Mamalishe wanatumia dawa ya Panadol kunogesha mapishi
Kuna kasumba imekuwa sugu sana kwa wauza mchele kuchanganya mchele na mafuta ya kupikia wengi ya nguruwe ili mchele uwe na mng'ao mzuri. Sasa mnaohusika na ubora wa vyakura vya binadamu yani mabwana afya na bi afya hebu tasaidieni tukifa
 

Utumbo, uwe wa mbuzi au wa ng’ombe kwa asili ni mgumu, hivyo kuhitaji muda wa kutosha wa kupika ili uive.

Baadhi ya watu katika mapishi ya utumbo, hutumia viungo kama vile tangawizi, limao, papai bichi, siki na ajinamoto ili kuufanya uive mapema.

Wapo pia wanaotumia sufuria isiyoruhusu mvuke kutoka wakati wa kupika (pressure cooker) ambayo huwezesha utumbo kuiva ndani ya muda mfupi.

Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni baadhi ya mamalishe hutumia dawatiba aina ya panadol wakidai inalainisha na kuwahisha utumbo kuiva.


Mamalishe anayefanya biashara Buguruni, aliyejitambulisha kwa jina la Mama Aziza anasema hutumia panadol kupika utumbo.

Anasema alianza kutumia dawa hiyo kutokana na ushauri aliopewa na rafiki aliyekuwa akifanya kazi kwenye mgahawa uliopo Kariakoo, jijini hapa.

“Sikuwa nafahamu matumizi haya ya panadol, rafiki yangu alipokuja kwenye biashara zangu aliniona naweka tangawizi na viungo vingine, ndipo aliponiambia ili mboga yangu iive haraka niweke dawa hiyo. Nilipojaribu niliona matokeo na ninatumia kidonge kimoja hadi viwili,” anasema.

Mama Aziza anasema hafahamu iwapo kuna madhara ya kuchemsha utumbo kwa kuweka panadol, lakini alitumia njia hiyo kwa kuamini ni kilainishi kama vilivyo vingine vinavyowekwa kwenye nyama.

Mamalishe eneo la Kimanga, jijini Dar es Salaam, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, anasema anatumia dawatiba hiyo ili kuokoa muda wa kuchemsha supu.

Anasema asubuhi ni muda wenye wateja wengi, hivyo hutumia kidonge kimoja kuivisha kwa haraka utumbo na pia kupunguza matumizi ya mkaa katika upishi.

Ernest Kimbau, mtaalamu wa ufamasia, anasema madhara yanaweza kuwapo kwa sababu dawatiba ina kiwango ambacho watu wanatakiwa kutumia.

Anasema panadol ina kiwango chake na kinapozidi ni kuwa mtu amejizidishia dawa na inabadilika kuwa sumu inayoweza kuleta tatizo kwenye ini. Anasema anayekunywa supu iliyowekwa panadol maana yake ni kuwa anakula dawa bila utaratibu, kitendo ambacho si kizuri.

Mwananchi
Sukari inafanya kazi hiyo hata maharage yanaiva haraka
 
Mdukuzi aliyejulikana kwa jina Arion Kurtaj, mwenye umri wa miaka 18, mkazi wa Oxford nchini Uingereza, ambaye alihusishwa na udukuzi wa program ya michezo ya video (Video Game) ya Grand Theft Auto VI, inayotarajiwa kutoka mnamo 2025, amehukumiwa kifungo cha muda usiojulikana ndani ya hospitali, hadi pale madaktari watakapoithibitishia mahakama kuwa kijana huyo si hatari tena kwa umma.
.
Kurtaj ambaye aliwahi kuwa mfuasi wa genge la kimataifa la udukuzi linalojulikana kama Lapsus$, anakabiliwa na hali ya usonji(Autism) na alibainika kuwa alifanya mashambulizi ya kimtandao dhidi ya kampuni ya Rockstar Games, ambao ndio watengenezaji wa GTA VI.
.
Kulingana na BBC, imeelezwa kuwa Kijana huyo, licha ya kunyang'anywa kompyutampakato(laptop), alipokuwa nje kwa dhamana baada ya kudukua kampuni ya Nvidia, ambapo aliwekwa hotelini chini ya ulinzi wa Polisi lakini bado alifanikiwa kuishambulia kampuni ya Rockstar Games kisha kuiba na kuvujisha video 90 za GTA VI, kwa kutumia Runinga(TV), Amazon Fire Stick ya chumba hicho pamoja na simu janja, keybord na kipanya cha kompyuta (Mouse).
.
Mahakama hiyo ilielezwa kuwa Kurtaj, alifanya vurugu alipokuwa kizuizini na kusababisha uharibifu wa mali na kwamba alionyesha dhamira yake ya kurudi kwenye uhalifu wa mtandaoni haraka iwezekanavyo.

#ITVUpdates #technology
FB_IMG_1703326446220.jpg
 
Baada waweke magadi Yale ya mlenda kidogo tu, wanaweka panado Tena kazi kweli kweli.
 
Kuna kasumba imekuwa sugu sana kwa wauza mchele kuchanganya mchele na mafuta ya kupikia wengi ya nguruwe ili mchele uwe na mng'ao mzuri. Sasa mnaohusika na ubora wa vyakura vya binadamu yani mabwana afya na bi afya hebu tasaidieni tukifa
"mabwana afya na bi afya hebu tasaidieni tukifa"! Unataka wakuzike au wakununulie sanda?
 
Back
Top Bottom