Clouds Media, kuweni makini na kujiingiza kwenye siasa. Mtasuswa na watanzania!

Clouds Media, kuweni makini na kujiingiza kwenye siasa. Mtasuswa na watanzania!

Ok
Ila mnakabili vipi Mwakyembe Kyela?
Unadhani mtamwangusha?

Maana nasikia kwenye watia nia 9 waliojitokeza ccm hakuna wa kumng'oa
 
Joseph Kusaga ukitaka kujua kwamba ccm ina wenyewe rudi nyuma miaka zaidi ya 25 iliyopita wakati ule unapiga Disco coco beach ukiwa na DJ Bonny love , ilikuwa ikifika saa 6 balozi Ammy Mpungwe anaagiza polisi kuja kuzima disco lile lilojaza vijana kibao huku wakicheza kwa amani na utulivu , Hawa ndio wenye ccm , katika kundi hilo wewe haumo , maana sisi pamoja na wewe tulikuwa tunaenda kulala baada Mzee Mpungwe kuzima disco , naamini bado hujasahau .

Chadema iliwahi kuwaamuru watanzania kuipuuza TBC na kuanzia hapo mpaka naandika uzi huu TBC imepuuzwa nchi nzima na hata watangazaji wake wakitangaza bila kuvaa nguo hakuna mwananchi atakayeangalia TBC.

Achana na Chadema jikite kwenye weledi , hawa watangazaji wanaokuja ambao hawajui hata clouds ilikotoka watakuponza , kutengeneza brand yaweza kuchukua miaka mingi lakini kuiharibu haichukui hata dk 5 , kuwa makini mno !

MAJUTO NI MJUKUU , Usije kusema hatukukuambia .

Clouds imegeuka "kikaragosi" cha CCM.
Clouds wanadhihaki wapigania uhuru uliporwa toka 1995 !
CHADEMA kupitia john mrema na Yericko Nyerere Tangazeni kampeni ya Ku-unfollow Clouds Insta, you tube, tweeter na kutoisikiliza kabisa kama TBC ilivyo fanyiwa baada ya kuwa MKE MWENZA WA CCM.
 
Huwashangaa sana wajinga wote wanaosusa vitu ajili ya mavyama as if ni wanufaika kumbe wapiga debe tu
 
Erythrocyte, TBC ndio nambari 1 kwa sasa, usifanya chuki zako dhidi ya CCM kuwa issue ya Taifa. Upinzani hauna maana tena
Fanya utafiti wako binafsi kwa majirani zako na ndugu zako wa karibu,utagundua zaidi ya asilimia 90 ikifika saa mbili kamili usiku wanaangalia taarifa ya ITV.
 
TBC ndio channel inayoongoza kwa kuangaliwa na na watu wa rika zote kwa local channel
Utakubaliana na Mimi kuwa majirani zako asilimia kubwa na ndugu zako pia ikitimu saa mbili kamili usiku wanaangalia taarifa ya ITV.
 
TBC ndio channel inayoongoza kwa kuangaliwa na na watu wa rika zote kwa local channel
Utakubaliana na Mimi kuwa majirani zako asilimia kubwa na ndugu zako pia ikitimu saa mbili kamili usiku wanaangalia taarifa ya ITV.
 
Erythrocyte, TBC ndio nambari 1 kwa sasa, usifanya chuki zako dhidi ya CCM kuwa issue ya Taifa. Upinzani hauna maana tena

TBC ni uchafu kama uchafu mwingine, wamebaki wazee huko vijijini ndio wanaangalia. Hakuna mtu anayejitambua anaweza kuangalia hiyo TV ya kizee.
 
CHADEMA bana na nyie muwekeze kwny media zenu achaneni na hao wafanyabiashara na wasaka fursa kila siku mnalalamika nyie tu ipo siku watu wataanza kuwapuuzia.
 
TBC wameji-update na aridhio wako vizuri siku hizi angalau inatazamika.
Bado sana maana hawana jipya.Ni zile zile propaganda mfu za miaka yote,kuwapa majina wapinzani wa kweli na kuwakandamiza kinyume cha haki za binadamu na kisheria.
 
Clouds inakufa taratibu kwa uhakika na ikiendelea na huu upuzi baada ya uchaguzi ndo itazikwa kabisa,leo hii TBCCM pamoja na kutumia mabilioni ya Watz kuboresha studio sijui ARIDHIO vitukani Watz hawana muda nao
 
TBC kwa sasa iko juu kuliko Huko ilikotoka. About clouds Media wanafanya sahihi hasa 360 wako vizuri sana. Ninyi mlifungua Chadema Media yenu ambayo hatujui inafanya nini au ndio moja ya pipe ya kusababisha the so called madeni ya mkopo mnaomlipa Mwenye Saccos ?

Pambaneni na hali yenu
 
Kimeingia, kimeuma hauwezi kujibu unarusha ngumi hewani

Nilichoandika cha uwongo ni kipi??

Wafanyabiashara hao lazima watalemea CCM

Mara ngapi mnawaambia watu wasisikilize clouds na bado ina wasikilizaji wengi?

Mara ngapi hao clouds wanatoa coverage za chadema?

Kuweni genuine na roho yako...nyie ndio mnakataaga wazazi wenu kuogopa watu

Jibu hoja, sitaki kukutukana, maana hauniwezi na sijawahi kushindwa

CDM ina miaka 25 sasa hawana TV, Radio na channel za maana wewe unataka mtu binafsi na utashi wake aache kufanya cha kumuingizia hela kisa akauogope wewe?

Huu umaskini wa akili mnautoa wapi? Au mbaona kila mtu yuko JF, Twitter na insta? Kitaa kila mtu ni clouds na hawana mawazo yenu ya ki patriotic but very childish kama wewe....
Mzee baba unaandika sana mapovu jukwaani

Maelezo mengi lakini pointless tupu
 
Embu angalieni st swahili basi kule hakuna siasa, hiyo tbc kifurushi kikikata ni kuzima tv na kutazama series tu hivi mtu na akili zako unaanzaje kuangalia tbc kweli
 
Wafuasi wa upinzani Tanganyika wanadai demokrasia wakati wao wenyewe hawawezi kuhimili mawazo mbadala.
Kuna mstari mwembamba Sana unaotenganisha Lumumba na Ufipa.
Akili zao Ni sawa tu ,wote hawataki kukosolewa Wala kuambiwa ukweli
 
Back
Top Bottom