Haji Manara popote ulipo au ukisaidiwa na Yanga SC Wenzako mkinijibu haya Maswali yangu Muhimu nitashukuru

Haji Manara popote ulipo au ukisaidiwa na Yanga SC Wenzako mkinijibu haya Maswali yangu Muhimu nitashukuru

" Wenye Akili Yanga SC nzima ni Watu Wawili tu Rais Mstaafu Kikwete na Baba yangu Mzazi Mzee Manara waliobakia wote hawana," alisema Haji Manara alipokuwa akihojiwa na EFM Radio Kipindi cha Sports Headquarters mwaka 2021.

Baada ya Nukuu ( Kumbukizi ) hii sasa Maswali Kuntu ya GENTAMYCINE yanaanza............

1. Haji Manara hivi ni Wewe ndiyo umetengeneza Brand yako kama unavyojitapa Kutwa au ni Simba SC na sasa Yanga SC uliko ndiyo zimekutengenezea Brand yako kutokana na Ukubwa wa Vilabu hivi Viwili na Ushawishi wao nchini?

2. Haji Manara hivi ungekuwa ni Msemaji wa Ihefu FC au Gwambina FC una uhakika ungejulikana na ungekuwa Maarufu mpaka kuwa na hiyo Brand yako Kubwa inayokudanganya mpaka Unadharau Watu na kujiona uko juu ya Mpira wa Tanzania?

3. Haji Manara kama umesema jana kuwa unajua Siri nyingi za TFF ( hasa Maadui zako Rais Karia na Katibu wa TFF Kidau ) je, kwanini hukuzitoa ( hukujilipua nazo ) Siku nyingi ili utusaidie Wadau wa Mpira kujua tusiyoyajua na badala yake Umeyatoa jana kwa Mtindo wa Kukomoa, Propaganda na Kulipiza Kisasi?

4. Haji Manara je, TFF ( Unayoichukia zaidi ) ingekuwa inakuonea ingekufungulia ilipoingia Madarakani baada ya Kufungiwa na aliyekuwa Rais wa TFF ( Mwana Yanga SC ) Jamal Malinzi?

5. Haji Manara bila Busara na Nguvu Kubwa ya TFF Kukulinda unadhani kwa Kosa lile Kubwa na la Jinai ulilomfanyia Mtangazaji wa Kike wa Michezo wa Clouds FM Prisca Kishamba na ile Kauli yako ya HATARI Kiusalama, Kimichezo na Kiutalii uliyoitoa dhidi ya Timu Ngeni zilizokuwa zikija Kucheza na Simba SC ( katika CAFCL na CAFCC ) kuwa wawe Makini kwani Simba SC inatumia Sumu na hata Kuua una uhakika kuwa leo hii usingefungiwa Maisha katika Medani za Soka na pengine hata Kufungiwa na Serikali?

6. Haji Manara aliyekushtaki hadi Kufungwa Kwako huko ni Uliyegombana nae Arusha Rais wa TFF Wallace Karia au ni Sekretarieti ya TFF? Je, ule Msamaha wako wa Kinafiki ulitakiwa uutoe wa Sekretarieti ya TFF au kwa Rais wa TFF Wallace Karia tena Nyumbani Kwake?

7. Haji Manara je, unajua kuwa kwa Kitendo chako cha Jana tu kusema ( tena Kijeuri kabisa ) kuwa Wewe bado ni Msemaji na Mhamasishaji wa Yanga SC wakati tayari Unatumikia Adhabu Kisheria kinaweza kukufanya Uongezewe Adhabu yako zaidi na sasa ikawa Kali kuliko hiyo Ndogo tu uliyopewa?

8. Haji Manara ni kwanini Matatizo yako Binafsi yakipelekea Wewe Kuadhibiwa na Mamlaka huwa unapenda Kuihusisha Klabu ya Yanga ili upate Huruma na Sapoti yao?

9. Haji Manara je, Maudhui yako ya Jana ( pamoja na Matusi, Dhihaka na Kashfa ) katika ile Press ya Jana yalikuwa ni yako Binafsi au yana Baraka za Yanga SC kwa 100%?

