Haji Manara: Paul Makonda ulinilaza Korokoroni, acha dunia izunguke kwenye Mhimili wake

Haji Manara: Paul Makonda ulinilaza Korokoroni, acha dunia izunguke kwenye Mhimili wake

Manara aishi kwa akili na sio mihemuko Makonda anaweza rudi tena kwenye uongozi ataificha wapi sura yake? Tunajua anapewa shinikizo na GSM hilo liko wazi.

Ghafla makonda karudi kuwa mkuu wa mkoa manara atauweka wapi uso wake?

Manara ni tapeli mkubwa, ametapeli wengi tu sijajua bifu lake na kigogo limeishia wapi.
Mkuu wa mkoa wa wapi?
 
Manara aishi kwa akili na sio mihemuko Makonda anaweza rudi tena kwenye uongozi ataificha wapi sura yake? Tunajua anapewa shinikizo na GSM hilo liko wazi.

Ghafla makonda karudi kuwa mkuu wa mkoa manara atauweka wapi uso wake?

Manara ni tapeli mkubwa, ametapeli wengi tu sijajua bifu lake na kigogo limeishia wapi.

Kurudi tena, NEVER.!

Makonda alishafutwa na Gwajima kwenye siasa kama Ndugai tu, walicheza na mpakwa mafuta.
 
Makonda hawezi safishika kwa lolote kwa jik wala steel waya wala kumloweka kwenye sabuni ya Omo na lile bichwa lilobeba meno tuu. Nakumbuka alivyokaidi ile alivyokuwa akitwa kanisani kwenye msiba wa Mh. Mengi na suruali zake za jeans................. yaani huyu mtu aombe sana maisha yake yako kama sijui hata nifananishe na nini shenzy kabisa yule... huwa namhurumia yule binti mzuri alieolewa na jitu kama lile mnyama sio mnyama fisi sio fisi... acha aanze kurudisha mali za wenyewe moja baada ya nyingine. Na jinsi hakuwa na akili kichwa ambacho ni hifadhi ya meno pekee anazozana na mali inayoosha sio yake
Mimi nakumbuka kipindi anazozana/anaongea na Baraza la Habari Tanzania alivyokuwa anaongea kwa nyodo, dah aisee huyu jamaa napenda alipwe kadili ya matendo yake
 
Umesema kweli kabisa,nilisikia Manara aliwekwa ndani kwa sababu alifanya kosa, yani mtu ufanye utapeli huko alafu ukamatwe leo uje umsingizie Bashite ndio alikukamata na hata kama ingekuwa Bashite ndio aliagiza Manara akamatwe bado ni sahihi tu
Mkuu unaweza sema jambo moja lingine ambalo bashote aliwahi kufanya kwa usahihi ili tujumlishe na hili la Manara?
 
cCM hawarudishagi mali, na hata ikitokea amerudisha zitaliwa na CCM wenzake, kwani zile Range rover zilizookotwa na mwenda zake pale bandarini na akasema zipigwe mnada zilipigwa ? Mali za sabaya zimekamatwa ? Ukiacha ile “vieitee” ambayo ipo Takukuru
Kuna vile vichwa vya Treni viliokotwa bandarini, hivi ishu yake iliishia wapi? Ajabu sana hii, eti serikali ya Jiwe imeokota vichwa vya treni bandarini
 
Mimi nakumbuka kipindi anazozana/anaongea na Baraza la Habari Tanzania alivyokuwa anaongea kwa nyodo, dah aisee huyu jamaa napenda alipwe kadili ya matendo yake
Ninachojua huwa htumii akili kabisa lile bichwa ni sehemu ya kuhifadhi meno aweze kula tuu... hana akili kabisa angalia hata ongea yake. acha sasa hivi dunia imfundishe na sidhani kama analijua hilo
 
Maskini akipata matako hulia mpwata mpwata mpyuuu [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 

✍️Heshimu watu brother...Cheo, Umaarufu na Pesa huondoka... Sponsors hufa!

📌Ni kweli Paul Makonda alikua na madhaifu mengi tu ya kiuongozi kama walivyo viongozi wengine..

Lakini kabla hujamnyooshea kidole jiulize wewe ukiwa Simba uliwatukana wangapi?
Angekuwepo Magufuli na wewe ukaendelea kubaki Simba ungeyasema haya?

📌Wewe sindio ulisema Yanga wenye akili ni Baba yako na Mzee Kikwete? Uliwaumiza wangapi kwa kauli yako hii?

