Msaada kwa wenye utaalamu na masuala ya dini je ni kweli Quran imeshushwa kutoka mbinguni?

Msaada kwa wenye utaalamu na masuala ya dini je ni kweli Quran imeshushwa kutoka mbinguni?

Waislamu wajanja, walipoona mapungufu kwenye Biblia wao wakaona waje na gear kuwa kitabu chao kilishushwa ili kupunguza maswali na migawanyiko kwenye dini yao. Mungu hajawahi kuandika kitabu chochote kile😅😅
 
Waislamu wajanja, walipoona mapungufu kwenye Biblia wao wakaona waje na gear kuwa kitabu chao kilishushwa ili kupunguza maswali na migawanyiko kwenye dini yao. Mungu hajawahi kuandika kitabu chochote kile😅😅
kwani wapi bible imetoka kwa Mungu au yesu alipewa bible ? ukionyesha naslimu
 
kwani wapi bible imetoka kwa Mungu au yesu alipewa bible ? ukionyesha naslimu
Umeona mahala popote nimesema Bible ilishushwa na Mungu? Yesu mwenyewe mpaka anakufa hajui kitabu kinaitwa Biblia wala dini inayoitwa uKristo. Hata hao mitume tunaambiwa waliandika Biblia hakuna hata mmoja aliyeondoka akaacha kitabu kinaitwa Biblia.
 
Huyo sterling mwenyewe Picha tu linaanza unaambiwa alizaliwa akiwa na jando tayari, hakuwa na kimvuli cha juwa wala mbalamwezi na alikuwa anaona upande zote bila kugeuka, na akilala fofo usingizini anawasikia story zenu zote mnazopiga.

Sasa hilo la kushushiwa Quran mbona Dogo, kwakweli hawa jamaa wa middle east wametuweza.
Sasa watwambie wanajua maana ya mtu kulala usingiz Fofo?
 
Umeona mahala popote nimesema Bible ilishushwa na Mungu? Yesu mwenyewe mpaka anakufa hajui kitabu kinaitwa Biblia wala dini inayoitwa uKristo. Hata hao mitume tunaambiwa waliandika Biblia hakuna hata mmoja aliyeondoka akaacha kitabu kinaitwa Biblia.
Sawa
 
Ndio wapo!


Okay, kwakuwa unadai unajua kiarabu basi naomba unipe tafsiri ya maneno haya:-

و الذين يدعون من دون الله لا يخلقون شيءا و هم يخلقون

اموات غير أحياء و مما يشعرون ايان يبعثون
 
Okay, kwakuwa unadai unajua kiarabu basi naomba unipe tafsiri ya maneno haya:-

و الذين يدعون من دون الله لا يخلقون شيءا و هم يخلقون

اموات غير أحياء و مما يشعرون ايان يبعثون
wale wanawaita Mungu hawajaumba chochote bali wao ndo wamumbwa na Mungu.


wafu hwana chochote wanachojua wanapofufuliwa.
 
wale wanawaita Mungu hawajaumba chochote bali wao ndo wamumbwa na Mungu.


wafu hwana chochote wanachojua wanapofufuliwa.

Tafsiri yake iliyonyooka ni hii:-

Na wale ambao wanaitwa badala ya Allah (hao) hawaumbi chochote bali wao wameumbwa.
Ni wafu, si wazima, na hawajui watafufuliwa lini. (Quran 16:20-21).

Aya hiyo ni ya Qur'an na kashushiwa mtume (saw), hapo anaambiwa kwamba Wale wote wanaoitwa Mungu badala ya Allah watu hao wameumbwa, hawaumbi na ni Wafu na hawajui watafufuliwa lini nabii Isa (as) naye yumo.kwenye kundi hilo la kuitwa Mungu kimakosa badala ya Allah soma Qur'an (5:116-117), hivyo kipindi aya hii inashuka ni lazima alikuwa kafariki zamani.

Tafakari kwanza hiyo aya kisha nitakuletea aya zingine.
 
