#COVID19 Chanjo za Kupambana na Corona (COVID-19): Nini Maoni na Mtazamo wako?
na wanawake wakichoma wanakua ma shemale nn au utafit haujakamilika nn
 
Tangu Serikali iruhusu chanjo ya Corona kuingizwa nchini mjadala mkali umezuka kati ya wapinga chanjo hiyo na wale wanaoikubali, hali hii ni tofauti kabisa na mataifa mengine kama majirani zetu Kenya ua Rwanda. Mpaka sasa wapinga chanjo(anti vaxxers) wakiongozwa na jemedari wao Askofu Gwajima wanaongoza katika mtanange huu na hakuna anayeleweka kwa wakubali chanjo kuanzia January, Kigwangalla mpaka Mbowe n.k.

Kwa kuangalia nyuzi,video, mijadala na michango katika mitandao ya kijamii kuanzia hapa JF na kwingineko, kwa kuwasikiliza watu wengi ninaowafamu (wengi wao wakiwa wasomi wazuri kabisa na washika dini) wapinga chanjo na wakosoaji wake ni wengi kuliko wanaoikubali.

Wapinga chanjo(anti vaxxers) wana hoja na maswali mengi yanayodhihirisha ujinga, upumbavu na uduni wa fikra katika idadi kubwa ya raia nchini(majority).

Zaidi sana wana ujasiri na nguvu kama Simba wa kusimamia ujinga uliowajaa tofauti na wenzao. Hakuna namna ya kuwashauri kuhusu umuhimu wa chanjo, mnaofanya hivyo mnapoteza nguvu na muda wenu tu.

Hali hii inadhihirisha kiwango kikubwa sana cha ujinga katika taifa letu na inamaanisha hata wanaopigania mabadiliko mengine makubwa na muhimu katika nchi hii haitakuwa rahisi kwao kufanikiwa.

Huo ndo uhalisia na ukweli mchungu wa kusikitisha kuhusu taifa hili.Kati ya wale maadui wakubwa watatu, adui ujinga ameiganda nchi kama ruba na hatoki leo wala kesho.

Maskini Tanzania.
 
Mwandishi hajaeleweka anatupasha habari gani MPYA.
Kikubwa hoja hujibiwa kwa hoja hapo ndipo serikali imekwama.
1.uhakika kama chanjo haina madhara.
2.kuweka chaguo kutopenda kuwajibishwa kama chanjo italeta madhara
3.licha mtu akichanjwa inaonesha ataambukizwa NA achukue tahadhari kama hajachanjwa
4.hawajatafiti
5.wanaenda kujaribu nchi nzima je ikitokea madhara?
Sasa kwanini Nikubali ujinga huu.
Au umeambiwa kenya korona imeisha?
 
M
Wapinga chanjo(anti vaxxers) wana hoja na maswali mengi yanayodhihirisha ujinga, upumbavu na uduni wa fikra katika idadi kubwa ya raia nchini(majority).
Mtatukana sana,lakini uchu wenu wa pesa ndo unatufanya tujilinde wenyewe na si kuwategemea wasomi uchwara.

Kwanini nasema hivyo, Kama una kumbukumbu, kulitokea kashfa ya mccm mmoja kuuza dawa feki za kupunguza makali ya ukimwi
na mpaka inagundulika watu walishaumia sana.

Sijui kesi yake iliishia wapi,haya leo hii dawa hizi za kawaida zikiisha muda wake
mnabadilisha tarehe ya kuisha muda wa matumizi ili msipate hasara,na huku mkijua fika kuwa mnawaletea watu magonjwa yasiyotibika.

Ndo maana wengi sasa wamepoteza imani na ninyi. Nje mmevaa makoti meupe lakini mioyoni mmevaa makoti meusi.

Mungu hakushindwa kutupatia akili ya pamoja tutumie kama "wifi" mtandao ukizima tuzime wote na ukiwaka tufanye kufikiri wote
badala yake kila mtu akampa akili zake ili aamue mambo yake,kuishi au kufa, kula au kushinda njaa,sasa kwa nini tulazimishane?

