Inawezekana tuna watu wasio na uwezo katika nafasi wanazozitumikia?

Inawezekana tuna watu wasio na uwezo katika nafasi wanazozitumikia?

Hayo anayoongea huyo CDF ni matokeo ya Magufuli kutawla bila kufuata Sheria, na kwa bahati mbaya hata hao wateule wake walikuwa wanafuata chochote anachoagiza bila kujali Sheria inasema Nini. Huyo CDF alikuwa anacheka kwenye kamisheni ya Jeshi huko Arusha wakati Magufuli anapokea wanaccm kwenye hafla ya kijeshi, wakati kikatiba jeshi limetengwa kabisa na siasa. Sikushangaa akimuagiza CDF aagize apelekwe kwao akafie nyumbani.

Hayo ndio yalikuwa maagizo yake kwenye mambo mengi. Ni nani hakuona jeshi likitumika kuvamia maduka ya kubadilishia fedha na kupora wafanyabiashara fedha zao? Nani hakuna jeshi likitumika kununua korosho za wakulima kwa shuruti? Katika mazingira hayo kwanini wahuni wasitumie mazingira hayo kufanya kinyume na katiba, maana tayari ilishazoeleka na huyo CDF alikuwa anakaa kimya.
Ulitaka CDF akatae kulitumia jeshi kununua korosho,,mabayo ingetafasiriwa ni Uasi..watu mkila ugali mmekaa nyumbani mnadhani mambo ni rahisrahis utakataa
 
Kama unataka kufia kwako si umwambie daktari? Kwa nini umwambie CDF? Yeye na masuala ya matibabu wapi na wapi?
Kuna vitu vingine tunahoji ambavyo havina mantiki. Nonsense.

Kwa maelezo ya CDF , hali ya afya ya Magufuli ilikuwa imebadilika. Ni kawaida kwa mwanadamu anapokabiliana na kifo kutanga tanga na kutafuta ahueni na namna ya kukimbia kifo. Binafsi sioni makosa ya mtu kama yule kwa hali ya afya yake ilivyokuwa. Kama baada ya masaa tu alifariki, unamuhukumuje na kumlaumu mtu ambaye ni dhahiri kabisa alikuwa ktk hatua za mwisho kuiaga dunia????

Ni kawaida kwa mwanadamu kupitia hali aliyoipitia Magufuli. Wapo wengine wakikaribia kifo huita ndugu na watu wao wa karibu sana kisha kuwaachia wosia. Hujawahi kukutana na Mgonjwa anataka labda chakula fulani???? Au anamtaka mtu fulani??? Na unakuta analazimisha kabisa?
 
Waliotaka kupindisha utaratibu wa kikatiba ni kina nani?

Hii kimsingi ni kesi ya njama za uhaini, kwa nini hatujasikia lolote kuhusu hawa watu kuchukuliwa hatua yoyote?
Mkuu hatua za kisiasa zilishachukuliwa kwa asilimia kubwa;~ Ndugai gone, Bashiru hana chake, pole pole katupwa huko Cuba, Siro yupo Malawi anapiga miayo, Lukuvi na Profesa wapo under radar na Diwani naye kule! The last man standing in SG ni PM tu!
 
Hatamimi nimeshangaa,
Makamba huyuhuyu ,
Ndio leo Kiranga anataka tumsikie na kumwamini anachokisema,!!!!

Ama kweli dunia ina mambo.

Makamba huyu ambaye anamzulia Mwendazake mambo kila siku, ndio tuamini kauli zake, Aiseee
Hizo kauli hazijaanzia kwa Makamba.

Zilikuwapo tangu Magufuli yupo hai kulikuwa na habari kwamba Samia anatengwa na anaburuzwa kwenye maamuzi mengi.

Tulizijua.

Makamba anathibitisha tu.

Na Makamba si mjinga kuropoka mbele ya Samia.

Na Samia hana shida ya kutunga uongo dhidi ya Magufuli.

Au mnataka tufukue mijadala ilivyoenda? Uzuri mijadala yote ipo JF hapahapa.
 
Mahojiano aliyofanya CDF Mstaafu Venance Mabeyo yamenifundisha kitu.

Nchi hii tuna shida kubwa sana ya watu kuwa kwenye nafasi za juu za maamuzi na uongozi ambao hawastahili kuwepo kwenye nafasi hizo kwa kukosa uwezo.

Hivi inakuwaje kwenye nchi tena yenye miaka zaidi ya 60 ya uhuru watu kwenye nafasi za juu kabisa za maamuzi hawajui kuwa kwenye chain of Command baada ya Rais ni Makamu wa Rais?

Hivi inakuwaje Rais anafariki wa kwanza kutarifiwa ni Mkuu wa Majeshi na sio Makamu wa Rais?

