Kuna ulazima hayo mashindano ya Quran yafanyike Mkapa Stadium? Siku ya mchezo Simba vs Orlando!?

Kuna ulazima hayo mashindano ya Quran yafanyike Mkapa Stadium? Siku ya mchezo Simba vs Orlando!?

Hakuna anayesema hayana muhimu, Ila kwa nini lazima yafanyike uwanja wa Taifa yasifanyike hata uhuru?
Ndio Mana vilabu vinatakiwa viwe naviwanja vyao.Unaambiwa waliotangulia kukodisha ni waislamu wameulipia na risti zote wanazo na walianza kutoa matanganzo.kisha mtu akuhamishe kirahisi rahisi .

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
 
Mashindano ya Qur-an ni bora zaidi ya huo upuuzi wa mpira wa simba na orlando,Uwanja ni wa taifa na unatumika kwa watanzania wote wawe waislamu au wakristo...mleta mada una chuki na uislamu na bado uislamu utazidi kupaa juu zaidi na mtabaki mnashangaa kama kule Times Square,Hoja za hovyo eti watu watatokaje uwanjani baada ya mashindano kuisha,hakuna muislam anayeweza kujaribu kujificha eti aangalie mpira bure..ilhali kaenda kwa dhati kabisa ya moyo wake kusikiliza maneno matukufu ya Mola wa ulimwengu huyo atakuwa kafiri na sio muislam..naamini baada ya shughuli kuisha watatoka wote ili kupisha wapenda mpira kuingia...uislamu ni dini ya haki hivyo hatuwezi kudhulumu haki ya mtu siku hiyo.
 
Waislamu wana mambo ya ajabu sana kwenye kila jambo lao, hata mtaani wanafunga barabara ety kisa cjui visherehe vyao vya kupotezeana muda.
Cheki zenu dhidi ya uislam hazitoisha mpaka kiyama hilo tunalijua, na uzuri wake ni kuwa tumefundishwa jinsi ya kuishi na nyinyi bila shida.
 
Hakuna anayesema hayana muhimu, Ila kwa nini lazima yafanyike uwanja wa Taifa yasifanyike hata uhuru?
Ule uwanja ni kwa ajili ya shughuli za kijamii, ili upewe ruhusa ya kuutumia kuna taratibu za kufuata.
Wanatumia hapo kulingana na mahitaji yao, hususani wingi wa watu wanao hudhuria shughuli hiyo. Uhuru ni mdogo.
Kingine ni hivi kipindi wanapewa kibali cha kutumia eneo hilo ratiba ya mechi ya simba ilikuwa bado haija pangwa tarehe.
Kikubwa ni kwamba tujifunze kutatua mambo yetu kwa busara, wakae pamoja pande zote waone jinsi gani watalitatua jambo hilo, mihemko haitosaidia chochote zaidi ya kuleta chuki katika jamii.
 
Tulia wewe Jini Maimuna. Ona sasa mnavyo hangaika kutafuta eneo la kufanyia hayo mashindano yenu!

Viwanja vyenu vyote mmeuza! Sheikh Ponda kapambana weeeh kuwasaidia kuvirejesha! Mkaishia tu kumuweka mahabusu. Tukio kama hilo lina ulazima gani wa kufanyia kwenye uwanja unaotumika kwa ajili ya michezo?
Mimi nimefunga sipo hapa kwa ajili ya matusi na kejeli na wala siyo mpenzi na mfuatiliaji wa hayo mashindano ,ila naona wana Jf(baadhi ya wakirsto) inapokuja maada inayohusisha na Uislamu hata kwa asilimia 1 mna chukua advantage ya kutukana hovyo na kwenda pakubwa nje ya maada iliyoletwa kiasi ambacho kinapelekea kukosa pasi na UADILIFU

Hapo uwanja wa Taifa miaka ya nyuma matamasha ya injili ya 'Msama promotion' kuna kipindi yalikuwa yakifanyika kila mwaka na hayo mashindano ya Qur'an kwa miaka mingi yamekuwa yakifanyika hapo
 
