Wengi wanaotaka wake zao wasifanye kazi wana upeo mdogo wa kufikiri halafu ni wabinafsi

Wengi wanaotaka wake zao wasifanye kazi wana upeo mdogo wa kufikiri halafu ni wabinafsi

Walipata uraias, uspika kutokea nyumbani?

Unajua Samia kaanza siasa lini? Unajua background yake? Unajua background ya Tulia? Unadhani walifika Hapo bila kazi zingine?

Wake za marais kuacha kazi ni protocal tu, wanapewa majukumu ya kinchi na ndo maana wanalipwa mishahara na sheria imepitishwa ya kulipwa mafao as well.

Wafungieni watoto wenu ndani muone kama watafika popote wataishia kutumika tu.
Mkuu Bufa tafadhali sana, jikite katika mada ya mke na mume. Na sibinti yako au wangu. Wewe binti yako/wangu nivizuri kua nahivyo vyeo je mume wake anazungumziaje hilo?.
 
Tafuta hela kijana mwanake kazi yake kulea familia. Ukishaona wewe na mke wako wote mnaamuka saa 11 asubuhi kwenda kupalangana basi wewe huna mke ila una partiner kwenye kuendesha maisha.
Yaani wewe huna uwezo wa kuitunza familia na kwa msingi huo uanaume wako ni wa mashaka. Kimsingi hukupaswa kuoa.

Ukiona umeoa mwanamke asiyefanya kazi na hutimiza mahitaji yake, ikiwemo mahitaji ya kusaidia au kutuma pesa kwa Wakwe zako. Jua hapo huna mke bali msukule.

Hakuna Mwanamke anayejielewa atakubali kuolewa na mwanaume mchawi kama anayekataza mkewe asifanye kazi
 
Chukua idadi ya wanaweke hao waliopo kwenye hizo nafasi kisha gawanya Kwa idadi ya wanawake wenye vigezo vyakupewa hizo nafasi kisha zidisha 100%, Kisha uone binti yako anaasilimia ngapi zakupata hiyo chance, kisha mpiganie. Kama wewe watamani hivyo, waulize waume zao hao wenye hizo nafasi wanajivunia wake zao kushika hizo nafasi?.

Kisha baada yahapo pia utambue msingi wa mada tunazingumzia mke wako/wangu. Na sio binti yangu/wako.

Binti yako ni mke wa mtu mtarajiwa. Kama wewe unataka mke goli kipa means unamuandaa binti yako awe goli kipa.

Sihitaji kwenda mbali kuuliza maana nimekua kwenye hayo mazingira, kwetu, meaning ukoo wetu, wake kwa Waume wamesoma na Wana nafasi zao professionally. Kwangu mwanamke kuwa goli kipa ndo jambo la ajabu, sihitaji mke au binti yangu awe hivyo. Hii ishakua imprinted in my brain.

Sio lazima awe rais/spika/mkurugenzi anaweza kuwa na profession yeyote ile ilimradi awe na profession yake. Naandaa binti wa namna hiyo siandai goli kipa.

Nyie kimsingi mnataka mke goli kipa na mnaandaa magoli kipa otherwise mnajipinga wenyewe kama hamtaki mabinti zenu wawe magoli kipa.
 
Walipata uraias, uspika kutokea nyumbani?

Unajua Samia kaanza siasa lini? Unajua background yake? Unajua background ya Tulia? Unadhani walifika Hapo bila kazi zingine?

Wake za marais kuacha kazi ni protocal tu, wanapewa majukumu ya kinchi na ndo maana wanalipwa mishahara na sheria imepitishwa ya kulipwa mafao as well.

Wafungieni watoto wenu ndani muone kama watafika popote wataishia kutumika tu.
Samia ni mtoto wa bilionea hajawahi kupata shida yoyote, usitake tuanze kuongea siri za watu hapa wasiojulikana waanze kututafuta bure

Mke ni pambo la nyumba, akitaka nimpe ruhusa kwenda kuhangaika na mafoleni huko barabarani apate kazi ya kuanzia million 10 kwa mwezi kwenda juu, siyo laki 5 tu tayari ashatelekeza watoto na nyumba kwa house girl
 
Mbona mnafanya ndoa ngumu sana, yaani kuna kusomesha na kujenga ukweni?

