Huyu mhalifu wa Selander alipaswa kukamatwa, siyo kuuawa
Vita ni vita mbona hufikilii askari wawili waliofariki
Huyo ameishaua watu wawili,tena polisi,au walitaka abambelezwe ili afunue vichwa vya wananchi kwa risasi za rashasha kisa eti niliangalia kwenye sinema ya Rainbow.
 
Polisi walipaswa kumtia nguvuni huyu mtu aliyekuwa na bunduki huko Kinondoni maeneo ya Selander. Lakini kwa kukosa weledi na kwa vile polisi Wana uoga uliokithiri wakamfyatulia risasi na kumuua.

Sasa watakosa taarifa muhimu kutoka kwa mhalifu huyu mfano:
-Ni nani?
-Katumwa na nani?
-Yuko na akina nani (wako wangapi)?
-Nini dhamira yao?

-Nini chanzo cha wao kufanya hivi?

Kwa kumuua hawajatatua tatizo.

Polisi wetu Wana ujasiri wa kuwakamata CHADEMA tu.

Kanda maalumu ya polisi jijini Dar imeshindwa vipi kumkamata mtu huyu mmoja tu??
Tukio lenyewe limedumu muda mrefu sana. Hao watu wangekuwa kama 10 je?
 
Point. Au hata angepigwa za miguu tu. Na aliyemuua ametumia risasi kama 5-8 hivi kupatia shabaha! Wakati jamaa mwenyewe alikuwa amesimama kama mti tu.
Angepigwa za miguu angeacha kuwashambulia askari? Nadhani hujawahi kishika Bunduki na hujui madhala ya bunduki. Huyo mtu alikuwa na bullet proof ndiyo maana zimetumika risasi nyingi kumuua.
 
Mungu azilaze mahali pema peponi roho za Askari wetu..

Mengine haya mnayoongea hayana umuhimu kabisa,kifo ilikuwa ni haki yake na kama kuchimba taarifa itajulikana tu zipo njia nyingi.
 
Marekani, Ufaransa, Sweden na Uingereza walishatokea watu kama hawa lkn walikamatwa na kuhojiwa.
Usifananishe marekani na hapa Bongo. Yule alikuwa na silaha angewadhuru watu. Tatizo kuna watu hawajapita JKT
 
Kuandika rahisi, ungekuwa hapo kwenye standoff usi type hiki ulichoandika

Ova
 
Mungu azilaze mahali pema peponi roho za Askari wetu..

Mengine haya mnayoongea hayana umuhimu kabisa,kifo ilikuwa ni haki yake na kama kuchimba taarifa itajulikana tu zipo njia nyingi.
Wale wa dodoma walishindikana huyu wataweza?
 
Naona hawakuwa na taarifa za kiinterijensia.., na sijuwi huwa wanategemea zaidi taarifa waletewe na nani. Njemba zingekuwa hata 3 tu mbona mchezo ungekuwa pouwa sana.
ingekuwa mechi kali siku ya leo.
 
Angepigwa za miguu angeacha kuwashambulia askari? Nadhani hujawahi kishika Bunduki na hujui madhala ya bunduki. Huyo mtu alikuwa na bullet proof ndiyo maana zimetumika risasi nyingi kumuua.
Wewe. Haya matukio yashatokea sehemu kibao huko duniani. Ufaransa kuna mwamba alitenda na mashine mahali penye mkusanyiko mkubwa kama mtaa wa Kongo pale Kariakoo. Akauwa wengi lkn polisi wanaojua upolisi hawakumuua
 
Point. Au hata angepigwa za miguu tu. Na aliyemuua ametumia risasi kama 5-8 hivi kupatia shabaha! Wakati jamaa mwenyewe alikuwa amesimama kama mti tu.
Yaaani za magotini zingemfaa zaidi😡😡🤬🤬
 
Back
Top Bottom