Mashindano ya Qur-an ni bora zaidi ya huo upuuzi wa mpira wa simba na orlando,Uwanja ni wa taifa na unatumika kwa watanzania wote wawe waislamu au wakristo...mleta mada una chuki na uislamu na bado uislamu utazidi kupaa juu zaidi na mtabaki mnashangaa kama kule Times Square,Hoja za hovyo eti watu watatokaje uwanjani baada ya mashindano kuisha,hakuna muislam anayeweza kujaribu kujificha eti aangalie mpira bure..ilhali kaenda kwa dhati kabisa ya moyo wake kusikiliza maneno matukufu ya Mola wa ulimwengu huyo atakuwa kafiri na sio muislam..naamini baada ya shughuli kuisha watatoka wote ili kupisha wapenda mpira kuingia...uislamu ni dini ya haki hivyo hatuwezi kudhulumu haki ya mtu siku hiyo.
Lakini ule ni uwanja wa michezo, Je hayo mashindano ni sehemu ya michezo?
 
Haina shida..quran itasomwa na simba itafuzu nusu fainali..
 
Kwan si kuna viwanja viwili?
Why wasipelekwe shamba la bibi wabaki kung'ang'ania wa taifa (lupaso) kama watt wadogo
 
Tunajua sote jinsi mchezo huu ulivyo muhimu kwa Simba na Taifa kwa ujumla, ndio wa kwanza katika historia ya Nchi yetu kutumia teknolojia ya usaidizi wa Video kwa Mwamuzi (VAR).

Zaidi ya hayo Sheria za CAF zinataka uwanja kuwa wazi angalau saa 72 kabla ya mchezo.

Pamoja na kwamba Wanasema saa 7 kamili hao washindani wa Quran watatolewa kwa usaidizi wa Polisi...

Lakini naona kabisa hapa kuna lawama zinaenda kutengenezwa sisi Waswahili tunajijua katika kutunza muda.

Lakini vipi kama mtu akaingia then akagoma kutoka ili aangalie mechi?

Lakini vipi kama hayo mashindano yakachelewa kwisha baada ya saa 7?

Ndio maana nauliza kuna ulazima haya mashindano kufanyika Lupaso?

N.B
Sina nia ya kukashifu Dini ya mtu.
Samia anachanganya dini na serikali.Anaharibu hii nchi,Jesuit mko wapi?okoeni hili taifa dhidi ya 'Nebukadreza'.
 
UWANJA NI WA SERIKALI NA IMETOA IDHINI YAFANYIKE MASHINDANO YA QUR'AN...Simba wangekuwa na uwanja yasingetokea haya
 
Hayo mashindano ya Quran ni ya msingi kuliko mchezo wa mpira, ni jambo jema kuliko hata maadhimisho ya kitaifa yanayofanyika hapo.Takbiiiir

Binafsi ni mkatoliki kindaki ndaki lakini napingana na mtoa mada, huwezi kulinganisha mchezo na jambo jema linalomhusisha Mwenyezi Mungu na kuwaongoza watu ktk njia ya haki na unyoofu.
Tumsifu yesu kristo...
Kanisa la kisinodi.....
Mwana kondoo ameshinda...
Salam aleykum...

Sizan km unajua ulichoandika
 
Na ikumbukwe kuwa haya mashindano ya quran hayana kiingilio

Watu wataingia bure lakini uwanja umekodiwa Watu waeshalipiwa kila Kitu Wetu waingie bure ndiyomana Wenye Uwanja hawezi kuyahairisha au kuyahamisha.

Hebu jaribu kufuatilia matangazo yao utaona Masponsor kibao pale wametoa mamilioni kulipia uwanja na Matangazo ya Moja kwa moja ya Television hivyo wanaosimamia Uwanja hawawezi kuhairisha kwasababu ya mechi ya mpira hata siku moja wakati kuna hela Cash wameshazinyaka wakichanganya na za mechi ya Simba tayari wameshanasa double payment hapo.

Ndugu uwanja ni Biashara hule.
 
Back
Top Bottom