#COVID19 Mtazamo, Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Serikali na Wananchi kuhusu Ugonjwa wa Corona - COVID-19
Hapo wa kumfananisha na Magufuli ni Trump pekee, hao wengine umeamua kujiweka upofu mwenyewe kuwaweka kwenye listi ya hao wawili.

Kutomweka Mseveni kwenye listi hiyo..., pengine hujui kilichofanyika huko Uganda. Mfano unaotuhusu moja kwa moja.

Nimesoma majina tu sijasoma ulinganisho ulioufanya hapo.
 
Katika ugonjwa huu, hakuna garantee kwamba kila kitu kilichofanyika nchi moja kinaweza kufaa nchi nyingine na kufanikiwa. Hii ni vita yako peke yako na watu wako
Hili sio kweli, na unajua hivyo. Sayansi haiwezi ikawa ya nchi moja na isiwe na matumizi sehemu nyingine.
 
/ndio uone Mungu alivyo wa ajabu!
Wale wenye uwezo kubwa zaidi, Marekani, ndio wanaoongoza kwa kuathirika.
Uwezo wao, utajiri, na utaalam hauja wasaidia sana.
Akili ndogo, je, unakubaliana na takwimu za nchi yako? Kwa nini watu wanalalama kwenye mtandao kuwa kila siku jiji linapeleka watu ktk eneo lililotengwa?
 
Njia zote zilizowahi kutumika na zinazoendelea kutumika kushughirikiwa hili janga, zinamateso na hazisaidii, Ijapokuwa Neno kujifungia ni tamu masikioni mwa watu,inapoelezewa inaviutia na kuonekana kama inaweza kuleta unafuu

Lakini ukweli mchungu, bado si sahihi, njia ambayo inaweza kuwa ni sahihi ni, Kwanza kumtambua adui yetu na huwa anaitumia Mbinu ipi kuwaathiri watu, baada ya hapo, njia salama ya kitalaamu ya kukabiliana naye bila kuathiri mambo mengine... Ni njia ya kuepukana kabisa na msongamano wa watu, kunawana kila wakati Kwa maji na sabuni, kuvaa barakoa Wakati wote.

Wakati huu wa hatari wa kuambukizana Corona, jilinde, muone kila mtu ni adui yako mwenye kunyemelea uhai wako, Lockdown ni mojawapo wa njia ya kujikinga Ila ni ya mateso nayo haina uhakika wa salimia zote

Fuata maelekezo yoote yanayotolewa na wataalamu wa Afya
 
/ndio uone Mungu alivyo wa ajabu!
Wale wenye uwezo kubwa zaidi, Marekani, ndio wanaoongoza kwa kuathirika.
Uwezo wao, utajiri, na utaalam hauja wasaidia sana.
Mkuu sisi silaha yetu ni kusema uongo otherwise kwa strategy zetu hizi tungewapiga gape kubwa sana
 
Jaribu kufanya hiyo kwenye mvuke wa degree mia Kama ulivyoshaukiwa uone chemical change inavyotokea mkuu
Huwa nawachemshia kuku wangu majani ya mwarobaini.. aisee ule mvuke ni balaa.. ni mkali sana
 
Huwa nawachemshia kuku wangu majani ya mwarobaini.. aisee ule mvuke ni balaa.. ni mkali sana
Mkuu acha watu wafate mawazo ya mkemia fake Kama wanadhani nyuzi joto 100 ni joto la kusogeza pua?
 
*NADHANIA* KUANZIA LEO, KILA MTU AVAE MASK, KUVAA MASK IWE LAZIMA UKIWE NDANI YA GARI , NJE, POPOTE PALE, UVAE MASK

GHARAMA ZA MASK ZIWE 1000, maana kale ka 3000 kanakuwa valid for just 4 hours, kwa masaa 12 unatoa 9000

muhimu hii
 
Hii ingesaidia sana Mbona sisi wabishi sana kuelewa?
Basi hata kuiga hatuwezi
Adjustments.jpg



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Tuliona Rais Yahya Jameah aliwahi kusema kuwa ana dawa ya kutibu HIV

Leo tumesikia Raisi wa Madagascar naye kasema ana dawa ya kienyeji inatibu corona

Mimi nakubariana na mengi ambayo raisi Magufuli amekuwa akiyafanya kipindi hiki cha corona ila kuna mambo ambayo jana yamenifanya kutafakari.

