Wengi wanaotaka wake zao wasifanye kazi wana upeo mdogo wa kufikiri halafu ni wabinafsi

Wengi wanaotaka wake zao wasifanye kazi wana upeo mdogo wa kufikiri halafu ni wabinafsi

Duh! Acha mawazo haya mkuu! mawazo huumba, majanga yakitokea tutajua njia ya kuyatatua lakini tusitandikie godoro matatizo, Ishi leo yako achana na kesho.
Hahaha,
Hapana mimi huwa napenda kuongea uhalisia wa vitu Ninavyoishi navyo.

Yupo mama alimsaidia mume wake alikuwa kitandani hajiwezi, huyu mama alikuwa na kimgahawa chake anapika na anatengeza bites.
Mume aliugua sana mke alikuwa anapanda na kushuka mpaka akaja kupona.

sasa nilikuwa nafikiria sentensi yako ya kwamba pesa ya mwanamke ni ya mwanamke tu na si ya familia.

Mimi na Mke wangu tunasaidiana kulipa ada ya mtoto na hajawahi kuona shida kutoa pesa yake kuhudumia familia
 
WENGI WANAOTAKA WAKE ZAO WASIFANYE KAZI WANAUPEO MDOGO WA KUFIKIRI ALAFU NI WABINAFSI

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Chizi sio lazima uokote Makopo, kuna Chizi Fresh ambao ndio wengi wapo kundi hili tena wengine wasomi. Alafu kuna ambao ni Chizi Maarifa hawa wengi ukiwaona kwa mbali unaweza kudhani wako timamu lakini ukiwatazama kwa ukaribu ni wendawazimu.

Unakuta kajamaa kametoka familia Maskini, kameoa kutoka Familia Maskini. Kanafanya kazi iwe kwa kuajiriwa au kujiajiri lakini pato lake kwa mwezi hata Milioni moja halifiki.
Lakini ukikasikiliza mawazo yake kuhusu uchumi na mahusiano utabaki kuona kalivyo na upeo mdogo.

Yaani kisa umenunua mwanamke kwa bei ya jumla(kutoa mahari) labda shilingi milioni nne. Basi Mwanamke huyo ambaye sasa ataitwa mkeo unasema asifanye kazi kisa umemuoa.

Ukiulizwa kwa nini asifanye kazi? Huna hoja ya maana hata moja zaidi ya kutokujiamini, ubinafsi na ukandamizaji kama sio unyanyasaji.

Unamwambia mkeo asifanye kazi au asimiliki kipato kingi tena inafikia hatua kwa uzuzu wako unamhujumu mkeo na kumuwekea vikwazo ili asifanikiwe. Ati unaogopa atakunyanyasa ati atakuwa jeuri. Chizi weeeh!

Mkeo asifanye kazi, unapesa za kumhudumia mahitaji yake yote?
Alafu wengi wenye mtazamo kama huu unakuta Wake zao hata mafuta ya kupaka hawana, nguo wanazovaa mtumba, tena bora mtumba lakini ziwe nyingi. Lakini hata pesa ya kuwanunulia wake zao nguo walau kila mwezi nguo moja au mbili hawana. Mke kapauka, kazeeshwa. Yaani hatamaniki tena. Kila siku kumlisha mkeo Maharage kazi kujambajamba. Alafu unakuta jitu linasema linahudumia mke. Alafu halitaki mkewe afanye kazi. Ili angalau pesa ya kubadilisha chakula hapo nyumbani iwepo sio kila siku ugali na mchicha au maharage. Nyama na samaki mpaka sikukuu. Familia inapitisha Wiki hata maziwa hakuna. Alafu ulivyo chizi unaona sawa tuu. Alafu ukijaribu mtandaoni huku ooh! Mwanamke asifanye kazi utadhani umemudu mahitaji yake. Mwehu wewe!

Watoto wako ada zenyewe zinakusumbua, lishe yenyewe hawali. Utapiamlo na kifaduro kinawasumbua. Watoto mpaka imefikia hata uwezo wa kufikiri hawana Kwa sababu kila siku unawalisha chakula kingi cha wanga kama ugali, mihogo, maandazi na maujiuji ya nafaka. Ilhali kiafya watoto chini ya miaka 20 wanatakiwa kula protein nyingi kuliko kundi jingine la chakula ili miili yao ijengwe vyema. Vyakula vya protini ambavyo vinatakiwa viwe vingi katika mlo wenu hapo nyumbani ni Samaki, nyama, maharage, maziwa, mayai n.k.
Lakini kwa vile kipato chako ni duni huwezi kuhudumia hivyo. Alafu kwa vile tayari unakifaduro cha ubongo huoni kama unahitaji usaidizi na kwa ubinafsi wako unataka watoto wako nao wakose lishe kama wewe ulivyokosa. Ati mke asifanye kazi au asikusaidie majukumu. Kwa huduma gani unazotoa mwehu wewe!

