Kabendera, Kitabu pekee hakina nguvu ya kumfanyia Mtu Character Assassination kwenye nchi Maskini hasa za Afrika

Kabendera, Kitabu pekee hakina nguvu ya kumfanyia Mtu Character Assassination kwenye nchi Maskini hasa za Afrika

Mimi binafsi sikuwa na mkubali
Lakini nakuambia hivi, chunguzi zangu tangu Akiwa HAI na sasa hayupo, Magufuli anapendwa Sana na watu wengi(Watanzania wa Tabaka la chini)
Upo sahihi kwasababu hata alipokua anashughulika na hao matajiri alikua anatumia neno fisadi, kwahiyo hii ilikua shangwe sana kwa watu WA hali ya chini na walikua wanamuona jamaa ni mtetezi wa wanyonge haswaaa, bila kujali kama alikua anatenda sawa au fyongo.
 
Upo sahihi kwasababu hata alipokua anashughulika na hao matajiri alikua anatumia neno fisadi, kwahiyo hii ilikua shangwe sana kwa watu WA hali ya chini na walikua wanamuona jamaa ni mtetezi wa wanyonge haswaaa, bila kujali kama alikua anatenda sawa au fyongo.

Watu wengi wa chini walimpenda kwa sababu alikuwa akiwanyoosha wenye navyo
 
Mimi naandikia wanaopenda kusoma.

Mimi ninayeandika ndiye najua kipi cha kuandika na kipi nisiandike, nawe msomaji unahaki na maamuzi ya kuaumua kipi cha kusoma na kipi usisome.

So jukumu Lako kama msomaji sio kuniambia niandikeje kama Mimi nisivyo na jukumu la kukuamulia usomeje
Tunahitaji uhalisia na uhakika usio na shaka hatuhitaji mambo ya hadithi.Wewe na kabendera mna tofauti gani?

Wewe sio wa kwanza hapa JF kuandika mambo ya kufikirika ,Wapo wengi na huwa wanaelezwa walete takwimu na ushahidi wanashindwa

Tatizo la watu kujitungia mambo ndio watu wakashauri iwepo JAMII CHECK hapa JF

Lete chanzo cha takwimu zako kuwa magufuli alipendwa na watanzania wengi
 
Kabendera alipofungwa alipata ugonjwa wa akili maana alinyanduliwa na wajelajela wenzake.Ameandika hicho kitabu akiwa na matatizo ya akili ndiyo maana kaandika 90%ni uongo
 
Watu wengi wa chini walimpenda kwa sababu alikuwa akiwanyoosha wenye navyo
All in all hakuna mkamilifu so alifanya alichofanya na amemaliza kiutawala na kidunia so angeachwa tu apumzike coz hizi blah blah zinazoemdelea haziwezi kubadilisha kitu na licha ya mabaya ambayo aliyafanya lakini pia kuna namna alileta kitu kipya kwenye utawala.
 
Ukweli ukikataliwa hugeuka kuwa Uongo na uongo ukikubaliwa huwa Ukweli.

Ukweli ni ishu ya kifalsafa lakini pia ukweli ni ishu ya kimahesabu
Lakini pia ukweli ni ishu ya kisayansi.

Mfano, watu wanasema siku hubadilika saa sita za usiku, na wengine wanasema siku hubadilika saa 12 jioni. Yupo hapo anasema kweli na yupi anasema Uongo?

..ukiupinga ukweli, kwa kudhamiria, au la, unaweza kupata madhara makubwa.

..John Magufuli alicheza na ukweli, ugonjwa wa korona, nadhani unajua kilichomtokea.
 
Tunahitaji uhalisia na uhakika usio na shaka hatuhitaji mambo ya hadithi.Wewe na kabendera mna tofauti gani?
Unahitaji wewe na Nani?
Mimi nimechambua muhtasari WA alichosema Kabendera kama utangulizi wa Kitabu chake

Wewe sio wa kwanza hapa JF kuandika mambo ya kufikirika ,Wapo wengi na huwa wanaelezwa walete takwimu na ushahidi wanashindwa
Unapenda ushahidi kwani wewe ni Mtoa hukumu?

