Mzee Mohamed: Tuna kazi kubwa sana kumuandaa kijana atakayefanana na Magufuli

Mzee Mohamed: Tuna kazi kubwa sana kumuandaa kijana atakayefanana na Magufuli

MZEE Mohammed Juma, Mkazi wa Unguja Zanzibar amesema kama Taifa tuna kazi kubwa sana kumuandaa kijana atakayefanana na Hayati Dk. John Pombe Magufuli na alikubali lolote limfike lakini Tanzania isonge mbele

“Tuna kazi kubwa sana ya kumuandaa kijana atakayefanana na Magufuli, tuna kazi kubwa sana , yule mzee aliingia pale hakuwa na tamaa yoyoye aliingia pale kwa niaba ya kuijenga Tanzania na alikubali lolote limfike lakini Tanzania isonge mbele” Mzee Mohamed Juma Mkazi wa Unguja, Zanzibar Tanzania.
Kuandaa makatili,mtoa roho,mjivuni,haambiliki,mporaji wa fedha za watu (Maduka ya kubadilisha fedha za kigeni) kujipendelea chato Airport,VETA,hospital ya rufaa,Zimamoto,mahakama,CRDB,Tanesco ........

Mungu aliipenda sana Tanganyika
 
..itachukua muda mrefu kupata kiongozi laghai, mbaguzi, mkabila, katili, na muuaji, kama Jpm.

..viongozi wa aina ile huzaliwa mara chache ktk taifa lolote lile.
Atatokea tena kizazi cha 3 kutoka sasa...vitukuu vyetu ataappear...!
 
Pumbavu sana, hili taifa halitakaa liongozwe na kichaa, mshamba, makabila na muuaji tena
Una miliki taifa gani hapa duniani, na una uhakika kuwa utaendelea kuwepo siku zote ili uhakikishe hilo halitokei?

Hizi akili mnatoa wapi?
 
Zungumzia uchaguzi wa 2020 ambao Mbelgiji haamini mpaka leo alivyotendwa na wapigakura na unapouzungumzia uchaguzi wa 2015 huku ukijua ushindani ulikuwa ni Kati Kati ya mwanaCCM kwa mwanaCCM ni kujitekenya na kucheka mwenyewe

Sijazungumzia uchaguzi wa 2020 maana haukuwepo. Uchaguzi wa 2019 na 2020 haukufanyika bali ni ujinga tu wa CCM na Magufuli.

Mtu mzima unaengua wagombea wa CHADEMA nchi nzima?. Halafu kuonesha ubaya unazima mtandao wa internet siku ya kupiga kura. Halafu Mungu alivyowaajabu, mwizi akizani amekomoa upinzani, akafa kifo Cha aibu.
 
Huyo mzee mjinga Sana. Kwa hivyo tumuandae dikteta Kama magufuli?. Watu wasio julikana?. Mimi kwangu rais yeyote anayedharau kundi Fulani kwenye jamii na kuona sio watanzania kufa na afe.
Ili utawale afrika kiongozi lazima uwe kauzu,magufuli hakufikia level ya kuwa diktekta,
Kwenye utawala wake ulishawahi kulala saa 12 jioni

Ova
 
Una miliki taifa gani hapa duniani, na una uhakika kuwa utaendelea kuwepo siku zote ili uhakikishe hilo halitokei?

Hizi akili mnatoa wapi?
Hatatokea, ilikuwa bahati mbaya sana 2015 nchi akapewa kichaa, wazee wa CCM hakuna wanachojutia zaidi ya kile
 
Eti hakuna rais Kama magufuli, mnalazimisha watu uongo. Kila Rais alifanya yake akaondoka. Haya ya kulinganisha Marais mmeanza nyie msiojua nchi imetokea wapi mpaka hapa ilipofikia. Kama Marais waliopita wangeweka misingi mibaya hata huyo magufuli asingefanya lolote.

Ila Ni kweli hakuna Rais aliyewahi kufia madarakani zaidi ya magufuli hapa Tanzania Bara.

Kuandaa makatili,mtoa roho,mjivuni,haambiliki,mporaji wa fedha za watu (Maduka ya kubadilisha fedha za kigeni) kujipendelea chato Airport,VETA,hospital ya rufaa,Zimamoto,mahakama,CRDB,Tanesco ........

Mungu aliipenda sana Tanganyika
Uwa kunatakiwa kuwe na mipaka Kati ya mzazi na mtoto hivyo naweza kusema Hayati ni kama mzazi na wengine ni kama watoto. Ukiachana na jukumu kuu la mzazi ambalo ni kulea pia jukumu hilo linaenda sambamba na kukanya na kuadhibu.

Hayati Magufuli hakuwa na sifa hizo ila watoto wakaidi lazima wamchukie mzazi mkali
 
MZEE Mohammed Juma, Mkazi wa Unguja Zanzibar amesema kama Taifa tuna kazi kubwa sana kumuandaa kijana atakayefanana na Hayati Dk. John Pombe Magufuli na alikubali lolote limfike lakini Tanzania isonge mbele

“Tuna kazi kubwa sana ya kumuandaa kijana atakayefanana na Magufuli, tuna kazi kubwa sana , yule mzee aliingia pale hakuwa na tamaa yoyoye aliingia pale kwa niaba ya kuijenga Tanzania na alikubali lolote limfike lakini Tanzania isonge mbele” Mzee Mohamed Juma Mkazi wa Unguja, Zanzibar Tanzania.

Akawadanganye wapumbavu wenzie waliozeeka akili labda.
 
Rest in Eternal Peace Mr. President, kivuli chako kitaishi nasi milele na milele. Kila uchao na uchwao kuna mtu anakukumbuka na kukulia,hakika ulikuwa zawadi kubwa sana kwa Tanzania yetu.
Afrika tutaendelea kuwa masikini miaka na miaka. Binadamu anakufa leo yupo kesho hayupo. Huyo kijana unamuaanda kesho anakufa halafu kinachofuata?
Pale Marekani hata ukimweka hata mtoto wa miaka 5 bado nchi itaendelea kwasababu wameweka sheria, katiba na mfumo imara ambao kila kiongozi lazima aufuate na ukiwa nje ya hiyo mifumo lazima mfumo ukuondoe. Mfano hai Trump
 
Hilo ni kweli tupu. Jana nilipita sehemu panapoendelea ujenzi sgr nikaona kazi inavyotembea na nikajisemea kweli Magufuli alikuwa kichaa. Kichaa mwenye maamzi magumu aliyekuja wakati mwafaka kabisa. Ndani ya miaka yake mitano aliweza ibadili tz kwa miundombinu pamoja na mambo mengine mazuri kedekede.

Nb. Kichaa si tu mwehu bali pia mtu mwenye maamzi magumu na mzee wa kazi kazi
 
Uwa kunatakiwa kuwe na mipaka Kati ya mzazi na mtoto hivyo naweza kusema Hayati ni kama mzazi na wengine ni kama watoto. Ukiachana na jukumu kuu la mzazi ambalo ni kulea pia jukumu hilo linaenda sambamba na kukanya na kuadhibu.

Hayati Magufuli hakuwa na sifa hizo ila watoto wakaidi lazima wamchukie mzazi mkali

Mzazi gani mbaguzi?. Unabomoa nyumba eneo Fulani kisa hawakukupigia kura na kuacha eneo jingine kisa walikupigia kura. Mara amwambie spika washughulikie ndani wakitoka nitawashughulikia. Mara sipeleki maendeleo kwa wapinzani.

Yule hakuwa na sifa za kuwa mzazi .
 
Back
Top Bottom