Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

Samahani bwana Malila nahisi nimechelewa sana hii thread ni toka 2009 lakini nahisi ntafaidika na usaidizi wako,nimeacquire hekari 100 sumbwanga Rukwa na hekari 20 hapo Bungu mkoani Pwani na nina vision ya kilimo kikubwa.....nimefikiria miti natarajia usaidizi wako mkuu wa kiushauri na connections.Email yangu ni willynyakua@gmail.com

Nitachangia cho chote ninachokijua ili ufikie malengo yako. Nimekutumia mail yangu kama una maswali binafsi, lakini yale ya kawaida tutapeana hapa hapa jamvini. Karibu tuanze kujadiliana.

Kwa Sumbawanga, nashauri anza na nafaka ( Mahindi,mtama,ngano,ulezi), au mazao yatoao mafuta,kisha anza kufanya utundu wa kujua namna ya kusindika nafaka hizo au mazao hayo. Nakuibia wazo, nenda pale Ihemi Iringa, kuna Wazungu wanasindika sembe, na wanaiita SEMBE TOFAUTI,na kweli ni sembe tofauti. Nenda kaibe ujuzi pale, hasa ujue mashine zao wamezitoa wapi mpaka ziwe tofauti na zingine. Usilime ili uwauzie mazao wenzako, sindika mwenyewe mkuu.

Njoo kwenye miti, najua utakimbilia mitiki kwa huko Bungu, je umejaribu Msederela, au acrocarpus. Navuta subira ili nijue miti fulani iliyooteshwa pale Msata msimu huu kama itafanya vizuri.

Nimekujibu jumla sana, lakini inabidi utoe sifa za ardhi yako ili wengine pia watoe mawazo yao sawa na wanacho kijua.
 
Ukisoma ushaur wa kila mtu unaweza kupata wazo pia maana naona kila mkoa umeguswa

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Mimi ni mfugaji, nitakushauri kufuga ngombe kwa mchakato ufuatao:

Ujenzi wa banda = Ths 500,000/=
Manunuzi ya Ngombe 5 x Tsh 900,000 = Tsh 4,500,000/=
(Ngombe utawanunua wakiwa na mimba ya miezi 6)
Kuwahudumia ng'ombe kwa miezi mitatu kabla ya production = Tsh 1,500,000/=
(inahusisha mshahara kwa wafanyakazi wawil + chakula + madawa)

Jumla = Tsh 6,500,000/=

Baada ya Miezi 3;

UZALISHAJI:

Ngombe hawa watakuwa wakitoa maziwa si pungufu ya lita 5 kwa asubuhi na jioni kwa kila ng'ombe. Hivyo uzalishaji kwa siku utakuwa lita 10 kwa siku kwa ng'ombe.

MAPATO

Lita 10 x Ng'ombe 5 = lita 50 kwa siku x Tsh 1000 (bei ninayouza mimi hapa) = Tsh 50,000 kwa siku
Mapato kwa mwezi = Tsh 50,000 x 30 = 1,500,000/=

Gharama za uendeshaji kwa mwezi = Tsh 600,000/=

Faida = Tsh 900,000/= kwa mwezi

BAADA YA MIAKA 5:

Kumbuka ng'ombe huzaa kila mwaka hivyo basi baada ya miaka mitano utakuwa na ng'ombe wasiopungua 25. Kipato chako kwa mwezi unaweza kufikia si pungufu Tsh 18,000,000 endapo utakuwa na ngombe jike 20 kati ya hao 25.




Dah kweli wewe ni mtu ndugu yangu, maana sisi wengine tuliokwepo nje tuna taka kurudi makwetu laki hatujui cha kufanya, unaambiwa tu kunabiashara nyingi za kufanya lakini watu hawa weki uwazi hizo biashara. Mimi nilipendelea sana mifugo, kama ngombe na kuku, lakini naona kuku watakua wa kienyeji, nitawafuga kwa njia ya kisasa, Watakua nje mchana kama kawaida, ni huduma ya chakula tu ndio nitaboresha, chapili ndio hiyo ya ngombe. Sasa ni kwamba kila mtu anasema lake, kuna mtu kaniambia ngombe anaweza toa lita 20 kwa siku, je kweli wapo hao, na hao ngombe wanapatikana kiurahisi au mpaka usubiri miezi au mwaka?
 
