu uchaguzi mdogo, nishauri tu katiba mpya idaiwe na tume huru ya uchaguzi bila kusahau shughuli za kisiasa kwa vya vyote zitambulike na mihimili isiingiliane!
 
1573416506018.png
 
CCM tuitishe maandamano kumpinga Jafo. Amepora ushindi wetu wa wazi na kuwarudisha waliopewa RED CARD uwanjani.

CCM hatukubali. Tutang'oa viti vyote na kuchomoa betri.
 
Mkuu utawafanya watu wanune.....

Umekosa mfano mwingine wowote, Bali utoe mfano wa mechi kati ya Liverpool VS Man City

Liverpool kabebwa na mwamuzi hadi aibu.
Hawana tofauti na CCM.
 
Kwenye mechi ya simba na yanga......unamweka Haji Manara ndio referee unategemea nini......
 
Halafu wasimamizi ni wale wale, huyu mtu anatuona sisi wote wajinga.
 
Hahahaaaaa......!

Umenikumbusha Mchungaji Erasto: Jaffo mnamuonea bure hana sifa ya Jaji

Maendeleo hayana vyama!
Kama hana sifa ya Jaji kwanini ajifanye kuwa na kutekeleza jukumu la Jaji kwa hiari hata kwa shinikizo? Ona sasa anakejeliwa na kudharauliwa yeye huku aliyemwagiza anaendelea na kazi anayopenda ya kuteua Jumapili akiachana na kanisa maana amegundua anawa-bore waumini wengine. Ashukuru tu katika uteuzi hakutenguliwa yeyote maana angekuwa mmoja wao kwani ni wa pwani lakini hata hivyo akae chonjo maana hatma yake itategemea hatua watakayochukua wapinzani kutokana na gia aliyobadili angani. Yes, yes kila wakati bila kupima na kuhoji mantiki yake huwa na madhara makubwa. Tuendelee kusubiri lakini wapinzani wasigeuke nyuma watakuwa jiwe la chumvi siyo lile.
 
Back
Top Bottom