Tafsiri yake iliyonyooka ni hii:-

Na wale ambao wanaitwa badala ya Allah (hao) hawaumbi chochote bali wao wameumbwa.
Ni wafu, si wazima, na hawajui watafufuliwa lini. (Quran 16:20-21).

Aya hiyo ni ya Qur'an na kashushiwa mtume (saw), hapo anaambiwa kwamba Wale wote wanaoitwa Mungu badala ya Allah watu hao wameumbwa, hawaumbi na ni Wafu na hawajui watafufuliwa lini nabii Isa (as) naye yumo.kwenye kundi hilo la kuitwa Mungu kimakosa badala ya Allah soma Qur'an (5:116-117), hivyo kipindi aya hii inashuka ni lazima alikuwa kafariki zamani.

Tafakari kwanza hiyo aya kisha nitakuletea aya zingine.
Point yako sioni naona unaruka nionyeshe wapi isa alikufa mara ulize hili mara hili😂😂😂...Ishu ni kuelimisha ila sioni point yao hapo wanaitwa ni wengi ni Miungu wapo msanamu ,miti mpaka wanyama wanaabudiwa na hawa wanawalichoumba kabisa ..



Ebu jaribu kuniambia wapi isa alikufa ? Unanitokea kweny madq unafanya collocation katika aya ambao haziendani....
 
Tafsiri yake iliyonyooka ni hii:-

Na wale ambao wanaitwa badala ya Allah (hao) hawaumbi chochote bali wao wameumbwa.
Ni wafu, si wazima, na hawajui watafufuliwa lini. (Quran 16:20-21).

Aya hiyo ni ya Qur'an na kashushiwa mtume (saw), hapo anaambiwa kwamba Wale wote wanaoitwa Mungu badala ya Allah watu hao wameumbwa, hawaumbi na ni Wafu na hawajui watafufuliwa lini nabii Isa (as) naye yumo.kwenye kundi hilo la kuitwa Mungu kimakosa badala ya Allah soma Qur'an (5:116-117), hivyo kipindi aya hii inashuka ni lazima alikuwa kafariki zamani.

Tafakari kwanza hiyo aya kisha nitakuletea aya zingine.
Tuseme sijui kitu ebu nionyeshe wapi isa alifariku mbona unanizungusha nipo humu online ila wapi unanizungusha😂😂😂..
 
Heri ya Pasaka?

Heri ya Mfungo kwa WAISLAMU.

Ndugu zangu wataalamu wa Masuala ya Biblia na Quran NAOMBENI MSAADA wa hili swali linalonisumbia Daima?

JE ni KWELI QURAN ilishushwa kutoka MBINGUNI?

1. Inamaana Mungu alitengeneza karatasi.

2. Akatafuta Penny Compyuta printer nk?

3. Mbona ni tofauti sana na KIPINDI Cha Musa Mungu aliandika zile Amri Kumi kwenye mabamba mawili ya mawe na kumpa Musa kwenye Mlima Sinai. (Kutoka 24:12-18) Zile Amri Kumi zimeorodheshwa kwenye Kutoka 20:1-17 na Kumbukumbu la Torati 5:6-21.

4 JE tuna ushahidi Gani kama Quran ilishushwa na Mungu?

Natamani Mjadala Huu tujikite kwenye kujibu hoja sio Dini .

Natanguliza shukrani nyingi.
Sikiliza video hii imeelekeza natumai utafahamu kitu ndugu yangu
 

Attachments

  • fb339ed40cd2135fae03621cb7126fe6.mp4
    11.2 MB
Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur’ani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.”

ADUI wa jibril si ni SHETANI, MAJINI NA MAPEPO.

KWAHIYO HAYA HII INATUAMBIA QURAN IMEANDIKWA NA ADUI WA MUNGU AMBAYE NI SHETANI.

Ukweli wote upo hapa sasa.
Kama Kuna mtu anahoja anakaribishwa ..............
 
Point yako sioni naona unaruka nionyeshe wapi isa alikufa mara ulize hili mara hili😂😂😂...Ishu ni kuelimisha ila sioni point yao hapo wanaitwa ni wengi ni Miungu wapo msanamu ,miti mpaka wanyama wanaabudiwa na hawa wanawalichoumba kabisa ..



