Uchaguzi 2020 'Charisma' ya Tundu Lissu itazidi kumpa shida sana Magufuli na CCM kwa ujumla

Uchaguzi 2020 'Charisma' ya Tundu Lissu itazidi kumpa shida sana Magufuli na CCM kwa ujumla

Charisma - compelling attractiveness or charm that can inspire devotion in others.

Kwa tafsiri ya kiswahili, Charisma ni ule mvuto mtu anaokuwa nao mpaka unatamani kama anaongea aendelee kuongea.

Katika siasa Charisma ni kitu cha umuhimu sana, kama huna Charisma, huwezi kuvutia watu wakakusikiliza.

CCM wana bahati mbaya sana kukosa viongozi wenye Charisma, ndo mana unaona kwenye kampeni wamekuwa wanatumia sana wasanii wa bongo fleva ili kuweka mvuto ambao ulistahili kuletwa na viongozi wao, kinyume chake ni sahihi kabisa, CHADEMA wana viongozi wenye Charisma ya hali ya juu sana, mtu kama Halima Mdee, Tundu Lissu, Mnyika, au Mbowe wakianza kuongea huwezi tamani ashushe mic, ni viongozi ambao wanaweza kuunganisha maneno mfululizo kwa lisaa lizima wakimwaga point ambazo hadhira inataka kuzisikia.

Nimemsikiliza leo Magufuli akiwa Shinyanga, honestly, unaona kabisa hata namna anavyounganisha sentensi, ni kama vile anakuwa anakosa coordination ya meneno. Magufuli anaweza kuongea sentensi kumi ambazo zinakinzana zenyewe kwa zenyewe, kitu ambacho kwa mtu unayemsikiliza ni rahisi sana kupoteza hamu ya kumsikiliza.

Ndo maana ya ule usemi wa kwamba, 'viongozi wanazaliwa' kama huna Charisma, huwezi kuongoza watu wakakupenda kwa sababu ni ngumu pia kwa mtu asiye na Charisma kuelewa changamoto za wengine. Ndo mana unamsikia Magufuli akituahidi tena kutumia mabilioni mengine ya kununua ndege, ni kama hajasikia na kuelewa vema kilio cha watanzania kwamba hizi ndege sio matumizi ya kipaumbele kwa taifa. Na hii ni moja wapo ya tabia za watu wasio na Charisma, daima hujali sana vipaumbele vyao dhidi ya wanaowazunguka.

Kama mambo yataendelea kwenda hivi, ni kwamba Magufuli ataonekana anaongea bila kuwa na hoja na mambo yanavoenda mvuto wa Magufuli kwa wapiga kura unazidi kupuputika, upande wa pili, Charisma inambeba Lissu kwa nguvu sana, wengine tulishakata tamaa na siasa lakini, namna Lissu anavofanya mambo mpaka sasa, ametuinua sana morali zetu, na hii yote ni nguvu ya Charisma aliyojaliwa ambayo wengine wamenyimwa.
Umeongea ukweli mtupu mkuu.
Kitu chengine cha kuongezea ni jinsi audience wa Lissu wanavokuwa engaged anapoongea Lissu. Hawa watu ukiwaangalia unaona shauku yao ya kutaka kujua na kufahamu wanachoambiwa. Kwa ufupi wako very attentive na wenye shauku wa kusikia na kujuwa kila sentensi inayotoka mdomoni mwa Lissu.

Ama kwa upande wa Magu hali inakuwa ni tofauti kabisa. Utakuta watu hawako engaged kabisa na kinachoongewa. Wengina wanaongea, wengine wanafanya biashara na katika uwanja kila mmoja yuko na direction yake! Na wengine wakiwa na shauku ya kuwaona na kuwasikiliza wasanii.

Unaona kabisa kwamba watu wengi ndani ya hadhara za Magu kila mmoja kaendea lengo lake. Kwa tathmini ya haraka haraka unaweza kuona kwa asilimia 70 au zaidi hawana hamu na kinachoongewa na mgombea.
 
Natofautiana na mawazo ya mleta mada.
 
Lissu hatoshinda.,,
Viongozi wote njaa walioanguka walikuwa na wapambe njaa kama wewe , walikuwa na watu wa kabila zao , waliwaapisha majenelari na Mapolisi waandamizi , kung'olewa kunapofika hakuna cha wapambe wala cha mswalie mtume
 
Walau wewe kidogo una akili.