Dah kweli wewe ni mtu ndugu yangu, maana sisi wengine tuliokwepo nje tuna taka kurudi makwetu laki hatujui cha kufanya, unaambiwa tu kunabiashara nyingi za kufanya lakini watu hawa weki uwazi hizo biashara. Mimi nilipendelea sana mifugo, kama ngombe na kuku, lakini naona kuku watakua wa kienyeji, nitawafuga kwa njia ya kisasa, Watakua nje mchana kama kawaida, ni huduma ya chakula tu ndio nitaboresha, chapili ndio hiyo ya ngombe. Sasa ni kwamba kila mtu anasema lake, kuna mtu kaniambia ngombe anaweza toa lita 20 kwa siku, je kweli wapo hao, na hao ngombe wanapatikana kiurahisi au mpaka usubiri miezi au mwaka?

wapo mpk wanaotoa lita 24 kwa sku ninao
 
fungua hardware, ila mwanzoni inataka moyo mambo yakishachanganya inakua poa sana
 
Anzisha mradi wa kufuga kuku wa kienyeji wilaya za nje ya mji wa dar es salaam utapiga hela mpaka umnung'unikie mumgu kwa nini hukujiunga JAMII FORUM mapema???
 
Kama uko Dar nenda Mkuranga kijiji cha Shungubweni au Funza au Mwalusembe utakuta ardhi haina mwenyewe. Inafikika mwaka mzima,tatizo wenyeji wavivu sana. /

Huko Funza nk sh ngapi ardhi?
 
Mkuu Mbu,

Sisi hatuchomi ndizi kwa biashara ya kumsubiri mteja tusiemfahamu, hatuhitaji matangazo wala utambulisho. Sisi ni wateja na wao pia ni wateja, hivyo kwa pamoja tunachoma ndizi.

Wow!! Hili ni bonge la biz!! Niuzie nikuuzie.
 
Nimesoma hii thread nimeishia page ya 10, nawahi sehemu nitaendelea nikirudi.
Mbu upo UK au Bongo? tuwasiliane nina good ideal, regardless hii thread ni muda mrefu lakini inaweza kuwa bado ni relevant.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Huko Funza nk sh ngapi ardhi?

Mkuu sasa hivi ni maumivu sana, bei imepanda sana kutoka 250 mpaka 500 kwa eka, sababu kuna waarabu wamenunua mapande makubwa sana, mchina kaingia anachimba madini, kuna beach ya boza nayo imevamiwa, eka moja 16M tzs,na yule jamaa mwenye zoo kalamba mapande, wenyeji wameshituka vibaya. Ila ukitumia wenyeji bado unaweza pata kwa laki nne kila kitu kwa eka moja.
 
Mkuu sasa hivi ni maumivu sana, bei imepanda sana kutoka 250 mpaka 500 kwa eka, sababu kuna waarabu wamenunua mapande makubwa sana, mchina kaingia anachimba madini, kuna beach ya boza nayo imevamiwa, eka moja 16M tzs,na yule jamaa mwenye zoo kalamba mapande, wenyeji wameshituka vibaya. Ila ukitumia wenyeji bado unaweza pata kwa laki nne kila kitu kwa eka moja.

Inabidi utupe contacts sasa maana hapa karibu weekend unaenda fasta.
 
Malila shukrani sana,najipanga nitakutafuta...Wana JF mbarikiwe sana kwa ideas ambazo si rahisi kuzipata sehemu nyingine
 
wadau ikiwa nataka kuimport bidhaa kutoka nje na kuziuza ndani ya nchi hapa,je ni bidhaa ipi itanilipa? mtaji kuanzia milioni 50 kwenda hadi milioni 200.
au kama una successfully business plan yoyote nisaidie ndugu yangu, sitakuacha.
 
Back
Top Bottom