Dereva Halima aliyekatika mkono asema 'Niliona mtu ninayemjua akivuka barabara kabla ya ajali'

Dereva Halima aliyekatika mkono asema 'Niliona mtu ninayemjua akivuka barabara kabla ya ajali'

Afrika ulozi upo sana tu..sema wafia dini za wazungu na waarabu watabisha.

Chamsingi omba yasikukute.

#MaendeleoHayanaChama
Mkuu kama wewe ni mfia imani ya ulozi hiyo ni imani yako,bado na wewe una uswahili wa kutujua nini maana ya imani.Kuamini miujiza ya imani hii na kuipinga ya upande mwingine ni kituko.
 
[emoji1787][emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Acheni kutupiga fix jamani. Madereva wa long trip za Bongo tu ndiyo wanakutana na vitu vingi na siyo sehemu nyingine duniani![emoji1787][emoji1787]
Unapinga
 
Mauzauza yapo barabarani,ilikuwa ni ghafla sana nilishutukia kitu kama Mbwa anakatiza barabara,sikutaka kumkwepa kwani umbali ulikuwa ni mdogo sana na ni usiku,nikamgonga na ngao ikapasuka nikasikia kabisa imedondoka na vipande vimepasuka kwa chini,Nikasimama kama mita 300 kuangalia nikakuta kweli imepasuka,nikasema ngoja nirudi labda naweza kuokoa baadhi ya vitu vilivyo dondoka,siku ona Mbwa,wala kilichoangauka,wala damu.Yani barabara ni nyeupe kama hakuna kilichotokea,kesho yake nikapita mchana ili niangalie vizuri sikuona chochote,ukichukulia kuwa pamenyooka kabisa.Nikaulizia wanaopafahamu wakaniambia hapa hivyo vitu vya kawaida sana.Wanaojua njia ya Babati Arusha karibu na daraja la Kiongozi...
Duuuhh..!!!mbona hatari ukikwepa unakutana na ajali na ukigonga unakutana na msala vilevile sa tufanyeje hapo....????
 
Akubali tu alishindwa kulimudu gari kwenye kona kutokana na kuwa katika mwendo mkali. Hayo mambo ya kumkwepa mtu anaye mfahamu, na kushindwa kulimudu gari na kupinduka; ni utetezi wa kufikirika.

Yaani ni sawa na mtu afanye kitendo cha ubakaji, halafu ajitete eti Shetani alinipitia! Alikupitia kwenda wapi!

All in all, pole nyingi kwake. Hata mimi niliyaona yale mahojiano yake na yule mwandishi wa Azam Media.

Exactly. Utetezi wa kijinga sana huu, anajua miafrika inaamini chochote kile in the name of ushirikina basi nae kapita hapo hapo.

Huyu gari lilimshinda aache ngonjera zilizopitwa na wakati.
 
Hilo linawezekana.

Uchovu, mawazo, mwili kuishiwa maji na safari za nenda rudi zisizoisha zinapelekea upatwe na hallucinations

Miafrika haiwezi kukuelewa sababu washaambiwa ni ushirikina. Zinapokuja story za ushirikina miafrika inatupa reasoning out the window.

Huyu gari lilimshinda au kama aliona kitu basi she was really hallucinating which can be scientifically diagnosed.
 
Mi kuna siku kama saa nne usiku niligonga fisi nzega pale mbele ya stend kwenye sheli fisi jamani inatoka wapi mjini
 
Msigwa huyo akaweka kiini macho ili dereva aangushe gari, abiria wafe yeye apate kafara, huyu baba atatuua wangoni wote khaaah.

Tutamchoka na tutamfurusha km mwenzie Ottawa. Msieeew zake.
Kwani gari zake zinapata Sana ajali
 
Back
Top Bottom