Yuko wapi Rais Magufuli? Msiache tetesi zienee. Kama anaumwa mnasema "ANAUMWA"

Yuko wapi Rais Magufuli? Msiache tetesi zienee. Kama anaumwa mnasema "ANAUMWA"

Status
Not open for further replies.
Mbona hauliziwi Job Yustino Supika Ndugai mnamuulizia huyo mwingine tu
 
💯 mijitu ya humu jf inashabikia mtu afe hiyo ndio ile mijitu ambayo ilizoea kuteleza short pass halafu itoboe kimaisha kiulaini Sasa magu ameibana fedha kazipeleka kwenye maendeleo inalia Lia na magu.na semaje wewe ambae unashabikia mwenzako afe utatangulia wewe pumbaaff
Una stress,hata sasa watu hawajaacha kuteleza au kutoboa kimaisha.Ni we tu utabaki unabwabwaja humu na chuki zako.

KUMCHUKIA ALIYEFANIKIWA HAKUKUFANYI WEWE KUWA TAJIRI KM YEYE. Tafuta ngawira mkuu, utachelewa.

Bill Gates aliwahi kunena haya... '' kuzaliwa maskini si kosa lako bali kufa maskini ni ujinga wako''
 
Mzee Mwanakijiji Uongo kila leo umejaa hii nchi..Rais nae ni mtu jameni kuna muda anaamua kupumzika tayari wanamzushia..Nadhani Rais ajue kuna wazushi hata kwenye serikali kuna mijitu miongo mizushi balaa.
Rais ni mkristu na kipindi hiki ni kwaresima lazima apate muda wa kuongea na Mungu, yeye ni kiongozi lazima amjue Mungu maana madaraka aliyo nayo yametoka kwa Mungu. Ni kipindi cha kutafakari maisha, kufunga na kuomba. Acheni Mungu aitwe Mungu
 
Haijalishwi mara ngapi inazushwa...ni Rais yeye. Mnapima uzito wa jambo linalozushwa...Rais mwenyewe alishawahi kusema aliwahi kuugua akiwa waziri... Trump alipata corona, Boris Johnson aliugua na kulazwa..Rais ni wa nchi siyo wa Ikulu...wangetaka watu wasijue basi waache kutuambia mambo mwingine anayofanyaga....
Mzee wangu nakuheshimu sana na ninaungana na wewe watoe taarifa Kama anaumwa ila sioni kuwa ni sahihi ikiwa haumwi watoe taarifa kwa ajili ya kujibu tuhuma maana hawa wapuuzi wamekua wakizusha sio Mara moja wala mbili ni kawaida yao, je unaona ni sahihi kuwajibu hivo tuhuma zao ovu kila Mara?
 
Kila kitu ni siri kuu.

Hata msiba wangeweza wangeufanya siri kuu.

Sikuona sababu ya Mheshimiwa kujichabganya kipindi hiki, hata chanjo huwa zinadunda.

Huko Zanzibar wanagombea udongo kwenye kaburi la Maalim mpaka wamepiga marufuku.

.... SUBIRA YAVUTA HERI...
 
Rais ni mkristu na kipindi hiki ni kwaresima lazima apate muda wa kuongea na Mungu, yeye ni kiongozi lazima amjue Mungu maana madaraka aliyo nayo yametoka kwa Mungu. Ni kipindi cha kutafakari maisha, kufunga na kuomba. Acheni Mungu aitwe Mungu
Acha Udodoki ....watu kama hawa ndio wapambe , akiondoka tu wanaanza kuponda kama sio wao ili wadandie gari mpya
 
Laiti kama Saddam na Gaddafi wangewaunganisha kondoo wangekuwa hai hata leo kosa lao kubwa ni kuwabagua kondoo.

Wale kondoo waliobaguliwa ikawa rahisi kushawishiwa na mbwa mwitu kuitafufa haki kulipiza visasi.

Salama pekee ya mwanadamu ni kuishi vyema na wanaokuzunguka hata adui akija hana nafasi na sio kumiliki vyombo vya ulinzi vya kisasa vya kuzuia wezi.

Wezi watashirikiana na watu wa nyumbani kwako kukuibia.
 
Rais wangu, wanaokuwazia mabaya wameshindwa na kuaibika! Kumbuka Mungu wako unayemwamini, unayemtegemea na kumpa utukufu yu upande wako! Tunakuombea kwa Mungu na kukutakia mema.

Tunamshukuru Sana Mungu aliye mwokozi na mponyaji wetu!! Usisikilize wala kutilia maanani maneno mabaya yanayonenwa juu yako na mawakala wa giza, bali sikiliza na tilia maanani maneno asemayo Mungu!

Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa na njia za kutoka mautini anazo Yehova Bwana! Maadui zako watakutokea kwa njia moja lakini watakimbia kwa njia saba! Walioko upande wetu ni wengi kuliko walio upande wao! Imani ni uhakika wa mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu!! Sitakufa bali nitaishi ili niyasimulie matendo makuu ya Mungu.

Nakushukuru Sana Rais wetu kwa kutuongoza vema hasa katika kipindi hiki cha janga la corona duniani!

Tunamshukuru Sana Mungu kwa ajili ya maongozi yako, watanzania tunajisikia kama tuko ndani ya safina vile.

Tunakutakia afya njema na maisha marefu katika Jina la Yesu -Amina.
 
Kwani ile ya china ilikuwa feki.Au ipo kwenye majaribio.Dawa za madagascar je ni og au feki, kujifukiza na maombi hata navyo vimeshindwa?
Wachina wana kipi cha kumpenda kaharibu uhusiano sana ...hao wakenya wenyewe wana kipi cha kumpenda kaharibu sana uhusiano ndani ya jumuia ..Mungu ampe kuishi ili ajirekebishe ......
 
Watanzania tuna roho mbaya
Kuna jamaa yangu yuko Nairobi ananiambia Nairobi Hospital hakuingiliki kabisa. Haijulikani kuna nini ila ulinzi wa pale haijawahi tokea, wagonjwa wanashauriwa kwenda Hospitali zingine.
 
Tatizo ni kuwa alikataa kuwa hakuna huo ugonjwa ameushindana akaacha kuchukua tahadhari akidai Mungu kahamia nchini mwake kuwalinda. Wanafiki wakampa hadi tuzo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom