Dar es Salaam ili uende kazini na kurudi lazima uandae elfu 10 ya usafiri pamoja na chakula. Maskini hana chake hapa nchini

Dar es Salaam ili uende kazini na kurudi lazima uandae elfu 10 ya usafiri pamoja na chakula. Maskini hana chake hapa nchini

Dah nmetoka kupiga jana tu hesabu ya mwezi maana nlidownload app ya budget playstore ambayo nilikua naandika kila income na expenses nlizokuwa natumia mbona macho yaligeuka mekundu na nguvu kuniisha

Maana daily 20k mafuta gari
Daily 20k home na hapo baadh ya vitu vipo
Bills umeme,maji nk 50k
Chakula job 10k hpo ndo kujibana
Vocha
Na mengineyo.
NB;
Sinywi pombe wala si mtu wa starehe
Umefka mwsho wa mwezi Expenses zimegonga 3m+ nikawa kama nimemwagiwa maji
Matumizi yako yanaendana na kipato chako, kunawengine wapo town, matumizi per month ni bajeti yako ya Vocha.
 
Naandika hii mada nikiwa na uchungu moyoni.

Sasa hivi nina miezi kama 4 hivi natumia Daladala kwenda na kurudi kazini na mara chache, tena chache sana huwa natumia bodaboda kazini mpaka home, home mpaka kazini.

Kutoka Nyumbani mpaka kazini nikipanda bodaboda direct ni elfu 15. Go and return inalala 30000 sh
Nikipanda bodaboda 1500 sh. mpaka kituo cha Daladala na nikipanda Daladala moja mpaka kazini awali nilikuwa natumia 1000 sh. Jumla 2500 sh, kwenda na kurudi natumia sh. 5000 kamili, nikipanda gari mbili nilikuwa natumia kama elfu 6 hivi. Pesa ambayo himilivu kwangu.

Ila sasa nikipanda Daladala itanilazimu nitumie takribani 7000 kwenda na kurudi.

Hapo ukiweka na chakula na maji around 5000.

Kwahiyo Mimi tu inabidi nitumie angalau elfu 12 kwaajili ya kazini. Familia kwa sasa hali ilivyo kwa siku ni sh. 10 -20 hapo mahitaji yote muhimu kama gas, mkaa, chumvi, Michele na unga viko ndani. Kama havipo lazima uangushe 20.

Kwahiyo inanilazimu kwa siku nitumie kuanzia elfu 30.

Vipi kwa anayelipwa laki 2.5 au laki tatu kwa Wahindi?

Vipi anayelipwa elfu 7 kiwandani kwa siku?

Kipato changu kidogo nahisi kupata msongo wa mawazo.
Kwa mwezi natumia karibu milioni 1 kwa chakula nyumbani , kazini , usafiri na dharura ndogondogo.
Hapo ukiweka dharura kubwakubwa kama kufiwa na ada za shule watoto mwezi mmoja naangusha zaidi ya milioni.

Serikali ipunguze nauli, watu wanashindia mihogo makazini Ili kubana nauli za kurudia nyumbani jioni.

Hakuna mtumishi wa umma au mwajiriwa wa sekta binafsi Dar es Salaam anaweza kununua kiwanja center labda awe fisadi. Wengi tunajuchanga tunapata viwanja Chanika, Bagamoyo, Kisarawe, Pugu n.k.

Kwa nauli hizi Ili ugeuke na gari upate seat lazima ujipange. Unakuta kila ukipiga hesabu 20 imeenda kwa usafiri na misosi.

Umaskini utaendelea kutupiga maana hatuna mtetezi.
Tutafute hela tu.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
JF kila mtu matawi..et natumia 15k kwenda kazini na kurudi mara chache dalaladala huwa natumia daladala..humu mnatupanga sana kama una uwezo wa kutumia 15k unalalamika nini hiyo nauli? Au ndo kipato chako laki 2.5 unajifanya unasemea wengine?
Wewe kwa siku unatumia kiasi gani cha pesa?
 
Kweli mkuu mfano watumishi wa umma wanaoishi mikoani haswa miji midogo huwa wana nafasi ya kufanya maendeleo kuliko walio mjini kutokana na gharama za maisha
Ni kweli.

Mara nyingi miji midogo ipo karibu na mashamba ambapo vyakula ni rahisi sana.

Kuna mtumishi alihamishiwa mji mdogo akitokea Jiji: alilalamika sana, ila alipofika kule akahamasika kulima.

Sasa hivi hataki kusikia kuhamishwa toka huo mji mdogo.

Nimeishi miji ya Kibaya (Kiteto), Kisarawe, na Kibaha. Ukweli usemwe tu watu wa huko ni 🔥
 
Sema na kuishi mbali sana jau,
Hapo mkuu kama hio ratiba ni kweli nakuonea huruma,

Sometimes tunakimbilia viwanja vya bei rahisi ila mara mia ulipe pesa kubwa upate sehemu nzuri sio kujificha huko porini.
Kuna jamaa alikataa kununua kiwanja tabata mwaka 1992.......leo?
 
kwahiyo kama unafanya kazi Kariakoo, ujenge Magomeni, Sinza, Keko, Chang'ombe nk, unajua bei ya maeneo karibu na hiyo unayosema kariakoo.

Watu wanaopt kukaa mbagara na huko Kibaha kutokana na bei ya viwanja kuwa rahisi maana hata hapo kwenye viwanja napo hapana control.

Serikali inajukumu kubwa kufanya standard ya maisha ya watu wake inakuwa nzuri na pia ina jukumu la kufanya bei za bidhaa na huduma zinaendana na uhalisia wa watu wake.

Kama Serikali inashindwa kucontrol mifumo inayopandisha gharama za maisha kwanini tusiilaumu, kama serikali imeshindwa kucontrol bei za mafuta, imeshindwa kujenga miundo mbinu na kurahisisha huduma za usafiri kwenye miji kwanini isilaumiwe?
Hata ukilaumu hakuna wakujibu au kutatua changamoto yako, Hata wapinzani sio wapinzani wa kweli.. labda Tuanzishe chama chetu cha siasa.. cha JF
 
Naandika hii mada nikiwa na uchungu moyoni.

Sasa hivi nina miezi kama 4 hivi natumia Daladala kwenda na kurudi kazini na mara chache, tena chache sana huwa natumia bodaboda kazini mpaka home, home mpaka kazini.

Kutoka Nyumbani mpaka kazini nikipanda bodaboda direct ni elfu 15. Go and return inalala 30000 sh
Nikipanda bodaboda 1500 sh. mpaka kituo cha Daladala na nikipanda Daladala moja mpaka kazini awali nilikuwa natumia 1000 sh. Jumla 2500 sh, kwenda na kurudi natumia sh. 5000 kamili, nikipanda gari mbili nilikuwa natumia kama elfu 6 hivi. Pesa ambayo himilivu kwangu.

Ila sasa nikipanda Daladala itanilazimu nitumie takribani 7000 kwenda na kurudi.

Hapo ukiweka na chakula na maji around 5000.

Kwahiyo Mimi tu inabidi nitumie angalau elfu 12 kwaajili ya kazini. Familia kwa sasa hali ilivyo kwa siku ni sh. 10 -20 hapo mahitaji yote muhimu kama gas, mkaa, chumvi, Michele na unga viko ndani. Kama havipo lazima uangushe 20.

Kwahiyo inanilazimu kwa siku nitumie kuanzia elfu 30.

Vipi kwa anayelipwa laki 2.5 au laki tatu kwa Wahindi?

Vipi anayelipwa elfu 7 kiwandani kwa siku?

Kipato changu kidogo nahisi kupata msongo wa mawazo.
Kwa mwezi natumia karibu milioni 1 kwa chakula nyumbani , kazini , usafiri na dharura ndogondogo.
Hapo ukiweka dharura kubwakubwa kama kufiwa na ada za shule watoto mwezi mmoja naangusha zaidi ya milioni.

Serikali ipunguze nauli, watu wanashindia mihogo makazini Ili kubana nauli za kurudia nyumbani jioni.

Hakuna mtumishi wa umma au mwajiriwa wa sekta binafsi Dar es Salaam anaweza kununua kiwanja center labda awe fisadi. Wengi tunajuchanga tunapata viwanja Chanika, Bagamoyo, Kisarawe, Pugu n.k.

Kwa nauli hizi Ili ugeuke na gari upate seat lazima ujipange. Unakuta kila ukipiga hesabu 20 imeenda kwa usafiri na misosi.

Umaskini utaendelea kutupiga maana hatuna mtetezi.
Ombeni uhamisho mkoani kwa pesa hiyo unafanya vitu vingi vya msingi ikiwemo uwekezaji mkuu
 
Mashambani kazi zimejaa hamtaki.
  • Je Uma maanisha vibarua vya mashamba ya makampuni ambavyo hulipa 5,000/- kwa siku inayoanza saa 1 mpaka 10 jioni?
  • Kama ni mamba ya kujilimia, kilimo si kazi lelemama kama wengi wanavyodhani.
  • Ushauri wangu: Ni vyema kijana kwenda mji mwingine wenye ahueni ya maisha - hasa miji ya mipakani - akaendeleze pambano huko.
 
Mkuu ukiwa unatafuta maisha , lazima uhakikishe kwa namna yoyote unajibana , ukipiga andazi la Mia 500 sidhani kama utakufa.

Kama haujatoka familia zenye uwezo unatakiwa uishi kibabe sana kutoboa.
Mwana wewe ni hustler nakumbuka zama zangu najitafuta nishapiga sana Andazi chai mchana siku Mambo yakiwa poa tunapiga menu CBE pale
 
Back
Top Bottom