Inakuwaje na Mkuu wa Majeshi anaingia Kuanza kusema nimfaarifu Waziri Mkuu au Katibu Mkuu Kiongozi na sio Makamu wa Rais?

Inakuwaje tuna viongozi kwenye nafasi za juu kabisa ambao hawajui hata Katiba ya Nchi inasemaje?

How comes wanaotuongoza hawaijui Katiba?

Kituko zaidi ni mtu aliyefika hadi kuwa Rais wa Nchi anaamuru Mkuu wa Majeshi aamuru atolewe hospitali na kupelekwa kijijini kwake?

Hivi alikuwaje Rais na hajui hata mipaka ya madaraka na uongozi?

Kusema kweli tuna tatizo kubwa kwenye hii nchi na hii ni kansa ambayo kusema kweli itatutafuna na kutumaliza kabisa.
Katiba inapuuzwa na hili litaendelea kuigharimu hii nchi.
 
Hakuna anayekataa kuwa CDF ni zaidi ya makamu wa rais, je katibu mkuu kiongozi na waziri mkuu nao vyeo vyao ni zaidi ya makamu wa rais? Kwanini wapewe wao taarifa ya hali ya rais kwanza Hadi kuitwa, huku akiachwa makamu wa rais? Punguza jazba jibu hoja kwa utulivu.
Zipo sababu za msingi kabisa ambazo hakukuwa na ulazima zisemwe hadharani za kwanini mh. Makam wa Rais ambaye ndiye Mh. Rais wa sasa alitafutiwa namna yake ya pekee kujulishwa habari hizi
 
Hakuna anayekataa kuwa CDF ni zaidi ya makamu wa rais, je katibu mkuu kiongozi na waziri mkuu nao vyeo vyao ni zaidi ya makamu wa rais? Kwanini wapewe wao taarifa ya hali ya rais kwanza Hadi kuitwa, huku akiachwa makamu wa rais? Punguza jazba jibu hoja kwa utulivu.
kwenye baraza la usalama Katibu mkuu kiongozi ni member, ila makamu sio member!....

CDF alimpa taarifa bashiru kama member wa Security Council
 
Hakuna anayekataa kuwa CDF ni zaidi ya makamu wa rais, je katibu mkuu kiongozi na waziri mkuu nao vyeo vyao ni zaidi ya makamu wa rais? Kwanini wapewe wao taarifa ya hali ya rais kwanza Hadi kuitwa, huku akiachwa makamu wa rais? Punguza jazba jibu hoja kwa utulivu.
Mkuu yawezekana hawakuitwa kwa ajili ya kupewa taarifa. ile ilikuwa ni deflective statement, maana taarifa alipewa rasmi makamu wa Rais na Familia yake.
 
Kuna vitu vingine tunahoji ambavyo havina mantiki. Nonsense.

Kwa maelezo ya CDF , hali ya afya ya Magufuli ilikuwa imebadilika. Ni kawaida kwa mwanadamu anapokabiliana na kifo kutanga tanga na kutafuta ahueni na namna ya kukimbia kifo. Binafsi sioni makosa ya mtu kama yule kwa hali ya afya yake ilivyokuwa. Kama baada ya masaa tu alifariki, unamuhukumuje na kumlaumu mtu ambaye ni dhahiri kabisa alikuwa ktk hatua za mwisho kuiaga dunia????

Ni kawaida kwa mwanadamu kupitia hali aliyoipitia Magufuli. Wapo wengine wakikaribia kifo huita ndugu na watu wao wa karibu sana kisha kuwaachia wosia. Hujawahi kukutana na Mgonjwa anataka labda chakula fulani???? Au anamtaka mtu fulani??? Na unakuta analazimisha kabisa?
Mkuu,

Tatizo wabongo wengi washamba hawajui instruments za basic human right zinazobeba roght of dying with dignity.

Hi ni pamoja na mtu anayeona maisha hayana maana tena (anaona anaendeleza siku za kuishi tu, lakini hana quality of life) kuamua afe tu.

Hii ni pamoja na mtu anayetumia madawa makali kama morphine ya kupunguza maumivu tu kwenye saratani, wakati ni lazima afe katika muda mfupi tu, hatoboi, kuamua afe mapema.

Hii ni pamoja na mtu ambaye anaona siku zake za kufa zimekaribia kupatiwa viongozi wa kiimani kufanya last rites anavyotaka,

Hii ni pamoja na mgonjwa aliyefikia stage hiyo kuamua afie nyumbani kwake akiwa amezungukwa na ndugu zake awaage kwa dignity ya kufia nyumbani kwake, si kufa kazungukwa na madaktari hata hawajui.

