Erdogan azitaka nchi za kiislamu kuungana dhidi ya taifa la Israel

Erdogan azitaka nchi za kiislamu kuungana dhidi ya taifa la Israel

Hizo nchi zenyewe za Kiislamu zinaongozwa na viongozi wakiambiwa wachague upande wa Marekani au Palestina watachagua Marekani.... maana ndio main sponsor wao. Egypt angeweza kuikomboa Palestina, lakini it is not in their leaders interest
Pole sana unaongea usichokijua.
Nchi za kiarabu zinatamani sana kuwa mbali na Marekani ila kwa mazingira waliyowekewa sasa hawawezi.
Ila wanatafuta wa kumtegemea haswa kijeshi,ndio uone USA atakavyokataliwa.
Huko Red sea Oman,Bahrain na mataifa kadhaa ikiwemo Saudi washaanza kuonesha upinzani kwa USA.
Ndio mara kwanza kihistoria nchi za kiarabu zimemkatalia USA kutumia kambi zao dhidi ya YEMENI.
Kama wangekua wanamhusudu sana Marekani si wangekubali Yemeni ipigwe kupitia kambi zao!??
 
Hii ni issue ya kuiunganisha dunia nzima dhidi ya Waisraeli, si issue ya kuweka mbele Uislamu na kuugawa upinzani dhidi ya Israel kwa misingi ya kidini.

Kwa kauli hizi kuna watu wataaminishwa hii ni vita ya kidini, Waislamu wanataka kutawala dunia, unaona wanaitana wao kwa wao tu kumpinga Mu Israeli?
Predictions ziko hivyo:
"Kuungana Kwa nchi za kiislamu dhidi ya Israel" . Laja! kama si Leo basi kesho. Isitoshe, uasama wa Palestine and Israel una chimbuko la kiimani Kwa hiyo sishangai.
 
Nikisema wewe hakuna unachojua nitakua nakosea!??
Hao BRAZIL,SPAIN,COLOMBIA,MEXICO,BELGIUM wote walifanya maamuzi baada ya kuona kilichofanyika na kilichosikika Arab peace summit.
Arab peace summit walihudhuria takriban MATAIFA YOTE YA G20 ikiwemo South Africa.
Kiongozi wa Brazil,Spain,Colombia n.k n.k wote walihudhuria,na wakatoa risala zao na maoni yao ya nini kifanyike juu ya mzozo wa Israel dhidi ya Gaza.
Na katika hiko kikao Elsisi na viongozi wengine walionesha ushahidi na mlolongo mzima wa kilichotokea Gaza kuanzia August mpaka kuja Oktoba 7.
Pia wakajadili mzozo kuanzia 1947 ilipochorwa mipaka ya Israel na Palestina kuja mpaka mipaka ya sasa ya Palestina iliyodhulumiwa.
Hadi ANTONIO GUTTERES GS wa UN alihudhuria.
Ndipo alitoa tamko UN security council akisisitiza kuwa"the cause of conflict is not October 7,this did not start October 7".
Asingeongea haya kama asingehudhuria Arab peace summit na kusikiliza na kuoneshwa ushahidi na WAARABU wenyewe kuhusu mzozo wa Gaza.
Na kikao kimoja cha mwisho kilifanyika wakati wa kutoa tuzo za UNRWA,kilifanyika DOHA QATAR.
Sheikh Tamim Al Thani alitoa hotuba ya wito wa mataifa yote kuungana na Palestina.
Hiko kikao viongozi wa mataifa ya EU walihudhuria akiwemo waziri wa haki za kibinadamu wa SPAIN.
Baada ya hapo ndipo mataifa yakaona alichofanya Israel ndio wakachukua hatua.
Kama isingekua WAZUNGU NA SOUTH AFRICA kuhudhuria Arab peace summit basi wasingejua ukweli uliotokea Gaza na wasingekua na mwangaza wa kufungua kesi na kwenda kinyume na Israel.
HUO USHAHIDI ALOTUMIA S.AFRICA KWENDA ICJ ALIUTOA ARAB PEACE SUMMIT.
Au wewe ulidhani kisa ni Arab peace summit basi walihudhuria mataifa ya kiarabu peke yake!!??
Hadi viongozi wa Botswana walihudhuria.
Walichofanya waarabu ni kumpa mbwa jina baya kwanza,walitumia mlengwa wa kisiasa ama kidiplomasia kuionesha dunia Israel ni taifa la namna gani,na hiyo imelipa.

Kiufupi Arab Peace Summit ndio iliyowaamsha South Africa na mataifa mengine kwenda kinyume na Israel.
Bado mweupe kuhusu huu mzozo wa middle east hujui siasa za dunia zinaendaje.
Hiyo Arab peace summit ilifanyika wapi na lini mkuu?

