Ni nani wa kujibu hoja za Tundu Lissu?

Ni nani wa kujibu hoja za Tundu Lissu?

Ametoa HOJA kuwa bandari zetu zote za bara wamepewa waarabu,

Lakini Bandari za Zanzibar hazijaguswa,

HOJA kama hiyo Badala ya kulijibu unaamua kuipuuza kweli?

Halafu akasema kesho Mei Mosi watu wataenda kulia na kumbembeleza Samia awahurumie adha za kikokotoo na mishahara. Kwa sababu mwaka wa 1964 Rais Nyerere alifuta Tanganyika Federation of Labor akaunda NUTA, ndo hii TUCTA , halafu Nyerere akasema kuanzia leo Rais wa NUTA atateuliwa na Rais wa Tanganyika. Ukawa mwisho wa maandamano, mwisho wa haki ya mfanyakazi.

Katiba mpya ikilinda uhuru wa vyama vya wafanyakazi madhila ya kikokotoo na kubembeleza mishahara yatakwisha.

Sasa nani serikalini humu unadhani anaweza kujibu hoja zinazo elucidate the weakening evolution of labor movement across the history of Tanganyika ?

Zahara Yunus ? Gerson Msigwa ? Mwenezi Nchimbi wa CCM masikini ya Mungu. They are in over their heads! It is very unfair and very inconsiderate kuwatupia hawa rookies zigo la kuwajibu wapinzani.
 
naona umerudia tu nilichokujibu kwa kifupi sana kwenye first reply yangu dhidi maswali yako ya mawili madogo ya msingi .....

hapa umefafanua majibu yangu kwa upana kidogo, meaning kwamba ulivyokua unauliza tayari ulikua na majibu yako ambayo ni sahihi na ni sawa na nilichokujibu 🐒

by the way enjoy workers day holiday 🐒
Sasa unatushauri Vipi Sukuma Gang..
Maana Bado tuna Machungu Na Rais wetu hatukumfaidi kabisa akafariki
 
Jibu la hili swali ni jepesi sana.
Jibu sahihi ni HAKUNA.

Unataka nifafanue kidogo hilo jibu?
Ni hivi: Serikali unayoisema ni ya CCM. Watumishi wake wote, hata hao akina AG ni mali ya CCM

Hebu niambie, wewe una kifaa chako, ni mali yako, kwa mfano nguo, au jembe. Si utavitumia kadri unavyoona wewe inafaa?
Lakini nisikuache na dukuduku kuhusu ufafanuzi wangu huu. Inanibidi nifafanue tena hiyo CCM na viongozi waliopo huko kutoweza kujibu swali lako pia.
Ni hivi: CCM ni chama cha unafiki. Ndani ya CCM hakuna anayeweza kumwambia mwenzie ukweli, hata kama ukweli huo uko wazi.
Muundo wa CCM ulivyo, tazama CC (Central Committee), wajumbe wake, na hata Halmashauri Kuu ya Chama hicho uwiano wa wajumbe wake, toka Tanganyika na Zanzibar.
Hawa wajumbe wa Tanganyika, hata siku moja utasikia wakiwagomea chochote wale wa Zanzibar; hasa katika maswala yanayohusu Zanzibar. Kwa hiyo maamuzi yanayochukuliwa kuhusu Zanzibar, ni uamzi wa wajumbe toka Zanzibar.
Asikudanganye mtu kwamba mambo ya Zanzibar yanaamuliwa na watu wa Tanganyika. Hao akina Jumbe kuachishwa uRais, ni waZanzibari ndani ya CCM ndio walikomaria swala hilo, na kuungwa mkono na akina Mwalimu Nyerere, kwa vile Jumbe alikuwa anashindana kulegeza muungano, ambao uliasisiwa na akina Mwalimu. Mwalimu asingekubali kuona juhudi zake zikisambaratika.

Kuna hizi stori za viongozi wa Zanzibar kuchaguliwa Dodoma. Huu ni uongo. CCM Zanzibar ndio huchagua viongozi hao, na kutegemea wenzao wa Bara kuhakikisha chaguo lao linapita kwa njia yoyote, hata kwa kumwaga damu.

Looo, nitatiririka hadi wapi sasa. Natumaini umenielewa mkuu 'Rabbon', pamoja na wasomaji na wachangiaji wa mada yako hii.
Ahsante ndugu Kalamu , Mimi nimeelewa,

Japo ndani ya CCM wapo watu aina ya Judge Warioba wanaopenda kusema Kweli na kujibu HOJA.
 
Salaam, Shalom.

Ni wiki sasa, Mwanasheria msomi Tundu Lissu ametoa HOJA nzito kuhusiana na Muungano wetu, bandari, na anatoa HOJA Kwa kutumia Katiba ya nchi iliyopo.