Ebu jaribu kuniambia wapi isa alikufa ? Unanitokea kweny madq unafanya collocation katika aya ambao haziendani....


Katika hiyo aya Allah anataka tujue kwamba watu wote waliokuwa wanaabudiwa kipindi aya hii inashuka walikuwa ni wafu, kumbuka Yesu naye alikuwa akiabudiwa hivyo naye kipindi aya hii inashuka alikuwa mfu, hiyo ndio point ya aya hiyo ambayo Allah anatufahamisha kama hiyo siyobpoint hebu leta point yako juu ya hiyo aya.
 
Tuseme sijui kitu ebu nionyeshe wapi isa alifariku mbona unanizungusha nipo humu online ila wapi unanizungusha😂😂😂..

Wewe unadhani katika Qur'an utapata aya inayosema, nabii fulani na fulani kafa!!, kwani Quran imekuwa ni kitabu cha matangazo ya vifo vya manabii?? Qur'an inapotaja vifo vya manabii huwa inataja kwa ujumla mfano katika (3:144) au inataja kwa namna ambayo inabidi mtu utumie akili kujua.

Sasa tuliza fikra zako na tutazame hizi aya mbili za Qur'an (tafsiri);

"Na Allah atakaposema; Ewe Isa bin Mariam! Je uliwaambia watu; Nishikeni mimi na mama yangu kuwa waungu wawili badala ya Allah??, (Isa) atasema; Wewe ndiwe mtakatifu hainipasi mimi kusema ambayo sina haki nayo, kama ningalisema bila shaka ungalijua; Unajua yaliyomo nafsini mwangu, lakini mimi siyajui yaliyomo nafsini mwako, hakika wewe ndiye ujuaye sana mambo ya ghaibu". [ Qur'an 5:116]


Aya inayofuatia ambayo ni muendelezo wa hiyo iliyotangulia inasema:-

"Sikuwaambia lolote ila yale uliyoniamuru ya kwamba; Mwabuduni Allah, Mola wangu na Mola wenu, na nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa kati yao, lakini uliponifisha Wewe ukawa mchungaji juu yao, na wewe ni shahidi juu ya kila kitu". [Qur'an 5:117]

Hilo ni swali Allah atamuuliza nabii Isa (as) siku ya Qiyama kwamba; yeye aliwaambia watu wamuabudu yeye na mama yake??, naye atajibu siku hiyo ya Qiyama kwamba hakuwaambia lolote isipokuwa yale aliyoamrishwa na Allah kwamba Wamuabudu Allah, na hajui huko nyuma kama watu walimuabudu yeye kama Mungu kwakuwa alikuwa kafariki.

Swali ni hili: kama nabii Isa leo yupo hai mbinguni na leo hii bado anaabudiwa kama Mungu sasa atawezaje siku ya Qiyama kumwambia Allah kwamba:- Sikuwaambia lolote ila yale uliyoniamuru kwamba Muabuduni Allah Mola wangu na mola wenu----- uliponifisha wewe ukawa mchungaji wao---!!??

Hapo ina maana Isa (as) hivi sasa hajui kama anaabudiwa yeye na mama yake kama Miungu wawili kwakuwa kafa na ndio maana siku ya Qiyama atajibu hivyo.

Hiyo ni aya inayothibitisha kuwa hivi sasa Isa (as) kafa ndio maana hajui kama yeye anaabudiwa na siku ya Qiyama atajitetea mbele ya Allah akisema kwamba kipindi anaabudiwa alikuwa hajui kwakuwa Allah alikuwa kamfisha na Allah mwenyewe ndiye hivi sasa amebaki kuwa mchungaji wa hao wanaomuabudu Isa (as), Isa leo hajui chochote kwakuwa kafa zamani mno (Qur'an 3:144).

Nimeandika kwa kirefu na kwa msisitizo ili kukufafanulia hii point muhimu ya kifo cha nabii Isa (as).

Qur'an ni kitabu cha watu wanaotumia akili.
 
Back
Top Bottom