Kwa namna ya kipekee nawashukuru sana watanzania wenzengu kwa kuipa CCM ushindi wa kimbunga kama tulivyowaomba. Naomba pia kwa namna ya kipekee kuwapongeza na kuwashukuru sana wote tulioshiriki nao hapa JF kuipigia kampeni CCM na kujibu hoja mbalimbali zilizojitokeza.

Watanzania wamezungumza kupitia kura zao. Tunaheshimu sana kauli zao na hakika sauti yao imezidi kuthibitisha imani kubwa waliyo nayo kwa CCM chini ya Jemedari wake Dkt Magufuli. Kauli ya watanzania ni kauli ya Mungu, CCM itaiheshimu na kutekeleza matarijio ya watanzania.

Kwa wenzangu wengine wa upande wa upinzani na wale wasio na vyama, tunawashukuru pia kwa uungwana wa kujadiliana kwa hoja. Ukiacha wachache walioporomosha matusi kila walipoandika, wengi wenu mlionesha ukomavu na kujadili hoja iliyowekwa mezani badala ya kurusha matusi. Ni muhimu tuendelee na hulka hiyo ya kiungwana na kuachana na matusi na tuombeana msamaha inapotekea tumekwazana kwa sababu za mihemuko ya kisiasa.

Sasa uchaguzi umeisha, maisha yetu yaendelee kwa amani. Maisha na maendeleo hayana vyama. Tushirikiane tuijenge Tanzania kwa pamoja.
 
Sawa mamaa
Watu lvel ya kijiwe samli utawajua tu. Wanadhani wakimwita mtu ''mama'' ndiyo wamemdhalilisha! Ulivyo mjinga hujui unaweza kuwa kweli unachati na mama yako! Primitive way of thinking! Fanya jitihada utembee duniani ujifunze ustaarabu ni nini na siyo unakuwa na maisha local ya kiswazi. Ndiyo maana unadhani hapa tunafanya ushabiki.
 
Yah n kweli nachat na mama yangu ndio maana nmekuita mama, au nimekukosea mama'angu.?
 
Nasema hivi wakati wa kupambana ni sasa hawa wahuni hawana hati ya miliki ya Tanzania wafanye uhuni, wizi na mauaji kisha waite ni uchaguzi. Huu uchaguzi ni batili na kuna ushahidi chungu nzima karibu kila kona Nchini kuonyesha kwamba uchaguzi huu haukuwa huru wala wa haki.
 
Hoja za nguvu za lissu kuibiwa kura?? Nyambaafff, lissu akagombee ubelgiji huko
#Chadema ni lazima ife, ni lazima ifee#
Hata huyo ''primitive man'' wako alikuwa anafikiria hivi hivi. Nasikia yeye na wapwa zake and co wanaita Chadema ''wanywa mbege'' na wametoa maagizo ''wanywa mbege'' wote wakwamishwe! Strangely, uchaguzi ulipofika hakuamini macho yake jinsi anavyochukiwa. Na bado! Ndiyo mtajua kuwa kuongoza siyo hasira na kuamuru watu wauawe! Very old and primitive way of leading! Huu ujinga walifanya kina Mobutu na hawakufika popote zaidi ya kuacha alama za ujinga wao mpaka sasa hivi zinajionyesha kwa vitu vya anasa walivyojenga vijijini kwao kwa ubinafsi na ushamba wao kama hilo-likiwanja la ndege litakavyododa baada tu ya mwaka mmoja.
 
Amini usiamini, uchaguzi huu umemuacha Rais John Pombe Magufuli uchi lakini kama ilivyo siku zote waumini wake hawasiti kumsifia alivyovaa na kuwa maridadi na pia kwa mbali uchaguzi wenyewe umenikumbusha Emperor Jean Bedel Bokassa wa iliyokuwa Central African Republic.

Tuache utani ndugu zangu, huyu mtu anachukiwa...Chuki dhidi yake sidhani kama ina kipimo!

 
Tuma hata picha uko barabara/eneo gani unaandamana kamanda. Tujiunge nawe.

Maana makamanda wengine wana andamana kwenye VPN tu.
 
Acha ujinga wewe hii ni 2020 kuna namna chungu nzima ya kupambana na Serikali dhalimu usidhani tuko mwaka 47.
Tuma hata picha uko barabara/eneo gani unaandamana kamanda. Tujiunge nawe.

Maana makamanda wengine wana andamana kwenye VPN tu.
 
Well, wajipange tu kwa ajili ya 2025.
 
Pole kamanda, kuna kibanzi nyuma hapo chomoa ukimbie.
Nipo barabarani naandamana
 
Acha ujinga wewe hii ni 2020 kuna namna chungu nzima ya kupambana na Serikali dhalimu usidhani tuko mwaka 47.
Tupo hapa tunaandamana lissu aachane na amsterdam.
#chadema ni lazima ife#
 
Acha ujinga wewe hii ni 2020 kuna namna chungu nzima ya kupambana na Serikali dhalimu usidhani tuko mwaka 47.
Kamanda ina maana utaandamana kwa emoji??? Ki software zaidi??
 
Pole kamanda, kuna kibanzi nyuma hapo chomoa ukimbie.
Nipo barabarani naandamana
Kampe pole mpwa wako aliyejenga uwanja wa ndege wa kifahari katikati ya watu wenye ufukara wa kutupwa! Huyo ndiye anayehitaji pole nyingi sana!
 
Reactions: BAK
Pole kamanda, kuna kanyama kamenatia hapo nyuma, chomoa ukimbie
#chadema ni lazima ife#
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…