Iko siku hii clip ya Magufuli itapata viewers wengi sana. Naitunza hapa

Iko siku hii clip ya Magufuli itapata viewers wengi sana. Naitunza hapa

Halafu inasemekana walipofika MOROGORO walilichoma moto gari walilotumia wakati wa kumshambulia Lissu
Misuse of public properties ndo inatakiwa kuwq addressed ili tusiingie gharama wananchi wa kawaida , imagine gari la milioni 100 plus , linachomwa moto ili ku fullfill political demands
 
Mojawapo ya hotuba bora kabisa kutolewa na Mkuu wa Nchi.
Kwa wendawazimu wenzie kama alivyokuwa yeye Magufuli na wajinga kweli ni hotuba bora. Lakini kwa watu wenye akili kwenye ubongo wanakudharau. Huwezi kupanga operesheni ovu halafu ukaweka na ushahidi wa maneno kwenye hotuba.

Ila wazungu wanasema "Karma never misses a location"
 
😆😆 Na hiki ndicho kinamtesa SSH,amewaachia wanaropoka kila tumbili anaropoka..

Mtu anaenda kwenye tv Kujifanya eti anamsemea mnyonge wakati hana hata msaada Kwa huyo mnyonge..

Unaanza kupinga maendeleo anapinga tozo as if tozo zinaenda kufanya mambo binafsi ya familia..

Watu wa hivi ni ku deal nao Ili Kazi ifanyike vinginevyo utaishia kuyumbishwa kila siku..

Kuna siku nilikuambia wekeni jedwali kuonyesha ujenzi wa hivyo vituo vya afya 234 vilivyojengwa kwa tozo. Baada ya jedwali lile kuwekwa mbali ya kutokuonyesha muda wa ujenzi kuanza wa hivyo vituo, bado vituo vingi kwenye lile jedwali vilikuwepo kabla ya tozo, ile ni kiashiria hata serikali hii ya Samia inaendelea na tabia ya Magufuli ya kupika data ili kupata sifa za kijinga za kisiasa. Yaani ni bonge la aibu. Hilo moja.

La pili, Haya unayosema ya watu kuzuiwa kuongea kwenye TV huyasemi kwa bahati mbaya, bali unajua fika kwakuwa taarifa nyingi ni za kupika, unajua fika ukweli utajulikana, na sifa zo uongo unazotaka mama Samia azipate hatazipata, jambo ambalo litakuumiza nafsi yako. Ni hivi, ni ngumu kuendelea kutawala watu kwa kutegemea kulinda uongo kwa vitisho, fahamu kuwa mtaji wa wajinga huwa unaisha.
 
Hii kauli aliyoitoa Magufuli kumwambia Spika awatimue wasaliti bungeni ili wakiwa nje washughulikiwe nae, inaonesha hapa ndipo polisi wetu walipotakiwa kuanzia uchunguzi wao dhidi ya shambulio la Lissu, ajabu polisi bado wanamsubiri Lissu arudi ili wamfanyie mahojiano.

Maneno mengi aliyozungumza Magufuli kwenye hiyo video yana viashiria vingi vya mtu aliyetaka kulipa kisasi, mfano anapomwambia Spika; "watoe huku nje tuwashughulikie, kwa sababu wakiwa kule bungeni wana immunity, wanaweza kuzungumza chochote".

Anaendelea kusema; "hatuwezi kuwa vitani, halafu tukiwa mstari wa mbele, anajitokeza mmoja wetu na kuanza kuwashambulia askari wetu, huyu tuta deal nae; bora unyamaze kimya, au ukalale".

Mpaka hapo, inashangaza bado polisi wetu hawakuona mahala pa kuanzia uchunguzi wao kuhusu shambulio dhidi ya Lissu, maneno yao yamekuwa ya kisiasa sana.
Akasisitiza kabisa ikibidi wasaliti walale moja kwa moja, yaani wafe" alikuwa katili huyo mzee
 
Tozo lazima zilipwe na tozo ziko specific kwa maendeleo ya Vijijini anaepinga ni mhujumu uchumi na msaliti..

Mwendazake angekuwepo tozo mngelipa na hakuna ambae angenyanyua Domo kama vile wanafanya kina Assad,Kitwanga,Chadomo na wapuuzi wengine..

Mnadekezwa na kuchelewa Sana na SSH na sielewi kama anajua hasa aina ya watu anaowaongoza..

Ni kipi Magufuli alifanya na watu hawakumpinga? Watu kulipa tozo hata sasa wanalipa, na ingekuwa wakati wa Magufuli bado wangelipa, sio kwa kukubali au kumuogopa yoyote, bali ni kwakuwa hawana jinsi.