Tatizo la watu kujitungia mambo ndio watu wakashauri iwepo JAMII CHECK hapa JF
😂😂
JF yenyewe imetungwa na Melo na mushi ndio maana wewe upo hapa. Bila utunzi, ubunifu nini kingeendelea hapa duniani. Kilo yako ni conservative

Lete chanzo cha takwimu zako kuwa magufuli alipendwa na watanzania wengi

Mbona kama imekuuma Mimi kusema hivi?
Kama Magufuli alikufanyia vibaya nikupe Pole Mkuu. Najua hakuwa mzuri kwa watu wote na wapo aliowaumiza Sana.

Lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa Watanzania wengi walimpenda
 
Katika marais waliowahi kuitawala nchi hii hakuna rais wa hovyo kama dikteta Magufuli na ndio rais aliyeua watu wengi akiwa ikulu.

Very hopeless indeed.
 
Katika marais waliowahi kuitawala nchi hii hakuna rais wa hovyo kama dikteta Magufuli na ndio rais aliyeua watu wengi akiwa ikulu.

Very hopeless indeed.
Aliua wangapi we pimbi?

Hivi unajua jk yalilipuka hadi mabomu?

Unajua kama walikufa watu 5 kwa mpiho kwa kurushiwa bomu la mkono kwenye mkutano wa chadema?

Hebu taja watu 5 waliouawa na JPM
 
Leo nimesikiliza mahojiano ya kabendeea na mwandishi Ghassani,...mwanzoni TU amesema lengo la kuandika kitabu kile ni Dunia ifahamu kilichotokea katika utawala wa yule mtu mbaya,yes ni mtu mbaya kabisa na muovu...na akasema kabisa mwanzo wa kitabu amejaribu kuelezea dondoo chache kuhusu nchi ya Tanzania ili mtu yeyote duniani akisoma ajue inazungumzwa nchi Gani. Leteni porojo zenu lakini Kabendera amefanya kitu kikubwa sana ili kuweka historia sawa. Shetani keshalala kule inatosha.
 
Leo nimesikiliza mahojiano ya kabendeea na mwandishi Ghassani,...mwanzoni TU amesema lengo la kuandika kitabu kile ni Dunia ifahamu kilichotokea katika utawala wa yule mtu mbaya,yes ni mtu mbaya kabisa na muovu...na akasema kabisa mwanzo wa kitabu amejaribu kuelezea dondoo chache kuhusu nchi ya Tanzania ili mtu yeyote duniani akisoma ajue inazungumzwa nchi Gani. Leteni porojo zenu lakini Kabendera amefanya kitu kikubwa sana ili kuweka historia sawa. Shetani keshalala kule inatosha.
Ile ni kumbukumbu itakayokumbukwa na vizazi vijavyo
 
Na wewe ni wale wale tu kama kabendera,Hakuna tofauti ya wewe na yeye

Umejaa mambo ya hearsay

Umehoji kundi la wasukuma halafu unatoa hitimisho watanzania kumbe umehoji kundi la wasukuma wa kabila lake

Takwimu kuwa magufuli alipendwa sana umezitoa wapi ?

Kama kitabu hujakisoma unatoa wapi nguvu ya kuandika vitu ambavyo unavisikia bila uhakika huo ni umbea tu

Unapoongelea Tanzania kwani Magufuli alikuwa ana mamlaka zanzibar? Umewahi uliza wanzibar kama walimpenda Magufuli?
Hata kitabu kilichoandikwa hakina Vivid data….. yaani data ambazo can be checked and verified beyond doubt but UMEKIAMINI. Ila unabisha suala la JPM kuwa ni kipenzi cha watu…. Nakuhoji data zimetoka wapi

interesting creature
 
Unazungumzia mambo usiyoyaelewa.

Watanzania hivyo vitabu vya Kiswahili vyenyewe hawasomi sembuse vya kingereza?

