Fei Toto agonga mwamba TFF, bado ni mali ya Yanga

Fei Toto agonga mwamba TFF, bado ni mali ya Yanga

Hii sio kesi ya Jamhuri dhidi ya Yanga, Kuna kesi na shauri na wenye shauri lao watapewa nakala ya maamuzi ya shauri lao, wakitaka wataweka public wasipotaka huna mamlaka ya kuambiwa wewe au umma vipengele walivyotumia. Yanga na Fei ndio wanaopewa nakala zao na usiwe bendera fata upepo. Sio kila kesi lazima iwe public, Kuna mapitio mengine yanabaki siri kwa wenye mashauri hayo.
Hakuna kitu kama hicho, wakina Shafii Dauda wanafungiwa kila kitu kilikuwa open

TFF ndio chombo kinachohitajika kufanya hayo yote kuweka kila kitu bayana, hizi habari za kusema wahusika hivi wahusika vile inaongeza mashaka kuwa maamuzi yaliyotolewa hayakuwa fair.
 
Yanga timu yangu pendwa, muachieni kijana aende zake pale nafsi yake inapomtuma, fei amekosea dhahri lakini kukosea kwake isiwe kigezo cha kumkomoa kijana huyu na kumuharibia maisha na kumuumiza kisaikolojia, fanyeni wema huo, aende zake huku mkimpa onyo.
 
Faini yenye faida kwa timu anayochezea?
Unapigwa na TFF sababu wao ndio wenye mpira wao na Yanga ni mwanachama wao.

Kwanza tushukuru tu Tz sio kama ulaya ila mbele ,wasingeishia hapo ,wangetrace ile mil 110 imetoka kwa Fei au kwa timu nyingine.

Tunajua nyuma hili sakata yupo Azam na Yusuph, sema kibongo bongo hili hatuto lifuatilia.
 
Yanga timu yangu pendwa, muachieni kijana aende zake pale nafsi yake inapomtuma, fei amekosea dhahri lakini kukosea kwake isiwe kigezo cha kumkomoa kijana huyu na kumuharibia maisha na kumuumiza kisaikolojia, fanyeni wema huo, aende zake huku mkimpa onyo.
Biashara haina huruma mkuu ukifanya biashara kwa kuoneana huruma utakufa masikini, unamkumbuka singano wa simba jinsi alivyowasumbua na kesi yake ya madai???
 
Mahakama gani umewahi kuona inaweka mwenendo wa kesi gazetini zaidi ya hukumu? Mbona mnajitoa ufahamu kama watoto?
Mchanganuo wa hukumu mbona unawekwa wazi

Hata kesi ya mbowe mbona watu tulikuwa tunajua kila nukta inayoendelea, hata jaji akikohoa tunajua
 
Mchanganuo wa hukumu mbona unawekwa wazi

Hata kesi ya mbowe mbona watu tulikuwa tunajua kila nukta inayoendelea, hata jaji akikohoa tunajua
Mahakama ipi uliona inaweka mwenendo wa kesi ya Mbowe zaidi ya Martine Maranja Masese ambaye ni mwanachama wa CHADEMA? Wewe ukajua Jaji ndo alikuwa anaandika mitandaoni?
 
Kuna watu Wana viwango vya chini vya uelewa mpaka unashangaa wanatembeaje barabarani bila kugongwa na magari.
Wewe na Uyanga wako jikite kwenye hoja achana na mipasho ya kimhemko haikusaidii chochote zaidi inakushushia credibility

Nimekupa mifano jinsi kesi zinavyotolewa mchanganuo wa kimaamuzi ikiainisha vifungu vya sheria walivyotumia kuhukumu

Kesi ya Mananra mbona TFF ilikaa masaa mawili mbele ya mic na waandishi wa habari ikitoa mchanganuo?

Una mahaba sana na Yanga mpaka unajisahau
 
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo tarehe 2 Machi, 2023 kwa ajili ya kusikiliza pamoja na mambo mengine shauri la mapitio (Review) ya uamuzi wake wa tarehe 9 Januari 2023 kati ya Feisal Salumu na Klabu ya Young Africans kama yalivyowasilishwa na muombaji Feisal Salum dhidi ya Klabu ya Young Africans.

Baada ya kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote mbili Kamati imeona kuwa shauri hilo la mapitio (Review) halina msingi wa kisheria kushawishi

Kamati kubadili maamuzi yake yaliyotolewa awali hivyo imetupilia mbali shauri hilo.

Sababu kwa undani za uamuzi huo zitatolewa kwa pande zote mbili zinazohusika katika shauri hilo siku ya Jumatatu 6 Machi, 2023.

View attachment 2535208
Huyu dogo alikuwa sahihi kabisa kujiita Fei Toto!
 
Yanga timu yangu pendwa, muachieni kijana aende zake pale nafsi yake inapomtuma, fei amekosea dhahri lakini kukosea kwake isiwe kigezo cha kumkomoa kijana huyu na kumuharibia maisha na kumuumiza kisaikolojia, fanyeni wema huo, aende zake huku mkimpa onyo.
Aondoke kisheria, sio kihuni. Ana/alikuwa na mkataba wa kisheria na Dar Young Africans, angetumia sheria kutengua mkataba wake na Yanga. Kijana anajiumiza na kujimaliza mwenyewe kisoka, soka ni career fupi sana, asipokuwa makini atajutia mda anaopoteza.
 
Unapigwa na TFF sababu wao ndio wenye mpira wao na Yanga ni mwanachama wao.

Kwanza tushukuru tu Tz sio kama ulaya ila mbele ,wasingeishia hapo ,wangetrace ile mil 110 imetoka kwa Fei au kwa timu nyingine.

Tunajua nyuma hili sakata yupo Azam na Yusuph, sema kibongo bongo hili hatuto lifuatilia.
OKey, embu tusubiri kama itatoka faini iwapo hatorudi na itakuwa kiasi gani na iwapo italipwa na kama haitolipwa ni nn kitatokea. Uwezekano wa Yanga kumwachia Fei bado upo, sioni "WIN" kwa Yanga iwapo hakuna dau kubwa la fei hata akirudi kambini akakaa tu.
 
Mahakama ipi uliona inaweka mwenendo wa kesi ya Mbowe zaidi ya Martine Maranja Masese ambaye ni mwanachama wa CHADEMA? Wewe ukajua Jaji ndo alikuwa anaandika mitandaoni?
Nani kasema jaji ndio anayepaswa kufanya hilo?

Unaelewa hata unachokiandika hapa?
 
Aondoke kisheria, sio kihuni. Ana/alikuwa na mkataba wa kisheria na Dar Young Africans, angetumia sheria kutengua mkataba wake na Yanga. Kijana anajiumiza na kujimaliza mwenyewe kisoka, soka ni career fupi sana, asipokuwa makini atajutia mda anaopoteza.
Geuka mzazi, mkataba uweke pembeni, huyu ni kijana, ujana maji ya moto.
 
Back
Top Bottom