Sasa, wabongo wengi hawajasomasoma mambo haya, wanakwenda kwa kufosi tu kwamba "kwa nini afie Chato?" kama vile Chato ni sehemu isiyostahili heshima.

Ni ukimbukeni wa hali ya juu kumkatalia marehemu kufia sehemu anayotaka.

Look. Naelewa inawezekana kukawa na sababu za kumkatalia mgonjwa ombi hilo.

Mfano, kama mgonjwa anaumwa sana kiasi cha kufanya hiyo safari yenyewe ihatarishe maisha yake afie njiani, au kama kwa mfano mgonjwa anaumwa Covid na kumfanyia isolation nyumbani inaweza kuwa kazi ngumu kuliko hospitalini. Hapo ita make sense madaktari kukataa. Na hii nafikiri ndiyo ilikuwa sababu kwa upande wa Magufuli.

Lakini vinginevyo, wamemnyima mzee wa watu ombi lake la mwisho la kufa nyumbani kwake akizungukwa na familia yake.
 
Hakuna anayekataa kuwa CDF ni zaidi ya makamu wa rais, je katibu mkuu kiongozi na waziri mkuu nao vyeo vyao ni zaidi ya makamu wa rais? Kwanini wapewe wao taarifa ya hali ya rais kwanza Hadi kuitwa, huku akiachwa makamu wa rais? Punguza jazba jibu hoja kwa utulivu.
CDF ni zaidi ya Makamu wa Rais katika mfumo gani mkuu?

Unafahamu kanuni ya "Civilian control of the military"?

Katika succession plan ya kurithi urais wa nchi ikiwa rais kafariki , Makamu wa Rais yupo namba ngapi na CDF yupo namba ngapi?
 
Hizo kauli hazijaanzia kwa Makamba.

Zilikuwapo tangu Magufukibyupo hai kulikuwa na habari kwamba Samia anatengwa na anaburuzwa kwenye maamuzi mengi.

Tulizijua.

Makamba anathibitisha tu.

Na Makamba si mjinga kuropoka mbele ya Samia.

Na Samia hana shida ya kutungabuongo dhidi ya Magufuli.

Au mnataka tufukue mijadala ilivyoenda? Uzuri mijadala yote ipo JF hapahapa.
Nini cha ajabu alichofanya Magufuli, mpaka ionekani hiyo ofisi imetengwa leo hii,

Mbona tawala zote zilizopita ilikuwa ni hivyo hivyo tu, mpaka na jina la utani tukawapa kwamba kazi yao ni kutembea na mkasi mfukoni.,

Hivi huyu Makamu wa leo ambaye tunaye , kama angekuwa ni mtu anayependa makuu, na mwenye makundi na machawa kama hao akina Makamba, si tungesikia mengi tu kutoka kwake kwamba anatengwa.

Mbona yeye yupo kimya tu.

Matikeo yake tunaanza kuwasiliza watu wenye nongwa.
 
Nini cha ajabu alichofanya Magufuli, mpaka ionekani hiyo ofisi imetengwa leo hii,

Mbona tawala zote zilizopita ilikuwa ni hivyo hivyo tu, mpaka na jina la utani tukawapa kwamba kazi yao ni kutembea na mkasi mfukoni.,

Hivi huyu Makamu wa leo ambaye tunaye , kama angekuwa ni mtu anayependa makuu, na mwenye makundi na machawa kama hao akina Makamba, si tungesikia mengi tu kutoka kwake kwamba anatengwa.

Mbona yeye yupo kimya tu.

Matikeo yake tunaanza kuwasiliza watu wenye nongwa.
Unatetea ujinga kwa sababu tumezoea kufanya ujinga siku zote mkuu?

Kwa hivyo tuendelee kufanya ujinga tu, kwa sababu tumekuwa tukifanya ujinga siku zote?

Makamu wa Rais ni msaidizi mkuu wa Rais, hawa watu, Rais na Makamu wake, wanatakiwa wafanye kazi kwa ushirikiano mkubwa sana, si kwa visirani na kununiana.

Sasa wewe unatetea ujinga wa Makamu wa Rais kutengwa kwa sababu huko nyuma ndiyo tumekuwa tukifanya hivyo?

That is a logical fallacy.

It is called "argument from tradition".
 
Wewe ndio ukikuwa humtaki,

Sisi wengine tulimtaka,

Acha kutusemea
"Alikuwa hatakiwi na kila mtu" ni tungo tata.

Inaweza kutafsirika kama "nobody wanted him". Hakuna aliyemtaka.

Au

"Not everybody wanted him". Si kila mtu alimtaka.

Nafikiri uliyemjibu alimaanisha "not everybody wanted him" not " nobody wanted him".

Kama ni hivyo, atakuwa sawa, kwa sababu, si kika ntu alimpigia kura Magufuli.
 
Back
Top Bottom