Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Mi nina biashara ya Tigo pesa,nisikufiche laki 5 haitoshi kwa kuanzia hasa kweny upatikanaji wa line.Kwa mfano Tigo line utaipata kwa kwa 250,000,Voda 150,000,Airtel 100,000 hapo bado gharama za frem labda 50,000 kwa mwez miezi 6 ni 300,000 bado hela ya mtaji labda 500,000 iyo ni kwa sehemu ambayo ni ya kawaida ila wastani wa ela ya luz in gush is isipungue 1,000,000.Hapo umejibana sana bado vitu kama meza,simu za kazi,mazingira ya usalama kama vile mlango wa gril n.k.
Maelezo hayo yatawaidia wengi,sio aliyeomba kujulishwa tu.
Pole sana kwa kupigwa Mkuu.

Laini za Vodacom zinatolewa bure.

Cha msingi uwe na TIN NUMBER & BUSINESS LICENCE.
 
Nenda kariakoo chukua viatu Sandoz, ila sijajua unalenga soko lipi na mazingira uliyokusudia kufanya biashara. Ni jambo njema ukaeleza uko wapi na biashara unaenda kufanya wapi.
 
Ni kweli kabisa line zinatolewa bure ila kwa utaratibu. Uwe na leseni na tin namba pia na mtaji usiopungua mil 1 baada ya hapo ujiandae kusubiri kwa muda usiojulikana ili kupata hizo line,mtandao wa Voda kwa sasa wamesitisha kuzalisha line za Wakala mpaka watakapo tangaza tena.Ukihitaji kwa haraka unazipata kama nilivoeleza hapo juu,ni hiyari yako kuchagua
 
Mi nina biashara ya Tigo pesa,nisikufiche laki 5 haitoshi kwa kuanzia hasa kweny upatikanaji wa line.Kwa mfano Tigo line utaipata kwa kwa 250,000,Voda 150,000,Airtel 100,000 hapo bado gharama za frem labda 50,000 kwa mwez miezi 6 ni 300,000 bado hela ya mtaji labda 500,000 iyo ni kwa sehemu ambayo ni ya kawaida ila wastani wa ela ya luz in gush is isipungue 1,000,000.Hapo umejibana sana bado vitu kama meza,simu za kazi,mazingira ya usalama kama vile mlango wa gril n.k.
Maelezo hayo yatawaidia wengi,sio aliyeomba kujulishwa tu.
Nashukuru kwa MAWAZO yako mkuu...
Yameniongezea kitu..!
 
Acha kumtisha mwenzako lain za uwakala hutolewa buree kama wewe uliombwa hela ujue ulipigwa na wajanja Wa mjini.... Mathalani ili kupata lain ya uwakala yoyote inakubidi uwe na tin number , lesen ya biashara, barua ya utambulisho kutoka serikali za mitaa na kitambulisho chako chochote kile...

Narudia tena lain ya uwakala ni buree cha msingi aende kwenye ofisi za kampuni husika usiende kwa wahuni Wa mitaani.....

NB. Baada ya lain kuwa tayari utaombwa shilingi ambazo si choni ya laki tatu kutegemea na kampuni
. kiasi hicho kitawekwa kama float au mtaji Wa kuanzia kwenye lain yako...
Ahsante kwa taarifa hii muhimu mkuu..!
Naamini itawanufaisha na wengine pia..!
 
Kulingana na hali halisi ya sasa mimi ninakushauri ujiunge na kampuni inayofanya biashara ya kusambaza bidhaa za afya na usafi pia kilimo. Laki 5 zinatosha kuanzisha biashara inayoweza kukupa faida ya laki 3 hivi kwa mwezi. So mimi nakushauri njoo tufanye wote pamoja, ni rahisi kikubwa uwe na dhamira ya kutoka kimaisha na uvumilivu.
Mawasiliano ni 0763797853
Mkuu...
Hiyo biashara tunaweza fanya muda wangu wa ZIADA..?
Maana me ni mwanafunzi..!
 