Ila manyumbu wenzio hata akili ya kutambua kuwa Lissu hatoshinda, hawana.
Kama vita mlikuwa mnavisikia mataifa mengine, mtaviona nchi hii iwapo Lisu atashinda na asitangazwe. Uzuri wa nyakati hizi teknolojia ya mawasiliano imefanya usiri usiwepo. Tutajumlisha namba za kura nchi nzima na matokeo tutakuwanayo. Ole wenu mtangaze tofauti, mtaikimbia nchi.
 
Charisma - compelling attractiveness or charm that can inspire devotion in others.

Kwa tafsiri ya kiswahili, Charisma ni ule mvuto mtu anaokuwa nao mpaka unatamani kama anaongea aendelee kuongea.

Katika siasa Charisma ni kitu cha umuhimu sana, kama huna Charisma, huwezi kuvutia watu wakakusikiliza.

CCM wana bahati mbaya sana kukosa viongozi wenye Charisma, ndo mana unaona kwenye kampeni wamekuwa wanatumia sana wasanii wa bongo fleva ili kuweka mvuto ambao ulistahili kuletwa na viongozi wao, kinyume chake ni sahihi kabisa, CHADEMA wana viongozi wenye Charisma ya hali ya juu sana, mtu kama Halima Mdee, Tundu Lissu, Mnyika, au Mbowe wakianza kuongea huwezi tamani ashushe mic, ni viongozi ambao wanaweza kuunganisha maneno mfululizo kwa lisaa lizima wakimwaga point ambazo hadhira inataka kuzisikia.

Nimemsikiliza leo Magufuli akiwa Shinyanga, honestly, unaona kabisa hata namna anavyounganisha sentensi, ni kama vile anakuwa anakosa coordination ya meneno. Magufuli anaweza kuongea sentensi kumi ambazo zinakinzana zenyewe kwa zenyewe, kitu ambacho kwa mtu unayemsikiliza ni rahisi sana kupoteza hamu ya kumsikiliza.

Ndo maana ya ule usemi wa kwamba, 'viongozi wanazaliwa' kama huna Charisma, huwezi kuongoza watu wakakupenda kwa sababu ni ngumu pia kwa mtu asiye na Charisma kuelewa changamoto za wengine. Ndo mana unamsikia Magufuli akituahidi tena kutumia mabilioni mengine ya kununua ndege, ni kama hajasikia na kuelewa vema kilio cha watanzania kwamba hizi ndege sio matumizi ya kipaumbele kwa taifa. Na hii ni moja wapo ya tabia za watu wasio na Charisma, daima hujali sana vipaumbele vyao dhidi ya wanaowazunguka.

Kama mambo yataendelea kwenda hivi, ni kwamba Magufuli ataonekana anaongea bila kuwa na hoja na mambo yanavoenda mvuto wa Magufuli kwa wapiga kura unazidi kupuputika, upande wa pili, Charisma inambeba Lissu kwa nguvu sana, wengine tulishakata tamaa na siasa lakini, namna Lissu anavofanya mambo mpaka sasa, ametuinua sana morali zetu, na hii yote ni nguvu ya Charisma aliyojaliwa ambayo wengine wamenyimwa.
Umemaliza kila kitu mkuu
 
Kama vita mlikuwa mnavisikia mataifa mengine, mtaviona nchi hii iwapo Lisu atashinda na asitangazwe. Uzuri wa nyakati hizi teknolojia ya mawasiliano imefanya usiri usiwepo. Tutajumlisha namba za kura nchi nzima na matokeo tutakuwanayo. Ole wenu mtangaze tofauti, mtaikimbia nchi na wake zenu tutazaanao.
Hiyo vita utapigana wewe na nyumbu wenzio?
 
Walau wewe kidogo una akili.

