BRUSSELS, UBELGIJI: Rais Samia akutana na Tundu Lissu na kufanya mazungumzo mafupi

Samia rais wa watu,za chini chini ni kuwa lissu amempigia magoti na kumbembeleza Sana mama Samia amuhurumie Dj Mbowe na ikiwezekana amwachie huru,keep calm wafuasi wa Mbowe huenda wakatabasamu this week.
Mkuu kwa hiyo Mahakama zinasikiliza SAMIA anataka nini?
 

Lissu ndio kaimu Mwenyekiti wa CHADEMA, amekutana na Rais wa nchi Kama kiongozi wa CHADEMA. Hivyo yote amefanya kwa manufaa ya CHADEMA.
 
Hii ni aibu kwa msajili wa vyama na system ya Tanzania kumbania Mh. Rais kukutana na Chadema. Ona sasa Mama kawageuka kakutana na Lissu.
Hii sio habari njema sana kwa wachumia tumbo wa Tanzania kama kina Siro and the like..
 
Hapo sawa, tunataka kiswahili chetu kitumike. Nashauri Heading ya uzi iwe, "Lissu akubaliwa kuzungumza na Rais Samia S. Hassan, mazungumzo yafanyika"
Utakufa na nongwa. Yeye afuatwe afu aombe kukubaliwa?!
 
Kitendo cha Mh. Mbowe kunyoosha mkono mahakamani tafsiri yake ilikuwa amekubali yaishe ni tofouti na watu wa nje walivyoitafasiri..

Mbona Pasaka anailia nyumbani kwake mwaka huu..

Serikali ndio imeamua yaishe kwa kukosa ushahidi wa maana na vilio kuwa vingi. Nadhani Viongozi wetu wanjaribu kuondoa siasa za uhasama.
 
Lissu ashambuliwe kwa kosa gani?
 
CHADEMA mtawakuta ACT WAZALENDO huko kwenye siasa za maridhiano walishatangulia.

CHADEMA huwa hairidhii Bali inafuatwa yenyewe. Rais kaenda mwenyewe ubelgiji na kukutana makamu wa CHADEMA. Maridhiano sio ACT Bali Ni CUF ndio waliingia na CCM na wananchi kupiga kura kukubali serikali ya umoja wa kitaifa. ACT amekuta kila kitu mezani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…