Kila baba wa familia ahakikishe amejenga nyumba ya familia yake na sio kumsubiri mkwe au mtoto aje akujengee. Yaani Mimi nimsubiri mwanangu au mkwe wangu aje anijengee, huo ni upumbavu
Umenena vyema.

Hata mwanaume huna mamlaka ya kuhudumia kwenu kwa namna yoyote ile sababu unajenga familia yako.
ILA utakapoanza kusaidia kwenu Halafu Mke wako unamuacha huo ni ubinafsi.
ILA kama utahudumia Mke na watoto vzuri basi hakuna shida.
 
Samia ni mtoto wa bilionea hajawahi kupata shida yoyote, usitake tuanze kuongea siri za watu hapa wasiojulikana waanze kututafuta bure

Mke ni pambo la nyumba, akitaka nimpe ruhusa kwenda kuhangaika na mafoleni huko barabarani apate kazi ya kuanzia million 10 kwa mwezi kwenda juu, siyo laki 5 tu tayari ashatelekeza watoto na nyumba kwa house girl

Umeanza story za vijiweni kama kawaida yenu. Tunamjua zaidi yako.

Kuwa billionaire si ndo angeamua tu kuwa goli kipa, kwanini alianza kufanya kazi? Sio ilibidi akae nyumbani siku nzima anasubiri mme wake tu.

Kazi ni kipimo Cha utu.
 
Ndio ujibu hoja.
Unaweza kukarabati na kujenga Ukweni?au kusomesha ndugu za mkeo?
Kama unaweza kutimiza majukumu ya mkeo ikiwemo kuhudumia wazazi wake basi unahaki ya kumzuia asifanye kazi.

Lakini elewa kuwa hakuna mtu aliyefanokiwa hata mmoja duniani ambaye mkewe ni mama wa nyumbani asiyefanya kazi ya uzalishaji
Wewe huo utafiti ulifanya wapi kwa kutumia sampling zingi na kwa njia ipi ya ukusanyaji data. Hapa ninapoishi kuna watu wana visima vya mafuta na wake zao ni mama wa nyumbani. Still, Mimi kwa macho yangu nimeishi na watu ambao wote ni watumishi lakini kipato Cha mke hakina msaada wowote kwa familia na hakihojiwi na mume kwa usalama zaidi.

Tatizo binadamu hasa wa tz wanapenda kukopi na kupesti, ndo maan nikasema siku zote mfumo wa maisha ktk ndoa ni wanandoa wenyewe. Sasa wewe unataka unavyofanya kwa mkeo basi kila mtu afanye. Siyo rahisi km unavyodhani.

Vijana tusikimbie majukumu, kumlea na kumhudumia MKE ni kazi ya mume. MKE ni mshauri tu namba moja.
 
Umeanza story za vijiweni kama kawaida yenu. Tunamjua zaidi yako.

Kuwa billionaire si ndo angeamua tu kuwa goli kipa, kwanini alianza kufanya kazi? Sio ilibidi akae nyumbani siku nzima anasubiri mme wake tu.

Kazi ni kipimo Cha utu.
Huyo ndugu yangu nimeachana kujibizana nae.
nilimuuliza swali kuna mtu asiyefanya kazi hapa duniani kisa ni tajiri, hajajibu.
 
Ukiona umeoa mwanamke asiyefanya kazi na hutimiza mahitaji yake, ikiwemo mahitaji ya kusaidia au kutuma pesa kwa Wakwe zako. Jua hapo huna mke bali msukule.