Cha kushangaza wanaibuka viongozi tena wenye hadhi ya juu kabisa na kumjibu TUNDU Lissu kiujumla jumla tu. Anauliza swali Kwa kunukuu Katiba ya nchi, lakini anajibiwa Kwa kauli nyepesi za kisiasa bila ushahidi wowote au nukuu yoyote kisheria, imekaaje hii?

Jamani, HOJA hujibiwa Kwa HOJA,

Angalau Serikali chini ya AG ingeitisha mdahalo wa wazi, Lissu akaalikwa na HOJA muhimu zikajadiliwa Kwa maslah ya Taifa Kwa uelewa wa umma wa wananchi.

Swali linabaki kuwa, huko serikalini hawapo watu wenye capacity ya kumjibu TUNDU Lissu Kwa HOJA?

Karibuni🙏
Lissu mtu ambae anaweza kufanya nae mdahalo ni mzee Warioba tu ila wengine siwaoni
 
Salaam, Shalom.

Ni wiki sasa, Mwanasheria msomi Tundu Lissu ametoa HOJA nzito kuhusiana na Muungano wetu, bandari, na anatoa HOJA Kwa kutumia Katiba ya nchi iliyopo.

Cha kushangaza wanaibuka viongozi tena wenye hadhi ya juu kabisa na kumjibu TUNDU Lissu kiujumla jumla tu. Anauliza swali Kwa kunukuu Katiba ya nchi, lakini anajibiwa Kwa kauli nyepesi za kisiasa bila ushahidi wowote au nukuu yoyote kisheria, imekaaje hii?

Jamani, HOJA hujibiwa Kwa HOJA,

Angalau Serikali chini ya AG ingeitisha mdahalo wa wazi, Lissu akaalikwa na HOJA muhimu zikajadiliwa Kwa maslah ya Taifa Kwa uelewa wa umma wa wananchi.

Swali linabaki kuwa, huko serikalini hawapo watu wenye capacity ya kumjibu TUNDU Lissu Kwa HOJA?

Karibuni🙏
HAKUNA MTU WA KUJIBU, maana wakijibu Lissu atawamiminia lisasi 32 zaidi hoja nzito nzito.
 
Lissu mtu ambae anaweza kufanya nae mdahalo ni mzee Warioba tu ila wengine siwaoni
Na mbaya zaidi Judge Warioba Yu pamoja na Lissu katika mstari wa Kweli na HAKI, haezi mjibu Kwa maana ya kumzima Kwa HOJA.
 
it is very simple, observe some technical 48laws of power...

you can't fight them join them and ofoz you will be safe 🐒
Ni Ngumu maana Tunataka Tume Huru ya Uchunguzi wa Kifo cha Kiongozi wetu..
Tumeanza kumtuna Luhaga Mpina ila wengine watakuja Pia
 
Mbona alipokuwa bungeni mlijaribu kumjibu Kwa HOJA?
Akirudi Bungeni atalazimishwa kuongea pointi na atajibiwa kwa pointi na sio kuropoka anakofanya Sasa hivi. Kumbuka ni watu wasio na uelewa tu na "issues" ndio wanamuelewa.
 
Lissu aana tatizo la kisaikolojia baada ya ile ajali yake ya kupigwa risasi na majambazi kwahiyo asichukuliwe siriazi tafadhali.
 
Kumpuuza inatokana na kukosa hoja zenye mashiko za kumjibu
inaweza kua katika mbinu na hisabati ya siasa,

kwani mbaya iko upande gani hoja yako ikipuuzwa na ukuanza kubabaika na kuhangaika mwenywe physically and mentally, that is science in politics 🐒
 
Kwani Ubongo unakaa miguuni alikopatia Ajali?
Ripoti za madaktari zinaonesha Lissu hawezi kuwa sawa tangu alipopata ile ajali kutokana na kumuharibu sana kisaikolojia kwahiyo inashauriwa asichukuliwe seriously kwa mambo anayoongea.
 
Ripoti za madaktari zinaonesha Lissu hawezi kuwa sawa tangu alipopata ile ajali kutokana na kumuharibu sana kisaikolojia kwahiyo inashauriwa asichukuliwe seriously kwa mambo anayoongea.
Kwahiyo wamasai hawakufukuzwa ngorongoro na mbuga kupewa waarabu?

Kwamba bandari zetu ni issue ya Muungano, iweje bandari za bara wapewe wageni, za Zanzibar zisiguswe?

Matokeo ya Urais 2020 kituo Kwa kituo, hayapo kwenye website ya Tume ya Uchaguzi, ni Kweli au Si Kweli?

Kati Yako na Lissu na wewe, nani yafaa apuuzwe?
 
Back
Top Bottom