10. Haji Manara je, una uhakika una Washauri wazuri na kwamba Watu wengi Wanaokuzunguka Wanakupenda na Wanakutakia Kheri kama Unavyojidanganya na Kujimwambafai Kutwa?

11. Haji Manara je, ikitokea Rais wa TFF Wallace Karia akiamua Kukushtaki 'Kijinai' kama tulivyohakikishiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya TFF iliyokuhukumu kuwa Ulimtishia Maisha Rais wa TFF Karia huku ukimwambia kuwa ATAKUKOMA na UTAMUONYESHA utaendelea kuwa Salama?

Wachezaji wa Kucheza Mpira ni Kumi na Moja ( 11 ) na Mimi GENTAMYCINE nimekuuliza haya Maswali yangu Kumi na Moja ( 11 ) na nasubiria sasa Majibu yangu kutoka Kwako Haji Manara na wana Yanga SC Wenzako wote hapa JamiiForums ili nijue kama mna Akili au hamna Kabisa kama inavyojulikana tokea Uhuru wa Taifa hili la Tanzania.
Huyu kabebwa na Simba baada ya kuondoka JERRY kwenye mpira ndioo manara kaonekana
 
Kama Rais Samia, Rais Mwinyi, Rais Mstaafu Kikwete wapo humu na ni 'Followers' wangu GENTAMYCINE Mtu Mmoja tu mwepesi Haji Manara ataacha kuwepo?

Kwa Taarifa yako tu ni kwamba 99% ya Mada zangu hapa JamiiForums nikiwa namuandikia Haji Manara ( hasa Kumsema ) huwa anafikishiwa na Chawa Wake na kupitia Kwako nikuibie Siri kuwa Haji Manara anajua kuwa Mimi GENTAMYCINE na hii ID ni Adui yake Mkubwa Mchambuzi Mahiri wa Soka wa EFM Jemedari Said Kazumari wakati hata siyo Kweli.

MImi ni Kalemera Rwigyema Mazimpaka Kadogoo Kisungura ( GENTAMYCINE) na siyo Jemedari Said Kazumari kama Haji Manara anavyodai na mara kwa mara huwa anadai hivyo.
[emoji95][emoji95][emoji817][emoji817]
 
Umeandika matapu tapu

1. Haji hakusema hivyo akihojiwa na Efm alisema hivyo akihojiwa na salama.


2. Kuhusu hoja mfu yako kusema Haji kasema Yanga hawana akili alimaanisha Yanga wanaipenda sana timu yao.

Hata mwanaume akimpenda sana mwanamke kupita kiasi anaonekana hana akili.

Bushman kama wewe huwezi kuelewa kiswahili cha watoto wa mjini.

Wasalimie Bunda vijijini
[emoji16][emoji16] duhhh kwaiyo Mzee kikwete na mzee manara ndio awaipendi yanga? ayo maneno manara aliyaongea kama unabisha tunakiwekea ja clip kabisa akiyatamka mimi ni yanga damu damu ila uyu jamaa amevuka mipaka mpira wa kistaarabu umemshinda
 
[emoji16][emoji16] duhhh kwaiyo Mzee kikwete na mzee manara ndio awaipendi yanga? ayo maneno manara aliyaongea kama unabisha tunakiwekea ja clip kabisa akiyatamka mimi ni yanga damu damu ila uyu jamaa amevuka mipaka mpira wa kistaarabu umemshinda

Hujasoma fasihi simulizi mkuu? Hujui kwanini akiwa exclude jk na baba ake? Nilisha ongea mara nyingi sana hiyo or do u want me to repeat?
 
umeuliza maswali mengi bt mi najibu la 1&2

ronaldo na mess wamechezea timu kubwa dunia bt wao wamekua maarufu zaidi kuliko wachezaji wengine kwa sababu ya upekee wa vipaji vyao.

taasisi husaidia kukuza brand bt upekee wa kipaji humfanya mhusika kujijengea dunia yake ktk jambo husika.

jiulize, wasemaji wangapi wamepita simba & yanga bt why hawajawa maarufu kama manara? jibu baki nalo mwenyewe.
 
1. Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

2. Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba

3. Waziri 'yupo yupo' Mzee George Huruma Mkuchika

4. Naibu Waziri wa Kilimo Antony Mavunde

5. Naibu Waziri wa Ardhi Ridhiwani Kikwete

6. Waziri wa TAMISEMI Bashungwa

7. Rtd. CDF Gen. Mabeyo

GENTAMYCINE nalisema hili mapema hivi na kwa nia njema tu kwani tayari kama Kawaida na Maono niliyobarikiwa nayo na Mwenyezi Mungu naona kuna HATARI Kubwa inakuja mbeleni kama Watajwa hawa hawatokaa pembeni ya hizi Jeuri zote za Mfungwa na Mdaiwa Haji Manara.

Msije kulaumu tu sikuwashauri sawa?
Siku zote kilema anajiona yeye yupo juu kuliko mtu yeyote, na ukimfanyia lolote ataona unamuonea! Wenye akili zao wanamtambua
 
😁😁😁
16588134714313.jpg
 
1. Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

2. Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba

3. Waziri 'yupo yupo' Mzee George Huruma Mkuchika

4. Naibu Waziri wa Kilimo Antony Mavunde

5. Naibu Waziri wa Ardhi Ridhiwani Kikwete

6. Waziri wa TAMISEMI Bashungwa

7. Rtd. CDF Gen. Mabeyo

GENTAMYCINE nalisema hili mapema hivi na kwa nia njema tu kwani tayari kama Kawaida na Maono niliyobarikiwa nayo na Mwenyezi Mungu naona kuna HATARI Kubwa inakuja mbeleni kama Watajwa hawa hawatokaa pembeni ya hizi Jeuri zote za Mfungwa na Mdaiwa Haji Manara.

Msije kulaumu tu sikuwashauri sawa?
CHUKI ZA MBUMBUMBU FC

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Ikiwa hivyo basi kila mwana yanga tutasema anampa kichwa manara. Sio sahih kuweka dhahania eti kisa kiongoz fulan ni mwanachama bas anampa jeuri.
Wao pia wanajua ishu za mipira hazingiliw na siasa.
 
Hoja namba 5 nzito mno kaka, ki ukweli amekosea lakini kama alivyotaka apewe hiyo nakala ya hukumu aangalie namna ya kukata rufaa.
 
Manara ni original Brand iliyotoka kwa Familia ya mchezaji wa zamani wa Yanga baba Mzazi wa haji Manara ndio ikatokea Simba wakawa na tamaa na kufuata hii Manara Brand sasa kwa kuwa Simba walitumia dawa iliyo expire ya Gentamisene basi wameshindwa Manara akarudisha Brand kwa Yanga

Sent from my SM-J730F using JamiiForums mobile app
Brand au alikuwa mwizi na tapeli kabla ya Mo kumuibua na kumleta msimbazi
 

Attachments

  • IMG-20220725-WA0006.jpg
    IMG-20220725-WA0006.jpg
    26.3 KB · Views: 3
Tatizo kubwa ninaliona mimi ni kuwa Manara alidekezwa sana na TFF, vyombo mbali mbali vya habari, watangazaji, viongozi wa vilabu, wawekezaji/wafadhili wa mpira, n.k. aidha kwa kumuogopa au kumuonea huruma kutokana na hali aliyonayo maana akiguswa tu siku zote anakimbilia ulemavu wake. Matokeo yake ndiyo haya ya kuchelea mwana kulia sasa TFF ndio italia. Manara alikuwa na makosa mengi sana tangu akiwa Simba lakini hakuchukuliwa hatua madhubuti kumuadhibu kwa kila kosa matokeo yake sasa amefanya kosa kubwa ameadhibiwa halafu anaona anonewa. Mbaya zaidi badala ya kufuata taratibu na kukata rufaa ili apate haki yake anaitisha "press" wakati siku zote taratibu za kutafuta haki ni kukata rufaa ngazi kwa ngazi.
Alipokuwa simba alikula adhabu kutoka kwa tff ya malinzi
Na utawala wa karia uliopita alipigwa faini ya mil 5 na onyo kali Mo akamlipia
 
Back
Top Bottom