Haya, mshahara wako wenyewe haukutoshi kutunza Wazazi wako.
Alafu hutaki mkeo asifanye kazi. Hivi unafikiri wazazi wake mwanamke watahudumiwa na kutunzwa na nani kama sio huyo mke wako. Mbuzi wewe.

Pesa yako hata milioni moja haifiki kwa mwezi. Unataka wadogo wa mkeo wahudumiwe na nani?
Unataka ile nyumba ya wazazi wa mkeo ifanyiwe ukarabati na nani kama sio mkeo.

Alafu haya machizi Fresh hapohapo unayasikia yakisema, usijenge Ukweni, mara Usitoe pesa Ukweni. Alafu hapohapo unayakuta yanazuia Wake zao wasifanye kazi. Hivi kama sio Ushetani na laana hizo ni kitu gani? Hivi kuna ubinafsi na ukatili wa kutisha zaidi ya huo?

Bado umfulishe na kumfanyisha makazi mengi bila kumpa lishe bora. Zaidi ya hapo umpige kisa ameona mambo sio mambo na umemgeuza msukule wake hapo.

Embu acheni Upumbavu wenu.
Ni mara elfu Mwanamke asioelewe au awe single Mother alee Watoto wake kitabutabu kuliko kuishi na mwanaume mwenye Ushetani wa namna hiyo.

Mwanaume elewa kuwa kama wewe unavyopenda na kuhitaji kuhudumia Wazazi wako ndio hivyohivyo mkeo naye anataka wazazi wake wahudumiwe.

Na ndio maana Watibeli Hawatoi Mahari kwa sababu inaharufu ya manunuzi au biashara ya binadamu kwa visingizio vya kishetani.

Hutaki mkeo afanye kazi alafu ukiombwa pesa ya kuwasomesha wadogo zake unapiga yowe na kulalamika. Wewe mwehu nini.

Na mimi nawaambia Wanawake hasa Watibeli ni lazima wafanyekazi. Kufanya kazi ni amri ya kila kiumbe ili kiwe huru na kujitegemea chenyewe. Binadamu asiyefanya kazi ni mfu.
Mtu mwenye akili na Mwanamke kamili na mke mwema hujisikia aibu na fedheha kumtegemea mumewe kwa kila kitu.

Mimi nimemaliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Daah hayajakukuta wewe! Tuulize tuliopo huku maofisini ndio tunajua wake za watu wanayofanyiwa!

1. Utajiskiaje kuona mke wako anapapaswa tako na wafanyakazi wenzake?

2. Utajiskiaje mke wako anakwambia ana semina ya wiki tatu mkoa flani? Tena mbaya zaidi anakwambia kaenda na bosi wake..

Kwenye mada hii nakupinga aisee!

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Dhana ya 50/50 wapewe furusa sawa, baada yakupewa furusa hizo Kwa upendeleo hao wanawake angalia impact yake ni nini katika msingi wafamilia ya baba, mama na watoto.
umenena vyema!

sasa tupe takwimu ya unachosema.
Yaani mtu kuomba ajue kusoma na kuandika baada ya miaka mingi mtoto wakike kuwa apelekwi shule unaona anataka kujilinganisha na wewe?

Una tofauti gani na mkoloni aliyewachapa babu zetu fimbo na kuenda kuwauza?

leta takwimu sasa.
 
Wewe unazo pesa za kumfanya mkeo na watoto wawe safi?
Unao uwezo wa kumpendezesha mkeo au ndio ninyi mnawavalisha kanga moja miaka nenda rudi?
Au huo ujasiri ni kwa sababu unatumia Fake I'd?

Unauwezo wa kuwahudumia wazazi wa mkeo na ndugu zake akimuomba ufanye hivyo?
Yaani uhudumie wazazi wa mkeo na ndugu zake hayo ndiyo majukumu ya mme?

Unawajibika namba 1 kwa familia uliyoianzisha wewe yaani wewe, mkeo na watoto wenu.

Hao wengine ni ziada kama unacho na una moyo unatoa lakini siyo lazima
 
Daah hayajakukuta wewe! Tuulize tuliopo huku maofisini ndio tunajua wake za watu wanayofanyiwa!

