Lissu: Watoto wangu wote ni raia wa Marekani

Lissu: Watoto wangu wote ni raia wa Marekani

Akili kichwani mzee.. Hii nchi walicho nacho wanatengezea mazingira mazuri sana kwa watoto wao na vizazi vyao.. Kesheshe ipo kwa wasio nacho makapuku.. Ubinafai umetalamaki, hadi inafikia viongozi wanatoa matamko ya ajabu tusio na ajira tukachekiwe mirembe, mala tupo wazembe mala tujiajiri.. Ila tu kwakuwa wao wameshiba.. Jobless kama mzabzab atatoka hapo 😅😅
Marekani haujaundwa kwaajili ya MINORITIES hasa hasa mtu Mweusi.

Saaana utaishi Kama Mbweha mpaka ukome.
 
I wish angekuwa kweli huo mpango wa CIA ili atusaidie kuiondoa ccm madarakani.

Baada ya hapo tutajua cha kufanya. Ila kwa sasa adui wetu namba moja kama Taifa, ni ccm! Na siyo Tundu Lissu, au hao CIA.
Yeah, niliishi London nikakuta Waarabu walokimbia na Jamsheed ni totally and unrepentantly incorrigible wana nyumba zao Stonetown. Wengine ni mabaharia stowaway wamechanganyikiwa akili zao nilikuwa nawasikia tu kumbe kweli mpo. CIA hoyee!
 
Wewe kila siku unaleta upuuzi mtupu, hakuna simu hata moja akili yako inakaa sawa?

Nani ilikuambia kuwa Lisu hana kazi? Kama hujui, uliza kwanza kabla ya kuropoka.

Baada ya yeye Lisu kuwa targeted na utawala wa kishetani, ulitaka watoto wabakie hapa ili nao washambuliwe kwa risasi kama ngiri, kama alivyofanywa Baba yao?

Usiwe mjinga, soma historical intelligency uelimike. Unafahamu Mwalimu Nyerere alienda kuificha wapi familia yake wakati wa kupigania uhuru? Unafahamu Samora alienda kuificha wapi familia yake wakati wa mapambano? Unafahamu Augustinho Neto alienda kuificha wapi familia yake wakati wa mapambano? Hivi unadhani wakati wa mapambano familia ya wewe kapuku itawindwa kwa nguvu sawa na familia ya kiongozi wa mapambano?
Kama kagame anataka kukumaliza, hata uende kujificha marekani vijijini, watakufikia tu,
Kitu kikubwa wapinzani waache lugha za dharau kwa mamlaka,, watawala wengine hawanaga ngozi ngumu kama JK au samia,,
Lugha sijui eti 2025 hakuna uchaguzi ni kujipalia makaa ya moto tu,, maana uhalisia uchaguzi lazima utafanyika iwe isiwe
 
Kawaida sana

George Weah ni Rais wa Liberia lakini mtoto wake ni raia wa Marekani na Juzi kaifungia goli nchi yake ya USA kwenye kombe la Dunia
Sema kuwa ni raia wa marekani, liberia na ufaransa (ana uraia wa nchi tatu) na mwingine ana uraia wa nchi mbili ambazo ni liberia na marekani...

Sio kwamba wana uraia wa nchi moja pekee

Pia ni kawaida ukiruhusu uraia pacha kupata raia wa namna hiyo kulingana na fursa zilizopo
 
George Weah ni Rais wa Liberia ila mwanae raia wa Marekani
Watoto wake hawana uraia wa nchi moja wana uraia wa nchi tatu na wengine mbili

Wana uraia wa marekani, liberia na ufaransa na wengine ni raia wa marekani na liberia

Hivyo sio wamarekani pekee bali wana sifa sawa ktk nchi zote tatu

Kama ilivyo kwa Elon ambaye ana uraia wa US, CA na SA
 
Kama kagame anataka kukumaliza, hata uende kujificha marekani vijijini, watakufikia tu,
Kitu kikubwa wapinzani waache lugha za dharau kwa mamlaka,, watawala wengine hawanaga ngozi ngumu kama JK au samia,,
Lugha sijui eti 2025 hakuna uchaguzi ni kujipalia makaa ya moto tu,, maana uhalisia uchaguzi lazima utafanyika iwe isiwe

Kwa akili hizi machawa hawataisha. Mbona uchaguzi ulifanyika 2020 na CCM kuiba kura zote. Ila hakuna jipya zaidi ya mgao, tozo, mfumuko wa Bei na ajira ngumu.
 
