Waziri Mkuu: Bandari imepewa DP-World kwa kuwa utendaji wa TICTS ni mdogo
Agreement na Mkataba, tofauti ni nini? Soma wewe huko google utuambie, mimi nimesoma sijaona tofauti, maana zote zinasainiwa na ni legally binding kinyume na ukivyodanganya, kwa agreement si legally binding
We si umekopi na kupaste toka Google ukaweka hapa agreement ni nini,fanya hivyo Tena kwa 'difference between agreement and contract'..rahisi tu,kelele za nini!?
 
Acha ujinga. IGA ndio mkataba mama ndio maana unaitaji kupitishwa nabunge. Hiyo mikataba mingine midogodogo mnaweza mkasaiana hata chooni, hiyo inaitwa ukiishakubali kuolewa hakuna kulala na pichu
IGA ungekua mkataba mama kwa nini ikipita miezi 12 bila contract kuingia IGA inakufa!?
 
IGA ungekua mkataba mama kwa nini ikipita miezi 12 bila contract kuingia IGA inakufa!?
Weka hicho kiengele kinachosema hivyo. Bro usiingizwe mjini kichwakichwa. Ule uliopitishwa na bunge ni kama cheti cha ndoa. Sasa ukipata mwanaume anayejua kuoa tu hajui kuacha. Unalo, hapo lazima jasho likutoke
 
Weka hicho kiengele kinachsema hivyo. Bro usiingizwe mjini kichwakichwa. Ule uliopitishwa na bunge ni kama cheti cha ndoa. Sasa ukipata mwanaume anayejua kuoa tu hajui kuacha. Unalo hapo lazima jasho likutoke
Kajadili na wajinga wenzio
 
Akielezea suala linaloendelea kuhusu mkataba wa DP-World na Tanzania ametoa sababu kuwa ni utendaji kazi mdogo wa TICTS ambao umesababisha meli nyingi ziwe zinashushia mizigo Lamu, Mombasa au Afrika kusini hali ambayo imepunguza wateja wa Bandari ya Dar es salaam...
Hamna hata mmoja ambae ametolea maelezo vifungu vyenye utata. Wao sanasana wanazungumzia kuongezeka kwa ufanisi, ajira zitakazoongezeka na pesa tutakazopata.

Watu hawapingi mambo hayo. Watu wanachopinga ni kile kinachoonekana kama tunapoteza sovereignty yetu katika masuala ya bandari, transport corridors na EPZ.

Amandla...
 
Akielezea suala linaloendelea kuhusu mkataba wa DP-World na Tanzania ametoa sababu kuwa ni utendaji kazi mdogo wa TICTS ambao umesababisha meli nyingi ziwe zinashushia mizigo Lamu, Mombasa au Afrika kusini hali ambayo imepunguza wateja wa Bandari ya Dar es salaam.

Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa amesema utendaji mbovu wa bandari unasababisha meli zitumie muda mwingi bandarini ambapo gharama ya meli kubaki bandarini huingia mfanya biashara hivyo bidhaa kuwa ghali mtaani. Amesema kwa sasa meli hutumia hadi siku saba kwa mzigo kupakuliwa.

Aidha, amesema awali TPA ilitambua utendaji mbovu na kumpa TICTS mkataba kwa miaka 20 lakini hakukuwa na utendaji mzuri ambapo mkataba huo uliisha 2017 na baadae aliomba kuongezewa miaka mitano ambayo imeisha 2022 na bado hakuweza kuleta vifaa vipya vya kuhudumia bandari.

Waziri Mkuu ameonesha suala la mkataba wa DP-World litarahisisha upakuaji wa mizigo.

Watanzania wametaka maelezo baada ya kuwa na utata katika baadhi ya vipengele vya mkataba huo ambao kwa kiasi kikubwa serikali na spika wa bunge wamekuwa wakivitolea maelezo.

 
Hizi zako ni hoja za mtu ambaye pengine hajawahi hata kutumia bandari maskini ya Mungu, hana bidhaa inayokwama katika kuitoa au kuipakia pale bandarini.

Ni hoja za mtu kakaa kwenye kiti chake

Ni mkataba unaodumu miaka na miaka
VijiSkripr hivi. Mwenyewe umeletwa humu kuja kujaribu kufunika ukweli.

Bandari imegawiwa. Rushwa zimetamalaki nq kuna hatari ya Ukoloni mamboleo kudumishwa Tanzania.
 
VijiSkripr hivi. Mwenyewe umeletwa humu kuja kujaribu kufunika ukweli.

Bandari imegawiwa. Rushwa zimetamalaki nq kuna hatari ya Ukoloni mamboleo kudumishwa Tanzania.
DP World ni muwekezaji makini mwenye uzoefu wa kutosha kwenye masuala ya shipping business.
 
Back
Top Bottom