Iran imepelekea ombi mbele ya Baraza la Usalama la umoja wa mataifa likitaka kulijadili Israel kutokana na mashambulizi yake ndani ya eneo la Iran. Ombi Hilo limeungwa mkono na Urusi, China na Algeria.
Iran inadai Israel imetenda kosa Chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1945 unaokataza nchi moja kuvamia nchi nyingine Kama uchokozi. Iran inaiomba Baraza Kuu kuiwekea vikwazo Israel kwa kuvunja mkataba huo wa umoja wa mataifa.
Kuanzia mleta mada hadi wagalatia wengine ni watu wasiokua geopolitics huwa zinachezwa vipi.
Eti wanadhani Iran kulalamika UN ni sawa na Iran imepigwa sana.
Wacheni uzwazwa,Iran imepata limited damage na shughuli zinaendelea kama kawaida ilichoharibika ni radar ya airport tu.
Iran anatafuta kinga akishambulia kulipiza kisasi asije akaonekana mkorofi na akawekewa vikwazo tena.
Msisahau Iran ikifanya jambo Israel inakimbilia kulia USA na USA inakimbilia UN kuweka package ya vikwazo.
Mfano mzuri turudi May Israel ilipolipua balozi ya Iran Syria.
Iran ililalamika UN kwanza kabla haijajibu shambulizi.
Ndio maana iliposhambulia ilitoka kulaani tu ila hakuna nchi iliyounga mkono kuwekwa vikwazo kwa Iran licha ya Israel na USA kulalamika UN.
Watu wameshasahau kuwa kabla ya Israel kulipa kisasi ililalamika UN tena saana kila kikao ilikua ikimtaja Iran.
Iran inapita njia hizo hizo anazopita USA na Israel ili kusiwe na visingizio vya kuwekeana vikwazo mbeleni.
Ila Iran haijaathirika inaendelea na shughuli zake kama kawaida.
BBC na Aljazeer hadi France 24 wana correspondent ndani ya Tehran ila hawajaleta habari zozote za athari huko Iran.
Shida JF imejaa watoto wa balehe hawajadili fact bali mihemko.
Hata namna ya kuwasilisha taarifa hawajui.
Unapoleta taarifa lete na credible source ulipoitoa,sawa
econonist !??