Kwa sababu huwa mimi nanyoosha Rula ya UKWELI!

chiembe kwa hili unayo hoja ya Msingi!

Ila kule kukaza kwako shingo kutetea wezi,ndio kutafanya hata Point zako zionekane za ki-chama zaidi.

Wakati kuna ukweli ndani yake.
Ila inabidi watu wenye mawazo mema,tafakuri jadudi ndio wanaweza kuielewa mantiki iyopo hapo!
Huyu bwege chinembe upeo wake ni duni sana.

Hivi anamwelewa Amir Jamal? Waziri ambaye Mwalimu Nyerere aliwahi kumwelezea:
'Nimfananishe na nani Amir Jamal? Nilimteua kuwa Waziri wa Fedha nchi ikiwa kwenye matatizo makubwa ya kifedha. Nilipotaka kuanzisha viwanda, sikuona mtu mwingine wa kulisimamia hilo. Nilimteua Jamal kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Afrika Mashariki ilipovunjika, tunataka kuunda mashirika yetu, sikuona mtu mwingine isipokuwa Jamal. Nchi ikiwa katika hali mbaya ya mawasiliano, tulitaka kuiunganisha mikoa yetu kwa barabara, nilifikiria sana nani aisimamie hiyo kazi, sikuona mtu mwingine, zaidi ya Jamal. Na baadaye teba tukarudi kwenye matatizo makubwa ya kifedha, ikanilazimu nimteue tena Amir Jamal kuwa Waziri wa Fedha. Amir Jamal alikuwa mzalendo wa kweli na mtoto wa Tanzania"

Maneno hayo aliyasema Mwalimu wakati wa kifo cha Amir Jamal mwaka 1995. Lakini Jamal mara baada ya kustaafu maisha ya siasa, aliondoka na kuhamia Vancouver, Canada. Na mauti yalimkuta huko. Hata hivyo, kwa kauli hii ya Mwalimu, kuihama Tanzania hakukuwahi kupunguza uzalendo wa Jamal.
 
Sema kuwa ni raia wa marekani, liberia na ufaransa (ana uraia wa nchi tatu) na mwingine ana uraia wa nchi mbili ambazo ni liberia na marekani...

Sio kwamba wana uraia wa nchi moja pekee

Pia ni kawaida ukiruhusu uraia pacha kupata raia wa namna hiyo kulingana na fursa zilizopo

Mbona ni Yale Yale?. Ni Rais ila mtoto wake ana uraia wa nchi zingine.
 
Uzuri wa Marekani haina mwenyewe washampa mkenya Obama inchi hakuna shida
 
Kwa akili hizi machawa hawataisha. Mbona uchaguzi ulifanyika 2020 na CCM kuiba kura zote. Ila hakuna jipya zaidi ya mgao, tozo, mfumuko wa Bei na ajira ngumu.
Mi nakuambia uhalisia,, uchaguzi utafanyika,, mimi sio ccm na lisu simchukii na ni ndugu yangu kabisa huyo,, lakini ukweli ni ukweli, uchaguzi utafanyika
 
Kauli hii ameitoa Tundu Lissu wakati akichangia mada katika space huko Twitter.

Kumbe wenzetu wanataka kuleta vurugu hapa nchini, wao wameshatanguliza familia zao nje ya nchi.! Wanahamasisha watoto wetu waandamane, wapigwe rungu, wa kwao wako Trump Hotels wanakula baga na pizza.

Kwa nini Lissu hawaambii watoto wake wakane uraia wa Marekani ili wafaidi matunda ya anavyopigania? Je, Lissu sio mpango wa C.I.A katika taifa letu?

Muda utasema. Kwa Sasa hana kazi ya kumuingizia kipato, lakini anatalii majiji ya Ulaya na Marekani akila maisha kwa fahari kuu, hatujui chanzo Cha mapato yake.

Napiga picha ikulu yetu imejaa raia wa marekani, wanazurura tu katika bustani, wanajisaidia vyooni, na kuoga, wanaleta marafiki zao, ambao pengine no majasusi wanapandikiza kamera na vinasa sauti, wanachomoa mafaili na kuondoka nayo, na kuhaki computer zetu, au ku-recruit staff wa ikulu dhidi ya nchi yetu
Akili fupi.
 