1. Utajiskiaje kuona mke wako anapapaswa tako na wafanyakazi wenzake?

2. Utajiskiaje mke wako anakwambia ana semina ya wiki tatu mkoa flani? Tena mbaya zaidi anakwambia kaenda na bosi wake..

Kwenye mada hii nakupinga aisee!

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
😂
Wake za watu ambao hawapo maofisini huwa hawafanyi hivyo?
Wote wanao- cheat ni wa ofisini tu?
 
Kuoa mke mfanyakazi eti kisa maisha kusaidiana ni woga wa maisha.
Kama una uhakika wa kipato na umewekeza kwenye vitu ambayo unexhausted woga wa maisha unatoka wapi?
Nimefanya kazi huu mwaka wa 9 nakaribia katika ofisi za umma.
Wake zenu wanawazalia watoto ambao si wenu. Kapime DNA halafu uje uandike tena kwa ujasiri hapa
 
Yeyote anayebisha muulize hatamani binti yake aje kuwa Rais, spika, waziri, mkurugenzi kama wanawake walivyoshika hatamu kwenye hii awamu? Anataka binti yake awe goli kipa tu that's it? They must be dumber than bricks 🧱

Watakuita mlamba lips.
Mtu mkewe hata kumhudumia hawezi. Hakumbuki mara ya mwisho kumnunulia nguo ni lini
Nyumbani kwake kunywa maziwa ni anasa wakati inatakiwa iwe sehemu ya mlo wa kawaida. Alafu anajifanya ati yeye ni mwanaume asiyehitaji usaidizi. Uone kama sio mgonjwa wa akili huyo
 
WENGI WANAOTAKA WAKE ZAO WASIFANYE KAZI WANAUPEO MDOGO WA KUFIKIRI ALAFU NI WABINAFSI

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Chizi sio lazima uokote Makopo, kuna Chizi Fresh ambao ndio wengi wapo kundi hili tena wengine wasomi. Alafu kuna ambao ni Chizi Maarifa hawa wengi ukiwaona kwa mbali unaweza kudhani wako timamu lakini ukiwatazama kwa ukaribu ni wendawazimu.

Unakuta kajamaa kametoka familia Maskini, kameoa kutoka Familia Maskini. Kanafanya kazi iwe kwa kuajiriwa au kujiajiri lakini pato lake kwa mwezi hata Milioni moja halifiki.
Lakini ukikasikiliza mawazo yake kuhusu uchumi na mahusiano utabaki kuona kalivyo na upeo mdogo.

Yaani kisa umenunua mwanamke kwa bei ya jumla(kutoa mahari) labda shilingi milioni nne. Basi Mwanamke huyo ambaye sasa ataitwa mkeo unasema asifanye kazi kisa umemuoa.

Ukiulizwa kwa nini asifanye kazi? Huna hoja ya maana hata moja zaidi ya kutokujiamini, ubinafsi na ukandamizaji kama sio unyanyasaji.

Unamwambia mkeo asifanye kazi au asimiliki kipato kingi tena inafikia hatua kwa uzuzu wako unamhujumu mkeo na kumuwekea vikwazo ili asifanikiwe. Ati unaogopa atakunyanyasa ati atakuwa jeuri. Chizi weeeh!

Mkeo asifanye kazi, unapesa za kumhudumia mahitaji yake yote?
Alafu wengi wenye mtazamo kama huu unakuta Wake zao hata mafuta ya kupaka hawana, nguo wanazovaa mtumba, tena bora mtumba lakini ziwe nyingi. Lakini hata pesa ya kuwanunulia wake zao nguo walau kila mwezi nguo moja au mbili hawana. Mke kapauka, kazeeshwa. Yaani hatamaniki tena. Kila siku kumlisha mkeo Maharage kazi kujambajamba. Alafu unakuta jitu linasema linahudumia mke. Alafu halitaki mkewe afanye kazi. Ili angalau pesa ya kubadilisha chakula hapo nyumbani iwepo sio kila siku ugali na mchicha au maharage. Nyama na samaki mpaka sikukuu. Familia inapitisha Wiki hata maziwa hakuna. Alafu ulivyo chizi unaona sawa tuu. Alafu ukijaribu mtandaoni huku ooh! Mwanamke asifanye kazi utadhani umemudu mahitaji yake. Mwehu wewe!