Hayo Mengine ya Matabaka nafikiri ubongo wako umejigusa baadhi ya nerves, zikatoa kitu kingine ambacho Mimi Wala sijakisema
Kama hawasomi vya Kiswahili, wewe inakuhusu nini wewe bwege? Ubongo ni smart ndiyo maana naona umeandika mavi. Hujui ulichoandika, unaongea ujinga, kumbe kitabu chenyewe hukusoma na wala hujakiona. Tuulize tuliopitia angalau muhtasari wa kitabu. Eti Magufuli alipendwa sana? Hivi wewe upo mzima kichwani, unapindisha ukweli kwa sababu zako. Mara eti watanzania wote wakisome....Hivi wewe una shida gani? Kwa akili yako unadhani watanzania wote Mil. 62 wanaweza kukisoma? Unapoongelea English au Kiswahili umeshaenda kwenye matabaka kaka, unapoongelea kitu chochote chenye kuonyesha section fulani hainufaiki, umeongelea matabaka. Ni kwamba umeongea kitu bila ya wewe mwenyewe kufahamu. Ndiyo maana ninakuwa na wasiwasi wa uelewa wako.
 
Umeongea kweli kabisa mkuu Mtibeli, hicho kitabu kusema ukweli hakitasomwa na wengi na kitawahi kuchuja sana masikioni mwa watanzania kama tu ilivyokuwa kwa kitabu cha wale jamaa kina Meena na wenzake.

Suala la watanzania kumpenda Magu liko wazi sana sijajua watu wengine wanachangamana na watanzania kwa kiwango gani maana kila penye mikusanyiko ya watu huwezi kukuta Magu anasemwa kwa mabaya na mpaka kuna baadhi ya sehemu watu bado wanapiga mpunga kila wiki kwa kuweka tu mkusanyiko wa hotuba za jamaa na kuna siku maalumu ya kusikiliza na watu wanajaa ukumbini.

Magu ni rais pekee nchi hii ambaye ameonyesha uthubutu wa kusimamia rasilimali za nchi na zikaleta manufaa makubwa ndani ya muda mfupi, kwa watanzania Magu ni kielelezo cha maamuzi magumu.

Nenda mashuleni kote asilimia kubwa kunapokuwa na debate zinazohusu uzalendo mfano pekee inaotumika wa kuwaonyesha watanzania uzalendo ni jina la mwamba JPM. Na mpaka wanashauri viongozi wetu wawe wachapakazi, wathubutu na wazalendo kama Magu.

Ukiacha udhaifu mkubwa wa kuogopa challenge Magu alilitendea vyema sana taifa hili kuliko kiongozi mwingine yeyote nisijue sana kwa Nyerere ila ukipitia mitandaoni na mijadala mbalimbali Magu ni kama anakubalika kwa kiwango kikubwa sana. Na hata ikifanyika poll yoyote humu au popote bado Magu atawaacha mbali sana kina Mkwere na Samia. Kumbuka hata utafiti waliofanya gazeti la mwananchi ulitoa matokeo ya Magu kushinda japo watawala waliopo hawakuridhishwa nao ikabidi mwananchi waombe msamaha.

Magu hachafuki kwa vitabu labda itokee flyover za Dar zivunjwe zote, SGR ihujumiwe, bwawa la Nyerere lipotee mazingira ya kutatanisha, mahospitali aliyojenga tuamue kufugia kuku, stand na masoko makubwa aliyoyajenga tusiyatumie, ikulu ya chamwino tuichome moto, daraja la busisi lipigwe bomu liteketee, ukarabati mkubwa wa shule kongwe uliofanyika uharibiwe makusudi, barabara alizojenga zisipitike, ukuta wa mererani tuuvunje, watu waliowekewa umeme kwa gharama ya Tshs 27000 wahamishwe wote nchini iwekwe imani nyingine kwa wakazi wapya watakaoletwa, ndege alizonunua tuzihujumu zote na mengine mazuri mengi aliyofanya ndipo tunaweza tukamsahau huyu mtu mchapakazi ambaye hajawahi kutokea nchini mwetu.
 
Back
Top Bottom