Mfano kusema watu wasifungiwe siku 14 iwapo wakipimwa wakakutwa hawana corona, wataalam wanasema dalili za corona zinatofautina baina ya mtu na mtu kutegemea na kinga yake. Kwa wengine inaweza kutokea siku ya pili na kwa wengine inachukua mpaka siku 13.

Kusema kwaamba kupuliza Chlorine hakuui kirusi cha corona? Hapa pia nina shaka maana niliona anajaribu kuchambua field ya utabibu ambayo sina hakika kama anaimudu.

Pia nimegundua kuwa raisi wetu anapenda sana conspiracy theories.

Siungi mkono watu kufungiwa ndani na namuunga mkono,lakini ninadhani hili lingeendana na hatua muhimu naona kama analicukulia hili jambo kawaida. Huenda siku zijazo akasema shule zifunguliwe.

Mara nyingi kinachoponza Afrika muda mwingine ni kutumia pesa nyingi kuwasomesha wataalam na kuwaajiri tukawalipa mishahara mikubwa, halafu utendaji na maamuz yao ya kitaaluma yakaingiliwa na wanasiasa.
Magu hakukosea kusema chlorine haina athari kivile dhidi ya corona virus bsli bacteria! Na pia hakukosea kusema pombe yaani alcohol kama methyl alcohol 70 % inakidhi zaidi ya chlorine! Pia hakukosea aliposema kufukiza ni tiba mbadala inayotumia joto la mvuke kupunguza kama sio kuondoa madhara ya mafua!
Kama ni msomaji basi fuata hiyo link! Ukimaliza nitakupa nyingine!

https://www.tandfonline.com/loi/best19

Magu ni kichwa! Watu wenye akili za kushikiwa hamtakuja muelewa!
 
Yule jamaa huwa anajiona anajua kila kitu.

Kukaa tu wizara ya UJENZI huwa anajichukulia, ashakuwa ENGINEER kabisa
Being a man with a simple mind as you are how can you understand a mind of a genious?
 
Mkuu acha ujinga,maji yakiwa na nyuzi joto Mia unadhani mvuke unaotoka hapo una nyuzi joto ngapi? Jaribu kufanya hivyo na huo ujinga wako uone Kama sura haitabadirika.mmekuwa wajinga hadi kupitiliza
Kumbe mambumbumbu wa kufukiza ni wengi hivi chuu niyo!!?
 
Magu hakukosea kusema chlorine haina athari kivile dhidi ya corona virus bsli bacteria! Na pia hakukosea kusema pombe yaani alcohol kama methyl alcohol 70 % inakidhi zaidi ya chlorine! Pia hakukosea aliposema kufukiza ni tiba mbadala inayotumia joto la mvuke kupunguza kama sio kuondoa madhara ya mafua!
Kama ni msomaji basi fuata hiyo link! Ukimaliza nitakupa nyingine!

https://www.tandfonline.com/loi/best19

Magu ni kichwa! Watu wenye akili za kushikiwa hamtakuja muelewa!
Mbona umejibu kitu ambacho sijaandika? Umesoma nilichoandika au umejibu alichosema yeye in general?
 
*NADHANIA* KUANZIA LEO, KILA MTU AVAE MASK, KUVAA MASK IWE LAZIMA UKIWE NDANI YA GARI , NJE, POPOTE PALE, UVAE MASK

GHARAMA ZA MASK ZIWE 1000, maana kale ka 3000 kanakuwa valid for just 4 hours, kwa masaa 12 unatoa 9000

muhimu hii

Naunga mkono hoja.

Hata hili nashangaa wanashindwa kutumia rungu la serikali kuenforce wakati iko obvious kabisa kuwa mask zinapunguza maambukizi.
 
Ndivyo unavyo weza kufikia uamuzi. Naam, University of Dar es salaam inabidi wajitathimini juu ya ubora wa PhD zao.

Hivi ni kweli hakuna chemicals zinazo ua virus?Fumigation chemicals zinaua bacteria na virus haraka sana.

Changamoto aliyo nayo binadamu kwa hawa corona virus ni pale anapo kuwa ndani ya mwili wa binadamu kwani ni lazima tumuangamize virus bila kuua cells za mwili wa binadamu.
Jana nime shanga mambo mengi sana. Inawezekana kweli?
 
Back
Top Bottom