Nilishasema mara nyingi, Lisu ni CIA project,, na sasa wanadai wameamua 2025 hakuna uchaguzi,, hii maana yake inaweza kuwa wanapanga kuanzisha machafuko,, time will tell

Dah aiseeh!. CIA Agent Tena?. Yani CIA agent wanajulikana hadharani?. Mtatafutia majina mengi, Ila Cha muhimu alishinda mipango miovu.
 
Kauli hii ameitoa Tundu Lissu wakati akichangia mada katika space huko Twitter.

Kumbe wenzetu wanataka kuleta vurugu hapa nchini, wao wameshatanguliza familia zao nje ya nchi.! Wanahamasisha watoto wetu waandamane, wapigwe rungu, wa kwao wako Trump Hotels wanakula baga na pizza.

Kwa nini Lissu hawaambii watoto wake wakane uraia wa Marekani ili wafaidi matunda ya anavyopigania? Je, Lissu sio mpango wa C.I.A katika taifa letu?

Muda utasema. Kwa Sasa hana kazi ya kumuingizia kipato, lakini anatalii majiji ya Ulaya na Marekani akila maisha kwa fahari kuu, hatujui chanzo Cha mapato yake.

Napiga picha ikulu yetu imejaa raia wa marekani, wanazurura tu katika bustani, wanajisaidia vyooni, na kuoga, wanaleta marafiki zao, ambao pengine no majasusi wanapandikiza kamera na vinasa sauti, wanachomoa mafaili na kuondoka nayo, na kuhaki computer zetu, au ku-recruit staff wa ikulu dhidi ya nchi yetu
Jiulize kwanza alifikaje huko ulaya,kwanini Yuko ulaya na si kwenye bunge la Tanzania!!?
Ukipata jibu,hao waliosababisha awe ulaya ndio wabaya kwa usalama wa nchi hii.
Hii nchi imeishauzwa,we uandamane,usiandamane,Lisu anajaribu kuwapa watu Elimu wajue haki zao,yeye alilipa kwa damu,alipigwa risasi 19!!mchana kweupeee!!
Harsfu waliompiga risasi,wewe ndio unawaona watu wa muhimu kwa nchi hii!
Lowasa,warioba,Mwinyi,Kikwete,Kinana,Makamba,Wana watoto na ndugu wenye uraia wa US,naUK,sio kitu Cha ajabu,
Hata Diamond watoto wake Wana uraia wa South Afrika,kwani Diamond Kuna kitu anachochea hapa nchini?,jadili hoja,acha kuwa kama mburukenge
 
Sasa kinachokushangaza ni kipi? Watanzania wangapi wanauraia wa marekani?
 
W
usimtukane aisee.ana hoja kwa kweli.TISS inatakiwa kuwa inachunguza maisha ya wagombea wetu kabla ya kupewa majukumu makubwa ya taifa .wato wako wote ni raia wa nchi nyengine.wawezaje kuwa rais wetu? usitoe mfano wa Trump au OBAMA. Watoto wao na wao wenyewe ni raia wa marekani.Sasa TL ni raia wa tanzania then watoto raia wa marekani.huoni kwamba watoto hawa ni usalama wa marekani wanaweza kudukua mambo yetu kwa kupewa siri na baba yao? tumia akili aisee.

Mbona Lissu watoto wake walizaliwa marekani?. Uraia wao ni wa kuzaliwa
 
George Weah ni Rais wa Liberia mtoto wake juzi kafunga bao na timu ya taifa ya marekani

So na George ni C.I.A?

Wakina Mandela waliishi Morogoro na Butiama wakati wa ubaguzi wa rangi south africa so hoja yako Haina mashiko.

Rais wa Congo wa Sasa aliishi Sana ubelgiji so na yeye ni mbelgiji?

Huyo trump mwenyewe na obama ukiwatazama hawana hata asili ya marekani lakini wametawala

Obama katumwa na kenya marekani na mke wake alitumwa na israel?

Hoja zako za kipumbavu Sana watu wataishi vipi kwenye nchi ambayo usalama wao hauna uhakika? Hakikisheni kwanza usalama wa watu ndio muanze kuwahukumu.

Wakina Akwilina, Azory, Mawazo wako wapi?
Acha zogo we we, hatuwezi mpa uraisi huyo kiherere
 
Back
Top Bottom