Ila manyumbu wenzio hata akili ya kutambua kuwa Lissu hatoshinda, hawana.
Kama umetoka kutoamini Lissu hatashinda mpaka kuamini kuwa Lissu atashinda ila hatotangazwa basi jiandae kuamini kuwa Lisu atashinda na atatangazwa
 
Kilichowazi na ccm wanajua ni kwamba kwanza hawakushinda Zanzibar wala bara 2015 ndio maana ya rais kutangaza vita dhidi ya upinzani alipoingia tu madarakani. Chaguzi za madiwani na wabunge walionunua wote mnakumbuka ilikuwaje. Watz wanajua nn kilitokea December mwaka jana uchaguzi serikali za mitaa.....
Kimsingi na ccm wanajua hakuna
1. Wakulima
2. Wafanyakazi
3. Wafanyabiashara
4. Wanafunzi
Wakuichagua ccm na ndio chanzo cha haya yote kulazimisha kubaki madarakani kwa nguvu ya tume km alivoahidi rais lkn pia kwa nguvu ya dola km alivyosema Bashiru
Mchwanwi nchi hii sio Jiwe ni Tume na vyomvo vya usalama vinavyompa kiburi
 
CCM Wanaujua ukweli ndo maana walizuia mikutano kwa miaka 5, walizuia bunge live, walimpiga lisasi, Sasa wamefungia magazeti, na kuzuia habari za charismatic leaders zisitangazwe
Wameshafeli Zinatangszwa bila kujua zinatangazwa na nani
 
Kama vita mlikuwa mnavisikia mataifa mengine, mtaviona nchi hii iwapo Lisu atashinda na asitangazwe. Uzuri wa nyakati hizi teknolojia ya mawasiliano imefanya usiri usiwepo. Tutajumlisha namba za kura nchi nzima na matokeo tutakuwanayo. Ole wenu mtangaze tofauti, mtaikimbia nchi.

Wewe inaonekana haujaposa bado... acha matusi bradha... haisaidii... na hata hivyo watakimbia wakiwasahau 'their better half' nyuma?
 
Charisma ya Lissu ni kama ya marehemu Thomas Sankara, yani huyo alikuwa akiongea hata kama huelewi lugha unapata mzuka. Halafu wote wanafanana kwa kujali maendeleo ya watu.

CCM walete wanamuziki toka Nigeria na Marekani ndio fiesta yao itabamba. Otherwise JPM ataendelea kuwa gumzo kwa pumba atakazoongea, Lissu atakuwa gumzo kwa madini atakayotema.
 
Kwa sisi watu wataalamu wa Sayansi ya Siasa tunaposhuhudia mgombea wa Chama Kikubwa Kikongwe (Vanguard Party ..ya Kijamaa) anapelekeshwa hivi tunajua tuna kitu hakipo sawa!

Kwa hii miaka mitano mfumo wa Utawala ulifsnya jitihada kubwa ,nyingi za kuua CDM matokeo yake Ni kinyume! Je Nini kimesababisha haya!

Mosi,mabadiliko makubwa ya kifikra ,na hii inaashiria Watanzania wao tayari kwa mabadiliko.Kinachosekana Ni wakala wa kuongoza haya mabadiliko! Na Sasa yaelekea Tundu anajaribu kuziba ombwe hili! CCM walitakiwa wajiuluze Sana kwa yaliyotokea 2015! ,Ambapo almanusura watu wampeleke Lowasa Ikulu !

Lowasa angekuwa na uwezo wa kujenga hoja Kama Tundu sijui Hali ingekuwaje!?

Pili,Kuna tatizo kwenye mfumo wa Uongozi wa CCM . Pengine Mwenyekiti Hana washauri wazuri au hashauriki.

Sababu ya tatu Ni Mwenyekiti kushika hatamu! Tumexhuhudia miaka 5 ya Zidumu Fikra za Mwenyekiti! Mawaziri, Wabunge, Wakuu wa Idara na Taasisi , RC, DC , WEO, Madiwani wote wanamtukuza Mwenyekiti! Na Bahati mbaya sana hili linafanyika kinafiki.

Nne', Kosa kubwa wanalofanya CCM, ni kutumia nguvu kuwanyamazisga wapinzani. Leo hii nguvu kubwa ileile inatumika kunadi Sera ziluzotukuzwa kwa miaka mitano!

Tano, CCM wameshindwa kubaini kuwa kizazi kiaminifu' na Sera za Chama bila kujali chochote kinapotea kwa Kasi. Hawa walizaliwa , wamekua na TANU,CCM na Nyerere huwaambii kitu!

Mwisho, CCM Ni muhimu wajiandae kuyapokea mabadilko makubwa Sana katika Fikra za Watanzania. Ni aibu na fedheha mtu mzima akitaka kuongea na wananchi kutumia nguvu kubwa namna hii .. wasanii na wachekeshaji!
 
Back
Top Bottom