Acha kumtisha mwenzako lain za uwakala hutolewa buree kama wewe uliombwa hela ujue ulipigwa na wajanja Wa mjini.... Mathalani ili kupata lain ya uwakala yoyote inakubidi uwe na tin number , lesen ya biashara, barua ya utambulisho kutoka serikali za mitaa na kitambulisho chako chochote kile...

Narudia tena lain ya uwakala ni buree cha msingi aende kwenye ofisi za kampuni husika usiende kwa wahuni Wa mitaani.....

NB. Baada ya lain kuwa tayari utaombwa shilingi ambazo si choni ya laki tatu kutegemea na kampuni
. kiasi hicho kitawekwa kama float au mtaji Wa kuanzia kwenye lain yako...
Samahani naomba uliza ni leseni ya biashara yoyote, na ni kwa mitandao yote ama?
 
Kachukue tin number tra ni bureeeeeeeeee.... Kachukue lesen ya biadhara halmashaur za miji au manispaa, huwa kuna tathmin ya utoaji Wa lesen ya biashara,. Nakuomba ukifika ofisin hapo sema unataka lesen ya biashara ya KUUZA VOCHA NA LAINI ZA SIMU..... Gharama yake ni kati ya elfu 30-50


Bravo
 
Salamu kwenu wana jamii...
Kama heading inavyojieleza...
Ni biashara gani nayoweza kufanya kwa mtaji wa shilingi laki tano za kitanzania..?
Nahitaji mawazo yenu KAKA na DADA zangu wa jamii forums katika jambo hili..!​
Nguo za mtumba na viatu
 
Nguo za mtumba na viatu
Kaka Mshana, hawa jamaa wanaotuuziaga wengi huwa wanasema wanafuata Mombasa ndo kuna mitumba grade ya juu. Kuna ukweli hapo?

Kama sivyo mzigo unapatikana wapi kwa hapa Dar?
 
Kulingana na hali halisi ya sasa mimi ninakushauri ujiunge na kampuni inayofanya biashara ya kusambaza bidhaa za afya na usafi pia kilimo. Laki 5 zinatosha kuanzisha biashara inayoweza kukupa faida ya laki 3 hivi kwa mwezi. So mimi nakushauri njoo tufanye wote pamoja, ni rahisi kikubwa uwe na dhamira ya kutoka kimaisha na uvumilivu.
Mawasiliano ni 0763797853
Mfano wa forever living.
 
Kaka Mshana, hawa jamaa wanaotuuziaga wengi huwa wanasema wanafuata Mombasa ndo kuna mitumba grade ya juu. Kuna ukweli hapo?

Kama sivyo mzigo unapatikana wapi kwa hapa Dar?
Saa nyingine ni kuaminishana tu hata hapa ipo shida ni kwamba wauzaji wetu hapa ni wachakachuaji
 
Mkuu George Betram Kuna wazo pale juu kakupa kaka mshana jr naomba ulifanyie kazi.

Sijajua upo mji gani na chuo gani, lkn nakushauri jiingize ktk biashara ya mitumba.

Anza na bidhaa za mitumba za wadada. Usinunue BARO, nenda kwa ile style ya KUPOINT zile unazoona zina ubora. Kwa upande wa nguo, kama ungekuwa DSM, ni kujihimu pale Karume alfajir ya kila Jumamosi, KUPOINT. Kwa hiyo laki5, inatosha kuchota laki 3 na kuanza biashara huku ukipima upepo ulivo.

Ukirudi chuo unaziongezea ubora kwa kuzipiga pasi. Uuzaji wako unakuwa ni wa kuwafuata wateja wako hostel kwao, chumba kwa chumba!

Ndani ya biashara hii utaanza kupata oda za wateja wako nini wanataka ukawaletee kutoka sokoni. Wadada wengi hawana muda wa KUZURURA ktk masoko ya mitumba.

Nimekushauri ujihusishe na bidhaa za wadada kwa vile ktk maisha ya Chuo, wadada wanaongoza KUSHINDANA KUVAA kuliko men. Pia wadada kama utakuwa makini hamtasumbuana sana ktk malipo.

Wanaume baadhi wawapo chuo huweka pembeni hobby ya mavazi na wengi huigiza HIP HOP ama UGUMU lkn nyuma ya pazia wanamaanisha.
 
Back
Top Bottom