Jamii yoyote iliyostaarabika mi lazima iwalinde wazee au senior citizens wao. Kwa sababu kwenye wazee ndio tunapata uzoefu na busara (with age comes wisdom and experience) ingawa sometimes age comes alone.
Wazee ni watu wenye umri mkubwa na mara nyingi kibinadamu umri mkubwa unaambatana na magonjwa mengi. Ndio maana wizara ya afya na who wanasisitiza kua tuwalinde wazee wetu kwa sababu wako susceptible na magonjwa kwa sababu wengi hua wanasumbuliwa na magonjwa mengine (other underlying medical conditions).
Rais wetu ni mzee, ana umri wa zaidi ya miaka 55, hivyo yeye na wazee wengine ndio prime suspect wa corona. Lakini pia Rais yeye ndie raia namba moja na lazima ahakikishiwe usalama wa afya yake kwa gharama yoyote. Hii ni jukumu la kwanza la kitengo maalum cha ulinzi wa rais, kuhakikisha wanafanya threat analysis zote zikiwemo za kisiasa na za kiafya za rais na kuhakikisha mzee anakua salama, kumuondoa eneo ambalo sio salama na kumficha eneo lenye usalama.
Sasa, kuna watu wanataka rais aje au arudi Dar kutokea Chato, kiusalama Dar sio salama kwa afya ya rais kwa sasa kwa sababu zilizowazi kabisa.
Tumuache Rais apumzike Chato. Hoja ya kumtaka kurudi Dar haina mashiko.