Hakuna Mwanamke anayejielewa atakubali kuolewa na mwanaume mchawi kama anayekataza mkewe asifanye kazi
Mpaka hapo wewe siyo mwanaume na hukupaswa kuoa. Matokeo yake siku hizi vijana mnaoana au kuolewa na wake zenu. Mnaamuka wote saa 11 na mnarudi wote saa 4 usku. Hupewi maji ya kuoga, hupikiwi, watoto wako hawawalelewi na mke wako. Mke wako anaweza asirudi nyumbani, anaweza safiri mwezi mzima. Katika mazingira haya hata mngekuwa matajiri kiasi gani, wewe hujaoa..Ila una mtu unashirikiana naye kwenye maisha.
This isnt a concept of marriage na inakinzana na misingi ya asili ya ndoa. Matokeo yake Kila siku vinana mnaachana hata wale mnaoendelea ndoa zipo mahututi.
Yaani kakijana kameoana au kuolewa na mwenzake halafu Kanataka kaonekane kamwanaume ndani.
Narudia tafuteni hela kazi ya mwanmke ni kulea familia. Kazi ya kutafuta hela ni ya mwanaume. Huwezi kutafuta hela usioe
 
Huyo ndugu yangu nimeachana kujibizana nae.
nilimuuliza swali kuna mtu asiyefanya kazi hapa duniani kisa ni tajiri, hajajibu.

Ana comprehension disorder. Kama ni billionaire wajiulize kwanini alikubali kuolewa mke wa pili na hakutaka kukaa nyumbani kuwa goli kipa?

Ujinga wanadhani tumemjua Samia juzi kumbe na sisi tuna file lake lote. Hizo story zao za vijiweni won't cut it here.
 
Umeanza story za vijiweni kama kawaida yenu. Tunamjua zaidi yako.

Kuwa billionaire si ndo angeamua tu kuwa goli kipa, kwanini alianza kufanya kazi? Sio ilibidi akae nyumbani siku nzima anasubiri mme wake tu.

Kazi ni kipimo Cha utu.
Kwa hiyo wewe unafikiri Samia alitoka nje nyumbani kwao kwenda kutafuta kazi? au aliitwa tu na kuambiwa kaa hapa ule mema ya nchi?

Vipi mme wake anajivunia na ana furaha ya kutosha sababu mkewe ni Rais?
 
Huyo ndugu yangu nimeachana kujibizana nae.
nilimuuliza swali kuna mtu asiyefanya kazi hapa duniani kisa ni tajiri, hajajibu.
Wewe ndiyo hujielewi kabisa

Hapa tunazungumzia wanawake walioajiriwa siyo wanaofanya kazi za kuosha vyombo au kufua nguo nyumbani, hata kuna mjumbe amekufafanulia hapo juu kuwa siongelei kazi za usafi nyumbani wewe bado unawaza kazi hata za kupika nyumbani nazo unaita kazi
 
Mpaka hapo wewe siyo mwanaume na hukupaswa kuoa. Matokeo yake siku hizi vijana mnaoana au kuolewa na wake zenu. Mnaamuka wote saa 11 na mnarudi wote saa 4 usku. Hupewi maji ya kuoga, hupikiwi, watoto wako hawawalelewi na mke wako. Mke wako anaweza asirudi nyumbani, anaweza safiri mwezi mzima. Katika mazingira haya hata mngekuwa matajiri kiasi gani, wewe hujaoa..Ila una mtu unashirikiana naye kwenye maisha.
This isnt a concept of marriage na inakinzana na misingi ya asili ya ndoa. Matokeo yake Kila siku vinana mnaachana hata wale mnaoendelea ndoa zipo mahututi.
Yaani kakijana kameoana au kuolewa na mwenzake halafu Kanataka kaonekane kamwanaume ndani.
Narudia tafuteni hela kazi ya mwanmke ni kulea familia. Kazi ya kutafuta hela ni ya mwanaume. Huwezi kutafuta hela usioe
Safi kabisa, waambie hawa mpaka wajielewe
 
Safi kabisa, waambie hawa mpaka wajielewe
Sasa hivi tuna kundi la vijjana wavivu wapendwa kitonga. Wanataka wapate wenza wawasidie kulea familia, wakati huo huo wanataka wapate heshima ya mwanaume ndani
 
Back
Top Bottom