Kuhusu UNRWA nitasema baada ya wewe kunipa jibu la Arab peace summit.

Ahsante sana kiongozi.
 
International laws hazipo hivyo unadhani mtu akijisikia tu anapeleka jeshi? Huoni sasahivi mambo yalivyogeuka kwa israel?
Balozi zao zina fungwa katika nchi nyingi
Wana kesi icj na icc na hadi nato members kama france na germany wamesema wapo tayari kumkamata
Waisrael wanashindwa kushiriki kwenye mikusanyiko ya kimataifa kwa kuhofia usalama wao na wakishiriki wanazomewa
Biashara zimekuwa ngumu maana mizigo yao imekuwa target baharini
VIongozi wa left wing walimuonya netanyahu kama anaiangamiza israel na sasa its too late image ya israel imeshaharibika netanyahu na hitler wapo kwenye sahani moja
European union wanataka kuvunja mkataba wao na israel na wanafikiria kuwawekea vikwazo
LEo balozi yao ya mexico imechomwa moto
Mambo yanamuharibikia vibaya sana netanyahu

View: https://youtu.be/RYWaQUEDlyU
 
Pole sana unaongea usichokijua.
Nchi za kiarabu zinatamani sana kuwa mbali na Marekani ila kwa mazingira waliyowekewa sasa hawawezi.
Ila wanatafuta wa kumtegemea haswa kijeshi,ndio uone USA atakavyokataliwa.
Huko Red sea Oman,Bahrain na mataifa kadhaa ikiwemo Saudi washaanza kuonesha upinzani kwa USA.
Ndio mara kwanza kihistoria nchi za kiarabu zimemkatalia USA kutumia kambi zao dhidi ya YEMENI.
Kama wangekua wanamhusudu sana Marekani si wangekubali Yemeni ipigwe kupitia kambi zao!??
Naona hujasoma nilichoandika vizuri.

Marekani ndio sponsor wa hao viongozi wa hizo nchi za Kiarabu, hawawezi kwenda kinyume na matakwa ya bwana mkubwa . Swala la kuwapenda au kutowapenda halina maana sana
 
Hao ni waarabu si inajulikana.
Anataka kupressure Israel iache kuumiza na kuua watu.

Kama ni vita Israel haina uwezo kupambana na Turkey.

Tuache story za six days war miaka ya 60.
Sasa huyo Turkey kama ana uwezo kwa nini siku zote hizo hajamtoa Israel hapo ili awaweke hao waislamu wenzake, kashindwa nini.!?
 
Edogan kasema waislamu waungane kupinga hilo. Na hata Iran pia aliomba nchi za kiislamu ziingilie kati.
Wewe ni nani hadi uone sio suala la waislamu?
Wao wanaona ni suala la waislamu, kinyume chake mtakuwa mnajipendekeza tu.
Hili ni suala la human right abuse, hao ni wabaguzi wa kidini tu wanaendekeza udini kwenye human rights issue.

Wewe pia ni mbaguzi wa kidini ndiyo maana unaona ubaguzi wa kidini ni sawa tu.
 
Sasa huyo Turkey kama ana uwezo kwa nini siku zote hizo hajamtoa Israel hapo ili awaweke hao waislamu wenzake, kashindwa nini.!?
Siasa za kimataifa haziendi hivyo mzee kama mpangaji anayehamishwa na mwenye nyumba.
Turkey inakemea inachofanya Israel hawajasema wanataka kuitoa Israel pale, au umemsikia Erdogan anasema anataka kuitoa Israel ilipo?
 
Mbona huyo muislam wa kwenye picha hapo yeye hana sijda? Au huwa hasali kwa kuinama?
Unachukia mpaka sijida!!..nyi watu mna chuki Sana,nikikuonesha Aya ya QUR'AN kuwa mtume alikua na sijida utapunguza kuichukia sijda au utazidisha chuki?
 
Predictions ziko hivyo:
"Kuungana Kwa nchi za kiislamu dhidi ya Israel" . Laja! kama si Leo basi kesho. Isitoshe, uasama wa Palestine and Israel una chimbuko la kiimani Kwa hiyo sishangai.
Sasa tatizo limeanzia kwenye imani, halafu unataka kulitatua humo humi ndani ya imani?

Unataka kuvunja nyumba wakati umo ndani ya nyumba, utaumia tu.

Albert Einstein alisema hivi:-

"No problem can be solved from the same level of consciousness that created it."

Hili ndilo tatizo la kutumia udini kutaka ku tatua mgogoro ulioanzia kwenye udini.
 
Kuomba kwako pia kunathibitisha Mungu hayupo.