📌Uliwatukana waandishi wa habari wangapi?
Nakukumbusha baadhi yao Shaffih Dauda,Priscar Kishamba ,Maulid Kitenge na wengine wengi tu.

📌Unadhani bila huruma ya GSM wewe ungekuwa wapi leo?
Unadhani GSM asingekuwepo Yanga, ungefanya kazi Yanga wewe?

📌Leo uko Yanga kila siku kumtukana Mohamed Dewji na Barbara Gonzalez hilo huoni kama ni tatizo?

📌Umewaumiza wangapi kibiashara ukiwa Yanga? Dauda, Clouds,Vunjabei na hata GSM mwenyewe kuna sehemu umemuumiza sana sema hataki kusema tu.

📌Kwanini huo uungwana unaouhubiri usiufanye wewe?

📌Ni kweli inafahamika upo Yanga kwa kazi moja tu ya kuitukana Simba (hasa Mo Dewji) na kuwasifia GSM

📌Ni kweli tunajua bado unaipenda Simba ndio maana hujawahi kuwakejeli wala kuwatukana wachezaji wa Simba ispokuwa Mo Dewji na Barbara Gonzalez waliokuondoa kwenye nafasi yako

📌Lakini, unajiskiaje unapomshambulia na kumtukana mtu kila siku ambaye hakujibu? Imani yako inasemaje?

📌Tatizo lako Brother unataka kila kitu uwe wewe...Yaani Diamond uwe wewe,Samatta uwe wewe, Mayele uwe wewe,Rais uwe wewe,Gharib uwe wewe nk

Unataka ku-trend wewe tu....!!

📌Kabla hujamnyooshea kidole mwenzio angalia hivyo vidole vitatu vinavyokuangalia wewe..

Credit Sospeter Ilagila
Kwenye mpira hakuna adui wa kudumu
 
Uko sahihi, lakini kusema Bashite alikuwa na madhaifu ya kiuongozi kama viongozi wengine siyo sawa, umerahisisha sana, jamaa alikuwa muuaji, katili na asiyeheshimu viongozi wenzake wala kujali mipaka yake.
Alimuua nani?

Tuwekee uthibitisho.
 
Habari za swaumu ndugu zangu,

Ni miezi mitukufu kwa waislam na wakristo kwa kila mmoja kwa imani yake wakitekeleza amri ya mungu ya kufunga kwa kujizuia kula na kunywa kwa kulingana na dini husika.

Kwa siku za karibuni kumekuwa na mgogoro au tofauti kati ya aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam bwana paul makonda na GSM ambao ni wadhamini wa dar young African ila issue sio huo utofauti bali ni mapokezi ya huo utofauti wao,

Katika hali isiyo ya kawaida yule mhamasishaji wa yanga akaingia king moja kwa moja kupambana na makonda ambaye kipindi yupo SIMBA alikuwa swahiba wake ila mambo yamekuwa tofauti baada ya kuhamia jangwani.

Sasa cha kuahangaza ni kitendo cha manara kupost picha au videos za kumkejeli makonda kupitia social network zake kitu ambacho watu walikipokea tofauti maana mpira na siasa haviendani ila manara hajawahi kukubali kushindwa na makonda vile hajawahi kurudi nyuma.

Manara ataiweza vita iliyomshinda ruge na baadhi ya viongozi wakubwa wa serikali hata kama kwa sasa hayupo madarakani ila bado ni mtu hatari kwenye mambo ya siasa na anajua umafia wote ndani na nje ya serikali ngoja tuone nani ataibuka mshindi japo makonda hajaanza kujibu mashambulizi bado.

Manara ataiweza vita ya makonda ngoja tuone nani mtoto wa mjini manara akipita hapa basi kweli yeye atakuwa mtoto wa mjini.
 
Sasa manara ana nn cha kumuweza makonda? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kitenge tyuuh anamshindwa, ndo amuweze Paul? Khaaah.
 
Manara ni mshamba ni mnafiki japo makonda kakosea sana ila manara ataingia kwenye 18 za watu ipo sku ajiangalie sana
 
vita na Mo imeisha mpaka ahamie kwa makonda
msukule sio mzima kichwani
 
Manara ni messenger tu kuna watu wako nyuma yake nae anawaamini.
 
Manara anaamini ronaldinho wa 2006 sio gaucho wa 2022,naona ndio maana kajiweka mbele.
 
Manara alipaswa ajiulize mala mbilimbili kabla haja Anza kirusha mawe kwenye nyumba ya vioo maana vingine unaweza rusha kumbe vioo ni bullet proof
 
Back
Top Bottom