Ok,si ninyi ni wasomi? kwanini mnashadadia dawa za wasomi wenzenu,na si zenu mlizogundua wenyewe?

alafu wakigundua ushoga wakawaletea mnapinga? kwanini msiupokee nao ili kuonyesha utiifu wenu kwao?

Weka hapa chanjo mliyogundua ninyi nami nitakuwa wa kwanza kuchanjwa.

nimalizie kwa kusema tusilazimishane.uzima ni wa mtu binafsi sio wa umma.
 
"Umeme umekatika,tunaishi kwenye nyumba isiyo na umeme,ila na bado umeme ukirudi utaskia uwooooo!"
 
Tangu Serikali iruhusu chanjo ya Corona kuingizwa nchini mjadala mkali umezuka kati ya wapinga chanjo hiyo na wale wanaoikubali, hali hii ni tofauti kabisa na mataifa mengine kama majirani zetu Kenya ua Rwanda. Mpaka sasa wapinga chanjo(anti vaxxers) wakiongozwa na jemedari wao Askofu Gwajima wanaongoza katika mtanange huu na hakuna anayeleweka kwa wakubali chanjo kuanzia January, Kigwangalla mpaka Mbowe n.k...
Serikali ni vizuri kuruhusu matumizi ya chanjo yawepo nchini na uzuri wenyewe ni hiyari ikiwa mtu atataka kuchanja. Kwa kuwa ugonjwa ungali upo basi tuchukuwe tahadhari, huu si wakati wa kulumbana katika jambo hili kwani tuna mambo mengi ya msingi yanahitaji kuyatafakari.

Hakika hakuna mwenye kujua uhalisia wa ugonjwa huu, si wenye kuikubali chanjo au wenye kuipinga chanjo, hivyo basi tubaki na misimamo yetu kwenye akili zetu. Ukiona chanjo itakusaidia basi chanjwa na ukiona chanjo haina mpango basi ikaushiye.
 
Kama hutaki kuchanjwa kwa nini uwadanganye wenzako watakuwa mazombi wakichanjwa?
Serikali ni vizuri kuruhusu matumizi ya chanjo yawepo nchini na uzuri wenyewe ni hiyari ikiwa mtu atataka kuchanja. Kwa kuwa ugonjwa ungali upo basi tuchukuwe tahadhari, huu si wakati wa kulumbana katika jambo hili kwani tuna mambo mengi ya msingi yanahitaji kuyatafakari. Hakika hakuna mwenye kujua uhalisia wa ugonjwa huu, si wenye kuikubali chanjo au wenye kuipinga chanjo, hivyo basi tubaki na misimamo yetu kwenye akili zetu. Ukiona chanjo itakusaidia basi chanjwa na ukiona chanjo haina mpango basi ikaushiye.
 
Tangu Serikali iruhusu chanjo ya Corona kuingizwa nchini mjadala mkali umezuka kati ya wapinga chanjo hiyo na wale wanaoikubali, hali hii ni tofauti kabisa na mataifa mengine kama majirani zetu Kenya ua Rwanda...
Mjinga namba moja ni wewe mtoa mada ngoja nikuulize unajua maana ya chanjo? Na kama unajua maana ya chanjo je unajua chanjo ya corona inayoletwa inauwezo gani?

Kama chanjo ya corona ya haiwezi kukukinga dhidi ya ugonjwa wa corona ina umuhimu gani sisi tupewe chanjo, wataalamu waliozitengeneza wanasema hizi chanjo hazizuii kupata maambukizi ya corona,

kwa hiyo unaweza kuzichoma na bado corona ukapata, na unaweza kuchoma na bado ukatakiwa kuzingatia mbinu zote za kujikinga na corona kama vile kuvaa barakoa,SASA NAKUULIZA NINI MAANA YA CHANJO?
 
Back
Top Bottom