Kwanini tukarabati kivuko kwa Tsh. bil 7.5 wakati kipya ni bil 8.5?

Kwanini tukarabati kivuko kwa Tsh. bil 7.5 wakati kipya ni bil 8.5?

Wadau nawasabahi.

Nikiwa mlipa kodi pamoja na tozo mbalimbali najisikia uchungu sana kusikia kuwa Serikali inataka kukarabati kivuko cha Mv Magogoni kwa bil.7. wakati bei ya kuunda kivuko kipya ni kati ya bil.8.5 -9

Najiuliza kwanini ufanyike ukarabati?

Kwanini kisinunuliwe kivuko kipya?

Hata kama kununua ni gharama lakini tofauti yake ni ndogo sana. Hebu watendaji wa serikali tuwe na uchungu na kodi za masikini wananchi wananchi wana maisha magumu sana hata kama mnatuamulia mtakavyo lakini tunaumia tunapohisi mnatuibia.

Juzi juzi mmetoka kutuibia kwenye ukarabati wa mv hapa kazi mlikikarabati kwa bil.4.5 wakati kivuko kipya ni bil 7.5 kumbukeni watanzania sio wajinga kihivyo

Ikiwa Ufalme wa Msoga umeamua hivyo,sie Watumwa wa Tanganyika ni nani hasa ata tupinge!!
 
Kuna shirika liliwahi karabati mashine zake 16 kwa 8 billions kwa kila moja wakati mpya na za kisasa ni 6.4 billions kwa moja. Kuna mambo Afrika basi tu tunakaa tunawaangalia wanatuonaga mafala sana
Cha mtu uliwa na mtu,ni chuma pekee uliwa na kutu!!
 
Wadau nawasabahi.

Nikiwa mlipa kodi pamoja na tozo mbalimbali najisikia uchungu sana kusikia kuwa Serikali inataka kukarabati kivuko cha Mv Magogoni kwa bil.7. wakati bei ya kuunda kivuko kipya ni kati ya bil.8.5 -9

Najiuliza kwanini ufanyike ukarabati?

Kwanini kisinunuliwe kivuko kipya?

Hata kama kununua ni gharama lakini tofauti yake ni ndogo sana. Hebu watendaji wa serikali tuwe na uchungu na kodi za masikini wananchi wananchi wana maisha magumu sana hata kama mnatuamulia mtakavyo lakini tunaumia tunapohisi mnatuibia.

Juzi juzi mmetoka kutuibia kwenye ukarabati wa mv hapa kazi mlikikarabati kwa bil.4.5 wakati kivuko kipya ni bil 7.5 kumbukeni watanzania sio wajinga kihivyo

Hata mimi nimeshangaa sana tena baada ya kutazama hii habari kwa tv , mdomo ulibaki wazi
 
Babu jinga inama ufikiri mali yako inaliwa. Ni ujinga wa kiwango cha SGR
 
Labda nikuongezee jambo! Unakumbuka ile meli iliyowekwa kwenye maji pale Mwanza? Inauwezo wakubeba abiria 1,200 na ukubwa wote ule kwa Trip moja sasa sijui we mv magogoni ulivyoambiwa inauwezo wa kubeba abiria 3,000 unajua kwa Trip? Utakuwa unaumwa wewe
Huna akili wewe, unafananisha Material ya Maji Chumvi na Maji Baridi??
Hivi huwa mnatumia Mik...nd..u kufikiri???
 
Hicho cha billion 8 ni kikubwa sana na itakuwa wastage ya pesa kukinunua maana eneo la kigamboni ni fupi sana kuhitaji kivuko kikubwa.

But kuna vivuko vya watu 70, 120, 150 etc ambavyo vinauzwa kwa,$250,000, $350,000, $400,000 hadi $ 500,000. Ambayo ukileta hela ya Tanzania haifiki hata one billion.

So hapo vivuko viwili vipya havikutakiwa kula hata 4 bilioni.

Ila kwasababu majizi yamerudi kazini shughuli imeanza.
Baadhi ya sisi ccm kindakindaki kwa hoja za aina hii tunakosa majibu kwa watanzania, mamlaka husika zitoe ufafanuzi wa kitaalam wa kuuridhisha umma.
 
Mwisho wa siku mpinga rushwa si mmemuita muuaji?

Mpinga rushwa ndie leo amekuwa mwizi!

Mtamkumbuka sana,wacha vijana wa Mama wale urefu wa kamba zao!
Ndiyo anakumbukwa hivyo kwa uuaji, ukatili, uporaji, ujambazi, utekaji, utesaji, kauli chafu na kwa madhila mengine mengi aliyousababishia umma wa Watanzania.
Anavuna alichopanda.
 
Kivuko kipya ni Shilingi ngapi? It's better kitengenezwe kipya
Kwa hiyo tuvunje Mkataba ambao tume sign Jana tu pale ferry,Tena live! Wwe unataka tushitakiwe huko Miga!? Au na wwe unafungu lako kwenye Mambo ya kuvunja Mikataba!!??
 
Waulizwe Wizara ya Ujenzi na kama ujuavyo Temesa ni wezi na wapigahi balaa, gharama ya matengenezo ya gari ya serikali Huwa kubwa mara mbili ya gereji za mtaani.

Swali kama Hilo Wabunge wakambane Mbarawa
Hivi huyu Prof. Mbalawa ni yule yule aliye wahi kuwa waziri wa maji awamu ya 5? Yule alikuwa makali na Mpakani kwa mali ya umma tofauti na huyu.
 
Sasa watu 200 unaleta hapa?? We jamaa una akili kichwani kweli?
Hiko kivuko kinachoenda kukarabatiwa unajua Capacity yake.
We jamaa maku kweli.
Mkumbushe pia hicho ni tani 10 na magogoni ni tani 500
 
Mkuu, mbona kama ombi lako limechelewa sana? Discovery zimekuwa kama IST kwa sasa, GWagon kila kona etc...

Unaambiwa, lidude limejengwa kwa 8b from the scratch; leo wanalikarabati kwa 7b, unataka wizi upi tena?

Nadhani labda useme tumerudi kwenye muziki wa cassette, side B ndo inapiga sasa! Wametupilia mbali CD yetu
Wizi kwa nchi zetu kawaida tu, magu na ukorofi wake katupiga sana, fikiria miaka mi5 kaficha ripoti ya CAG ili atupige, kanunua ndege kwa siri, ndege kanunua bl2 screpa kakarabati kwa bl 2 tunaambiwa bei yake bl 9
 
Muda huu watu wana compensate hasara ya kutopiga pesa miaka 5 iliyopita. Usipolamba asali saizi shauri yako...
Mawazo ya wajinga tu, mbona simu za Sumsung ukiua tachi au kioo kuweka kipya ni zaidi ya nusu ya bei ya manunuzi
 
Back
Top Bottom