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo kusingekuwa nan haja ya mtu yeyote kuombe chochote.

Ukiona mtu yeyote anamuomba Mungu ujue huo ni uthibitisho kwamba huyo Mungu hayupo.

Angekuwepo, kwa sifa zake hizo za ujuzi wa yote, uwezo wote na upendo wote, angewapa waja wake wote mahitaji yao yote mazuri kabla hawajamuomba, na yasiyofaa angewanyima hata uwezo wa kuyajua was8ngeweza kuyaomba.

Umeelewa?
Mkuu sijakuelewa.
 
Lakini kwa nini hii issue iwe about Waislamu na si wapenda haki wote tu wa dunia?

Tunaidogoshaje issue ya haki za binadamu, kitu ambacho ni universal, iwe issue ya Waislamu tu?
Erdogan anajaribu kuuamsha ulimwengu wa kiislamu kuitetea pia Palestine,wasibakie kimya ndugu zao wanaponyanyaswa.
 
Unataka aje huku kwa binaadamu kama yule mungu wenu aliyetandikwa msalabani hadi na yeye akaomba msaada kwa mungu?
Cha kusikitisha tu ni kwamba aliowafia lakini hawajitambui na bado wanamtumikia shetani ni wengi na moja wao ni wewe.
 
Siasa za kimataifa haziendi hivyo mzee kama mpangaji anayehamishwa na mwenye nyumba.
Turkey inakemea inachofanya Israel hawajasema wanataka kuitoa Israel pale, au umemsikia Erdogan anasema anataka kuitoa Israel ilipo?
Angalau wewe unaelewa ukweli ulivyo kwamba hakuna mbabe wa kuweza kuiondoa Israel pale alipo, hakuna.
 
Mkuu sijakuelewa.
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kama angekuwapo, angekupa hicho unachoomba kabla hujajua kwamba unakihitaji.

Ukijiona unahitaji kitu mpaka ukaamua kumuomba Mungu akupe, kitendo cha wewe kuhitaji kitu mpaka ukafikia stage ya kumuomba Mungu ni uthibitisho kwamba Mungu huyo hayupo.
 
Cha kusikitisha tu ni kwamba aliowafia lakini hawajitambui na bado wanamtumikia shetani ni wengi na moja wao ni wewe.
Kwahiyo mungu amekufa? Makubwa haya
Mzee wa upako ana ujumbe wako hapo chini
 

Attachments

  • Screenshot_20240530-084924_Instagram.jpg
    Screenshot_20240530-084924_Instagram.jpg
    230.2 KB · Views: 1
Kwakuwa naujua Uislamu vizuri hapa sisemi kitu.
Hizo nchi zisizo za kiislamu na zinajifanya kuutetea Uislamu iko siku watajuta.
Napinga mauaji yoyote yale ya Binadamu hata wanyama.

Kiundani hii ni vita kamili ya Uislamu na Uyahudi.
Kwa nje ni vita ya kijamii na jamii kupigania haki na maslahi.

Udini ndio unao changia kwa kiasi kikubwa vita ua Israeli na Palestina.
Kama dini hazina Upendo na msamaha, haziwezi kumaliza vita.
waacheni wachinjane mpala mmoja amuheshimu mwenzake au wote waishe.

Kama Kongo, Sudani, Somalia watu wanaamua kuchinjana wenyewe kwa wenyewe na hawataki mazungumzo ya kukaa pamoja na kuelewana hao Wapalestina na Wayahudi wana nini cha maana zaidi?

Waacheni wachinjane hadi waheshimiane.
Hakuna Upendo na Msamaha duniani bila kumjua Kristo Mwokozi.

Uislamu unafundisha Jino kwa Jino.
Uyahudi unafundisha jino kwa jino.

Waacheni wachinjane hadi akili iwarudie.

wafe wote sisi tunao onekana wajinga kwa kufundishwa upendo na msamaha takazikalie hizo nchi.

Hao wote si wanafundishana Wazinzi na Wezi wapigwe mawe hadi kufa na wazinzi na wezi wanao jificha.

Waacheni hao Wazinzi waliojificha na kuwauwa wengine kwa kuwaonea wapigane mawe hadi wafe wote.
Wafu wakawazike wafu wao.

Napenda kumtambua Mkuu wa Mkoa wa Arusha. Mheshimiwa Makonda kwa kazi nzuri anayo ifanya.
Wakuu wa Mikoa wengine waendelee kukaa ofisini wakipungwa na viyoyozi.
Chai na kahawa iko pembeni.

Naomba Ukuu wa Wilaya nijaribu kufanya kazi kama Mheshimiwa Makonda.
Nikifuzu nipewe Ukuu wa Mkoa.
 
Back
Top Bottom