Watoto wako ada zenyewe zinakusumbua, lishe yenyewe hawali. Utapiamlo na kifaduro kinawasumbua. Watoto mpaka imefikia hata uwezo wa kufikiri hawana Kwa sababu kila siku unawalisha chakula kingi cha wanga kama ugali, mihogo, maandazi na maujiuji ya nafaka. Ilhali kiafya watoto chini ya miaka 20 wanatakiwa kula protein nyingi kuliko kundi jingine la chakula ili miili yao ijengwe vyema. Vyakula vya protini ambavyo vinatakiwa viwe vingi katika mlo wenu hapo nyumbani ni Samaki, nyama, maharage, maziwa, mayai n.k.
Lakini kwa vile kipato chako ni duni huwezi kuhudumia hivyo. Alafu kwa vile tayari unakifaduro cha ubongo huoni kama unahitaji usaidizi na kwa ubinafsi wako unataka watoto wako nao wakose lishe kama wewe ulivyokosa. Ati mke asifanye kazi au asikusaidie majukumu. Kwa huduma gani unazotoa mwehu wewe!

Haya, mshahara wako wenyewe haukutoshi kutunza Wazazi wako.
Alafu hutaki mkeo asifanye kazi. Hivi unafikiri wazazi wake mwanamke watahudumiwa na kutunzwa na nani kama sio huyo mke wako. Mbuzi wewe.

Pesa yako hata milioni moja haifiki kwa mwezi. Unataka wadogo wa mkeo wahudumiwe na nani?
Unataka ile nyumba ya wazazi wa mkeo ifanyiwe ukarabati na nani kama sio mkeo.

Alafu haya machizi Fresh hapohapo unayasikia yakisema, usijenge Ukweni, mara Usitoe pesa Ukweni. Alafu hapohapo unayakuta yanazuia Wake zao wasifanye kazi. Hivi kama sio Ushetani na laana hizo ni kitu gani? Hivi kuna ubinafsi na ukatili wa kutisha zaidi ya huo?

Bado umfulishe na kumfanyisha makazi mengi bila kumpa lishe bora. Zaidi ya hapo umpige kisa ameona mambo sio mambo na umemgeuza msukule wake hapo.

Embu acheni Upumbavu wenu.
Ni mara elfu Mwanamke asioelewe au awe single Mother alee Watoto wake kitabutabu kuliko kuishi na mwanaume mwenye Ushetani wa namna hiyo.

Mwanaume elewa kuwa kama wewe unavyopenda na kuhitaji kuhudumia Wazazi wako ndio hivyohivyo mkeo naye anataka wazazi wake wahudumiwe.

Na ndio maana Watibeli Hawatoi Mahari kwa sababu inaharufu ya manunuzi au biashara ya binadamu kwa visingizio vya kishetani.

Hutaki mkeo afanye kazi alafu ukiombwa pesa ya kuwasomesha wadogo zake unapiga yowe na kulalamika. Wewe mwehu nini.

Na mimi nawaambia Wanawake hasa Watibeli ni lazima wafanyekazi. Kufanya kazi ni amri ya kila kiumbe ili kiwe huru na kujitegemea chenyewe. Binadamu asiyefanya kazi ni mfu.
Mtu mwenye akili na Mwanamke kamili na mke mwema hujisikia aibu na fedheha kumtegemea mumewe kwa kila kitu.

Mimi nimemaliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Tafuta hela kijana mwanake kazi yake kulea familia. Ukishaona wewe na mke wako wote mnaamuka saa 11 asubuhi kwenda kupalangana basi wewe huna mke ila una partiner kwenye kuendesha maisha.
Yaani wewe huna uwezo wa kuitunza familia na kwa msingi huo uanaume wako ni wa mashaka. Kimsingi hukupaswa kuoa.
 
Uyu ajakua ngoja yamkute kapata kidemu Cha chuo washapanga mipango wajenge kwa pesa ya mwanamke
Anaona Me yeyote aoaye Mke wa nyumbani ni mshamba bila kujua ni muda tu utafika atapigwa tukio hadi aache ujuaji wa hivi viumbe.

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.
 
Ktk jamii yoyote classes are inevitable. These cases of gender equality and equity put them aside. Human beings cannot live homogeneous, never ever, suala la kuendesha maisha ktk ndoa ni utaratibu wa mtu na mke wake siyo kufuata mkumbo au kushauriwa, "because what is good to you cannot be good to all". Tatizo vijana wengi hasa hawa wasomi uchwara wanaotembea na vibegi mgongoni na kuvaa visuruali na vishati vya kubana wameathiriwa na Beijing agenda. Pole sn.
 
