CHADEMA yajiondoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Waziri Jafo awashangaa kususia uchaguzi

CHADEMA yajiondoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Waziri Jafo awashangaa kususia uchaguzi

Yaani wew jamaa ni mnafiki mkubwa, unamtofautishaje jiwe na haya makando kando yanayoendelea? Ina maana unajifanya ufahamu aliyetugawa watanzania kufika hapa.
'mkurugenzi nimekuteua mim, nakulipa mshahara, posho, gari na nyumba alafu ole wako umtangaze mpinzani ameshinda'
Hivi watendaji wanaonajisi mchakato wa uchaguzi, ni kiongozi gani anayewabariki kufanya wanayoyafanya bila kuchukuliwa hatua zozote madhubuti?

Wako wapi takukuru waliojinasibu kufuatilia na kukomesha rushwa na uzandiki wa kipumbafu unaofanywa na machumia tumbo?

Mimi ni shabiki sana wa Magufuli, lakini mambo wanayoyafanya viongozi aliowapa dhamana ya kusimamia uchaguzi ni matusi ya nguoni kwa serikali anayoiongoza.

Yuko wapi Jafo wa Tamisemi, kiongozi kijana anayejinasibu kutenda vema na haki kila apewapo jukumu la kusimamia?

Ccm wana hofu gani na chaguzi hizi za ngazi ya chini hadi kupelekea kujivua nguo hadharani na kutembea uchi hadharani bila ya soni?
Hivi kunafuraha gani timu pinzani kujiondoa uwanjani kabla ya mechi?

Utendaji wa Magufuli jinsi unavyokubalika, ninadhani kuna maadui wa ndani kwa ndani, wameamua ki mbinu na ujanja wa hali ya juu kumvua nguo kwanjia hiyo ili ionekane amewa tuma yeye, jambo ambalo nitakuwa wa mwisho kuamini hivyo.

Hili jambo halina manufaa hata kidogo kwake binafsi, bali kwa wale walioamua kumchafulia sifa zake alizokwisha kujizolea kwa waTz.

Haiwezekani uchaguzi wa serikali za mitaa ukachafuliwa na baadhi ya watu, halafu akaendelea kuwanyamazia na kuwakingia kifua.

Achukue hatua na hatua zionekane zimechukuliwa dhidi ya hawa wavurugaji ili kukomesha vitendo vinavyotengeneza chuki zisizo na sababu kila kifikapo kipindi cha uchaguzi.
 
Huyo anatii amri ya Jasusi Membe,

anasubiri maelekezo kutoka kwa mlezi wa chama
 
Na wabunge wasusie hivyo hivyo hapo sasa ccm itakuwa imetoka madarakani
Kigololi kimekushuka unatafuta basha
tapatalk_1564893878930.jpeg
 
Kuna Waziri mmoja anaitwa "JAFO", bila aibu wala kupepesa macho leo anasema eti kususia uchaguzi ni kuwanyima raia haki yao.

Hivi inaingia akilini kweli "CCM" wamejipitisha nchi nzima bila kupingwa, wamewakata wagombea wa upinzani wote, na kama mgombea akipitishwa bila kupingwa maana yake hakutakua na uchaguzi wowote wa mitaa.

Swali kwa Jafo,

Hao wapinzani wanawanyima haki gani raia??? Au ni serikali kwa mabavu ndio wamewanyima haki raia ya kuchagua wagombea wanaowafaa na kuwachagulia viongozi kwa nguvu???

Wasifanye watanzania wapumbavu. Ama kweli tanzania hatuna mawaziri wala serikali. Aibu hii dunia nzima.

#CCM subirini wananchi wenye hasira kali #2020.
Na domo lake lile limepinda kama mkia wa pweza hovyo kabisa.
 
Kauli ya Raisi ni sheria, Raisi ndio mwajiri mkuu, haujui kauli ya Raisi imemfanya DPP hawasamehe makosa watuhumiwa wa Uhujumu Uchumi endapo wakikubali kutoa mzigo?
Kwa upande wa uchaguzi hauwezi kwenda kwa maelekezo kwa kuwa ni chombo huru kinachojitegemea.
 
Sasa, Mhe. Suleiman Jafo, anashangaa nini apo. Ni mwananchi gani anayenyimwa haki yake ya msingi baada ya CHADEMA kujitoa, ama ni nani katika ya watendaji na CHADEMA wanaowanyima wananchi haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wawatakao? Yani, kabisa Mhe anashangaa, kwamba haelewi bado uzito wa sababu za CHADEMA kujitoa katika uchaguzi. Nafikiri CHADEMA wametumia busara kubwa sana kujitoa, maana consequences za kuendelea kwao,zingekuwa kubwa na za gharama sana kwa watanzania.
 
Zitto atakuwa mjinga sana kama atatoa Chama chake katika uchaguzi maana haina faida kubwa kulko hasara zake.Wapinzani kwa viherehere vyao hadi walihamasisha watu kujiandikisha wakati zoezi liliposuasua sasa wananchi wamejiandikisha halafu mjitoe tena.Ni ujinga kama watafikiria kuisusia UCHAGUZI CCM ni kuikomoa maana toka waanze kususa haijawa msaada kwao.Zanzibar CUF na CHADRMA walisusia najua tunajua nini kilitokea.Njia bora ya kumsinda adui ni kupambana nae sio kumkimbia.
 
Hata Zitto akishiriki hapati kitu maana wananchi hawatashiriki atapigiwa kura na nani? Yaani hapo ndio Zitto na Act yake wanaenda kuumbuka kama ni mpinzani wa kweli au msakatonge mtu wa kitengo, safari hii Zitto atajianika mwenyewe.
 
Zitto atakuwa mjinga sana kama atatoa Chama chake katika uchaguzi maana haina faida kubwa kulko hasara zake.Wapinzani kwa viherehere vyao hadi walihamasisha watu kujiandikisha wakati zoezi liliposuasua sasa wananchi wamejiandikisha halafu mjitoe tena.Ni ujinga kama watafikiria kuisusia UCHAGUZI CCM ni kuikomoa maana toka waanze kususa haijawa msaada kwao.Zanzibar CUF na CHADRMA walisusia najua tunajua nini kilitokea.Njia bora ya kumsinda adui ni kupambana nae sio kumkimbia.
Inatakiwa Zitto atoe chama chake kwenye huu uchafuzi unaoitwa uchaguzi kwa sababu ukishiriki wakati unajua kuna figisu na maagizo yapo wagombea wa upinzani wasitangazwe Washindi maana yake ni kuubariki uchaguzi haramu uonekane halali, Watanzania hawatamuelewa kabisa.
 
Back
Top Bottom