Uchaguzi 2020 Zitto: Kura yangu nafasi ya Urais nitampigia Tundu Lissu (CHADEMA)

Uchaguzi 2020 Zitto: Kura yangu nafasi ya Urais nitampigia Tundu Lissu (CHADEMA)

Na Mimi Kura Kwa Lissu!

1. Uhuru- Saivi tunaishi kwa wasiwasi uki- comment tu hata huko twitter kukosoa unaweza kujikuta una kesi ya money laundering.

2. Haki- Ukiwa mpinzani sahau kupata haki hapa nchini.

3. Maendeleo ya watu- tuna midege na mavitu ya pesa kubwa lakini hali ya maisha ni ngumu sana, ajira usiseme.

Tundu Antipas Lissu umepata kura yangu.

Mungu Akubariki Sana, Mkombozi wetu.
Duuuh
 
Kifupi Lissu mwenyewe kapitea njia alitakiwa yeye na CHADEMA wajiunge CUF huko CHADEMA walikoenda siko .Mark my words muda umebaki kidogo siku 9 tu hawawezi Chadema rekebisha makosa too late ila wamechemka .CCM Zanzibar tunashinda mapema mno na Lisu ataachwa njia panda atamwona Seif huyooo anapeta na miluzi barabarani wakikumbatiana na Mwinyi na Magufuli
 
Kifupi Lisu mwenyewe kapitea njia alitakiwa yeye na Chadema wajiunge CUF huko Chadema walikoenda siko .Mark my words muda umebaki kidogo siku 9 tu hawawezi Chadema rekebisha makosa too late ila wamechemka .CCM Zanzibar tunashinda mapema mno na Lisu ataachwa njia panda atamwona Seif huyooo anapeta na miluzi barabarani wakikumbatiana na Mwinyi na Magufuli
Endeleeni kupiga domo.mimi kama mwanachama hai wa ACT na wenzangu kura ya urais ni kwa Tundu Mughwai Lissu
 
MSIMAMO RASMI WA ACT WAZALENDO KUSHIRIKIANA NA CHADEMA.

Hivyo basi, baada ya maelezo hayo, natangaza rasmi kwa Wanachama, Wafuasi, wapenzi wa ACT Wazalendo na Watanzania kwa Ujumla, kuwa:

1. Pale kwenye Kata ama Jimbo ambalo ACT Wazalendo tuna Mgombea, tunaomba Muwapigie Kura wagombea wa ACT Wazalendo.

2. Pale ambapo kwenye Kata au Jimbo la Uchaguzi hakuna Mgombea wa ACT Wazalendo, lakini kuna wagombea wengine wa Vyama vya Upinzani, ACT Wazalendo tunawaomba MPIGIE KURA MGOMBEA WA CHAMA CHA UPINZANI mwenye nguvu zaidi ili kutokutawanya Kura.

3. Kwa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mimi Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe NITAPIGA KURA YANGU kwa ndugu Tundu Antipas Mughwai LISSU. Huyu ndiye Mgombea wa Upinzani ambaye ana nguvu ya kumshinda Mgombea wa Chama tawala, amefanya kampeni nchi nzima, mwitikio wa Wananchi kwake ni mkubwa sana, ameeleza kwa ufasaha dhamira yake ya kuleta mabadiliko na sina mashaka na dhamira hiyo, pamoja na anayotaka kuyafanya kama Rais, ni mambo hayo ndiyo yaliyonipa msukumo wa kumpigia Kura Lissu.

Zaidi NINAMUAMINI LISSU kutokana na historia yake ya kupigania Haki za Watu. Ninaomba kila mpenda Haki na Mabadiliko nchini ampigie kura ya URAIS ndugu Tundu Lissu ili awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Natanguliza Shukran kwenu

Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Bangwe, Kigoma Mjini
Oktoba 16, 2020
[emoji3577]
 
Kifupi Lisu mwenyewe kapitea njia alitakiwa yeye na Chadema wajiunge CUF huko Chadema walikoenda siko .Mark my words muda umebaki kidogo siku 9 tu hawawezi Chadema rekebisha makosa too late ila wamechemka .CCM Zanzibar tunashinda mapema mno na Lisu ataachwa njia panda atamwona Seif huyooo anapeta na miluzi barabarani wakikumbatiana na Mwinyi na Magufuli
Wazalendo maslahi tunaenda kuwakataa rasmi siku sii nyingi.oct 28.
 
Tunaangalia maslahi ya Taifa. Membe katumwa na CCM kutuvuruga afadhali zitto kamshtukia.
Kwani tofauti ya Zitto ,Membe na Maalim Seif Ni Nini?

Lisu karibu kwenye mdomo wa mamba tukutane October 28 Zimebaki siku Tisa za kampeni no reverse gear for Chadema

Too late
 
Hata Membe naye atangaze kumpigia kura Lissu mapema asisubiri lala salama
 
Back
Top Bottom