Kuoa mke mfanyakazi eti kisa maisha kusaidiana ni woga wa maisha.
Kama una uhakika wa kipato na umewekeza kwenye vitu ambayo u exhausted woga wa maisha unatoka wapi?
Nimefanya kazi huu mwaka wa 9 nakaribia katika ofisi za umma.
Wake zenu wanawazalia watoto ambao si wenu. Kapime DNA halafu uje uandike tena kwa ujasiri hapa

Wewe mkeo ambaye yupo nyumbani pima watoto DNA alafu uje utoe ripoti hapa.
Mnashindwa Kuelewa maamuzi na tabia ya mtu ni tofauti na kazi.

Mwananmke anaweza akafungwa jela na akapata Mimba
 
Yeyote anayebisha muulize hatamani binti yake aje kuwa Rais, spika, waziri, mkurugenzi kama wanawake walivyoshika hatamu kwenye hii awamu? Anataka binti yake awe goli kipa tu that's it? They must be dumber than bricks 🧱
Chukua idadi ya wanaweke hao waliopo kwenye hizo nafasi kisha gawanya Kwa idadi ya wanawake wenye vigezo vyakupewa hizo nafasi kisha zidisha 100%, Kisha uone binti yako anaasilimia ngapi zakupata hiyo chance, kisha mpiganie. Kama wewe watamani hivyo, waulize waume zao hao wenye hizo nafasi wanajivunia wake zao kushika hizo nafasi?.

Kisha baada yahapo pia utambue msingi wa mada tunazingumzia mke wako/wangu. Na sio binti yangu/wako.
 
That's another issue

Huwezi kumlinganisha Rais, Spika wa bunge na mwalimu wa chekechea anayelipwa laki mbili na nusu kwa mwezi

Mama Salma Kikwete hata Mke wa Magufuli wote walikuwa walimu lakini waume zao walipopata urais wake zao nao waliacha kuwa waajiriwa

Walipata uraias, uspika kutokea nyumbani?

Unajua Samia kaanza siasa lini? Unajua background yake? Unajua background ya Tulia? Unadhani walifika Hapo bila kazi zingine?

Wake za marais kuacha kazi ni protocal tu, wanapewa majukumu ya kinchi na ndo maana wanalipwa mishahara na sheria imepitishwa ya kulipwa mafao as well.

Wafungieni watoto wenu ndani muone kama watafika popote wataishia kutumika tu.
 
Ktk jamii yoyote classes are inevitable. These cases of gender equality and equity put them aside. Human beings cannot live homogeneous, never ever, suala la kuendesha maisha ktk ndoa ni utaratibu wa mtu na mke wake siyo kufuata mkumbo au kushauriwa, "because what is good to you cannot be good to all". Tatizo vijana wengi hasa hawa wasomi uchwara wanaotembea na vibegi mgongoni na kuvaa visuruali na vishati vya kubana wameathiriwa na Beijing agenda. Pole sn.

Ndio ujibu hoja.
Unaweza kukarabati na kujenga Ukweni?au kusomesha ndugu za mkeo?
Kama unaweza kutimiza majukumu ya mkeo ikiwemo kuhudumia wazazi wake basi unahaki ya kumzuia asifanye kazi.

Lakini elewa kuwa hakuna mtu aliyefanokiwa hata mmoja duniani ambaye mkewe ni mama wa nyumbani asiyefanya kazi ya uzalishaji
 
Tulishakubaliana wazazi wahudumiwe wakifikisha miaka 60, sasa haya ya kujenga ukweni yanatoka wapi?

Ndio wakifika hiyo 6o unaweza kuwahudumia na kuwajengea au kukarabati makazi yao ikiwa tuu mahitaji ya nyumbani kwako yamakushinda na pesa ya maziwa tuu unaona ni kazi?
 
Watakuita mlamba lips.
Mtu mkewe hata kumhudumia hawezi. Hakumbuki mara ya mwisho kumnunulia nguo ni lini
Nyumbani kwake kunywa maziwa ni anasa wakati inatakiwa iwe sehemu ya mlo wa kawaida. Alafu anajifanya ati yeye ni mwanaume asiyehitaji usaidizi. Uone kama sio mgonjwa wa akili huyo
Mada nimke wako/wangu kaka Robert nasio Binti yangu/wako. Wewe kama mzazi unatamani Binti Yako awe raisi/waziri/mkurungezi nisawa Sasa muulize mume wake anafuraha nabinti yako kuwa na hivyo vyeo ndio msingi wahoja ulipo katika ngazi yafamilia ya baba/mama na watoto.
 
Back
Top Bottom