Wakati wa Magufuli alifanya ubabe wa kishamba, si biashara nyingi zilifungwa na akawa anashutumiwa hadharani kuwa ameharibu uchumi? Kwani sababu ya yeye kunajisi uchaguzi ni nini, si kwakuwa alijua fika matokeo halisi yangetangazwa hadharani ingekuwa fedheha kwake na chama chake?

Ukiona unaamua kutumia nguvu dhidi ya wakosoaji, ujue umefika mwisho wa uwezo wako kiuongozi, na hiyo ni dalili kuwa uko madarakani bila ridhaa ya umma, hivyo unahofia wenye ushawishi kwa umma wakiongea utapuuzwa.
 
Ni miaka 5 sasa Magufuli alipotoa kauli hii saa chache baadaye Tundu Lissu alishambuliwa Dodoma.

Nawawekea watu wa Forensic kuna siku tusiyoijua clip hii itakuwa ushahidi muhimu
Kwani shida ni nini juu ya hii kauli. Alimaanisha alichokisema wala haihitaji forensic. Yeye ni mtawala na wewe unatumwa kudanganya wananchi tukikamata makinikia wawekezaji watakimbia, mara tutashitakiwa MIGA au taifa litafilisiwa. Dawa ya waropokaji alikuwa nayo huyo Mwamba.
 
Anaendelea kusema; "hatuwezi kuwa vitani, halafu tukiwa mstari wa mbele, anajitokeza mmoja wetu na kuanza kuwashambulia askari wetu, huyu tuta deal nae; bora unyamaze kimya, au ukalale".
Ukiangalia vizuri ndugu yangu hapo huo mfano ni mzuri tu hauna kasoro yoyote:

Alikua anawazingumzia Ma-SNITCH au kiswahili kozuri Wasaliti

Wapo hata kwenye familia zetu snitch yupo tayari akuroge uwe na maisha magumu au ikiwezekana ufe kabisa upotelee uko ili yeye afurahi

Hakuna alipotaja Lisu hapo mboni ni story ya kawaida tu hio na inaeleweka sema wewe ume-generalize mambo tuwe na kiasi jamani sio vizuri

Hata wewe ukiwa unafanya mambo yako akajitokeza snitch mmoja anaenda kinyume na wewe unavyotaka lazima mzinguane hio ni matter of nature hakuna binadamu mwenye moyo wa chuma bro

Mimi binafsi nachukia sana u-snitch for real yaan I am telling you yaan ukiniletea u-snitch we are done nakuzima mazima kuanzia mawasiliano piga block naku-ignore for life kila kitu sikufuatilii usinifuatilie na sina tena time na weewe haijarishi wewe ni ndugu yangu baba yangu shangazi yangu au wewe ni nani yangu sipendi kabisa ma-snitch

Ukileta u-snitch nakuzima ma zi ma
 
Na yule Gentlewoman, alikuwa nani sikumbuki,labda Saada Mkuya,aliyemwambia Tundu Lissu bungeni,nusu sàa kabla ya kushambuliwa,"Tundu Lissu,hayo maneno unayozungumza sasa hivi, huwezi kuyasema kwa upole?". Tundu Lissu akamtazama tu halafu akaendelea na hotuba yake. Je,huyo mama pia achunguzwe na Polisi?
 
Kwa taarifa yako hakutegemea hatakufa maana yeye sio Mungu. Na ifahamike Lisu aliwahishwa Nairobi sehemu ambayo hakuwa na mamlaka nayo. Ingekuwa alipelekwa Muhimbili kama alivyotaka, leo hii Lisu na yeye wangekuwa na sifa ya marehemu.
Kwa maelezo yaliyopo, inasemekana TL alitakiwa azikwe bila heshima yoyote. Haraka haraka.
 
Tatizo maagizo aliyatoa public na kunji define jinsi alivyo. Operator mkuu hakumfunda jinsi kagame anavyo dili na anaodili nao.

Kivyovyote vile mshahara wa dhambi ni mauti kama alitoa order bila shaka ameshapata adhabu yake. Na kama kweli lissu alikuwa kwenye njia ya kusaliti taifa naye amesha pata ijara yake
Hapana huo ulikuwa ni ujumbe kwa wasaliti wengine pia. Wakati anaongea haya tayari mawasiliano ya tundulissu yalidukuliwa na TISS akiomba nyaraka kutoka Barrick ili awasaidie namna ya kupambana na serikali.

Kwa lugha nyingine tundulissu aliamini anapambana n Magufuli badala ya kupambania taifa. Hiyo mentality ya kuamini anapambana na mtu ndio iliyomletea ulemavu wa kudumu. Vinginevyo hadi sasa angeendelea kusimama kwenye vizimba vya mahakama akiwapambania watanzania.
 
Back
Top Bottom